popiexo
JF-Expert Member
- Oct 26, 2010
- 742
- 184
Mbowe alishaweka wazi kuwa CDM iko tayari kufanya kazi na chama makini but they are not bounded, kama CUF & co. wametubu na wamevunja kambi yao then they are welcome lakini wasije kwa nia ya kupata vyeo.
Source: Mtanzania 24/01/2011 UK. 2
Diwani awapiga kijembe waislamu
Diwani wa viti maalum, kata ya Kariakoojijini Dar, Aisha Sururu (CCM), amedai maendeleo duni waliyonayo Waislamu nchini yanasababishwa na uvivu wa kufikiria wa viongozi wa dini hiyo.
Suruna ambaye pia ni muislamu alikiri kuwa, jamii kubwa ya kiislamu ipo nyuma katika maendeleo ikilinganishwa na jamii ya dini nyingine, hali ambayo alidai inachangiwa na viongozi wa dini hiyo kukosa dira na mipango ya maendeleo.
Aliyasema hayo Dar muda mfupi kabla ya kugawa vyeti kwa waitimu wa kozi maalum ya wanawake wa kiislamu...
Mafunzo hayo ya wiki nane, yalihusisha wanawake 41, ambao walijifunza maarifa ya dini ya kiislamu, ikiwa pamoja na somo la Qur-an, elimu ya wanawake, tabia njema (akhlaq), maziko na jinsi ya kusitiri maiti.
Katika mazungumzo yake, Sururu aliwataja Masheick, maimamu na wanazuoni wa kiislmu chini ya BAKWATA, kwamba wote kwa ujumla wamebweteka na hawana mipango yoyote ya maendeleo dhidi ya jamii hiyo.....
Maelezo zaidi soma gazeti