CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

Nyinyi mbona vichwa vya Samaki! Hivi mafumbo ya Mwalim NYERERE hamjafahamu? Kwamba bila Muungano, hakuna kitu kinachoitwa Zanzibar, yaani inaguezwa ardhi halali ya Uridhi wa Tanganyika, Zanzibar waarabu waliridhi kwa Wareno. Kwa hiyo kama Zanzibar imechoka kupewa heshima ya ndani basi watarudishwa kwa lazima hilo lieliweke. Anaebisha ajaribu kufanya fujo kama kile kikundi cha Karume na kuna Mansur, Uamsho.
 
Nyinyi mbona vichwa vya Samaki! Hivi mafumbo ya Mwalim NYERERE hamjafahamu? Kwamba bila Muungano, hakuna kitu kinachoitwa Zanzibar, yaani inaguezwa ardhi halali ya Uridhi wa Tanganyika, Zanzibar waarabu waliridhi kwa Wareno. Kwa hiyo kama Zanzibar imechoka kupewa heshima ya ndani basi watarudishwa kwa lazima hilo lieliweke. Anaebisha ajaribu kufanya fujo kama kile kikundi cha Karume na kuna Mansur, Uamsho.

Acha pombe wewe, yani Nyerere unamfanya kam ndio Mungu wako sio, Wazanzibar hatuogopi wala hatuzitii akilini kauli za mwehu yule, MPIGA DOMO, eti "ningekuwa na uwezo ningevisogeza mbali visiwa vile Shabbash!! ameondoka yey Zanzibar ameiyacha pale pale, na ndivyo watavyondoka Watanganyika wote wenye nia mbaya na Zanzibar yetu, wakaungane na Jahili mwenzao Nyerere!!
 
HII NI HOJA YA MSINGI NI LAZIMA WABARA WAWEZE KUMILIKI ARDHI VISIWANI ILA KWA KIWANGO MAALUMU NA NDIO UTAKUWA UDUGU WA KWELI NA MUUNGANO WA HAKI,ONA WALIVYOJAZANA BARA NA MAEKARI WANAYOMILIKI! bara ni lazima tushinikize hilo ati!

Mushindikize kupitia chombo gani wakat Tanganyika yenu hamuijui ilipotokomea, hilo kwa Wazanzibar halitafanyika na daima hatutakubali kuchafuliwa ardhi yetu na watu Pori kutoka Tanganyika!!
 
Chama Cha Wananchi(CUF) kimepinga wazo na rai ya kupunguza masharti ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ili kulegeza nguvu zake kisheria na kuwapa fursa Watanzania Bara kumiliki ardhi Visiwani Zanzibar.

Msimamo huo umetolewa na Mkurugenzi wa Habari na Mwasiliano ya Umma wa CUF Salum Bimani katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana visiwani humo, siku chache baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Muungano) Samia Suluhu Hassan, kushauri Katiba ya Zanzibar kuangaliwa upya na kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar.

Bimani alisema kuwa suala la ardhi siyo la Muungano tangu mkataba wa awali wenye orodha ya mambo ya Muungano na siyo sahihi kufanyika marekebisho ili kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar kwani ni ndogo na ndiyo sababu hata waasisi wa Muumgano waliamua ardhi hiyo imilikiwe na wazanzibari pekee. Chanzo mwananchi

Safi sana - inabidi pia Wazanzibar na Wapemba wanaomiliki ardhi bara wanyang'anywe kwani wanamiliki isivyo halali [sheria zetu haziwapi ruhusa wageni kumiliki ardhi na kwa kuwa wazanzibari siyo raia wa tanganyika ardhi yeyote wanayo imiliki Tanganyika wanaimiliki kinyume cha sheria na kama wana hati yoyote ile basi hiyo hati ni NULL & VOID
 
..hao wanawatia hofu tu Wazanzibari.

..Zanzibar iondokane na sheria hiyo ya kibaguzi dhidi ya wa-Tanganyika.

..masuala ya supply vs demand ndiyo yanayopaswa kuamua ni jinsi gani Watanganyika wana access na ardhi ya Zanzibar.

..mpaka sasa hivi wa-Zanzibari wengi zaidi wanahamia Tanganyika kuliko kinyume chake.

..katika masuala ya ardhi migration huwa ni kutoka kwenye eneo dogo[Zanzibar] kwenda kwenye eneo kubwa[Tanganyika]. suala lingine linaloathiri migration huwa ni neema na opportunities za kiuchumi.

cc takashi, GHIBUU, gombesugu, Nguruvi3

Mkuu JokaKuu,

Hishma yako ndugu yangu na nimekusoma!

