naibu katibu mkuu wa cuf,julius mtatiro amezungumzia mikakati ya chama chake kurejesha heshima yake,
Akizungumzia mikakati ya CUF katika kujijenga na kurejesha heshima yake ya kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania bara, Mtatiro anasema Heshima ya CUF iko palepale. Haijakwisha wala haiwezi kumalizwa na CCM wala Chadema.
Sisi bado ni chama cha upinzani chenye nguvu na ndio maana unaona sasa tuna maadui wengi zaidi
Anaongeza zamani tulikuwa tuna mpinzani mmoja tu yaani CCM, sasa wameongezeka Chadema naye ni mpinzani wetu na ndio maana kila mara utasikia akitushambulia kwa kauli zisizo na maana, hii ni kutokana na hofu waliyo nayo juu ya CUF ambacho ndicho chama makini na chenye wafuasi wa kuaminika anasema
Anasema mashambulizi yanayofanywa na Chadema dhidi ya CUF ni ishara kuwa ndicho chama kinachowanyima usingizi na kutamba kuwa hiyo inatokana na uimara wake na mafanikio kilicho nacho katika siasa nchini.
Mtatiro anasema CCM na Chadema vimekuwa vikieneza propaganda zenye nia ya kukichafua chama hicho kutokana na kukihofia na kujigamba kuwa hata hivyo juhudi hizo haziwezi kufanikiwa kwa kuwa wananchi wanajua mbivu na mbichi na kamwe hawawezi kudanganyika.
Anasema watanzania ni wenye kuelewa na kuwa wamevishtukia vyama hivyo vinavyotafuta umaarufu kwa kukichafua CUF na kusema uchaguzi mkuu ujao ndio utakaomaliza ubishi wa kipi kati ya chama chao na vyama hivyo kinafanya siasa safi na zenye kukubalika na Watanzania.
Akizungumzia mikakati ya CUF katika kujijenga na kurejesha heshima yake ya kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania bara, Mtatiro anasema Heshima ya CUF iko palepale. Haijakwisha wala haiwezi kumalizwa na CCM wala Chadema.
Sisi bado ni chama cha upinzani chenye nguvu na ndio maana unaona sasa tuna maadui wengi zaidi
Anaongeza zamani tulikuwa tuna mpinzani mmoja tu yaani CCM, sasa wameongezeka Chadema naye ni mpinzani wetu na ndio maana kila mara utasikia akitushambulia kwa kauli zisizo na maana, hii ni kutokana na hofu waliyo nayo juu ya CUF ambacho ndicho chama makini na chenye wafuasi wa kuaminika anasema
Anasema mashambulizi yanayofanywa na Chadema dhidi ya CUF ni ishara kuwa ndicho chama kinachowanyima usingizi na kutamba kuwa hiyo inatokana na uimara wake na mafanikio kilicho nacho katika siasa nchini.
Mtatiro anasema CCM na Chadema vimekuwa vikieneza propaganda zenye nia ya kukichafua chama hicho kutokana na kukihofia na kujigamba kuwa hata hivyo juhudi hizo haziwezi kufanikiwa kwa kuwa wananchi wanajua mbivu na mbichi na kamwe hawawezi kudanganyika.
Anasema watanzania ni wenye kuelewa na kuwa wamevishtukia vyama hivyo vinavyotafuta umaarufu kwa kukichafua CUF na kusema uchaguzi mkuu ujao ndio utakaomaliza ubishi wa kipi kati ya chama chao na vyama hivyo kinafanya siasa safi na zenye kukubalika na Watanzania.