Comoro yatamani Muungano na Tanzania

Comoro yatamani Muungano na Tanzania

mie ugonjwa wangu ni wale ma binti wa kingazija

it doesnt matter sie tuchukue tuu ile nchi bwana weee ah

GT,
Yaani kuwapata hao mabinti mpaka muungano? Inaonekana domo zege (lol)sasa unadhani muungano ndio utakaokutongozea. Wewe nenda hata sasa kama unaweza (which I doubt) ukachukue hata mia.
 
Aaaaaaaaaaaaaaa! sitaki hata kuskia habari kama hizi, huu muungano uliopo tu watu wa visiwani zenj tabaaaaaani hatutaki hata kuusikia ukitajwa tajwa, tunaomba kama kesho CCM waondokea waiache huru zanzibar, ijipumulie stori za comoro aaaaa
 
Kuungana na Comoro,
Mhh, Mbona visiwa vya Martinique/Guadelope hadi leo ni Ufarannsa? Mbona Surinam ni Holland? Mie nafikiri umbali si shida sana.

Hawa jamaa ni Watanzania zaidi kuliko hata tunavyofikiri. Nilishawahi kukutana na jamaa tukaongea nae kwa Kiswahili na kusema kweli ingawa tulikuwa nje ya Africa na Waafrica walikuwepo kibao, jamaa alifurahi zaidi kuniona mie na tukawa tunaongea Kiswahili zaidi kuliko Kiingereza.

Sasa ukiangalia mila na jadi na hata utamaduni, kama Mzalendo alivyosema, tuko karibu nao zaidi kuliko hao Waganda/Wakenya. Kwa majirani wetu, ni WaRwanda na Burundi tu ndiyo tupo nao karibu. Wakenya na Waganda hata lugha ya Kiswahili hadi leo inawapa shida "ogelea kwa moto.."!!!!! Pia Comoro, kwa nini wasiseme kuwa wanatokea Mozambique au Madagascar? Ukiunga na hii ya watu wa Fiji/Kiribati wana asili ya Tanzania, unaanza kuamini kuwa zamani sana watu waliishi Tanzania na baadaye wamekuwa wakikimbia, ila wajukuu wameachiwa habari wakumbuke wanatoka wapi. Waizrael walienda hadi Ethiopia, Russia, nk kwenda kuchukua watu wao. Cha muhimu ni kuwa tubadilike tabia zetu. Tujione kama Wazazi wa hao watoto wapotevu na kuwasaidia mara wanapohitaji msaada. Tuwasaidie kujenga demokrasi na hata wakitaka kurudi basi wapatiwe passport na uraia bila bughudha. Nyumbani ni nyumbani. Ila na sisi wazazi tuanze kuwa mfano wa kuigwa. Rostam ni Mzazi gani? Liyumba? Mramba? Anna Che Nkapa, Idriss, Mataka? nk Hatuwezi toa funzo kwa wanenu hawa kwa hali hii.
 
Hili swala la muungano na comoro si geni hata kidogo, waliwahi kumuomba Mwalimu miaka ile ya sitini tuungane kama ilivyo Zanzibar lakini Mwalimu kwa Kuona mbali alikataa akawambia wao wako mbali mno kijografia na Tanganyika mainland enzi hizo, akawaambia utakuwa si muungano kihalisia ila Comoro itaonekana kuwa ni koloni la Tanganyika hivyo siku moja vizazi vijavyo vitadai uhuru wao.Mwalimu aliona ni kupotosha maana ya muungano.
 
kaka tukiacha nafasi hii, basi tena. wabongo tuchangamkie hii tenda, tuwachukue hao jamaa. wakati zenji wanaona sisi wabaya, wengine wanatutaka. tuwachukue hawa jamaa bila kuchelewa jamani.
 
I remember Prof Baregu's Regional Integration class in particular on the principles of integration, there is what he call the imperatives for integration! there are four but I only remember two of them which fits well in an analysis of this move; Love and threat, so there are those who are saying we have common history,social proximity not geographical and of course some of us are even going further by thinking of beautiful Comoro ladies! the Lundengas and their establishment may even think of winning the Miss world crown! why not!but again there are those who are saying no way! this people are proposing union not because they love us but bse of threat! disentergration, dissenting voices some of the islands want to maintain some autonomy from the main Island, so the solution is to unite with a super power, one which is stable and there fore everything will be fine taken care of, again there is another imperative which he calls 'gains' countries may decide to unite on the basis of mutual gains, what am going to benefit out of the union may be on economic terms which I think may be irrelevant as we are already trading with them,so may not be the motive!