Hapo nilipo-BOLD kwenye hiyo bayana yako...nafikiri ni muhimu pia tukajaribu kutazama vigezo/vipengele vilivyotumika na hilo Baraza la Wawakilishi wakti huo na mpaka ikawalazim kupitisha sharia hiyo ya umiliki wa ardhi pale Zanzibar!?

Kama pana mwenye navyo na avilete hivyo vipengele hapa jamvini,ili tuvitazame soote kwa pamoja...kuliko kuviita vya "kibaguzi" bila ya kujua mantiki/madhumuni yake kiundani na kutazama validity yake kitaaluma,khasa katika haya "mazingira" yaliyopo hivi sasa katika huo "Muungano"!?

Hayo ndo maoni yangu kiduchu,kwa sasa!

Ahsanta.
 
Lazima Tuwe wakweli. Hivi wakija Watu millioni 2 tu kutoka Bara wakataka ardhi kweli tunayo ardhi hiyo. WaZanzibari wapo 1.2 million kuna matatizo ya kugombea ardhi

hao watu mil 2 waje kwani hawana ardhi walikotoka? Haki ya kumiliki ardhi inampa uhuru mtz kuishi popote anapojipatia kipato mfano ni hao mapolisi au wafanyakazi wengine wa bara huko visiwani ni watz wanahaki ya kumiliki ardhi. kwani wabara walioko visiwanii ni milioni 2? acheni kuongea vitu vya kusadikika.
 
mushindikize kupitia chombo gani wakat tanganyika yenu hamuijui ilipotokomea, hilo kwa wazanzibar halitafanyika na daima hatutakubali kuchafuliwa ardhi yetu na watu pori kutoka tanganyika!!

utumbo wa samaki unaongea
 
ninavyojua mimi ni kwamba wako Watanzania bara wengi tu wenye
kumiliki ardhi huko visiwani pamoja na makanisa ambayo ni ya bara;
au vp? Kiongozi anaemiliki hecta 500 Morogoro, 300 Bagamoyo, 250
Mbeya na bado anatamaa ya hect 400 Zanzibar ili azihodhi tu haiewzekani.

una ushahidi gani ---- makanisa yaliyoko huko ni ya bara angali yalikuwapo toka enzi za sultani? unaweza kuthibitisha usemacho au ni udini umekujaa? zanzibar hakuna mashamba watu wanataka viwanja.
 
Usiwe mbumbumbu wa sheria! Hata kama Wazanzibari hawautaki muungano ni lazima kuwe na utaratibu wa kuliendea jambo hilo.

Kwani CHADEMA kwa nini wanakwenda bungeni wakati kile ambacho wanakitaka CCM ndicho kinachopitishwa?

Halafu eti na wewe pia unajinasibu kaw jina na GT!
Ktaiba ya 2010 imeondoa utaratibu wa kawaida na kuwapa utaratibu wanaoweza wao. Umeshaisoma na kuielewa.
Nenda kwanza maktaba ukishafunguka njoo tujadiliane yakhe

Wasalimie hapo kibandamaiti.
 
ni suala la muda tu, hakuna atakaye mwonyesha mwenzake njia

Tatizo ni kuwa tu wanafiki na laiti uwezo na ukubwa ungekuwa ndio unaoleta uamuzi basi huo muda ungalikwishakuja zamani!
 
Mkuu Averoes.

Hawa jamaa wanafiki sana jaribu kwenda kwao Kibosho au Rombo ukanunue ardhi kama watakuuzia mimi nilikuwa nataka shamba Kibosho walininyima kwa ubaguzi wao.

sheria za nchi zinakunyima kumiliki ardhi kibosho?katiba inasema huruhusiwi kumiliki ardhi kibosho?

tambua hapa hatusemi kuwanyang'anya au kulazimisha waznz wawauzie wabara ardhi, hapana hayo ni maamuzi ya watu binafsi hapa tunasema pale kiwanja kinapouzwa au kugawanywa na serikali isiwepo sheria ya kumnyima mtanganyika kisa ni mtanganyika.
 
Wakati mwingine hawa watu wanazungumza utadhani kichwani kuna madudu fulani hivi... yaani hata hisabati za seti hawazielewi... Wazanzibari hawana ardhi ndogo... NO THEY DON'T...ila utakapofika wakati kweli watakuwa na ardhi ndogo kwelikweli.

hofu ya hao akina bimani sio muungano bali ni dini, wengi hudhani watanganyika wakinunua ardhi basi wakristo wengi watahamia huko hilo ndio hasa tatizo. wanajua faida ya kumiliki ardhi pamoja kwa kuwa tanganyika iko kubwa ya bure ila hilo la dini ambalo wao hawasemi dini bali hutafutia sababu yeyote kuongelea maslahi ya dini bila kutaja dini.
 
