CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

Naomba mwenye kuijua hiyo sheria au kipengele, akiweke hapa tufanye reference
 
Kama Zanzibar wameweka masharti makali dhidi ya watanganyika, kwanini nao wasidai serekali yao na kulipa mapigo ? Au innkua gere ?

Tulichokifanya huku Zanzibar ni kueka katiba yetu kwa maslahi ya watu wetu, sasa hii haijawazuia watanganyika kufanya watakacho kama wataona kina manufaa kwa watu wao....
 
Chama Cha Wananchi(CUF) kimepinga wazo na rai ya kupunguza masharti ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ili kulegeza nguvu zake kisheria na kuwapa fursa Watanzania Bara kumiliki ardhi Visiwani Zanzibar.

Msimamo huo umetolewa na Mkurugenzi wa Habari na Mwasiliano ya Umma wa CUF Salum Bimani katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana visiwani humo, siku chache baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(Muungano) Samia Suluhu Hassan, kushauri Katiba ya Zanzibar kuangaliwa upya na kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar.

Bimani alisema kuwa suala la ardhi siyo la Muungano tangu mkataba wa awali wenye orodha ya mambo ya Muungano na siyo sahihi kufanyika marekebisho ili kuwapa nafasi Watanzania Bara kumiliki ardhi Zanzibar kwani ni ndogo na ndiyo sababu hata waasisi wa Muumgano waliamua ardhi hiyo imilikiwe na wazanzibari pekee. Chanzo mwananchi


Ni vizuri wanasiasa na Wazanzibari wote wakaelewa na kujipanga, kuwaandalia Mazingira au maeneo ya kuhamia Wazanzibar kwa walioko huku Bara kwa sasa.
Maana kama hawatakuwa tayari kufungua milango kwenye zoezi la Uhuru wa kumiliki ardhi kwa pande zote za Muungano. Uwepeo wa Tanganyika baada ya Katiba hii hautawacha salama Wazanzibar wote walioko Tanganyika na hii haitaishia hapo itakwenda mbali (Unguja VS Pemba).

Wengine mtakumbuka Maneno ya Hayati JK-Nyerere.

NB.Ni vigumu Wazanzibar wakafurahia Ardhi Bara na wabara wawe wakuja wakiwa Kule zanzibar wacha tu subiri!
 
Lazima Tuwe wakweli. Hivi wakija Watu millioni 2 tu kutoka Bara wakataka ardhi kweli tunayo ardhi hiyo. WaZanzibari wapo 1.2 million kuna matatizo ya kugombea ardhi
Ok ardhi ni ndogo, basi suala la mafuta libaki kwenye muungano.
 
Najaribu kuivutia picha ya opération Kimbunga Mara baada ya Muungano kusambaratika.
Maana opération hiyo itakua ni zaidi ya ile ya wanyarwanda, hii hadi wananchi nahisi watashiriki kuwatafuta nyumba hadi nyumba na kuwaburuza kutoka popote oale watakapowapata hadi ufukweni na bandarini.
 
Hapa nilipo kuna jirani yangu ambaye ni mzanzibar pure na anamiliki ardhi ya kutosha. Sasa huu uzi umenifungua macho kuwa kumbe ile ardhi inaweza kuwa yangu muda wowote,ni suala la muda tuuuu. Huyu jirani yangu alishawahi kumkatalia mtoto wangu wa mwanaume alipoenda kuchumbia kwake kwa kigezo cha kwamba suala la kuoleana si la muungano!!!!, kumbe hata ardhi nayo cyo suala la muungano!! Huyu jamaa atanikoma kwenye hili suala la ardhi lazima alikimbie jiji la sivyo akubali kijana wangu amuoe binti yake.
Hahaha! Hii kiboko
 
Mkuu utakuwa umezaliwa juzi tu basi. Kwa sababu mi tangu nizaliwe Cuf nimegundua kuwa CUF ya zanzibar ipo kutetea maslahi ya WAZANZIBARI, sera zake zimejikita zaid katika UZANZIBARI, na pia haina sera ya kuvunja muungano bali serikali 3!!! Chadema tangu nzaliwe naona wao wapo katika ukanda tu, ukabila, udini, kutafuta umaarufu kupitia matukio, kutafuta sympathy ya wananchi, kufuja mali za chama kwa kukopeshana, kuzuia demokrasia na kumfukuza kila anaitishia kuchukua madaraka ya bamkwe na padre, kikubwa Zaidi, CHADEMA hakina nia nzuri na zanzibar, wala zanzibar hawana time nayo. Nikuweke wazi kidogo, fikra inayokufanya uone kuwa CUF ni cha cha waislam ambayo ni fikra batil, tambua kuwa Cuf ni waasi wa Ccm, na zanzibar tangu kipindi icho waislam ni 99% sasa sijui ingetosha vipi 1% wakristo kuonekana katika chama icho na hasa ukizingatia wakristo wao ni CCM kwa zanzibar, mngelikuwa cdm mpo zenjy mngeliwachukua wakristo weni
kwa ubaguzi huu zanzibar iachwe iende salama! Umejaa ubaguzi mpaka kwenye kope.!
 
