Coronapocalypse

Coronapocalypse

Kumbe ni overrated? ila tatizo idadi ya vifo inatisha.
Idadi ya vifo inatisha lakini against what?? Namba ya waathirika wote??

Ni hivi.... Mortality rate ya Hii virus ni 3-4% kwa takwimu za wiki iliyopita yaani katika kila watu 100 walioambukizwa basi ni watatu pekee wanaofariki.

Kwahiyo ukisikia watu elfu tatu wamekufa mpaka sasa then fahamu kuna watu laki moja wamesurvive mpaka sasa.
 
Ah wapi!

Mimi siyo ‘panicker’ kabisa.

Sijajaza mivyakula wala toilet paper kuliko ilivyo kawaida.

Bado nawashangaa tu wanaofanya hivyo!

Sasa hivi nimetoka kununua shampoo hapa.

Hali bado iko vilevile. Hebu ona ilivyo kwenye aisle ya mikate na jams.

Jams zipo. Mikate ndo ya kuhesabu.
View attachment 1389545

Kwenye maziwa nako hali si nzuri kivile.

View attachment 1389546

Kule kwenye paper products ni kweupe.

View attachment 1389547

Hawa watu bana


Nasikia Seattle wamepata chanjo
Waambie wasipanic
Sisi huku hata barabara ni tupu unaweza kulala


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Idadi ya vifo inatisha lakini against what?? Namba ya waathirika wote??

Ni hivi.... Mortality rate ya Hii virus ni 3-4% kwa takwimu za wiki iliyopita yaani katika kila watu 100 walioambukizwa basi ni watatu pekee wanaofariki.

Kwahiyo ukisikia watu elfu tatu wamekufa mpaka sasa then fahamu kuna watu laki moja wamesurvive mpaka sasa.
Ina maana vyombo vikubwa vya habari mfano CNN,BBC n.k vinalikuza tu hili gonjwa? Au sababu limeanzia China?
 
Kuna uzi niliwaambia watu hili jambo kuwa waathirika wengi wana recover jamaa wakanicheka kinyama.
huu ugojwa ni wakawaida sanaa sema midia zime ukuza mnooo ila takwimu zina kataa kusema kuwa ni ugojwa hatari tena kwa africa watu weusi hatuna sababu yakuogopa sababu hakuna historia ya virusi vya jamii ya mafua kuwahi kuwa tishio kwa mtu mweusi mwenye asili ya bara la africa.

Na ndiomana pamoja na virusi hivi kubainika katika baadhi ya nchi za africa bado kasi ya usambaji na madhara ya virusi vya corona kwa afya ya mtu mweusi ni nadra sana watu wafwatilie data na sio kupanic kwa porojo za vyombo vikuu vya habari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Corona inachinibla tu ni kwamba inasababisha mambo yasiende.

Ila it is not that deadly.

Hata ikinipata probability ya kupona ni kubwa kuliko kufa. Hainitishi.
 

Nasikia Seattle wamepata chanjo
Waambie wasipanic
Sisi huku hata barabara ni tupu unaweza kulala


Sent from my iPhone using Tapatalk

Hata pande hizi barabara ni tupu!

Watoto wanasoma kupitia iPads.

Wazazi wanabeba boksi kupitia laptops.
 
Gumzo la dunia hivi sasa ni kirusi cha Corona.

Kirusi hiki kimeleta kizaizai na sokomoko kila pembe ya dunia.

Nchini Marekani kuna sintofahamu kubwa.

Hakuna ajuaye mwisho wa huyu kirusi.

Hali hiyo imepelekea kutokea kitu kinachoitwa ‘panic buying’.

Sasa hivi ukienda kwenye maduka-masoko [supermarket] mengi kuna baadhi ya bidhaa kuzipta ni mbinde.

Bidhaa hizo ni kama karatasi za chooni, taulo za karatasi, jeli za kusafishia mikono, na kadhalika.

Rafu za maduka-masoko mengi zipo tupu. Hiyo ni kwa sababu watu wengi wanazinunua hizo bidhaa kwa wingi kuliko ilivyo kawaida. Jambo linalopelekea kuwepo na uhaba wa hizo bidhaa kwa sasa.

Hebu ona hizo rafu hapo chini. Ni kutoka duka-soko la Publix.

View attachment 1388155View attachment 1388157View attachment 1388158View attachment 1388159

Sielewi kwa nini watu wanakimbilia sana kuzinunua hizo bidhaa na kuzihodhi majumbani mwao.

Kwangu jambo lenye mantiki zaidi na bora ni kujiwekea akiba ya pesa kuliko kutumia pesa na kununua vitu ambavyo kama itatokea umeugua na hicho kirusi, havitakusaidia kupata nafuu.

Badala ya kununua dawa, watu wananua makaratasi ya chooni!

Halafu Wamarekani wana tabia ya ku-panic sana.

Corona siyo kiama. Lakini jinsi watu wanavyofanya mambo hivi sasa, utadhani kiama ndo kimefika.

Sielewi. Na wala siogopi.

I ain’t never scared 💪🏿
I can understand the hype and panick behind over-buying of saniters, and masks.
Ila toilet papers? Why? Hivi toilet papers zinakuzuia vipi against corona au zinakusaidia vipi pale unapopata COVID-19?
Nyani Ngabu
 
I can understand the hype and panick behind over-buying of saniters, and masks.
Ila toilet papers? Why? Hivi toilet papers zinakuzuia vipi against corona au zinakusaidia vipi pale unapopata COVID-19?
Nyani Ngabu

Hata sielewi aisee!!

Watu hadi wanapigana kwenye supermarkets kwa ajili ya toilet paper.

Huu ni umajinuni kabisa.

 
haya ni mafua tu kwa african ila hawa wenzetu ndio ina madhara ( biological )
 
Wanajihami mapema huenda wakaambiwa wasalie majumbani mwao siku zijazo.
Anyways, labda ni utofauti wa culture and habits.
Mimi hata nikijua kuwa nitalazimika kutotoa nje ya nyumba kwa siku kadhaa, and i have to stock-pile my needs; Toilet papers hata sitaifikiria kabisa, maana natumia maji, swafiiiiii kabisa, mi toilet paper ya kazi gani sasa?
Hapa ndo mtu una appreciate vizuri utofauti wa mahitaji kulingana na tamaduni na tabia.
Proved
 
Anyways, labda ni utofauti wa culture and habits.
Mimi hata nikijua kuwa nitalazimika kutotoa nje ya nyumba kwa siku kadhaa, and i have to stock-pile my needs; Toilet papers hata sitaifikiria kabisa, maana natumia maji, swafiiiiii kabisa, mi toilet paper ya kazi gani sasa?
Hapa ndo mtu una appreciate vizuri utofauti wa mahitaji kulingana na tamaduni na tabia.
Proved

Una mawazo kama yangu!

Kama nipo ndani tu na hakuna shida ya maji na hakuna hofu ya kwamba kutakuwa na shida ya maji, kila nikienda haja kubwa nitaoga tu.

Sina matumizi ya lazima ya karatasi za chooni niwapo kwangu.
 
Hata pande hizi barabara ni tupu!

Watoto wanasoma kupitia iPads.

Wazazi wanabeba boksi kupitia laptops.

Umeiona hii Mkuu
Adjustments.jpg



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Hizo tishu za msalani ndizo wanatumia kama vifungashio vya pua? Kwa nini wanazikimbilia?
 
Back
Top Bottom