COL.MAHFUDHI: Zanzibari and Tanzanian internationalist

Tatizo la ndugu zetu watanganyika ni kuwa hamuielewi vizuri historia ya Zanzibar lakini nyinyi munajifanya ndio wataalamu na madaktari wa kila baya liliopo Zanzibar. Historia halisi ya Zanzibar imo kweye vichwa vya watu walioishuhudia haya mambo na sio hiyo ya kwenye vitabu vya ushabiki wa kisiasa. Cha kusikitisha ni kuwa kwa hapa Tanzania hakuna mtu hata mmoja alieishuhudia historia hii ambae yuko tayari kuielezea bila kuongeza chumvi za kisiasa, kila mmoja akiwemo Salim Ahmed Salim wanaogopa kumwaga unga wao, hii inanyima future generations haki yao ya kuujua ukweli.
Ni kweli kuna wakati fulani tulikuwa tukijaribu kuwafuata wale wana-Mapinduzi (walipokuwa hai na wapo mapumzikoni -sio ulingoni) watueleze kilichojiri na walivyoshiriki siku ile- wapi hatukupata ukweli bali tulibabaishwa tu na ah. basi tukatangaza tu tena zile porojo.
 
Pasco, usizungumzie juu ya utawala wa sheria when you talk of Zanzibar. Hayo aliyokuwa akiyafanya Sultani kabla ya Mapinduzi yalikuwa ya sheria au tumeyasahau leo? Maovu ya Sultani yasingeliweza kuondoshwa kwa kutumia utawala wa sheria. Utawala wa sheria is a way to enslave the masses! Hilo unalijua, kwani kwetu Danganyika, with a rule of law ufisadi will always shine among our midst - wether we are under CCM, Chadema, CUF, etc!
Kusema kwamba Karume hakushiriki Mapinduzi ya Zanzibar is to tarnish the history and the revolution of Zanzibar. Mapinduzi sio kurusha mawe au kufyatua risasi, else sote tungelikuwa wana-Mapinduzi. There was a lot behind organizing the revolution than what we saw on January 12th. Without Karume the Zanzibar revolution would have failed and I am damn serious about this!. Yule jamaa alikuwa kweli shujaa, bila ya yeye bado ndugu zetu Zanzibar mpaka leo wangekuwa wametawaliwa na Sultani. Kweli akina Natepe, Said Washoto, Bavuai, Mahfudhi walifyatua risasi za mwanzo, but the brain behind them was Karume and that is why he was whisked away to DSM for the sake of the success of the revolution. He never fled to DSM as you suggested. He was taken by the ZRC to DSM for the good sake of the revolution itself.
So, what if Karume came from Malawi? Kafanya mengi kuliko wewe unaetoka Mbeya au hao mafisadi wetu wanaotoka Monduli au mimi ninaetoka Songea. Without Karume downtown Zanzibar would still have been a gutter till this date as left by the Sultan. Kaondoa vibanda mjini - nani mwengine kafanya hivyo???? He was also an economist japokuwa hakufika shule na pesa zake ndio tulizoshindia vita ya Kagera na kuweza kumuondoa yule Nduli (Iddi Amin).
So, please, let's not besmirch the good name of Karume!
Karume was a sacred person - hata Nyerere akijua hivyo. Please don't touch his name in unreliable stories. Mimi sio CCM, else nisingelikuwepo hapa, wala sio CUF. Mimi ni Mwana-Chadema halisi, but I know our past and I will never mingle it with any party feelings!
Mchana mwema Bwana Pasco!
Mh! sijui huyu kama kafika hata darasa la saba.

PASCO HESHIMA KWENDA MBELE MKUU.. MFUNZE HUYU,INAONEKANA ELIMU NDOGO MAANA KAANDIKA PUMBA TUPU.
 
Mh! sijui huyu kama kafika hata darasa la saba.

PASCO HESHIMA KWENDA MBELE MKUU.. MFUNZE HUYU,INAONEKANA ELIMU NDOGO MAANA KAANDIKA PUMBA TUPU.
WATU wengine bana,sasa hapa pumba iko wapi,na maswala ya darasa yanakujaje, DONT hit the keyboard just for the sake-bring in something constructive
 
kuandika kizungu ndo kusoma mkuu? pumba maana sikufurahishwa na maelezo yake kwanza ni uongo mtupu alichoongea halafu na kajaribu kuwakashifu kundi flani wakati si kitu cha kweli,chuki zake za ki-CCM analeta hapa.
 