Lazima Tuwe wakweli. Hivi wakija Watu millioni 2 tu kutoka Bara wakataka ardhi kweli tunayo ardhi hiyo. WaZanzibari wapo 1.2 million kuna matatizo ya kugombea ardhi

Wanzanzibar acheni unafiki, Acheni ubinafsi na mtawafanya wanzanzibar walioko Bara wavamiwe na kunyanganywa mali zao. Kwanza mnatutesa sana ondokeni mtuachie nchi yetu. Na mkiingia Bara mnaingia na passport. Tumewalea sana. Mara tuwasomeshe bure, mara tuwaleteee maharagwe bure. kilakitu bure.:target:
 
I can tell you, Land issue is a real test of the 'honesty' of Zanzibaries and emotional control of Tanzanians.
 
ninavyojua mimi ni kwamba wako Watanzania bara wengi tu wenye
kumiliki ardhi huko visiwani pamoja na makanisa ambayo ni ya bara;
au vp? Kiongozi anaemiliki hecta 500 Morogoro, 300 Bagamoyo, 250
Mbeya na bado anatamaa ya hect 400 Zanzibar ili azihodhi tu haiewzekani.

Kanisa lipi la bara mkuu? Tujuze uzuri wengi tulikuwa tunajua makanisa mengi yanatoka ulaya
 
Hivi watanganyika mna matatizo ya ardhi mpaka mupewe na ardhi ya zanzibar?sie wenyewe haitutoshi kaeni huko kwenu tanganyika mulime,zanzbr kwanza.

..hao wanawatia hofu tu Wazanzibari.

..Zanzibar iondokane na sheria hiyo ya kibaguzi dhidi ya wa-Tanganyika.

..masuala ya supply vs demand ndiyo yanayopaswa kuamua ni jinsi gani Watanganyika wana access na ardhi ya Zanzibar.

..mpaka sasa hivi wa-Zanzibari wengi zaidi wanahamia Tanganyika kuliko kinyume chake.

..katika masuala ya ardhi migration huwa ni kutoka kwenye eneo dogo[Zanzibar] kwenda kwenye eneo kubwa[Tanganyika]. suala lingine linaloathiri migration huwa ni neema na opportunities za kiuchumi.

cc takashi, GHIBUU, gombesugu, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Lazima Tuwe wakweli. Hivi wakija Watu millioni 2 tu kutoka Bara wakataka ardhi kweli tunayo ardhi hiyo. WaZanzibari wapo 1.2 million kuna matatizo ya kugombea ardhi

Hivi kweli kuna Mtanganyika na akili yake timamu anaenda kutafuta ardhi Zanzibari? Mimi kama Mtanganyika si amini, na kama yupo basi atakuwa kichaa. Ardhi yenyewe Zanzibari ipo wapi?
 
Cuf kina wabunge unguja na pemba. Ccm kina wabunge unguja tuhivyo ccm ni chama cha wabara walokuja na mwenge na vibaraka wachache

Na kina wabunge wangapi bara(tanganyika)? Au lengo limeshatimia yakhe?
 
Kwa kuwa suala la ardhi si la muungano basi hata Wazanzibari walioko bara wasiruhusiwe kumiliki ardhi bara. Wapemba waliojazana bara watambue kwamba wao ni wapangaji tu. Wakamiliki ardhi kwao na si bara!
Wanajuwa vizuri kuwa huko si kwao ni shamba la Bibi tu, wajomba wakichacha watarudi kwao!
 
nkongu ndasu
Kwani Mhe. Al Arfi ni Msukuma? Nyoyo zenu zimejaa maradhi ya chuki na Mwenyezi Mungu atawazidisha hayo maradhi yawaangamize.
kahtaan, gombesugu, Ritz
Mkuu Averoes.

Hawa jamaa wanafiki sana jaribu kwenda kwao Kibosho au Rombo ukanunue ardhi kama watakuuzia mimi nilikuwa nataka shamba Kibosho walininyima kwa ubaguzi wao.
 
Last edited by a moderator:
Wazanzibar wanatamani mambo ya zanzibar yawe ya kwao, wakati wanataka ya tanganyika iwe ya wote! Huu muungano ni wa kihuni kwelikweli!

Unahesabu wachache na manufaa yao kuwa ndio Wazanzibari wote?
 
Back
Top Bottom