Coronavirus: Tanzania bila lockdown tutakufa tuishe

Coronavirus: Tanzania bila lockdown tutakufa tuishe

Hivi haya Mawazo waTz mnayatoa wapi?
Kama watu tu bila lockdown watu wanalala na njaa uje ufungie watu ndani kwa Uchumi upi?.. hayo magonjwa ndo yameanza leo.. mbna TB inatembea na wateule kila Mwaka, Malaria inakamua na neti zipo.. homa ya ini vilevile.. Tena takwimu za kutisha kabisa.. mbna hatujaskia nchi ikifungwa. Sio kila kitu Ni cha kuiga iga hovyo.. utaskia ooh wagonjwa wanaongezeka.. we kwenu Nani kaugua? Cha msingi tufuate Maagizo ya Wataalamu huku shughuli za kiuchumi zinaendelea, unataka Watu waje kula kwenu?
Dah! Afrika tuna kazi nzito sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ujue cutelove nakupendaga sana ila naona kama unanizingua vile😂😂
 
Hata mimi nawaza kweli hali itakavyokua. Mbele kuna giza panatisha. Watu wanachukulia mzaha sana hili swala lakini lina athari kubwa sana.
giza gani mama ? wakati nuru ndio inachipukiza wewe unasema giza!!!!! pole!
 
Alafu wewe dada jiheshimu na uache kueneza uwongo kwenye mitandao.

Unachokizungumzia juu ya uturuki kwamba maambukizi yako na Kasi kuliko USA mbona Ni tofauti. USA kwa siku inarepot wagonjwa 15000+

Uturuki usiku huu ipo na 3000+

Punguza uvumi watanzania, wasikilizeni wanaowaongoza.
Duh, yawezekana huendi na updates, yawezekana haupo updated, ingia YouTube angalia BBC Swahili ya leo usiku madaktari wa Uturuki waliopo Marekani wanavyosikitika na kasi ya maambukizi Uturuki zaidi ilivyokuwa China, Italia, Spain na USA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkimuua Shangazi yangu kule Maswa kwasababu ya lock down !! Nitawashitaki.

Labda hiyo lock down iwe watu wasiingie nchini wala wasitoke.
Lockdown mara nyingi ni kwenye sehemu zenye msongamano wa watu,mijini,ila vijijini ni kuweka marufuku kusafiri kuingia mjini au kutoka mjini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unataka Lockdown wakati uwezo wa kuweka hata backup ya chakula 5kg ndani hauna,wee maliza kwanza rejesho la watu uliokopa kikoba harafu ndio uje kuandika huo ushubwadu wako JF,unadhani Lockdown ndio kama shughuli ya kumtoa mtoto 40 aka kibeseni??.

Lockdown ni mziki mwngn hautopata hata nafasi ya kwnd kudanga Sinza nje wajeda wametanda hata mtoto akiumwa unaambiwa kaa ndani Hanna kutoka na huko uswahili kwenu Chumba hapa choo Mbagala mbona mtajiharishia ndani mwezi mzima badala ya kufa kwa Corona mtakufa kwa njaa na kipindupindu.
Bila lockdown tutaisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wengine bhana hujui hata mambo yanavyoenda unaleta porojo tu... Kaangalie video za jirani zetu South tu hapo ndo uone hicho unachokililia... Jinga sana wewe
 
cutelove
Lock down isn't the best solution kwetu Bongo
Wasafari kutoka mkoa mmoja kwenda Mwingine Wapimwe kwenye vituo vyao vya Mabasi Sana Sana Dar es Salama, Arusha na Moshi

Watu kila Leo wanapeleka ugonjwa vijijini huko
Leo yenyewe katangazwa Mmoja Mwanza alitokea Dsm huyu humo Safarini kaambukiza Wangapi ??
 
Lockdown sio kitu cha kukililia, sio kitu kirahisi cha kusema tu serikali ikurupuke, si o kitu unachodhani unaweza ukaSurvive kwa 7,800 dada yangu, Lockdown kwa Tanzania ni hatari.

Kumbuka: Kinga haitakiwa kuwa mbaya zaidi ya ugonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Muda utaongea,nenda Kinsasha pata habari ilivyoanza na sasa kinachoendelea,panua akili sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom