CWT waunga mkono uanzishwaji wa bodi ya kitaalam ya walimu Tanzania

Suala la Fatma ni la kisiasa.

Hilo hatuwezi kulilinganisha na Walimu ambao hatuwaoni kwenye uharakati.

Lengo la Bodi ya Ualimu(kama zilivyo bodi zingine za kitaaluma) ni kulinda miiko, maadili ya utendaji kazi kupitia usajili na leseni zao za kazi.

Kuna mambo mengi yanayofanywa na Walimu ambayo ni kinyume na maadili ya kazi zao na wameshindwa kuwajibishwa kisa hamna chombo kinachosimamia taaluma yao.

Mwalimu akihofia kupoteza ugali kwa kwenda kinyume na maadili hatathubutu kufanya kosa.

Haya ndio mambo ambayo Bodi itatakiwa kujihusisha nayo.

Sambamba na hilo, Bodi itaweza kuwapika Walimu kupitia mchakato wa mafunzo kwa vitendo pamoja na mitihani ya usajili. Walimu akifuzu hizo hatua atakuwa kaiva kwa kiasi fulani ukilinganisha na ambaye hajapita hizo hatua, na hatimaye atasajiliwa na kupewa leseni ya kazi.
Unasemaje ni la kisiasa wakati bodi ya mawakili (TLS) imeshiriki kumfutia uwakili? Kwa nini ulione ni la kisiasa wakati halijafanywa kwenye jukwaa lolote la chama chochote bali limefanywa mahakamani na kwenye kamati za chama cha mawakili (professional)? Na mahakama ikaja kubaini kuwa taratibu hazikufuatwa

Kuna hii kesi ya Mwalimu Ezekiah Olouch Ezekiah T. Olouch vs The Permanent, Secretary, President's Office, Public Service Management & Others (Civil Appeal No.140 of 2018 ) [2020] TZCA 2; (06 January 2020) | Tanzania Legal Information Institute, Katibu Mkuu wa Wizara alimfukuza kazi huyo mwalimu pasipo kuwa na mamlaka wala pasipo kufuata taratibu na CWT alikokuwa Naibu KM wa Chama nako wakamsimamisha kazi baada ya KM kumfukuza kazi. Mwalimu amepambana sana na hatimae Mahakama ya Rufaa ikaamuru kuwa uamuzi wa KM ulikuwa batili maana hakuwa na mamlaka ya kumfukuza kazi jamaa na hivyo akarudi kazini.

Sasa hiyo bodi ya walimu inayopambaniwa ndio itakuwa fimbo rahisi ya kuwachapia walimu kwa kuwafutia uanachama ili wasifanye kazi licha ya kuwa na elimu. Huo ni ujinga, badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma

Kuhusu mafunzo ya vitendo, hakuna mwalimu anayekuwa mwalimu bila kufanya mazoezi ya vitendo, kwa hiyo yatakuwa ni marudio tu ya kilichofanyika tayari. Walimu huenda BTP/Field na kudeal na kazi halisi (wanafunzi halisi, masomo halisi nk).
 
Yap, mtu anaweza kuwa mwalimu wa somo fulani kwa sababu ya cheti, kumbe ni mweupe kabisa. Bodi itaondoa hilo.
Inawezekana hujaelewa hizo bodi zinavyopata watu wake. Huwa wanafanya mitihani (theory) na inasahihishwa waliofaulu wanatunukiwa hiyo profesheni level..sasa hii mitihani haina tofauti yoyote na ile, ni theoreical tu, haimfanyi mtu kuwa konki. Yaani kufaulu au kufeli mtihani huo sio kipimo cha ukonki wa somo zima. Halafu miaka yote hii ambavyo hawana bodi kumekuwa na malalamiko ya uwezo wa kitaaluma wa walimu?
 
Inawezekana hujaelewa hizo bodi zinavyopata watu wake. Huwa wanafanya mitihani (theory) na inasahihishwa waliofaulu wanatunukiwa hiyo profesheni level..sasa hii mitihani haina tofauti yoyote na ile, ni theoreical tu, haimfanyi mtu kuwa konki. Yaani kufaulu au kufeli mtihani huo sio kipimo cha ukonki wa somo zima. Halafu miaka yote hii ambavyo hawana bodi kumekuwa na malalamiko ya uwezo wa kitaaluma wa walimu?
Kada za afya wanafanya hiyo mitihani. Na ukifeli hupewi leseni ya taaluma. Inasaidia kuchuja hasa kwa jinsi vyuo vilivyokuwa vingi.
 
Kada za afya wanafanya hiyo mitihani. Na ukifeli hupewi leseni ya taaluma. Inasaidia kuchuja hasa kwa jinsi vyuo vilivyokuwa vingi.
Hapo ni kuongezeana vyeti ili uambiwe ww ni professional uvimbe kichwa utake mshahara wa juu usiajirike private sector.

Kama NBAA tu, hawawasaidiii watu wao kupata njia za kipato, CPA wengi tu hawana ajira, private sector diploma wengi na certificates wameajiriwa na kuwaacha CPA's wakijiita professionals mitaani na mabegi yao bila ajira.

Wanasheria wao wanajitahidi kwa kuwapa fursa za kutumia mihuri kirahisi.
 
