CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

CUF yapinga bara kupewa ardhi Z’bar

..yaani Maalim Seif amiliki mashamba makubwa makubwa pamoja na majumba huku Tanganyika, lakini Prof.Lipumba hana ruhusu ya kumiliki ardhi Zanzibar hata kiduchu?

Daah! Teeh! Teeh! Teeh!...yaani hapo,"kisu kimegota mfupani"! Umenivunja mbavu!

Traditionally,hakuna Mtanganyika alozuiliwa ati kuwa na ardhi/kumiliki pale takriban Zanzibar yoote. Mie binafsi nawafahamu wenyeji wengi tu wa Mwambao/Pwani hiyo ya Tanganyika ambao wana mahusiano ya centuries nyingi pale Zanzibar na pia wanamiliki ardhi pale,bila ya matata!

Halikadhaklika hata ndugu zetu wa Zanzibar nao pia kwa centuries nyingi mno wakimiliki ardhi huko mabara/Tanganyika katika maeneo mbalimbali!

Lakini kama tutatazama tu kwa jicho la kukhis "ubaguzi" kwenye hiyo sharia ya umiliki wa ardhi pale Zanzibar,itakua hatuwatendei haki ndugu zetu wa Zanzibar!

Kwani leo hii pana Wagogo au Watanganyika wangapi ambao sio Wachaga...wenye kumiliki ardhi pale Marangu au Machame!? Jibu itakua zero au hata kama wapo,basi itakua hawafiki hata chembe ya thuluthi!? Daah!

Sasa hiyo sharia ambayo labda sio ya "kibaguzi" huko Bara/Tanganyika...hapo ndo ina function vipi!? Nafikiri ni muhimu pia wakti mwangine sisi Wananchi pia kutumia ile common sense,busara na hikma tulizojaaliwa!...though I appreciate that common sense can be a bit of grey area!

Pale Unguja...nakumbuka kwenye myka ile kabla ya "zogo" la vyama vingi kungia...palikua na Wabara/Watanganyika wengi tu,ambao tena walikua wala si wazaliwa wa visiwani mle...lakini waliruhusiwa kumiliki ardhi na wakiishi kwa raha mstarehe bila ya kubughudhiwa!

Wengi wao wakti huo walikua kule maeneo ya Dole na Mwakaje...tena walijenga hata Makanisa yao machache...namkumbuka Marehemu Padri Mabura...nafikiri huyu jamaa alikua ni Mnyamwezi!? Alikua ni mstaarabu na wenyeji nao pia walikua wakimpa staha zake!

Nafikiri kama ulivyosema majuzi,yakua pia pana Wanasiasa uchwara na pia labda watu wachache,wenye nia mbaya/potofu na hiyo social cohesion kiduchu iliyopo hapa nchini!?...ambao wanajaribu ku-exploit current political situation na kuzidisha khofu na mihemuko kwenye takriban kila jambo litokealo hivi sasa! Daah!

Lakini hapa hatujagusia asilan,ile history/fact ya kwamba hata hicho kipande cha Mwambao takriban woote/Coastal strip ya East Afrika pia ilikua ni mali ya ile Zanzibar Empire na Wazanzibary!

Hata baada ya huo "Muungano",pia taratibu hata za Serikali hizo mbili kupeana ardhi kwa mikataba makhusus mbona pia ziliendelea!?

Mfano ni lile Shamba/Ranch ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar-SMZ pale Makurunge-Bagamoyo...iliyokua kubwa mno na ya kisasa mno kwa wakti ule! Ambayo hatimae ikafanziwa ufisadi na ubadhilifu mkubwa mno chini ya uongozi wa yule Hassan Nassor Moyo na kundi lake! Daah! Nakhis tuyaache haya,maana hapa si pahala pake!?

Kwa kifupi,inalazim tujue zile sababu na mantik/criteria zilizomo kwenye hii sharia iliyopo hivi sasa kwenye umiliki wa ardhi pale Zanzibar!?

