COL.MAHFUDHI: Zanzibari and Tanzanian internationalist

Karume alirithi Zanzibar yenye Neema ....alikuta palace imejaa pesa na dhahabu baada ya kuwa Sultani kakimbia........pia wakati huo bei ya karafuuu ilikuwa mzuri na idadi ya watu haikuwa kubwa......haikuwa ajabu kumudu kufanya maendleo hayo.......lakini naamini kabisa Kama Karume angekuwa mtulivu na kuwatumia wasomi waliokuwa wamemzunguka ...Kama kina Abdulrahman Babu,Kassim Hanga ,Abdul Jumbe Mwinyi na wengine ......Zanzibar ingepiga hatua zaidi.....ya hayo magorofa ya wananchi na TV ambayo ndie imekuwa litania ya Kipimo cha maendleo

Ungeniambia ingekuwaje Karume angeendelea kuwepo miaka 5 tu mingine naona Angefika mahala angekwama kwa Aina ya uongozi wa mabavu na mauwaji.......pesa zilikuwa zinaelekea kwisha .......na kufikia Kati Kati ya 70s bei ya karafuuu ikaanza kushuka .....na Uchumi wa dunia uliyumba Sana ...na pia kulitokea njaaa na serikali za kiafrika ziliyumba kwa kutumia pesa nyingi kuagiza vyakula.....Sioni Kama Wazanzibar wangeweza kuendelea kuvumiliaaaa kuona Ndugu zao wakitoweka ....ingefikia mahala angebaki Hana pakukamata..........

When people run of ideas...wanatumia mabavu kuendelea kuwepo.
 
Sijui source yako ya hii habari inatoka wapi lakini it's a well known fact kwamba hakushiriki na kwamba kuna strong evidence kuonyesha hivyo, kuna vitabu vimeandikwa na independent writers (sio wana mapinduzi au waliopinduliwa) kuhusu hili jambo visome halafu come to your own conclusion, kimojawapo kinaitwa "Zanzibar Revolution: An American Cold War Tale" by Don Peterson, huyu Don Peterson alikuwa ni Mmarekani pekee aliekuwepo ubalozi wa Marekani Zanzibar katika kipindi chote kabla na baada ya mapinduzi na alishiriki katika majadiliano baina ya Revolutionary Council na serikali za Marekani/UK, majadiliano yalihusu mambo mengi yakiwemo kuwaachia raia wa nchi hizi kupanda manuwari ya kimarekani iliyokuja kuwachukua na pia kuhusu Marekani/UK kuyatambua mapinduzi, nchi hizi hazikuyatambua mapinduzi na ilipita zaidi ya miezi miwili mpaka kuyatambua!!!!. Yeye kwa ufupi anasema kuwa hata katika majadiliano yao kiongozi alikuwa ni Okello na sio Karume, uamuzi wa mwisho ukitoka kwa Okello, sasa kama wewe ndio kiongozi wa Mapinduzi inakuwaje maamuzi ya mwisho anakuwa nayo Okello - inaeleweka hii?.

Vile vile katika chama cha ASP kulikuwa kuna kundi ambalo lilitaka kufanya kila njia ili chama hicho kitwae madaraka na kundi ambalo lilitaka ASP iheshimu mfumo wa siasa uliokuwepo (akiwemo Sultani) na wafanye mgomo baridi ndani ya baraza la kutunga sheria (bunge) la Zanzibar, Karume alikuwa kwenye kundi hili la mgomo baridi na wala hakuwafiki mambo ya fujo pengine akiogopa yatakayomfika pindi wakishindwa.

La mwisho na ombi kwa wale wanaoweza wamuulize Natepe ukweli ni upi, nasikia keshasema kuna kitabu kakiandika kuhusu mapinduzi na kitachapishwa akishafariki maana anaona wasaliti wa mapinduzi leo wanaitwa wana mapinduzi!!!!! - habari ndo hiyo.
Kuna ukweli mwingi nyuma ya mapinduzi unafichwa,kwa faida ya wanasiasa wachovu na waoga wanaoogopa vivuli vyao.Tunajua kuwa aliye taka sana kutumiwa njia ya fujo ni Babu.Huyu mkomunisti ndiye alianzisha mpango wa kupokonya madaraka kwa kuwatumia vjana waliotoka cuba na urusi.Karume alipendelea zaidi Mazungumzo zaidi.Babu alipendelea fujo zaidi na aliamini ndio njia pekee ya kumtoa sultani(rejea hotuba ya babu ya siku ya uhuru 1963).Hata historia ya Tanganyika nayo inapotoshwa makusudi ili kujustfy mambo waliyo fanya kinyume.Ndipo namuelewa mzanganyika anaposema juu ya usaliti..(rejea sababu za samul doh kuchukua madaraka)
 
sasa huyo polisi aliyetoa silaha,Edington kisasi aliishia wapi? NA je huyu somebody HANGA je did he play any part katika haya mapinduzi?
Ndg kwanza la kufahamu ni kuwa,okello alijipenyeza zanzibar baada ya maumau na "kumalizana"na kenyata.Alifanikiwa kuingia hata kuwa police kwenye serikali ya sultan.Kilicho saidia mapinduzi ni kutimuliwa kazi kwa askari polisi wengi akiwemo okelo.Askari wapya hawakuwa na uzoefu wa kutosha wa mapambano.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom