JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Staa wa Manchester United, Cristiano Ronaldo ametangaza kufiwa na mtoto wake wa kiume jioni ya leo Jumatatu Aprili 18, 2022.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ronaldo amesema mtoto huyo wa kiume bila kufafanua ni yupi amefariki licha ya juhudi kubwa za madaktari katika kuokoa uhai wake.
Ikumbukwe hivi miezi ya hivi karibuni ilitangazwa kuwa mpenzi wa Mreno huyo, Georgina Rodriguez alikuwa mjamzito wa watoto pacha.
Hili ndilo andiko la Ronaldo na mpenzi wake Georgina Rodriguez :
“Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kuwa mtoto wetu wa kiume amefariki dunia, ni maumivu makali ambayo mzazi yeyote anaweza kuyapata.
“Kuzaliwa kwa mtoto wetu wa kike ni Faraja kwetu kuendelea kuwa na furaha.
“Tunawashukuru madaktari na wauguzi wote kwa juhudi zao walizozifanya.
“Sote tuna huzuni kwa kumpoteza mpendwa wetu, kwa pamoja tunaomba suala hili libaki kuwa la familia wakati huu mgumu.
‘Mwanetu wa kiume, wewe ni Malaika, tutaendelea kukupenda.”
Source: Ronaldo page
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ronaldo amesema mtoto huyo wa kiume bila kufafanua ni yupi amefariki licha ya juhudi kubwa za madaktari katika kuokoa uhai wake.
Ikumbukwe hivi miezi ya hivi karibuni ilitangazwa kuwa mpenzi wa Mreno huyo, Georgina Rodriguez alikuwa mjamzito wa watoto pacha.
Hili ndilo andiko la Ronaldo na mpenzi wake Georgina Rodriguez :
“Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kuwa mtoto wetu wa kiume amefariki dunia, ni maumivu makali ambayo mzazi yeyote anaweza kuyapata.
“Kuzaliwa kwa mtoto wetu wa kike ni Faraja kwetu kuendelea kuwa na furaha.
“Tunawashukuru madaktari na wauguzi wote kwa juhudi zao walizozifanya.
“Sote tuna huzuni kwa kumpoteza mpendwa wetu, kwa pamoja tunaomba suala hili libaki kuwa la familia wakati huu mgumu.
‘Mwanetu wa kiume, wewe ni Malaika, tutaendelea kukupenda.”
Source: Ronaldo page
Tamko la Ronaldo kuhusu msiba.
Ronaldo akiwa na familia yake, mpenzi wake alivyokuwa na ujauzito wa watoto pacha.