asanteni jokakuu kwa kuanzisha hii mada na wakuu wote mnaotoa michango yenu mizuri.mimi ni mbara na siku zote nimekuwa na hamu kubwa kujua kiini cha mapinduzi ya zanzibar,wahusika wake halisi ni kina nani na utawala wa Karume(senior) baada ya mapinduzi na hata wahusika wa kifo chake.
Wakuu endeleeni kumwaga nondo,wenyewe tutachambua pumba na mchele
 
kuandika kizungu ndo kusoma mkuu? pumba maana sikufurahishwa na maelezo yake kwanza ni uongo mtupu alichoongea halafu na kajaribu kuwakashifu kundi flani wakati si kitu cha kweli,chuki zake za ki-CCM analeta hapa.


sasa kama hukufurahishwa na maelezo yake si uyapinge kwa hoja?unasema pumba,wewe ambaye una point andika hizo point na huo ukweli tukusome basi.
vinginevyo kaa kimya acha watu wamwage data hapa.
 
sasa huyo polisi aliyetoa silaha,Edington kisasi aliishia wapi? NA je huyu somebody HANGA je did he play any part katika haya mapinduzi?

Abdallah Kassim Hanga was also a brilliant guy, lakini yeye na Othman Sherrif walitolewa muhanga na Nyerere. Nyerere maishani mwake alijua kuwa alifanya kosa kubwa baada ya kuwarejesha wao into the filthy hands of SMZ. Wao waliuliwa kishenzi na siku hio Zanzibar was under curfew and all the ZRC members including Karume and Sheikh Thabit Kombo trotted around in Zanzibar in millitary uniforms. Sijui walikuwa wakimtisha nani.
Hanga alitiwa tu kwenye mapinduzi, kwani yeye alikuwa ndio kwanza karejea masomoni na alikuwa wa kwanza kuutangazia ulimwengu in english katika radio Zanzibar kama Zanzibar kumetokea mapinduzi.
Babu na Mahfudh hawakupelekwa Zanzibar na Nyerere japokuwa walikuwa wakitakiwa huko, kwasababu Nyerere alijua kuwa yatawakuta yale yale yaliyowakuta akina Hanga na Othman Sherrif.
Huyu Mchaga aitwae Edington Kisasi sio kama alitoa bunduki na kuwapa akina Okello mkononi, lakini alifanya mambo mazuri yaliyowasaidia wapiganaji wa ASP kuteka Bomani kwa haraka.
Edington Kisasi hakusahauliwa na Karume kwa msaada na wema wake huo na kwahivyo alipandishwa cheo na akawa the first african Commissioner of Police in Zanzibar and a member of the inner circle of Zanzibar Revolutionary Council. Baadae alipata pia nyazifa za uwaziri katika wizara mbali mbali. Mwanawe anaitwa Remis ni Civil Engineer na nadhani bado yupo Zanzibar. Anamradi wake wa baa pale nyuma ya Kilimani. He is a respected gentleman in Zanzibar for the part played by his father in the liberation of the Isles.
Jambo zuri zaidi alilolifanya Karume na kuharakisha mapinduzi ni kuwaunga mkono Hizbu ili Zanzibar ipate uhuru mapema tena kwa haraka. Wengi walistaajabu kwanini alikuwa anataka Zanzibar iwe huru na muingereza aondoke wakati akijua fika kuwa nchi itakuwa chini ya Sultani na Hizbu. Watu walikuwa hawajui what he was concoting in his mind. Hii ilimpelekea hata wana-ASP wengine kutaka kumgeuka na kumwita kibaraka wa Sultani, kwasababu walikuwa hawajui nini kinakuja. Kama Zanzibar isingelikuwa huru, mapinduzi yasingeliwezekana, kwani ilikuwa chini ya himaya ya Uingereza na Malkia angelileta askari dakika moja tu kutoka Kenya - kama alivyofanya huko nyuma.
Karume kwa kweli alikuwa above the average intelligence na ndio maana mapinduzi yakafaulu. Ikiwa mtu anasema kuwa Karume alikuwa of an average intelligence, basi kwa criteria hio hawa Ma-Rais waliomfuatia jamani sio watakuwa hawana akili kabisa - yaani wendawazimu!!!
 
Ni mtu maarufu sana ugenini lakini Znz hana bao ni msaliti tu.

Mola amlaze panapostahiki.
 
Ndugu Nkazahau, Kwa kweli mimi sina haja ya kuuendeleza huu mjadala. Karume ni wenu nyinyi na kama mnamuona hakufanya kitu hilo ni lenu nyinyi. Sisi katuletea balaa la milele. Kama unavyosikia kuwa Pemba jana vurugu zishaanza tena. Zanzibar to us is a thorn in our ass! Kama nyinyi hamuutaki Muungano sisi hatuutaki mara mia. Mnatutia aibu internationally na huo ugomvi wenu baina ya wapemba na wazanzibari usiokwisha maisha – katika kila uchaguzi!!!.
Øchama kilikuwa tayari kinasambaratika na hakikuwa na uwezo wa kukaa chini na kupanga hata kikao cha ndani mbali mapinduzi?, Sasa unatueleza Mapinduzi yalikuwa organized na Hizbu wenyewe?
Othman Sherrif, Moyo, Idiria, Hanga na mlevi Jumbe na wengine hawakujua mipango ya Mapinduzi. Karume alikuwa hawaamini wasomi tokea hapo mwanzo, kwani wangetoa siri. Karume aliwaamini akina Seif Bakar, Saidi Washoto, Bavuai, etc - watu ambao hawakupita shule kama yeye. In fact kama Karume angelijua kuwa atakufa siku ile, basi angelimuachia urais wa Zanzibar hayati Seif Bakar!