But all in all lets get sober, discuss and debate this move but at the end of the day of course we expect Tanzanians to be consulted,people of Comoro as well and then other things may follow suit, yes why not some of us may be taking tours out there and turn it into the Bahamas of Africa, Cayman etc
 
Itatusaidia sana kuwa taifa lenye nguvu.Na negativity ya kuungana kwa nchi za kiafrika itapungua.Other countries will learn from us.titafute kura ya maoni ..ila ni jambo zuri kuungana.
 
Kuungana na Comoro,
Mhh, Mbona visiwa vya Martinique/Guadelope hadi leo ni Ufarannsa? Mbona Surinam ni Holland? Mie nafikiri umbali si shida sana.

Hawa jamaa ni Watanzania zaidi kuliko hata tunavyofikiri. Nilishawahi kukutana na jamaa tukaongea nae kwa Kiswahili na kusema kweli ingawa tulikuwa nje ya Africa na Waafrica walikuwepo kibao, jamaa alifurahi zaidi kuniona mie na tukawa tunaongea Kiswahili zaidi kuliko Kiingereza.

Sasa ukiangalia mila na jadi na hata utamaduni, kama Mzalendo alivyosema, tuko karibu nao zaidi kuliko hao Waganda/Wakenya. Kwa majirani wetu, ni WaRwanda na Burundi tu ndiyo tupo nao karibu. Wakenya na Waganda hata lugha ya Kiswahili hadi leo inawapa shida "ogelea kwa moto.."!!!!! Pia Comoro, kwa nini wasiseme kuwa wanatokea Mozambique au Madagascar? Ukiunga na hii ya watu wa Fiji/Kiribati wana asili ya Tanzania, unaanza kuamini kuwa zamani sana watu waliishi Tanzania na baadaye wamekuwa wakikimbia, ila wajukuu wameachiwa habari wakumbuke wanatoka wapi. Waizrael walienda hadi Ethiopia, Russia, nk kwenda kuchukua watu wao. Cha muhimu ni kuwa tubadilike tabia zetu. Tujione kama Wazazi wa hao watoto wapotevu na kuwasaidia mara wanapohitaji msaada. Tuwasaidie kujenga demokrasi na hata wakitaka kurudi basi wapatiwe passport na uraia bila bughudha. Nyumbani ni nyumbani. Ila na sisi wazazi tuanze kuwa mfano wa kuigwa. Rostam ni Mzazi gani? Liyumba? Mramba? Anna Che Nkapa, Idriss, Mataka? nk Hatuwezi toa funzo kwa wanenu hawa kwa hali hii.


Mkuu Sikonge heshima mbele.

Naomba kutofautiana na wewe hasa katika kipegele unachosema eti Tanzania tuna ukaribu zaidi na Comoro kuliko Uganda na Kenya.
Mkuu Sikonge mila,desturi na utamaduni wa mmasai wa Kenya na watanzania ni mmoja kiasi kwamba ni vigumu sana kumtofautisha mmasai wa Kenya / Tanzania mambo ni hayo hayo kwa wahaya wa Tanzania na waganda mila na utamaduni wao unafanana sana.

Tusilazimishe muungano kwa kukimbilia hoja dhaifu hatupaswi kufikiria muungano na dola dhaifu kama comoro.Muungano wetu na Zanzibar sasa unatimiza miaka 45 lakini hatuna cha kujivunia kwani kila mara wenzetu wa Zanzibar wanalalamikia muundo wa muungano.
 
loh! Hivyo ndivyo unavyodhani?
Kama wazenji wako huku wanalazimika kwa vile kule meweka vibaraka wenu ambao wanayafanya maisha ya wazanzibari kuwa magumu ha hivyo wasio na moyo ndio wanaamuwa kuloweya huko. Lakini mkuu zanzibar ni nchi nzuri nasi wenyewe tunajivunia lakini kwa vile mnatutawala na kutuwekea majeshi huku vibaraka wenun wakifanya walivyotaka wakijua kuwa mnawalinda basi tunalazimika tuwepo huku.


..vibaraka kina nani wakati kura mnapiga wenyewe ..hamuangalii sera mnaangalia erhnicity....hata kama ni maruwani..,zanzibar ikiachwa leo pemba itakuwa nchi.., na unguja itaachwa ,na ukweli zanzibar wazioutaka ni kuwa pemba ndiko kwenye wasomi na wachapakazi!!!!.....unguja maneno mingi..darasani ...tia maji tia maji!!!

Pemba wakijitenga unguja wataomba tukakomboe pemba kijeshi ....kama comoro walivyooomba tukaikomboe anjouan!!! Huo ndio ukweli.....nadhani muungano hauhitaji kudhihakiwa !!
 