Unasemaje ni la kisiasa wakati bodi ya mawakili (TLS) imeshiriki kumfutia uwakili? Kwa nini ulione ni la kisiasa wakati halijafanywa kwenye jukwaa lolote la chama chochote bali limefanywa mahakamani na kwenye kamati za chama cha mawakili (professional)? Na mahakama ikaja kubaini kuwa taratibu hazikufuatwa

Kuna hii kesi ya Mwalimu Ezekiah Olouch Ezekiah T. Olouch vs The Permanent, Secretary, President's Office, Public Service Management & Others (Civil Appeal No.140 of 2018 ) [2020] TZCA 2; (06 January 2020) | Tanzania Legal Information Institute, Katibu Mkuu wa Wizara alimfukuza kazi huyo mwalimu pasipo kuwa na mamlaka wala pasipo kufuata taratibu na CWT alikokuwa Naibu KM wa Chama nako wakamsimamisha kazi baada ya KM kumfukuza kazi. Mwalimu amepambana sana na hatimae Mahakama ya Rufaa ikaamuru kuwa uamuzi wa KM ulikuwa batili maana hakuwa na mamlaka ya kumfukuza kazi jamaa na hivyo akarudi kazini.

Sasa hiyo bodi ya walimu inayopambaniwa ndio itakuwa fimbo rahisi ya kuwachapia walimu kwa kuwafutia uanachama ili wasifanye kazi licha ya kuwa na elimu. Huo ni ujinga, badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma

Kuhusu mafunzo ya vitendo, hakuna mwalimu anayekuwa mwalimu bila kufanya mazoezi ya vitendo, kwa hiyo yatakuwa ni marudio tu ya kilichofanyika tayari. Walimu huenda BTP/Field na kudeal na kazi halisi (wanafunzi halisi, masomo halisi nk).
Ishu ya Fatma ni ya kisiasa kutokana na yeye kukosoa utawala wa mwendazake, serikali ya mwendazake ndio iliyoshinikiza afutiwe leseni kupitia Bodi ya mawakili, baadae ndio mahakama ikasema utaratibu haukufuatwa tena baada ya mwendazake kuondoka maana ndio mahakama ilipata kupumua ukilinganisha na kipindi alipokuwepo mwendazake.

Hivi ukitoa maoni yako kwa kukosoa utawala ni kukiuka maadili ya taaluma yako kweli? Sijasikia sheria yeyote ya Bodi yeyote ya kitaaluma ikataze watu kutoa maoni yao.

Kuhusu maadili na miiko ya kazi za kitaaluma, mara kadhaa tumeona na kusikia wauguzi wakifutiwa leseni baada ya kufanya makosa katika kazi zao mfano kuwapiga wagonjwa. Huko ndio kukiuka maadili ya kazi na hapo ndio inatakiwa tuone makucha ya Bodi.

Hivi ndivyo tunavyotaka iwepo pia kwa Walimu pindi wanapofanya makosa katika maeneo yao ya kazi ili waweze kuwajibishwa bila kuonewa
 
Inawezekana hujaelewa hizo bodi zinavyopata watu wake. Huwa wanafanya mitihani (theory) na inasahihishwa waliofaulu wanatunukiwa hiyo profesheni level..sasa hii mitihani haina tofauti yoyote na ile, ni theoreical tu, haimfanyi mtu kuwa konki. Yaani kufaulu au kufeli mtihani huo sio kipimo cha ukonki wa somo zima. Halafu miaka yote hii ambavyo hawana bodi kumekuwa na malalamiko ya uwezo wa kitaaluma wa walimu?
Mitihani watakayoifanya ni kutokana na mambo waliyoyafanya kwa vitendo kazini(Internership), itabase kuuliza vitu walivyojifunza kwa vitendo. Hii ni hatua ya kuhalalisha usajili na upewaji wa leseni kwa wahusika.

Ni kweli kufaulu hiyo mitihani haimaanishi mtu kaiva kwa 100% ila inakuwa ni afadhali kuliko na yule ambaye hajapitia hizo hatua.

Ubovu wa walimu upo ingawa hakuna malalamiko unayoyasikia, nina imani hata wewe wakati unasoma uliwahi kukutana na walimu wazuri na wabovu katika ufundishaji.
 
Hapo ni kuongezeana vyeti ili uambiwe ww ni professional uvimbe kichwa utake mshahara wa juu usiajirike private sector.

Kama NBAA tu, hawawasaidiii watu wao kupata njia za kipato, CPA wengi tu hawana ajira, private sector diploma wengi na certificates wameajiriwa na kuwaacha CPA's wakijiita professionals mitaani na mabegi yao bila ajira.

Wanasheria wao wanajitahidi kwa kuwapa fursa za kutumia mihuri kirahisi.
Hivi hao Diploma na Certificate si na wao wanasajiliwa na NBAA?

Kuhusu suala la ajira, mwajiri siku zote anaangalia maslahi yake na anaona bora aajiri mtu ambaye atamlipa kidogo ndipo unaona private sectors wanaajiri Diploma na Certificate holders
 
Hivi hao Diploma na Certificate si na wao wanasajiliwa na NBAA?

Kuhusu suala la ajira, mwajiri siku zote anaangalia maslahi yake na anaona bora aajiri mtu ambaye atamlipa kidogo ndipo unaona private sectors wanaajiri Diploma na Certificate holders


Sasa kwann mwajiri akulipe mshahara wa professional kwa miaka 4 ya yeye kukufundisha kazi usioijua ili upate uzoefu ndo aanze kuinjoy uwepo wako?

Maana diploma fresh from school na professional fresh from board wote wanafananaga tu hawana uzoefu zaidi ya vyeti.
 
Back
Top Bottom