ØKarume alikuwa na average intelligence, alikuwa ni layman with a good common sense - period. Angalia kila alichokifanya utakiona kuna common sense lakini hakuna deep understanding,
Sasa tueleze ni kipi kilichofanyika tokea 1972 ambacho kina deep understanding na sustainability hata tunafika kusema kuwa Karume yeye alikosea? Ni hizo picha za video za porno za wasichana wa ki-zanzibari tunazoziona nje siku hizi? Kukosa Karume Michenzani ingelibakia bwawa la maji machafu mpaka leo. Kukosa Karume TV isingelifika Zanzibar milele. If you say that is an average intelligence, then it is better to have that. Common sense is indeed very uncommon with many people. Only intelligent people like Karume have common sense. Most of us don’t have it though it is said to be common!.

Øjee unajua kwamba mwenyekiti wa kwanza wa baraza la mapinduzi ni Okello na sio Karume?
That makes sense. It took days to find out that the revolution succeeded. Sasa kama Karume angelirejea haraka haraka na siku yapili mngereza kaleta majeshi je ingelikuwa vipi? Nyerere hakutaka Karume arejee Zanzibar siku yapili baada ya Mapinduzi wakati Mapinduzi yalikuwa hayajatambulika na ndio maana akamueleza Karume angojee kwanza kule Bagamoyo mpaka mambo yakae sawa na hapo ndipo alipopata ukumbi Okello ili pasiwepo vacuum!

Okello katokea Pemba alikokuwa akipiga matuta na alikuwa hana mtu Zanzibar anaemjua na kwahivyo asingeliweza ku-organize mapinduzi. Pia Okello asingeliweza kumjua yule ndugu yetu Mchaga Edington Kisasi (Police Officer in the Sultan’s army) ambae ndie aliyetoa bunduki Bomani na zikafanikisha Mapinduzi. Hio kusema mmepindua kwa mapanga na mashoka ni nyimbo za watoto wa shule tu. Mapinduzi bila ya huyu Mchaga yangelikuwa magumu, kwani yasingelipata silaha ya kuenda kuiteka ile kambi nyengine.

Jambo alilokosea Nyerere ni kuwa pale Karume alipotaka Muungano ili asalimike na wamanga Nyerere angelimueleza kuwa achanganye nchi kabisa na sio kumkubalia nusu nusu kama walivyofanya. Karume was not interested in the Union, lakini Nyerere [/QUOte

Haya maelezo yako hapo juu just proved my case, hizo takwimu na hayo majina ya watu yote yanaupotosha ukweli, watanganyika hamuijui historia ya Zanzibar munachupiachupia tu na mukianza kuwa challenged basi munaleta chuki zenu kwa wazanzibari, sasa haya ya "zanzibar to us is a thorn in our a--" yametokea wapi tena, maana sikumbuki kama tulikuwa tuna discuss kuhusu zanzibar kwenu ni nini?, kama ningelikuwa na muda basi ningelipigishana kelele na wewe lakini naona itakuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa so I rest my case.
 
<Haya maelezo yako hapo juu just proved my case, hizo takwimu na hayo majina ya watu yote yanaupotosha ukweli, watanganyika hamuijui historia ya Zanzibar munachupiachupia tu na mukianza kuwa challenged basi munaleta chuki zenu kwa wazanzibari, sasa haya ya "zanzibar to us is a thorn in our a--" yametokea wapi tena, maana sikumbuki kama tulikuwa tuna discuss kuhusu zanzibar kwenu ni nini?, kama ningelikuwa na muda basi ningelipigishana kelele na wewe lakini naona itakuwa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa so I rest my case>.

