Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,884
#COVID-19: TUWAJIBISHANE
Mnamo Tarehe 28/3/2020 niliwaeleza Watanzania kuwa nimemwandikia barua Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumshauri mambo makubwa 8 ili nchi yetu iweze kukabili maambukizi ya virusi vya Korona. Tarehe 4/4/2020 Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa Maalim Seif Sharif Hamad alizungumza na Wananchi kuwataka kujihadhari na virusi vya Korona. Hadi siku Mwenyekiti anazungumza Tanzania ilikuwa na wagonjwa 20 tu. Leo Tanzania ina wagonjwa 257 na Serikali imeripoti vifo vya watu 10. Kati ya Aprili 1 na Aprili 20, maambukizi yaliyotangazwa yamefikia 1,170%.
Kama Viongozi wa Upinzani nchini kwa wiki kadhaa sasa tumekuwa tunatoa ushauri kwa Viongozi wa Serikali na kuelimisha umma kudhibiti #COVID19TZA. Tumejitahidi kuunganisha Nchi yetu dhidi ya Virusi hivi. Sasa umefika wakati wa KUWAJIBISHANA.
Wakati Nchi ikiwa katika maambukizi mtu mwenye Mamlaka ya Juu kabisa katika Nchi yetu, Rais John Pombe Joseph Magufuli haonekani kuendesha mapambano kama tunavyoona kwa mataifa jirani kama Kenya, Rwanda, Uganda, Afrika Kusini nk. Mara chache ambazo Rais amejitokeza ametoa kauli zinazoonyesha kuwa COVID 19 sio tatizo na hivyo kushawishi watu kuendelea na shughuli za mikusanyiko ambazo zinakuza maambukizi. Pia tumeona Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na baadhi ya watu wa karibu na Rais wakihamasisha mikusanyiko ya watu.
Mwalimu Julius Nyerere alitafsiri Kitabu cha Shakespeare Merchants of Venice (Mabepari wa Venice). Kundi hili la Viongozi walioendelea kushawishi Watanzania kuendelea na shughuli za mikusanyiko, Mwalimu Nyerere angewaita Mabepari wa Vifo (Merchants of Deaths). #MerchantsOfDeaths ni watu ambao wakielekezwa kutofanya matendo fulani ili kuepuka maafa wao hufanya. Pia watu wenye Mamlaka ambao wanashindwa kutumia mamlaka yao kuzuia maafa. Vile vile watu wa imani ambao wanaaminisha waumini wao mambo ambayo husababisha maafa. Wanashtakika
Kutokana na maandalizi mabovu ya Serikali kwa Watumishi wa Afya - Madaktari, Manesi, Watumishi wa Maabara - maambukizi yamesambaa miongoni mwao na hata wengine kuanza kupoteza maisha. Licha ya Serikali kukusanya mabilioni ya Fedha kutoka Sekta Binafsi na yenyewe kutotenga Bajeti Maalumu ya kupambana na Korona, watumishi walio mstari wa mbele kwenye vita wanaachwa bila vifaa (PPE). Nchi yetu ipo kwenye hatari ya kupoteza wataalamu wengi wa Afya ambao wamesomeshwa kwa gharama kubwa na kwa muda mrefu. Watumishi hawa pia wanahatarisha familia zao.
Namna Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyokabili mlipuko wa Korona inathibitisha kauli kuwa Tanzania imekuwa na miaka 5 ya uholela, yaani 5 Years Of Incompetence. Mgawanyo wa Kazi wakati huu umekuwa;
- Naibu Waziri Afya: kuelimisha Umma maana ya Corona na kuvaa Barakoa
- Waziri wa Afya: Kutangaza Idadi ya visa vya Corona na vifo na kuelezea maamuzi mbalimbali ya Serikali
- Waziri Mkuu: Kukusanya michango ya Wadau (Serikali yenyewe haijaweka wazi Bajeti yake ya Corona
- Makamu wa Rais: Hajulikani alipo
- Rais: Kajificha Kijijini Chato huku akitaka Wananchi waendelee kwenda Kanisani na Misikitini
Hatuwezi kuendelea namna hii huku wagonjwa wanaongezeka, Watanzania wanapoteza maisha, huduma za Afya zinazidiwa na kupoteza wataalamu muhimu na uchumi unaanguka. Itabidi kuendelea kupambana na Korona huku tunawajibishana.
Namtaka Rais Magufuli afanye yafuatayo
1. Amwagize Waziri wa Fedha kupeleka Bungeni Bajeti ya Dharura kukabiliana na Korona na baada ya Bajeti hiyo Bunge lisimamishe vikao vyake mpaka Korona itakapokomeshwa nchini. Bajeti hiyo ihakikishe Wataalamu wetu wa Afya wanapata vifaa vya kuwalinda ili kupambana na Korona
2. Ahutubie Taifa mara moja na kuwataka Wananchi kuacha shughuli zao za kila siku na kwa kutumia Sheria ya Bunge kuifunga Nchi (partial lockdown). Wananchi wasaidiwe kwa mujibu wa mapendekezo tuliyoyatoa, kila kaya ipatiwe shs 300,000
3. Kama hawezi kuyafanya haya ajiondoe madarakani ili watanzania wengine wafanye hiyo kazi ya kulinda Nchi yetu.
Mwisho nawaomba Wanasheria nchini kuandaa mashtaka ya kukusudia kuua dhidi ya watu wote ambao wametoa matamko ambayo yaliwafanya wananchi waendelee na shughuli za kuambukiza virusi vya Korona.