Baada ya hapo ndo tutazame labda validity ya hiyo sharia,au vipi wenzangu!?

Ahsanta.
 
..una maana gani unaposema kuifuta Zanzibar?

..mimi nadhani mnajenga mazingira ya hofu tu.

..kama kungekuwa hakuna sheria inayoruhusu wa-Znz kumiliki ardhi Tgk basi hakuna ambaye angepiga kelele.

..wa-Znz wanaishi kila mahali kama ulivyoeleza ktk post yako. lakini hakuna nchi yoyote ile iliyopokea wa-Zanzibar wengi kama Tanganyika.

..haiwezekani wa-Znz kwa maelfu mhamie huku Tanganyika, wakati huo huo mkisema hamuwataki wa-Tanganyika ktk ardhi yenu.

cc gombesugu

Nimekusoma arguments zako Mkuu!

Ningependa kugusia kiduchu kwenye hiyo point niliyo-BOLD kwenye bayana yako!

Kama mazingira ya khofu yapo au "yanajengwa" kama unavyodai...basi nafikiri hapo ndo ingalikua shughuli ya Wanataaluma wa masuala ya ardhi,Viongozi wa ngazi za juu kitaifa na Wanasiasa wangine...kutufahamisha kwa undani/kitaaluma na kutuondoa khofu hiyo,au vipi!?

Kama tukiendelea tu kuachwa humu njiani/barabarani na kuchekwa,yakua ati tuna "khofu" invalid/"isiyo na mashiko"...sasa,sisi Wananchi/wazanzibary tusojua,ndo tutajuaje!? Si italazim tubaki tu na hii "khofu" yetu ili kuteteta ardhi/haki yetu kwa manufaa ya wanetu/next generations! Daah!

Ahsanta.
 
ya tanzania bara mnawapa wazungu alafu mchukue ya zanzibar ya nini? waachieni ardhi yao
 
umekuwa zombi kiasi hicho, hebu tuoneshe wapi Maalim Seif anamiliki ardhi yenu ya Tanganyika...?
Kisha Wazanzibar hatuna udugu na watu mafedhuli, makatili, watwana wa Mrima, kama ni ndoa tunaishia BagaMoyo mbali tunafika Tanga ama Kondoa hao ndio ndugu zetu sisi...!!

..utwana, ufedhuli, na ukatili, upo katika kauli na matendo ya mhusika.

..tabia hizo hazina mahusiano yoyote yale na asili ya mtu, au siyo monopoly ya watu wa eneo fulani.

..dunia yetu imebadilika sana. hatuko katika zama zile za kusema watu wa eneo fulani hawafai, au watu wa eneo fulani ni bora kuliko wengine.

..Huku Tanganyika tumekaribisha wa-Zanzibari zaidi ya laki 3. Wazanzibari hao wanafanya shughuli zao kama wa-Tanganyika bila kubugudhiwa kwa namna yoyote ile.

cc gombesugu
 
Last edited by a moderator:
..utwana, ufedhuli, na ukatili, upo katika kauli na matendo ya mhusika.

..tabia hizo hazina mahusiano yoyote yale na asili ya mtu, au siyo monopoly ya watu wa eneo fulani.

..dunia yetu imebadilika sana. hatuko katika zama zile za kusema watu wa eneo fulani hawafai, au watu wa eneo fulani ni bora kuliko wengine.

..Huku Tanganyika tumekaribisha wa-Zanzibari zaidi ya laki 3. Wazanzibari hao wanafanya shughuli zao kama wa-Tanganyika bila kubugudhiwa kwa namna yoyote ile.

cc gombesugu

Hata Zanzibar pia Watanganyika wamejaa kila chochoro kwanzia mjini tens stone town mjini wenye sura ya Zanzibar hadi wamejazana wala hawabughudhiwi na mtu, ukienda mashamba utawakuta tena habari hawana, sasa shida ikowapi?
 
Last edited by a moderator:
Naona unachanganya mambo, haki ya kuishi katika inchi ya kigeni na haki ya kumiliki ardhi katika nchi ya kigeni ni vitu viwili tofauti... Maelfu ya wa tngk wanaishi Zanzibar, vile vile maelfu ya wa znz wanaishi tngk...Linapokuja suala la kumiliki ardhi hapo ndio tunatofautiyana.Kwa mfano , Tanzania iwe na uhusiano mzuri na china au India halafu kuwe na makubaliano ya kila raia wa upande mmoja awe na haki ya kumiliki ardhi upande mwengine , sasa hapa nani ataathirika ?
takashi,

..ninachopendekeza mimi ni kwamba wa-Tanganyika waruhusiwe kumiliki ardhi Zanzibar.

..mapendekezo hayo yanatokana na ukweli kwamba wa-Zanzibari wanaruhusiwa kumiliki ardhi huku Tanganyika.

..tuwe na sheria sawa ya kumiliki ardhi. baada ya hapo umiliki wa ardhi utakuwa determined na nguvu za soko[supply & demand].

. gombesugu ametoa mfano wa maeneo ya Marangu na Machame ambako kuna ardhi ndogo. Pamoja na ukweli huo serikali yetu haijapitisha sheria ya kubagua wa-Tanganyika wasio wazawa wa maeneo[marangu,machame] hayo kuhamia huko na kumiliko ardhi huko.

..wa-Tanganyika na wa-Zanzibari wana mahusiano ya kindugu kwa karne kadhaa sasa. Haipendezi mahusiano hayo kuanza kutiwa mushkel ya sheria za kibaguzi kama hii iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

NB:

..Balozi Seif Idi anapigana vikumbo na walalahoi huku Tgk kupata viwanja kule Kigamboni, lakini Prof.Ana Tibaijuka waziri wa ardhi huku Tanganyika hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.

..Dr.Mohamed Seif Khatib ameuziwa nyumba za serikali ya Tanganyika na waziri John Pombe Magufuli. Nyumba zile hazikuwa na uhusiano wowote na muungano, wizara ya ujenzi si ya muungano. Lakini huyu Pombe Magufuli hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.

Foum Jnr
, W. J. Malecela, Chris Lukosi, Kibunango, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Hata Zanzibar pia Watanganyika wamejaa kila chochoro kwanzia mjini tens stone town mjini wenye sura ya Zanzibar hadi wamejazana wala hawabughudhiwi na mtu, ukienda mashamba utawakuta tena habari hawana, sasa shida ikowapi?

..shida iko kwenye sheria iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

..sheria hiyo haikuzingatia mahusiano ya kindugu baina ya wa-Tanganyika na wa-Zanzibari.

..sheria hiyo inawabagua wa-Tanganyika kwa kuwazuia kumiliki ardhi Zanzibar.
 
..shida iko kwenye sheria iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

..sheria hiyo haikuzingatia mahusiano ya kindugu baina ya wa-Tanganyika na wa-Zanzibari.

..sheria hiyo inawabagua wa-Tanganyika kwa kuwazuia kumiliki ardhi Zanzibar.

Tatizo lenu Watanganyika hamutaki kuelewa na hii yote nadhani mnajiona kama kwamba Zanzibar ni mali yenu, ila bado tunasema ARDHI sio suala la Muungano, hivyo Zanzibar inapaswa kusimamia ardhi yake, kwa upande wa Tanganyika kwa vile mumeizika hivyo mumehalalisha kila kitu kiwe cha Muungano, hilo kwetu halituhusu ni jukumu lenu kuirejesha Tanganyika yenu iwasimamie mambo yasiyo ya Muungano kwa upande wenu, ila mukilalama kuhusu hili mutatuanya tuelewe kwamba dhamira yenu ilee ya kuimeza Zanzibar, hebu twendeni kwa misingi ya sheria tusihemkwe kwa utashi wetu,
 