Nd. Nkazahau,
Sasa ndugu yako Calipso anakutegemea wewe utosomeshe sisi Watanganyika wa darasa la saba na wewe naona unaikimbia kazi hio. Ni kweli kabisa kuwa mimi sitokufahamu na wala sina haja ya kukufahamu na itakuwa kama "unampigia mbuzi gitaa" tu, lakini wengine hapa JF ni binaadamu kama wewe na wangekufahamu vizuri sana na wangejua ukweli ni upi.
Ukweli gani huo unaopotoshwa kuhusu Zanzibar? Mapinduzi kwani hayakutokea kweli? Au mnataka jina la Karume liwe blackened out from the history books of Zanzibar?
Au kwasababu nimemwita Karume shujaa na genius? Au kwasababu nimemgusa Sultani? Kama ni hilo mnalolitaka basi kila penye jina la Karume tutatia jina la Sultani &#8211; maanake huyo Sultani ndio ugonjwa wenu mkubwa!
Au huyo Edington Kisasi nae hakuwepo kweli na wala hakushiriki kabisa katika Mapinduzi sawa na Karume - kama mnavyoeleza? Au nimechukiza kwasababu nimeandika kuwa Kisasi alikuwa ni Mchaga? Yeye alikuwa ni Mchaga jina tu, but he identified himself as a true Zanzibari kwa maneno na kwa vitendo vyake vya January12th, 1964, and he loved Zanzibar just like any other true Zanzibari.

Ø watanganyika hamuijui historia ya Zanzibar munachupiachupia tu
That is true. Sasa kwanini hamuitumii hii nafasi mkapata kutuelimisha sisi Watanganyika wa darasa la saba? The truth is that tunakujuweni vizuri sana. Usisahau kuwa tupo na nyinyi pamoja for 45 years now. Please, pray to Almighty God to keep us united for another 45 years! Else, mwenyewe unajua nini matokeo yatakuwa pale Watanganyika tutakaposema tumechoka!!!!
 
Michango ya watu mbali mbali ktk hii mada inachanganya mpaka nakosa nishike lipi niache lipi.
 
Asante kukumbushia Col. Mahafudh. Huyu ni miongoni mwa ma strategists wa Zanzibar Revolution, yeye, akina Abrahaman Mohamed Babu.Feild Marshal John Okello, Abdalah Said Natepe na wengine. Siku ya mapinduzi yenyewe, January 12, Karume aliikimbia Zanzibar na kujificha bara. Baada ya mapinduzi, ikaamuliwa Karume aliongoze Baraza la Mapinduzi kwa heshima tuu lakini power halisi zilikuwa zishikwe na Okello, Mnganda. Hili lilimuogopesha Karume, akamwambia Julius amuite Okello Dar, Tarehe 14 January 1964, baada ya ile picha ya pamoja ya Baraza la kwanza la Mapinduzi, John Okello alitwa Dar na masikini kumbe ndio ilikuwa safari yake ya mwisho.
Taarifa za ujio wa Okello Dar zilizagaa ambapo wajeshi walimsubiri kama shujaa.
Okelo alipofika tuu bara, badala ya mapokezi ya kishujaa, alipokelewa na detention kitu kilichowatia wazimu wajeshi ambao nao tarehe 18-20 Wakafanya Maasi na sasa ilikuwa ni zamu ya Julius kutoroshwa kwa boti kufichwa Zanzibar.Jaribio likazimwa, jeshi likavunjwa na kuundewa upiya chini ya Sarakikya.
Upande wa Zanzibar, ikumbukwe Karume (Mmalawi) hakushiriki physically aliwekwa tuu sasa aliwageuka wenzake akajipa madaraka yote in full na akawa hasikilizi tena ushauri wala cha mtu, ni yeye na Julius tuu.
Hata uamuzi wa kuungani aliufanya Karume sio kwa mapenzi na wabara, bali convenience ya usalama wa Zanzibar dhidi ya maadui nwa ndani, waliofanikisha mapinduzi na maadui wa nje, manowari ya Muingereza ulikuwa umeshatia nanga Lamu.

Baada ya Karume kujitwalia madaraka yote, yako maovu aliyoyafanya ambayo hata Julius hakuyaunga mkono, alisitisha utawala wa sheria, aliyonga kila aina ya wahalifu. Aliruhusu weusi wajitwalie vibinti vya kiarabu kwa kuwabaka, ikumbukwe baba zao ndio waliochinjwa wakati wa mapinduzi, no wonder kwa nini Wazanzibari wana jazba sana.

Ndipo mipango ya kumfix Karume ikafanywa ndani kwa ndani, azma iliyotimizwa 1972. Wako watu waliongamia akiwemo Shamte, baba wa Mwandishi/Mhariri wa Makala wa gazeti la Mwanachi na corespondent wa Sauti ya Ujerumani, Deustche Welle (Dochi Vella), Bi. Hawra Shamte.
Abdulrahaman Mohamed Babu na Col. Mahafudh waliepuka kifo kwa kukingiwa kifua na Julius, walitiwa kizuizini na kusalimishwa roho zao kwa Babu kukimbizwa uhamishoni London na Mahafudha kuchukuliwa na Samora.
Aliyekuwa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki na Makamo Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora, Mahafudha Hamid Alley maarufu kama Untie Ummie, ni binti wa Col. Mahafudh, na wanaomfahamu huyu mama kwa karibu, ni miongoni mwa wanawake wachache wa shoka toka visiwani Zanzibar wenye misimamo isiyotetereka kwa jambo wanaliamini.[/Q

huyu aunt ummie alley hana uhusiano kabisa na mahfoudh huyu ni mtoto wa mzee mmoja mwenye asili ya tabora (mnyamwezi) mohamed alley na mama mmoja mwenye asili ya kiarabu fatma ali al-marejb. mahfudha hamid alley ni dada wa baba na mama mmoja na dj chuchu pale znz.
 