Imetolewa na:
Zitto Kabwe
Kiongozi wa ACT Wazalendo
21 Aprili, 2020
Mnamo Tarehe 28/3/2020 niliwaeleza Watanzania kuwa nimemwandikia barua Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumshauri mambo makubwa 8 ili nchi yetu iweze kukabili maambukizi ya virusi vya Korona. Tarehe 4/4/2020 Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa Maalim Seif Sharif Hamad alizungumza na Wananchi kuwataka kujihadhari na virusi vya Korona. Hadi siku Mwenyekiti anazungumza Tanzania ilikuwa na wagonjwa 20 tu. Leo Tanzania ina wagonjwa 257 na Serikali imeripoti vifo vya watu 10. Kati ya Aprili 1 na Aprili 20, maambukizi yaliyotangazwa yamefikia 1,170%.
Kama Viongozi wa Upinzani nchini kwa wiki kadhaa sasa tumekuwa tunatoa ushauri kwa Viongozi wa Serikali na kuelimisha umma kudhibiti #COVID19TZA. Tumejitahidi kuunganisha Nchi yetu dhidi ya Virusi hivi. Sasa umefika wakati wa KUWAJIBISHANA.
Wakati Nchi ikiwa katika maambukizi mtu mwenye Mamlaka ya Juu kabisa katika Nchi yetu, Rais John Pombe Joseph Magufuli haonekani kuendesha mapambano kama tunavyoona kwa mataifa jirani kama Kenya, Rwanda, Uganda, Afrika Kusini nk. Mara chache ambazo Rais amejitokeza ametoa kauli zinazoonyesha kuwa COVID 19 sio tatizo na hivyo kushawishi watu kuendelea na shughuli za mikusanyiko ambazo zinakuza maambukizi. Pia tumeona Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na baadhi ya watu wa karibu na Rais wakihamasisha mikusanyiko ya watu.
Mwalimu Julius Nyerere alitafsiri Kitabu cha Shakespeare Merchants of Venice (Mabepari wa Venice). Kundi hili la Viongozi walioendelea kushawishi Watanzania kuendelea na shughuli za mikusanyiko, Mwalimu Nyerere angewaita Mabepari wa Vifo (Merchants of Deaths). #MerchantsOfDeaths ni watu ambao wakielekezwa kutofanya matendo fulani ili kuepuka maafa wao hufanya. Pia watu wenye Mamlaka ambao wanashindwa kutumia mamlaka yao kuzuia maafa. Vile vile watu wa imani ambao wanaaminisha waumini wao mambo ambayo husababisha maafa. Wanashtakika
Kutokana na maandalizi mabovu ya Serikali kwa Watumishi wa Afya - Madaktari, Manesi, Watumishi wa Maabara - maambukizi yamesambaa miongoni mwao na hata wengine kuanza kupoteza maisha. Licha ya Serikali kukusanya mabilioni ya Fedha kutoka Sekta Binafsi na yenyewe kutotenga Bajeti Maalumu ya kupambana na Korona, watumishi walio mstari wa mbele kwenye vita wanaachwa bila vifaa (PPE). Nchi yetu ipo kwenye hatari ya kupoteza wataalamu wengi wa Afya ambao wamesomeshwa kwa gharama kubwa na kwa muda mrefu. Watumishi hawa pia wanahatarisha familia zao.
Namna Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyokabili mlipuko wa Korona inathibitisha kauli kuwa Tanzania imekuwa na miaka 5 ya uholela, yaani 5 Years Of Incompetence. Mgawanyo wa Kazi wakati huu umekuwa;
- Naibu Waziri Afya: kuelimisha Umma maana ya Corona na kuvaa Barakoa
- Waziri wa Afya: Kutangaza Idadi ya visa vya Corona na vifo na kuelezea maamuzi mbalimbali ya Serikali
- Waziri Mkuu: Kukusanya michango ya Wadau (Serikali yenyewe haijaweka wazi Bajeti yake ya Corona
- Makamu wa Rais: Hajulikani alipo
- Rais: Kajificha Kijijini Chato huku akitaka Wananchi waendelee kwenda Kanisani na Misikitini
Hatuwezi kuendelea namna hii huku wagonjwa wanaongezeka, Watanzania wanapoteza maisha, huduma za Afya zinazidiwa na kupoteza wataalamu muhimu na uchumi unaanguka. Itabidi kuendelea kupambana na Korona huku tunawajibishana.
Namtaka Rais Magufuli afanye yafuatayo
1. Amwagize Waziri wa Fedha kupeleka Bungeni Bajeti ya Dharura kukabiliana na Korona na baada ya Bajeti hiyo Bunge lisimamishe vikao vyake mpaka Korona itakapokomeshwa nchini. Bajeti hiyo ihakikishe Wataalamu wetu wa Afya wanapata vifaa vya kuwalinda ili kupambana na Korona
2. Ahutubie Taifa mara moja na kuwataka Wananchi kuacha shughuli zao za kila siku na kwa kutumia Sheria ya Bunge kuifunga Nchi (partial lockdown). Wananchi wasaidiwe kwa mujibu wa mapendekezo tuliyoyatoa, kila kaya ipatiwe shs 300,000
3. Kama hawezi kuyafanya haya ajiondoe madarakani ili watanzania wengine wafanye hiyo kazi ya kulinda Nchi yetu.
Mwisho nawaomba Wanasheria nchini kuandaa mashtaka ya kukusudia kuua dhidi ya watu wote ambao wametoa matamko ambayo yaliwafanya wananchi waendelee na shughuli za kuambukiza virusi vya Korona.
Imetolewa na:
Zitto Kabwe
Kiongozi wa ACT Wazalendo
21 Aprili, 2020
#RaisTokaChato