Watakaoingia choo cha kike ni hao watakaokimbilia hizo unaziita Ai na watakuja kulia muda si mrefu
Unaposema app ni ndogo haina maana unamaanisha nini? Nini kinafanya app hii uione ndogo na hii ni kubwa?
Ni mara ngapi hiyo Facebook Yenyewe inadukuliwa pamoja na ulinzi wake wote?
Siwezi kutoa hela mwanangu akasome coding, bora nimfundishe kuzalisha funza
Hakuna platform ambayo ni 100% attack free kwasababu zimeundwa na binadamu na ni binadamu wanaokuja na mbinu mpya za kufanya attacking.
Lakini security iliyoandikwa na coder hailingani na iliyowekwa na drag and drop. Hata jf japo unanunua software, ila ndio maana kuna coders wanafanya matekebishi ya codes kuimprove security.
App ndo ni zile zinafanya vitu basic tu. Mfano uuende tovuti static kwa drag and drop.
Huwezi kuunda platform kama ya mpesa kwa drag and drop.
Drag ans drop haiwezi kukupa kitu exactly kama unavyotaka kifunction hata kwenye uunzi wa website.
Lazima uchape code. Na ndio maana hata kuchapa code kuna watu hata hawataki matumizi ya frameworks pia wanataka kila kitu wakiunde wenyewe waimplement security, performance and execution.
AI kwanini useme watalia? AI ni future ya vitu vingi inakuwa intergrated kwenye devices na vifaa vingi. Models mbalimbali za AI zinakuwa developed kufanya vitu tofauti.
Jana nilikuwa natazama demo ya bot fulani ya microsoft, unaiandikia aina ya mziki unaotaka inaandika lyrics na kukuunda mziki in a matter of seconds.
Mimi ni.mpenzi wa miziki ya EDM, niliambia iniundie nyimbo ambazo zinasound kama faded kwa kuelezea nataka ianze na nini, lyrics ziweje na vitu kama hivyo ikaunda nyimbo kadhaa ambapo 3 waimbaji walikuwa sauti ya ike na 2 sauti za kiume.
Hii ni early stage ya AI, zinaenda kubadilisha mambo mengi