Tatizo lenu Watanganyika hamutaki kuelewa na hii yote nadhani mnajiona kama kwamba Zanzibar ni mali yenu, ila bado tunasema ARDHI sio suala la Muungano, hivyo Zanzibar inapaswa kusimamia ardhi yake, kwa upande wa Tanganyika kwa vile mumeizika hivyo mumehalalisha kila kitu kiwe cha Muungano, hilo kwetu halituhusu ni jukumu lenu kuirejesha Tanganyika yenu iwasimamie mambo yasiyo ya Muungano kwa upande wenu, ila mukilalama kuhusu hili mutatuanya tuelewe kwamba dhamira yenu ilee ya kuimeza Zanzibar, hebu twendeni kwa misingi ya sheria tusihemkwe kwa utashi wetu,

..ndugu yangu, usitetee ubaguzi kwa kisingizio kwamba Tanganyika haipo.

..hata serikali ya Tanganyika ikirejeshwe sitarajii, na sitaunga mkono, kupitishwa kwa sheria yoyote ile ya kuwabagua wa-Zanzibari.

..kuhusu Zanzibar "kumezwa" huko nako ni kuwatia hofu wananchi.
 
unajua wabara tutumie akili wakati mwingine,hiko ki Zanzibar ni kama mkoa m1 tu hapa kwetu then sis huku bara tuko 42milioni kama tukitaka usawa wa ardhi tutakua na akili kweli hapo? wenyewe kwnza wana kieneo kidogo(2,650 km²) yetu (945,203 km²) check ratio ss hapo?
 
result of abuse of authority , the authority may use his power and misused his position . this is true for all forms of power , whether political , moral , economic , and military. we can go back and see a clear abuse potential as a dictatorship of the person or group, ideology to incorporate elements of a particular group of people to violate the law and commit evil aggression against the rest in other people . and this is done by the group if they do not , groups with military force . conditions and influences to feel great and you will not love you justify things because of the title, take and use power would be capable of understanding the issues involved in governing this or take advantage of someone forcing things by force , to feel the pride of power, to be a genius to feel that I am older, legalize everything legal is to follow the law in every thing whatever that the law will exercise a right or not , POWERS THAT NOT CAPABLE Qualified , they would like pride to hide his weakness and when they can not provide the service expected by communities they manage is . when a person in power has been on a sense of leading like a dictator for a man of violence and forcing things instead of using force to move the focus to advise and influence people , the man is shown arrogance and anger and to do so he hid his manner great feel and lack of security. Such a person sees himself becomes a god and feel he is above all others , to seek personal benefit from the power , through exploitation, or self, that is doing the corruption of power.
 
takashi,

..ninachopendekeza mimi ni kwamba wa-Tanganyika waruhusiwe kumiliki ardhi Zanzibar.

..mapendekezo hayo yanatokana na ukweli kwamba wa-Zanzibari wanaruhusiwa kumiliki ardhi huku Tanganyika.

..tuwe na sheria sawa ya kumiliki ardhi. baada ya hapo umiliki wa ardhi utakuwa determined na nguvu za soko[supply & demand].

. gombesugu ametoa mfano wa maeneo ya Marangu na Machame ambako kuna ardhi ndogo. Pamoja na ukweli huo serikali yetu haijapitisha sheria ya kubagua wa-Tanganyika wasio wazawa wa maeneo[marangu,machame] hayo kuhamia huko na kumiliko ardhi huko.

..wa-Tanganyika na wa-Zanzibari wana mahusiano ya kindugu kwa karne kadhaa sasa. Haipendezi mahusiano hayo kuanza kutiwa mushkel ya sheria za kibaguzi kama hii iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

NB:

..Balozi Seif Idi anapigana vikumbo na walalahoi huku Tgk kupata viwanja kule Kigamboni, lakini Prof.Ana Tibaijuka waziri wa ardhi huku Tanganyika hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.

..Dr.Mohamed Seif Khatib ameuziwa nyumba za serikali ya Tanganyika na waziri John Pombe Magufuli. Nyumba zile hazikuwa na uhusiano wowote na muungano, wizara ya ujenzi si ya muungano. Lakini huyu Pombe Magufuli hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.

Foum Jnr
, W. J. Malecela, Chris Lukosi, Kibunango, Nguruvi3
Mkuu, mimi kwa kifupi nauchukia huu muungano na huwa nasema wazi siku zote bila kuficha

Zanzibar ni kupe asie na shukurani
 
Kwa kuwa suala la ardhi si la muungano basi hata Wazanzibari walioko bara wasiruhusiwe kumiliki ardhi bara. Wapemba waliojazana bara watambue kwamba wao ni wapangaji tu. Wakamiliki ardhi kwao na si bara!

Sio tu mnalalama na kunung'unika WEKENI KATIKA KATIBA YENU KAMA WALIVYOFANYA ZNZ.
Mnakhofia nini? au ndo unafiki wenyewe huo?

 
..shida iko kwenye sheria iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

..sheria hiyo haikuzingatia mahusiano ya kindugu baina ya wa-Tanganyika na wa-Zanzibari.

..sheria hiyo inawabagua wa-Tanganyika kwa kuwazuia kumiliki ardhi Zanzibar.

Joka kuu

Huwezi pata Znz huru bila kumiliki ardhwi.

Znz wameanza na nyie kama MNA UTHUBUTU INABIDI MFUATE.

WAACHWE ZNZ WAPUMUE



 
..ndugu yangu, usitetee ubaguzi kwa kisingizio kwamba Tanganyika haipo.

..hata serikali ya Tanganyika ikirejeshwe sitarajii, na sitaunga mkono, kupitishwa kwa sheria yoyote ile ya kuwabagua wa-Zanzibari.

..kuhusu Zanzibar "kumezwa" huko nako ni kuwatia hofu wananchi.

sijui dhana ya ubaguzi kwako unaidefine vipi, ila mi nadhani Mzanzibar kulinda na kutetea haki zake za msingi huo ni ubaguzi kwa Mtanganyika! anyway; bado hujajibu na nakuhisi hautanijibu hoja yangu, unalotaka wewe eti Muungano huu uendeshwe kiurafiki bila ya kuzingatia misingi ya sheria kwa mambo ya Muungano tuliyojiwekea, hilo lilifanyika huko nyuma tukaona athari zake kwa upande wa Zanzibar hatimae tulianza na mambo 11 sasa yapo 21 kwa huo urafiki na umazoea, ila kwa sasa Nooo!!! lazima tuzingatie mambo ya msingi ya Muungano, ambayo hayaoneshi kwamba Ardhi ni mali ya Muungano..!! tuache kuendesha Muungano kimazoea!!!
 
takashi,

..ninachopendekeza mimi ni kwamba wa-Tanganyika waruhusiwe kumiliki ardhi Zanzibar.

..mapendekezo hayo yanatokana na ukweli kwamba wa-Zanzibari wanaruhusiwa kumiliki ardhi huku Tanganyika.

..tuwe na sheria sawa ya kumiliki ardhi. baada ya hapo umiliki wa ardhi utakuwa determined na nguvu za soko[supply & demand].

. gombesugu ametoa mfano wa maeneo ya Marangu na Machame ambako kuna ardhi ndogo. Pamoja na ukweli huo serikali yetu haijapitisha sheria ya kubagua wa-Tanganyika wasio wazawa wa maeneo[marangu,machame] hayo kuhamia huko na kumiliko ardhi huko.