I say, kwa kweli bado ninacheka mpaka leo na hizi postings za JF kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar. Ati Karume alikimbia Zanzibar! Karume alikimbia Zanzibar, nani tena jamani aliyapanga Mapinduzi? Hivyo haya maneno watu wanaandika kikweli kweli au ni sababu ya swaumu tu? Au sababu ya kushiba uji wa tapo? Tunaishi hapa hapa Tanzania na hatujui nani aliyapanga Mapinduzi ya Zanzibar na vipi yalitokea. Tutawaeleza nini watoto wetu na wajukuu zetu hapo baadae? Hii ni chuki ya Mapinduzi au kutokuja mambo?

Karume hakushiriki physically!!! Hahahahahahah. Wakitaka wamuone Karume anarusha mawe pale Darajani, hapo tena wangejua kuwa Karume kashiriki. Kuna ubaya gani ikiwa Kikwete hayupo tukamuona Sh. Ali Moh'd Shein anamkaimu Rais? Au tutasema Kikwete kakimbia? Sasa hio sio distribution of labour? Ukiwa wewe haupo mimi ninaendelea na kazi mpaka hali itakapokuwa nzuri na ukarejea?
Tunajua kuwa kama wangempata na kumuua Karume kabla ya Mapinduzi basi Mapinduzi yasingelitokea tena? Sio tumeshaona, baada ya 1972 imetokea nini Zanzibar zaidi ya uroho wa Jumbe wakuunganisha vyama for political gains ambazo alaidhania atazipata na hakuzipata, kwani Nyerere alimpiga ngwala.

Hivyo nikiuliza kwanini Mapinduzi yalitokea on Saturday nitaweza kupewa jibu hapa na hao wenye madarasa makubwa? Au jibu litakuwa kwasababu weekend askari wa Sultani walikuwa off? Au sitojibiwa kwasababu darasa langu ni dogo sana? Au kunijibu itakuwa ni sawa sawa na kumpigia gitaa mbuzi au ng'ombe????

No, really, tuacheni utani jamani, nauliza kweli kweli, tunajua kwanini Mapinduzi yalitokea on Saturday before Monday? Watoto wetu watakuja kutuuliza na tutawajibu nini? Nini kilikuwa kitokee on Monday kwenye Legico? Kuna mtu anaweza kumpigia gitaa mbuzi na tukasikia majibu yake?

Abdalla Said Natepe jamani mnamjua? Mpasuweni roho yake Natepe na mumtizame nani yupo rohoni kwake! Mtamkuta Karume. Karume na Natepe walikwa kama watu wawili waliozaliwa pacha.
Natepe akiitwa Karume-Yeka!!! Natepe awemo kwenye Mapinduzi bila ya Karume!!! This is IMPOSSIBLE!!!
Kwa wale wasiojua ni kuwa, the Zanzibar revolution of 1964 was an offspring of the political disturbances which took place in 1961. Mapinduzi ya Zanzibar yanatokana na ghasia za 1961. Mafanikio ya ghasia za 1961 zikawafanya wana-ASP kujua kumbe inawezekana na hapo tena ndio Karume akaambiwa asipinge matakwa ya Hizbu ya kutaka Uhuru by 1963!
Kama Karume kukimbia, basi angelikimbia 1961 na sio 1964.
Anyway, ikiwa mtu hata Auntie Ummie hamjui, sitegemei kama atamjua Karume au kuyajua Mapinduzi ya Zanzibar!
 
