takashi,
..ninachopendekeza mimi ni kwamba wa-Tanganyika waruhusiwe kumiliki ardhi Zanzibar.
..mapendekezo hayo yanatokana na ukweli kwamba wa-Zanzibari wanaruhusiwa kumiliki ardhi huku Tanganyika.
..tuwe na sheria sawa ya kumiliki ardhi. baada ya hapo umiliki wa ardhi utakuwa determined na nguvu za soko[supply & demand].
.
gombesugu ametoa mfano wa maeneo ya Marangu na Machame ambako kuna ardhi ndogo. Pamoja na ukweli huo serikali yetu haijapitisha sheria ya kubagua wa-Tanganyika wasio wazawa wa maeneo[marangu,machame] hayo kuhamia huko na kumiliko ardhi huko.
..wa-Tanganyika na wa-Zanzibari wana mahusiano ya kindugu kwa karne kadhaa sasa. Haipendezi mahusiano hayo kuanza kutiwa mushkel ya sheria za kibaguzi kama hii iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.
NB:
..Balozi Seif Idi anapigana vikumbo na walalahoi huku Tgk kupata viwanja kule Kigamboni, lakini Prof.Ana Tibaijuka waziri wa ardhi huku Tanganyika hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.
..Dr.Mohamed Seif Khatib ameuziwa nyumba za serikali ya Tanganyika na waziri John Pombe Magufuli. Nyumba zile hazikuwa na uhusiano wowote na muungano, wizara ya ujenzi si ya muungano. Lakini huyu Pombe Magufuli hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.
Foum Jnr,
W. J. Malecela,
Chris Lukosi,
Kibunango,
Nguruvi3