...DAATAZ NI KATI YA WATUMISHI WOTE WA UMMA ...ZANZIBAR ..WATAALAMU NI ONLY 8%...YAANI ASLIMIA 92& HAWANA UJUZI ...KIMSINGI KWA TEKNELOJIA SIKU HIZI HATA WAFAGIZI NA WATUNZA BUSTANI WANATAKIWA WAWE NA ELIMU UFUNDI STADI YA VETA AU CHUO CHA UTALII[HOUSEKEEPING]

ASILIMIA KUBWA WANASIASA.....KWA NCHI NDOGO ILE NI HASARA KUWA NA COMPELX STRUCTURE YA UTAWALA KAMA ILE ..INASABABISHA BUEAUCRACY...WEWE FIKIRIA KUNA SHEHA,MTENDAJI,DIWANI ,MBUNGE,MWAKILISHI,MKUU WA WILAYA ,MKUU WA MKOA,MAWAZIRI,MANAIBU WAZIRI,.....BADO KUNA KMKM.,VALANTIA,MGAMBO,JKU,MAFUNZO,ZIMAMOTO ,KIKOSI MAALUM[USALAMA YAO] etc.....thats too complicated...big chunk of budget is used in the payroll...
 
PM,
Basi imetosha maneno mazito saana, maana wazanzibar umewakata mkia bila hata kuweka ganzi.
 
PM

Muungano umesaidia kuweka vile visiwa pamoja!

Sema akina Seif saa ingine hawataki to appreciate this!

Sasa Komoro tukiwa nao akina Seif watanyamaza tu.. maana sauti ya Upemba itapungua
 
Last edited:
Rais Sambi alitishiwa Maisha Exim kufungua Tawi Comoro

Rais wa Muungano wa Visiwa vya Comoro, Ahmed Sambi, amesema alipokea vitisho, vikiwamo vya kuuawa baada ya kukubali kuanzishwa kwa Benki ya Exim mjini Moroni kisiwani Ngazija.

"Niliambiwa kama nataka kubaki madarakani au kuendelea kutawala, nisilete benki yoyote Comoro… nikasema kama ni kufa acha nife, lakini benki hii lazima ianze kazi hapa,"
alisema Sambi kwenye uzinduzi wa tawi la kwanza la Benki ya Exim.

Akiwa na mgeni wake, Rais Jakaya Kikwete, Sambi alisema umuhimu wa benki kwa nchi yake ulikuwa ni mkubwa na sasa fursa nyingi za biashara zinaweza kufanyika kati ya nchi hizo mbili.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Bodi ya Exim, Yogen Manek, hiyo ni benki ya kwanza kutoka Tanzania kuwekeza nje ya nchi ambapo ina mwaka mmoja sasa Comoro na wateja 5,000 na kabla ya mwishoni wa mwaka huu, itafungua matawi mengine Sudan na Djibouti.

Sambi aliwataka Watanzania wengi zaidi kuja kwa wingi kuwekeza Comoro, ikiwa ni njia mojawapo ya kurejesha fadhila kwa Tanzania kuikomboa Anjouan. "Marafiki zetu njooni mtusaidie kuboresha maisha ya watu wa Comoro, nchi yetu ni kama bikira katika uwekezaji, ina vivutio vya kutosha," alisema.

Kabla ya tawi la benki, Comoro ilikuwa na benki mbili; ya Posta inayomilikiwa na Serikali na ile ya BIC. Rais Sambi alimpongeza Rais Kikwete, kwa kusema alikuwa muungwana kuikomboa Anjouan kwa mtutu wa bunduki, na sasa amekuwa muungwana kuikomboa kifedha (kiuchumi). Rais Kikwete alikuwa na ziara ya siku tatu katika visiwa hivyo na alitarajiwa kurejea nchini jana.

Maskini,

Huyu Raisi ndo maana yuko desperate kuomba kuungana na Tz!

Yaani tu kukubali Tz kufungua Benki anatishiwa maisha?

Yaani imenisikitisha sana!

Leo hii Visiwani wanapiga kelele?? Hawajaona uchungu kama huu wa Sambi!


Source: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=111
 
..vibaraka kina nani wakati kura mnapiga wenyewe ..hamuangalii sera mnaangalia erhnicity....hata kama ni maruwani..,zanzibar ikiachwa leo pemba itakuwa nchi.., na unguja itaachwa ,na ukweli zanzibar wazioutaka ni kuwa pemba ndiko kwenye wasomi na wachapakazi!!!!.....unguja maneno mingi..darasani ...tia maji tia maji!!!

Pemba wakijitenga unguja wataomba tukakomboe pemba kijeshi ....kama comoro walivyooomba tukaikomboe anjouan!!! Huo ndio ukweli.....nadhani muungano hauhitaji kudhihakiwa !!