Hapa nilipo kuna jirani yangu ambaye ni mzanzibar pure na anamiliki ardhi ya kutosha. Sasa huu uzi umenifungua macho kuwa kumbe ile ardhi inaweza kuwa yangu muda wowote,ni suala la muda tuuuu. Huyu jirani yangu alishawahi kumkatalia mtoto wangu wa mwanaume alipoenda kuchumbia kwake kwa kigezo cha kwamba suala la kuoleana si la muungano!!!!, kumbe hata ardhi nayo cyo suala la muungano!! Huyu jamaa atanikoma kwenye hili suala la ardhi lazima alikimbie jiji la sivyo akubali kijana wangu amuoe binti yake.


Unamahesabu makali sana , hata mimi ningekomaa.
 
Ktaiba ya 2010 imeondoa utaratibu wa kawaida na kuwapa utaratibu wanaoweza wao. Umeshaisoma na kuielewa.
Nenda kwanza maktaba ukishafunguka njoo tujadiliane yakhe

Wasalimie hapo kibandamaiti.

Wasalimie pia Simanjiro!
 
Katiba ya znz ya mwaka 1984 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 imetoa uwezo kwa BLW kufanya jambo lolote bila idihini ya JMT. Wamefanya hivyo si kwa jambo moja bali zaidi ya 10 na hakuna aliyewazuia.
Hivyo uwezo wanao isipokuwa ni woga na sijui ni kwanini.

Leo wasingekuja Dodoma nani angejadili muungano wasioutaka?
Leo wasingekuwa na hoja ya serikali 3 nani angejadili muungano?
Leo wasingekuwa na hoja za mkataba nani angejadili muungano?

Makundi yote ya wznz hakuna, narudia hakuna hata moja lililowahi kuja na option tofauti na hizo hapo juu. Leo unatuaminisha wamefungwa mikono. Wameanzisha kila kitu chao bila hata kuulizwa. Wana wimbo wa taifa, bendera yao, nembo yao, Ikulu yao, BLW, SMZ. Hakuna hata siku moja mwakilishi ndani ya BLM au BLW ameahi kufikisha mswada wa kukataa muungano.

Leo wanaotafuta cha uvunguni ni hao akina Pandu, Duni na Jusa.

Oktoba 6 2012 pale bwawani wafutao wamesema kwa meneno yao wanataka muungano
Jusa Ismail
Nasor Moyo
Manosur Himid
Prof Sheriff

Maalimu yeye keshachukua kitambulisho pale kareimjee mapema kabisa.
Naye pia hataki muungano!!! lakini ana kitambulisho mfukoni

Sheni juzi kazindua sherehe za muungano Maalim Seif akiwa pembeni, nao wanataka cha uvunguni eti.
Vuai keshasema muungano wanautaka.

Hawana mtu aliyewashika, na ndani ya BMLK siyo lazima ni hiari ya mtu.
Walikuwa na hiari ya kusema hatuji Dodoma kwasababu hatupendi kuwa wajumbe, hadi hapo muungano unegefika tamati. Wamejaa tele Dodoma wanavuta laki 3 useme eti wameshikiliwa na system! Kweli, real hoja ina chembe ya mantiki hiyo.

Nguruvi3

Nimesoma bayana zako umewashutumu sana kina Jussa,Nassor Moyo,Prof Sheriff na wengine,hivi unakumbuka kauli ya mwanasheria wa Chadema Tundu lissu kwamba muungano Umeshavunjika?

Je Chadema kwenda kusimamisha mgombea znz ni unafik/uzandiki au ni uroho wa madaraka unawasumbua?

Nguruvi ni sababu gani ilimfanya Nyerere kupata msukumo wa kufanya muungano wa Tanganyika na Zanzibar?

Je Nyerere alikuwa hajui huu muungano utawaathiri watanganyika hasa ile mikoa ya kusini Mtwara na Lindi kwasababu mgao wa bajet inayotoka Tanganyika kwenda Zanzibar ingeenda kuwasaidia watu wakusini?
 
Hili ni sawa tu hata sisi tumekataa wakenya ,waganda na wanyarwand wasije kumiliki ardhi hapa kwetu save kwa wapemba ambao tumewaruhusu kwa muda,lakini wakati ukifika nao wataambiwa warudi kumili ardhi kwao.Kimsingi unapozungumzia suala la Ardhi kumilikiwa na Mbara hakuna tofauti nakutaka mtanganyika akamiliki ardhi somalia. Zanzibar ni Foreign Jurisdiction as long and as far as to lend.
 
Back
Top Bottom