Neemababy
Senior Member
- Apr 1, 2016
- 118
- 166
- Thread starter
- #241
Nashukuru sana kwa haya maneno yako, yamenbariki sana sana, kupita kiasi mpendwa1111Msamaha wa kweli toka kwa muumba ni pale utakapo amua kuacha kwa dhati mabaya yote uliyofanya, unayofanya na uliyo taraji kufanya kwa dhahiri na kwa kuficho.
Kuungama ni sehemu muhimu sana katika safari ya kuelekea kwenye mwanga wenye matumanini ya maisha bora ya duniani na kwa mungu pia. Nafsi yako ndio shahid namba moja wa maovu yote uliyo fanya. Mabadiliko ni wewe na kwakuwa umeonyesha utashi wa kuachana na rubish na kubadilika basi mungu atakuongoza vema.
Kwa imani yoyote unayofuata kwanza jaribu kuwa karibu na mungu kwa kufanya ibada, yaani hudhururia msikitini/Kanisani bila kukosa. Vitabu vitakatifu ndio iwe sehemu ya maandishi unayopenda kusoma zaidi.
Watu wako wa karibu pia wasiwe wale uloshirikiana nao katika kuudhalilisha ufalme wa muumba na kwenda kinyume na matakwa yake. Hapa ni muhimu sana kubadili kuangalia mwenendo wa kila aliye karibu nawe ili iwe rahisi kwako kupata hamasa ya kutotaka kabisa kurudi ulikotoka.
NOTE; Si kila atakaye kushangaa au kukudhihaki kwa ulichoandika ni mtu mwema mbele ya Mungu na jamii kwa ujumla. wapo wengi wenye mabaya zaidi yako na bado hawajajaaliwa uwezo wa kujitafakari na kuona kile ulichokiona.
Mungu akubariki sana sana, na akujalie haja ya moyo wako mpendwa!! Ahsante sana BAGAMIKA