wandugu kusema kwamba marehemu Abeid Karume aliruhusu waafrika wawabake mabinti wa kiarabu itakuwa ni makosa na uzushi ,nafikiri wengi mnayajua mapinduzi yaliyotokea visiwani kupitia watu wenye chuki za kibinafsi na watu wa visiwani,ukweli wa mambo ni kuwa hayati Abeid Karume alijaribu kuondoa baadhi ya vikwazo vilivyokuwa vimewekwa na utawala wa kibaguzi wa waarabu,zamani kabla ya mapinduzi ilikuwa hairuhusiwi kwa mwafrika yeyote kumuoa binti wa kiarabu au kihindi huko visiwani na ndio maana alipojitwalia madaraka kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwachafua sultans kwa kuondoa sheria zao za kibaguzi dhidi ya waafrika ambao ndio wenye nchi yao.Alichokifanya Abeid Karume ilikuwa ni kuruhusu mwafrika yeyote yule kama kuna mtoto wa kiarabu au kihindi kampenda na anamtaka kumuoa aende report kwenye office maalum na atahahakikishiwa kuozeshwa huyo binti kwa hiari au kwa kutumia nguvu,wengi sana walijitwalia vibinti vya kiarabu kupitia njia hiyo mara baada ya kumtoa sultani visiwani.Wengi wenu hamjui nini sultani aliwatetendea watu weusi visiwani,huwezi kuamini kuwa visiwani enzi za sultani kulikuwa kama apartheid regime ya Africa Kusini,ubaguzi ulikuwa ni mtindo mmoja dhidi ya mtu mweusi na ndio maana hizo elements za kibaguzi zingine bado zinaendelea visiwani hadi leo,na hata hawa jamaa zetu wa visiwani hivi leo wengine chuki zao dhidi ya wabara zinashinikizwa na ubaguzi bado umo ndani ya damu zao hawa jamaa ni wabaguzi sana watakuthamini ka rangi yako ni brown ka ya baadhi yao na ukiwa ka mwenzangu mimi utabaguliwa kama kazi mbele yao huwezi kuthaminiwa mimi nimejionea mwenyewe hizi tabia za kurithi kutoka kwa Sultans,inasikitisha sana kuona kasumba kama hizi bado zinaendelea mpaka hivi leo.Utakuta mzanzibari mweusi hata kutushinda sisi wabara na bado atajinasibu kuwa yeye ana damu ya waarabu au wairani ni aibu tupu sisi waafrika tunaionyesha dunia,kuna kipindi kimoja kilikuwa kinaendeshwa na mmarekani mmoja mweusi kilionyeshwa jamaa alikwenda nchini Kenya sehemu za coastal region na alifanya mahojiano flani na jamaa wa swahili na walijinasibu kuwa wao sio waafrika walijinasibu kuwa wao ni wairani kabila la Shirazi,ni kweli labda walikuwa wana hiyo damu au back ground ya hiyo kabila lakini hiyo ni story ya zamani sana jamaa alishangaa sana kuwasikia wakisema kuwa wao sio waafrika,sasa tabia ka hizo ni bado zinaendelea mpaka leo visiwani na ndio maana hayati Karume na mzee Kambarage waliamua kuwapelekea jitu kama Okello kuwatisha waarabu ni kweli wengi walishindwa pigana baada ya kusikia jitu likiongea katika radio station ya visiwani kwa accent ya ajabu sana,jamaa ni ya kumleta ilikuwa ni kufanya intimidation dhidi ya waarabu.Kwa leo ni hayo tuu.
 
wandugu kusema kwamba marehemu Abeid Karume aliruhusu waafrika wawabake mabinti wa kiarabu itakuwa ni makosa na uzushi ,nafikiri wengi mnayajua mapinduzi yaliyotokea visiwani kupitia watu wenye chuki za kibinafsi na watu wa visiwani,ukweli wa mambo ni kuwa hayati Abeid Karume alijaribu kuondoa baadhi ya vikwazo vilivyokuwa vimewekwa na utawala wa kibaguzi wa waarabu,zamani kabla ya mapinduzi ilikuwa hairuhusiwi kwa mwafrika yeyote kumuoa binti wa kiarabu au kihindi huko visiwani na ndio maana alipojitwalia madaraka kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwachafua sultans kwa kuondoa sheria zao za kibaguzi dhidi ya waafrika ambao ndio wenye nchi yao.Alichokifanya Abeid Karume ilikuwa ni kuruhusu mwafrika yeyote yule kama kuna mtoto wa kiarabu au kihindi kampenda na anamtaka kumuoa aende report kwenye office maalum na atahahakikishiwa kuozeshwa huyo binti kwa hiari au kwa kutumia nguvu,wengi sana walijitwalia vibinti vya kiarabu kupitia njia hiyo mara baada ya kumtoa sultani visiwani.Wengi wenu hamjui nini sultani aliwatetendea watu weusi visiwani,huwezi kuamini kuwa visiwani enzi za sultani kulikuwa kama apartheid regime ya Africa Kusini,ubaguzi ulikuwa ni mtindo mmoja dhidi ya mtu mweusi na ndio maana hizo elements za kibaguzi zingine bado zinaendelea visiwani hadi leo,na hata hawa jamaa zetu wa visiwani hivi leo wengine chuki zao dhidi ya wabara zinashinikizwa na ubaguzi bado umo ndani ya damu zao hawa jamaa ni wabaguzi sana watakuthamini ka rangi yako ni brown ka ya baadhi yao na ukiwa ka mwenzangu mimi utabaguliwa kama kazi mbele yao huwezi kuthaminiwa mimi nimejionea mwenyewe hizi tabia za kurithi kutoka kwa Sultans,inasikitisha sana kuona kasumba kama hizi bado zinaendelea mpaka hivi leo.Utakuta mzanzibari mweusi hata kutushinda sisi wabara na bado atajinasibu kuwa yeye ana damu ya waarabu au wairani ni aibu tupu sisi waafrika tunaionyesha dunia,kuna kipindi kimoja kilikuwa kinaendeshwa na mmarekani mmoja mweusi kilionyeshwa jamaa alikwenda nchini Kenya sehemu za coastal region na alifanya mahojiano flani na jamaa wa swahili na walijinasibu kuwa wao sio waafrika walijinasibu kuwa wao ni wairani kabila la Shirazi,ni kweli labda walikuwa wana hiyo damu au back ground ya hiyo kabila lakini hiyo ni story ya zamani sana jamaa alishangaa sana kuwasikia wakisema kuwa wao sio waafrika,sasa tabia ka hizo ni bado zinaendelea mpaka leo visiwani na ndio maana hayati Karume na mzee Kambarage waliamua kuwapelekea jitu kama Okello kuwatisha waarabu ni kweli wengi walishindwa pigana baada ya kusikia jitu likiongea katika radio station ya visiwani kwa accent ya ajabu sana,jamaa ni ya kumleta ilikuwa ni kufanya intimidation dhidi ya waarabu.Kwa leo ni hayo tuu.