Pengine hazihaki bali anasema ukweli. Hivyo nani huwalinda watawala wa CCM kule visiwani? Nani aliekwenda akauwa na kubaka kule visiwani? Na kwanini kila uchaguzi unapokuwa tayari huwa mnapeleka majeshi kule? Mwaka 1995 baada ya Salmini kushindwa Nyerere alifanya nini? Bado unataka ushahidi wa namna mnavyowalinda watawala?
ETI mtatakiwa majeshi iwapo Pemba ikijitenga? Kweli kwani tu maexpert wa kupigana na watu wasio na uwezo wa kijeshi lakini tunapokutana na wengine watu wa vita tunakataa kupeleka majeshi yetu na ndio maana tunajaliwa na wakimbizi wa jirani zetu lakini hatuna ubavu wa kwenda huko.
 
...DAATAZ NI KATI YA WATUMISHI WOTE WA UMMA ...ZANZIBAR ..WATAALAMU NI ONLY 8%...YAANI ASLIMIA 92& HAWANA UJUZI ...KIMSINGI KWA TEKNELOJIA SIKU HIZI HATA WAFAGIZI NA WATUNZA BUSTANI WANATAKIWA WAWE NA ELIMU UFUNDI STADI YA VETA AU CHUO CHA UTALII[HOUSEKEEPING]

ASILIMIA KUBWA WANASIASA.....KWA NCHI NDOGO ILE NI HASARA KUWA NA COMPELX STRUCTURE YA UTAWALA KAMA ILE ..INASABABISHA BUEAUCRACY...WEWE FIKIRIA KUNA SHEHA,MTENDAJI,DIWANI ,MBUNGE,MWAKILISHI,MKUU WA WILAYA ,MKUU WA MKOA,MAWAZIRI,MANAIBU WAZIRI,.....BADO KUNA KMKM.,VALANTIA,MGAMBO,JKU,MAFUNZO,ZIMAMOTO ,KIKOSI MAALUM[USALAMA YAO] etc.....thats too complicated...big chunk of budget is used in the payroll...

Unajuwa Uchache wa Wataalamu wa Zanzibar na wingi wa wamiliki wa vyeti vya utaaamu walioko Bara hauna tofauti? Hivyo huu utaalamu tulionao huku Bara umesaidia kiasi gani kuitowa nchi kwenye umasikini? Tumevumbua nini au tumeboresha nini kwa maisha ya wananchi wa kawaida? Pengine namna wananchi wa kawaida wanavyoishi ni bora kule visiwani kuliko huku Bara. Ama kwa UFISADI kweli tumewashinda wale wa visiwani na kama tutawapa uhuru wa kujiendeleza basi hao wataalamu kiduchu walionao watawafikisha mbali.
Nikupe siri moja kama hujaipata kule visiwani hata yule asienda shule hata darasa moja huwezi kumfananisha na mwenzake wa Bara.
 
NAOMBA KUKUULIZENI WALE MNAOSHANGIRIA MUUNGANO NA COMMORO. JEE MLIONA PICHA YA SAMBE NA JK KWENYE MAGAZETI?

NIWAKUMBUSHE JAMBO ZITO AMBALO KWA HAPA KWETU NI LA MUHIMU SANA LAKINI KWA HAMU ZETU ZA KUTAKA KUWATAWALA WADOGO TUNASAHAU KULITIA MAANANI.

JEE TUKO TAYARI KUUNGANA NA WAARABU IWAPO NDANI YA NCHI YETU HATUTAKI WAWE VIONGOZI? lABDA KWA HLI LA KUTAWALA ITAKUWA SI HARAMU KUMTAWALA MWARABU?
 
NAOMBA KUKUULIZENI WALE MNAOSHANGIRIA MUUNGANO NA COMMORO. JEE MLIONA PICHA YA SAMBE NA JK KWENYE MAGAZETI?

NIWAKUMBUSHE JAMBO ZITO AMBALO KWA HAPA KWETU NI LA MUHIMU SANA LAKINI KWA HAMU ZETU ZA KUTAKA KUWATAWALA WADOGO TUNASAHAU KULITIA MAANANI.

JEE TUKO TAYARI KUUNGANA NA WAARABU IWAPO NDANI YA NCHI YETU HATUTAKI WAWE VIONGOZI? lABDA KWA HLI LA KUTAWALA ITAKUWA SI HARAMU KUMTAWALA MWARABU?

Ngekewa,

Kwani Waarabu sii binadamu?

Visiwani kuwa Waarabu, waafrika n.k mbona tumeungana tu!!

Mbona Amir Jamal alikuwa Mwarabu Bara na alipewa uwaziri? Dr. Bryeson

Mzungu nae alipata kuwa waziri wa Afya Bara wakati wa Nyerere!

Hakuna cha ubaguzi..ni fikra tu sizizo sahihi!

Komoro wao wameonyesha nia na kuomba kutaka kuungana nasi!

Je kuna ubaya?
 
Back
Top Bottom