CUF iko juu ya sheria Tanzania?

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Katika hali ya kushangaza V4C iliyozinduliwa na CUF imejulikana lengo lake kubwa ni kufanya kampeni za Urais kwa ajili ya mgombea wa kudumu wa chama hicho Prof Ibrahim Lipumba.
Katika mkutano uliofanyika jangwani wapambe karibu wote walikuwa wanamuombea kura Lipumba za mwaka 2015.Hayo hayo yamejirudia kwenye mkutano wao waliofanya kule Arusha.
Tunapenda kuiuliza tume ya uchaguzi ni lini imetangaza nafasi ya Urais iko wazi? Je hiki ni kipindi rasmi cha uchaguzi?
Je ingekuwa CDM ndiyo inazunguka mikoani na kumuombea kura Dr Slaa au Freeman Mbowe serikali ingekaa kimya? Si ingetangazwa wanachofanya CDM ni uhaini?
Tunamuuliza Msajili wa vyama vya siasa hili ni sawa? Au kwa vile linafanywa na mshirika wa CCM sio kosa?
Ikumbukwe msajili huyu huyu alisema hataki kuona M4C ya CDM kwa madai isubiri kipindi cha uchaguzi ufike.Lakini kwake ni sawa Lipumba akiombewa kura sasa za urais wa 2015.

Source:Tanzania daima Jumapili Makala.
 
Mkuu sijakuelewa, CUF kusema Lipumba kuwania Urais 2015 ni kosa? Kifungu gani cha sheria kimevunjwa? Kama kuna kifungu cha sheria kinachokataza mtu kutangaza nia ya kuwania Urais, basi kifungu hicho ni kandamizi na lazima kiondolewe katika katiba mpya.
Naunga mkono kwa wenye nia ya kugombea Urais 2015 wajitokeze, tuanze kuwafuatilia na kujua misimamo yao.
 
Cuf hawawezi kuzuiwa maana wanajua hawana madhara kwa ccm,naamini hata wakitaka kuandamana sio lazima waombe kibali na polisi hawawezi kuwafanya chochote.
 
Molemo, tambua kuwa wanachokifanya cuf kwa kumwombea kura lipumba ni maelekezo ya serikali ya ccm. wanafanya hivyo wakijua lipumba hawezi kuwa rais wa nchi hii, bali hofu yao kubwa ipo kwa chadema.
wamechanganyikiwa kutokana na M4C, wanadhani wanachokifanya kinaweza kuwasaidia
 
Last edited by a moderator:
Mkuu sijakuelewa, CUF kusema Lipumba kuwania Urais 2015 ni kosa? Kifungu gani cha sheria kimevunjwa? Kama kuna kifungu cha sheria kinachokataza mtu kutangaza nia ya kuwania Urais, basi kifungu hicho ni kandamizi na lazima kiondolewe katika katiba mpya.
Naunga mkono kwa wenye nia ya kugombea Urais 2015 wajitokeze, tuanze kuwafuatilia na kujua misimamo yao.

Tofautisha kati ya mtu kujitangaza na chama cha siasa kutembea na mwanachama wake mikoani na kufanya mikutano ya hadhara na kumuombea kura za urais 2015.
Najua wewe ni CUF lakini nikuulize ni Lini ilipitisha jina la mgombea urais wa uchaguzi mkuu ujao?
Swali la 2-Kwanini msajili wa vyama vya siasa Tendwa aliropoka kwamba hakubali M4C ya CDM kwa madai inapiga kampeni za uchaguzi wakati si kweli na haina mgombea inayemnadi mikutanoni kama CUF inavyomnadi kwa wananchi na kumuombea kura?
 
Nilini CUF walikaa kikao na kumptisha Profesa kuwa mgombea Urais? CUF wanacho fantasy ni kampeni za kumnadi Profesa, so wao kwao wamisha maliza swala la nani awe mgombea wait. HAKI SAWA KWA PROFESA NA MALIM SEIFU SHALIFU HAMAD
 
Cuf hawawezi kuzuiwa maana wanajua hawana madhara kwa ccm,naamini hata wakitaka kuandamana sio lazima waombe kibali na polisi hawawezi kuwafanya chochote.