Acha kasumba mbovu hizo mimi binafsi babu yangu alikuwa ni muafrika na bibi yangu ni muarabu na walioana toka hata hayo mapinduzi hayana nia.
 
Au ulitaka mpaka wapanda minazi na washona viatu nawao waowe watoto wa kihindi?


Hii naona hata sasa hivi haiwezekani
 
Last edited:
wandugu kusema kwamba marehemu Abeid Karume aliruhusu waafrika wawabake mabinti wa kiarabu itakuwa ni makosa na uzushi ,nafikiri wengi mnayajua mapinduzi yaliyotokea visiwani kupitia watu wenye chuki za kibinafsi na watu wa visiwani,ukweli wa mambo ni kuwa hayati Abeid Karume alijaribu kuondoa baadhi ya vikwazo vilivyokuwa vimewekwa na utawala wa kibaguzi wa waarabu,zamani kabla ya mapinduzi ilikuwa hairuhusiwi kwa mwafrika yeyote kumuoa binti wa kiarabu au kihindi huko visiwani na ndio maana alipojitwalia madaraka kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwachafua sultans kwa kuondoa sheria zao za kibaguzi dhidi ya waafrika ambao ndio wenye nchi yao.Alichokifanya Abeid Karume ilikuwa ni kuruhusu mwafrika yeyote yule kama kuna mtoto wa kiarabu au kihindi kampenda na anamtaka kumuoa aende report kwenye office maalum na atahahakikishiwa kuozeshwa huyo binti kwa hiari au kwa kutumia nguvu,wengi sana walijitwalia vibinti vya kiarabu kupitia njia hiyo mara baada ya kumtoa sultani visiwani.Wengi wenu hamjui nini sultani aliwatetendea watu weusi visiwani,huwezi kuamini kuwa visiwani enzi za sultani kulikuwa kama apartheid regime ya Africa Kusini,ubaguzi ulikuwa ni mtindo mmoja dhidi ya mtu mweusi na ndio maana hizo elements za kibaguzi zingine bado zinaendelea visiwani hadi leo,na hata hawa jamaa zetu wa visiwani hivi leo wengine chuki zao dhidi ya wabara zinashinikizwa na ubaguzi bado umo ndani ya damu zao hawa jamaa ni wabaguzi sana watakuthamini ka rangi yako ni brown ka ya baadhi yao na ukiwa ka mwenzangu mimi utabaguliwa kama kazi mbele yao huwezi kuthaminiwa mimi nimejionea mwenyewe hizi tabia za kurithi kutoka kwa Sultans,inasikitisha sana kuona kasumba kama hizi bado zinaendelea mpaka hivi leo.Utakuta mzanzibari mweusi hata kutushinda sisi wabara na bado atajinasibu kuwa yeye ana damu ya waarabu au wairani ni aibu tupu sisi waafrika tunaionyesha dunia,kuna kipindi kimoja kilikuwa kinaendeshwa na mmarekani mmoja mweusi kilionyeshwa jamaa alikwenda nchini Kenya sehemu za coastal region na alifanya mahojiano flani na jamaa wa swahili na walijinasibu kuwa wao sio waafrika walijinasibu kuwa wao ni wairani kabila la Shirazi,ni kweli labda walikuwa wana hiyo damu au back ground ya hiyo kabila lakini hiyo ni story ya zamani sana jamaa alishangaa sana kuwasikia wakisema kuwa wao sio waafrika,sasa tabia ka hizo ni bado zinaendelea mpaka leo visiwani na ndio maana hayati Karume na mzee Kambarage waliamua kuwapelekea jitu kama Okello kuwatisha waarabu ni kweli wengi walishindwa pigana baada ya kusikia jitu likiongea katika radio station ya visiwani kwa accent ya ajabu sana,jamaa ni ya kumleta ilikuwa ni kufanya intimidation dhidi ya waarabu.Kwa leo ni hayo tuu.