..wa-Tanganyika na wa-Zanzibari wana mahusiano ya kindugu kwa karne kadhaa sasa. Haipendezi mahusiano hayo kuanza kutiwa mushkel ya sheria za kibaguzi kama hii iliyopitishwa na baraza la wawakilishi.

NB:

..Balozi Seif Idi anapigana vikumbo na walalahoi huku Tgk kupata viwanja kule Kigamboni, lakini Prof.Ana Tibaijuka waziri wa ardhi huku Tanganyika hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.

..Dr.Mohamed Seif Khatib ameuziwa nyumba za serikali ya Tanganyika na waziri John Pombe Magufuli. Nyumba zile hazikuwa na uhusiano wowote na muungano, wizara ya ujenzi si ya muungano. Lakini huyu Pombe Magufuli hana haki ya kumiliki ardhi Zanzibar.

Foum Jnr
, W. J. Malecela, Chris Lukosi, Kibunango, Nguruvi3
Kutokana na uhaba wa ardhi Kilimanjaro, wakazi wa huko wanahamia maeneo ya mikoa mingine kama Handeni, Korogwe, Arusha, kiteto, Mkuranga.

Huko wanapewa ardhi bila matatizo. Na hakuna mwananchi kutoka mkoa mwingine aliyenyimwa ardhi Kilimanajaro. Ukienda Wilaya ya Same kule gonja utawakuta akina Chacha wanamiliki ardhi. Ukienda Rombo Hai utawakuta akina Molel, akina Mhina wanamiiliki ardhi n.k. Ukitaka kununua nyumba Moshi ni kisu chako tu, hakuna sheria inakuzuia

Hawa wznz wanasema hilo si jambo la muungano. Vipi mbona elimu ya juu n.k. si mambo yua muungano lakini bado wanataka wapewe tena wakidai utadhani ni haki yao. Wanadai hela za elimu ya juu licha ya kupewa nafasi 1000 bila mkopo na kwa upendeleo.

Mimi nadhani wenye matatizo hapa ni Tanganyika, kama ingelikuwepo msumeno ungekata mbele na nyuma.
Sheria za znz zinatumika Tanganyika. Hakuna sababu ya kupigizana kelele ni kuweka sheria tu za kuwabana mambo yanaisha. Sasa hivi hakuna Tanganyika wanakuja na mgongo wa Tanzania.
 
Kutokana na uhaba wa ardhi Kilimanjaro, wakazi wa huko wanahamia maeneo ya mikoa mingine kama Handeni, Korogwe, Arusha, kiteto, Mkuranga.

Huko wanapewa ardhi bila matatizo. Na hakuna mwananchi kutoka mkoa mwingine aliyenyimwa ardhi Kilimanajaro. Ukienda Wilaya ya Same kule gonja utawakuta akina Chacha wanamiliki ardhi. Ukienda Rombo Hai utawakuta akina Molel, akina Mhina wanamiiliki ardhi n.k. Ukitaka kununua nyumba Moshi ni kisu chako tu, hakuna sheria inakuzuia

Hawa wznz wanasema hilo si jambo la muungano. Vipi mbona elimu ya juu n.k. si mambo yua muungano lakini bado wanataka wapewe tena wakidai utadhani ni haki yao. Wanadai hela za elimu ya juu licha ya kupewa nafasi 1000 bila mkopo na kwa upendeleo.

Mimi nadhani wenye matatizo hapa ni Tanganyika, kama ingelikuwepo msumeno ungekata mbele na nyuma.
Sheria za znz zinatumika Tanganyika. Hakuna sababu ya kupigizana kelele ni kuweka sheria tu za kuwabana mambo yanaisha. Sasa hivi hakuna Tanganyika wanakuja na mgongo wa Tanzania.

Unatetea Muungano hadi unachoka ki-akili,
Nani alosema Elimu ya Juu sio suala la Muungano..? kama hujui uliza kwanza usikurupuke....!!!
 
Back
Top Bottom