Point noted and taken.
 
Molemo, tambua kuwa wanachokifanya cuf kwa kumwombea kura lipumba ni maelekezo ya serikali ya ccm. wanafanya hivyo wakijua lipumba hawezi kuwa rais wa nchi hii, bali hofu yao kubwa ipo kwa chadema.
wamechanganyikiwa kutokana na M4C, wanadhani wanachokifanya kinaweza kuwasaidia

Ni kweli mkuu Mungi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu sijakuelewa, CUF kusema Lipumba kuwania Urais 2015 ni kosa? Kifungu gani cha sheria kimevunjwa? Kama kuna kifungu cha sheria kinachokataza mtu kutangaza nia ya kuwania Urais, basi kifungu hicho ni kandamizi na lazima kiondolewe katika katiba mpya.
Naunga mkono kwa wenye nia ya kugombea Urais 2015 wajitokeze, tuanze kuwafuatilia na kujua misimamo yao.

Mkuu kampeni za urais haijatangazwa bado. Ingelikuwa ni chadema wanafanya hivyo ungemsikia msajili wa vyama vya siasa kada wa ccm John Tendwa akiropoka kutishia kukifuta usajili.
Wenye mamlaka ya kutangaza kuanza kwa kampeni ni tume ya uchaguzi, si mwingi awaye yote.
 
Nilini CUF walikaa kikao na kumptisha Profesa kuwa mgombea Urais? CUF wanacho fantasy ni kampeni za kumnadi Profesa, so wao kwao wamisha maliza swala la nani awe mgombea wait. HAKI SAWA KWA PROFESA NA MALIM SEIFU SHALIFU HAMAD

Mkuu wangu hata mimi nashangaa.Nilihudhuria ule mkutani wao wa Jangwani.Utadhani bado miezi miwili uchaguzi mkuu ufanyike kwani karibu kila kiongozi alivaa Tshirt yenye sura ya Lipumba na vibwagizo ilikuwa Chagua Lipumba Urais Tanzania.
 
CUF ni chama cha dini ya Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Zanzibar na Makamu wake wote wawili, IGP, Judge Mkuu, Judge Kiongozi na Mkuu wa Uhasama wa Taifa.
Nani atanyanyua mdomo wake kukikemea?
 
Mkuu kampeni za urais haijatangazwa bado. Ingelikuwa ni chadema wanafanya hivyo ungemsikia msajili wa vyama vya siasa kada wa ccm John Tendwa akiropoka kutishia kukifuta usajili.
Wenye mamlaka ya kutangaza kuanza kwa kampeni ni tume ya uchaguzi, si mwingi awaye yote.

Mkuu wangu wanachokifanya CUF ni aibu kubwa na ubakaji mkubwa wa Demokrasia.Ni kikao gani kilimpitisha Lipumba kuwa mgombea Urais? Au ndiyo usultani wenyewe?
 
Tatizo la taifa letu ni kufanya mambo kiubaguzi, haiwezekani sheria moja ikatafsiriwa tofautitofauti. Pili kwa cuf inaonekana tayari mgombea wao ni lipumba na maalim seif, kama kawa demokrasia ndani ya cuf ni msamiati!
 
Mkuu wangu wanachokifanya CUF ni aibu kubwa na ubakaji mkubwa wa Demokrasia.Ni kikao gani kilimpitisha Lipumba kuwa mgombea Urais? Au ndiyo usultani wenyewe?

CUF wamejaribu kuiga M4C, lakini walichochemka ni kumwombea kura Lipumba. ninapata mashaka na uprofesa wa Lipumba, ama anajua wanaomwombea kura ni chakula cha wasomi (wajinga).

Kuna watu wenye nia mbaya wameanza kueneza mtindo huo wa kumwombea kura lipumba mpaka misikitini inasikitisha sana. hawana nia njema na cuf.
 
Back
Top Bottom