Dear Ndugu Karenga
, nime-click THANKS button mara 3, lakini naona haitoshi. You really made my day today na kwahivyo unanidai crate moja la beer. I am NOT joking! Na kama unafunga mwezi huu mtukufu basi futari kwangu mpaka ishe hii Ramadhani. Tafadhali tuwasiliane privately kwasababu naona I can do business with you! If you think I am joking basi utakula hasara wewe mwenyewe. I am damn serious!
Wazanzibari wamejaa mayaani mengi. Hawamalizi neno moja lazima watatia YAANI au YAKHE. Kiswahili chao wakizungumza inakuwa kama wanaimba. Mimi kwa kweli hufurahi nikizungumza nao na wakati mwengine hutaka niwarekodi ili niwasikilize tena na tena baadae. Kwa hilo ninawasifu sana. Nami kama ningelikuwa ninazungumza kiswahili chao basi ningeliringa sana tena sana hapa nchini. Hii ndio maana kila leave ni lazima niende Zanzibar kutembea. Juu ya hivyo, lakini kwenye mapinduzi inatakiwa sauti ya simba - ile ya kutisha kama baragumu. Kama angepewa Natepe position ya Okello basi kila mtu asingeliamini kama mapinduzi yametokea. Watu mitaani Darajani wangekuwa wanajiuliza....YAKHE NANI HUYU - YAANI HUYU ALIYETANGAZIA??? Hii ndio maana ikabidi awekwe mbele mtu mwenye kiswahili kama cha Okello. Hapo Karenga umesema sawa kabisa na hivyo ndivyo ilivyokuwa. In fact, kiswahili chake Okello hakikuwa kibaya hivyo, lakini aliambiwa akifanye kiwe na accent mbaya zaidi ili waarabu washituke na wasijue huyu jamaa ni nani na anatoka wapi. Ninastaajabu wewe Mtanganyika mwenzangu umeyajua wapi haya, kwani hizi ni habari za ndani kabisa! Au mwenzetu unakaa Ilala? Au umeoa Visiwani? Kama ni hivyo nami nitafutie mchumba kutoka Visiwani ili nipate kufundishwa kiswahili!
Kwa siku zile kama mtu babu yake kaoa mwarabu basi hio ilikuwa ni kitu cha ajabu sana - ilikuwa ikitokea lakini ilikuwa ni nadra sana. Hapa tunazungumzia general trend iliyokuwepo siku zile. Kwani hata huko South Africa siku zile za apartheid mwaafrika mmoja katika milioni alioa mzungu. Basi na huyo babu yake rafiki yako (Dos.2020) ndio ilikuwa hivyo hivyo.
Karenga, yale uliyoyaeleza sio kasumba. Ni vizuri kuyasahau, lakini tusiyadharau ili yasije kutokea tena, kwani sote ni binaadamu na sote mbele ya Muumba ni sawa!
Vipi sasa crate lako? Ukichelewa sana offer itakufa. Kazi kwako. Nitafute kwa haraka!
 
Au ulitaka mpaka wapanda minazi na washona viatu nawao waowe watoto wa kihindi?
Hii naona hata sasa hivi haiwezekani


Kwanini mpanda minazi au mshona viatu asioe mtoto wa kihindi kama wamependana?
Kushona viatu au kupanda minazi sio kazi tu? Dume la kweli lachagua kazi?
Hujui mpanda minazi (Saidi Washoto) na mshona viatu (Seif Bakar Omar) ndio waliokuokoa wewe tarehe 12 January, 1964 mpaka leo ukawa unaweza kusema uyatakayo?
45 years of liberation have passed, but your mind is still living under the delirium of enslavement!
Siamini kuwa bado mnawaona wahindi ni bora kuliko wengine mpaka hii leo.
Huko kwenu inaonesha kazi Karume hakuimaliza (bado ipo), lakini sijui nani ataimaliza kazi hio. CUF????? Sidhanii. Labda waifanye kuwa ngumu zaidi!
 
ngida eti kweli katika hili pilikapilika la kuoa kinguvu,Thabit kombo alioa mdosi kwa nguvu.waziri mkuu wa india akamuomba nyerere aingilie ili swala la watu kuozeshwa kinguvu-to the dismay of the world nyerere was powerless kumwambia strongman karume anything
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom