Daah Ajira ngumu aisee!

Daah Ajira ngumu aisee!

jaribuni kutafuta kazi za marketing, kwanza zipo nyingi alafu hawakulipi ila unajilipa mwenyewe, kikubwa ninachopendea hizi kazi ni exposure, inakupa confidence, inakufanya unakuwa mbunifu na kufikiri zaidi.
binafsi katika kutafuta kazi tena kwa kupitia zoom nilipata kazi ya sales kwenye kampuni ya furnicher posta, natafuta mteja nikipata nnalipwa 4%, na bado mhindi anakata kodi, katika kazi hiyo hiyo nilifahamiana na watu wengi, lakini baadae nilipata kazi nyingine nzuri ya ofisini.
 
Ushirikina sipendi kaka.
 
Kumpata Lowasa nampataje sasa
kwa mfano?..na huko aliko naendaje?..kwa miguu ama??..kaka unaongea ma
vapour tu hapa. Tindikali..viongoz wakubwa kama hao si rahisi kuwaona
kirahisi rahis kiivo. Pritenda mkubwa....

Lowassa anaonana na vijana wengi na anawasaidia, hata hapa dar anapatikana, ukimsotea unampata... Huo ufisadi ni wake, cha msingi we unamueleza shida yako.

Nimekupa mwanga tu, hata mr Mengi na yeye uwa anasaidia..

Sasa mimi napokupa alternative, afu wewe unaanza kuongea maneno ya shombo, kwa mfano unasema naongea "ma vapour", kwa kweli nashindwa kukuelewa... Okay, endelea kusota....
 
plz jaribu hata kufanya kazi kwa kujitolea ktk auditing firms, hawa jamaa watakupa nauli pamoja na msosi, simply google all auditing firms found in TZ, nyingi zipo dar, then jaribu kuwacontact moja baada ya nyingine kwa kupeleka barua ya kuomba kufanya kazi kwa kujitolea, naamini hapo utafanikiwa tu kwa uwezo wa Mungu.
 
Dah mkuu nimesoma hadi mwishonilifikiri story itaishia vizuri kwamba umepata kazi unfortunately dah..pole kaka..siku yako ipo inakuja utachagua pa kwenda mwenyewe.
 
Mimi nilipomaliza chuo nilikaa mwaka mmoja bila shughuli yeyote,
Baadaye nikaenda kwenye kakampuni nikawa natembeza vyombo, unauza bei ya juu, unakata pesa ndiyo mshahara wako, usipouza na wewehela huna, nilivumilia ili tu kukicha niwe na pa kwenda. Nilijifunza five steps to sell, Sijui eight steps to success lakini baada ya mwaka mmoja sikuona gain yeyote, nilikuwa napata hela ya kula tu halafu kazi ngumu kwrlikweli, unatembea mitaani hadi sole za viatu vinaisha, hujauza

Baada ya mwka mmoja niliacha, nikaenda kufundisha shule za kata, imagine, graduate unafundisha form one na form two physics na hesabu,mshahara elfu 70, nikawa nafundisha vishule viwilikwa wakati mmoja, Nikawa napata pesa ya nauli kwenye interviews mbalimbali,

Baadaye nikapa sehemu nzuri kutokana na elimu yangu, sasa hivi mambo safi.

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa nilikaa almost miaka mitatu ndipo nikapata sehemu ya maana.

Kwa hiyo na wewe kama umesota kwa mmiaka miwili au mitatu usiogope, ndivyo ilivyo.
 
pole mkuu.nimesikitika pale ulipo pata kazi ya ualinzi,kuripoti wanadai jina halionekani.
Imewahi kunitokea inayofanana na wewe baada ya kufanya interview sita za mchujo na kupita na kupigiwa simu ya hongera na kwamba nikachukue mkataba ofisini kwao ili niende nao kwenye kituo chao cha kazi,bahati nilikuwa sikai mbali na kituo.Ile kufika pale nakutana na wengine walioambiwa wachukue mikataba yao ya kazi,nikiwa nafuraha huku naomba nipewe mkataba wangu, muhusika anadai jina langu halipo wala mkataba wangu,nikawaambia mbona mmenipigia simu kama saa 1 imepita ,yule mdada akanijibu kimkato ,haoni jina langu, kwa hiyo sikuipata hiyo kazi.
Sijapata kazi mpaka sasa na wala sitafuti, ila mambo yangu yataenda kupitia ajira binafsi(mikakati imeanza), Kila mtu ana njia yake Mungu aliyomuandikia ya kupata kipato.
pole,ila usivunjike moyo mkuu endelea na aina nyingine ya jitihada
 
Pole sana mkuu...jitihada zako ni kubwa sana ipo cku tu mungu atakusaidia na mambo yatakuwa mwake!
 
Duh, mkuu pole sana na mwombe Mungu sana siku moja utafanikiwa kwani kuhangaika kote huwezifananisha na mkaa bure
 
Asante kwa ushauri mzuri.
 
Jana nilikua down sana...daah kumbe nilikutukana bro??..nsamehe sana kaka. Nashukuru kwa ushauri pia
 
Nashukuru sana kwa ushauri. Umenipa moyo sana. Asante sana.
 
Asante bro. Appreciated!!
 
Asante sana. Hapa nna mawazo ya kua kuli pale bandalini. Sijui nako wanabana??
 
Polisi sitaki kabisa kuwasikia. Jamaa waliwahi kunivuta korodan zangu. Sitaki kabisa hata hilo jina. Mavi mavi

Hahahaha,mkuu haki yako inatia huruma ila nimeshindwa kujizuia hapo...
 
Pole sana dogo.
Siri moja ya kupata kazi tanzania siyo mbinu unayotumia.kamwe huwezi pata.ukiona tangazo kwenye gazeti au mtandaoni jua tayari zilishajzwa hapo wanafanya tu kukamilisha utaratibu.

fanya hivi.
1:We tumia wafanyakazi waliopo katika sekta unayotaka wawe wanakupa update ya uwezekano wa kazi na ukipata hiyo update jaribu kuwatumia watu wanaojuana na mhusika ili uweze kumuona faragha kwanza(siyo rushwa).
2:Omba kazi ya kujitolea katika baadhi ya tahasisi kwani wengine tulipata kazi kupitia njia za kujitolea ambapo unapiga mzigo mpaka boss anakuita jembe,kila kitu wewe,unakuwa kiraka.siku ukitaka kuondoka utaganganiwa na kuajiriwa.

3.Tumia ofisi ya kujitolea kama address na kukuza CV yako.vijana wengi from school kwa sasa hajui mambo ni lundo tu la vyeti,ufanisi ziro.jitambue kwanza,jishushe kijana,elimu yako weka pembeni saka ajira kama ambaye hajasoma theni ukipata basi hapo tumbua nk.
 
Kweli bro..jamaa hawafai
 
Asante bro. Ushauri mzuri pia
 
Back
Top Bottom