Nimemuona kijana naye mtambua kwenye picha! Nikamuuliza, hivi ni kitu gani kinachokupeleka coco beach wakati madhari yake haina mvuto hata kidogo! Akanijibu, "mimi naijua coco beach! kuanzia naijua mpaka leo iko hivyo hivyo, kwani inatakiwa iwaje? Na mimi nikamjibu kwa swali iko hivyo hivyo manayake nini? watu kibao ila bei za vitu na usafiri ndivyo vinakuwa shida! Nikamuuliza vipi kuhusu mazingira unaridhika nayo? Akaniuliza kivipi yaani? Nikafafanua, na maanisha mahali pa kukaa, usafi, ulinzi? Akanijibu! Duh! hayo mambo yenu nyie sasa! Koko ni kivyako vyako na washikaji kula gudtimes basi, tena ukifanikisha kufika ni mtoko babukubwa, hayo ya mazingira mi siyaoni!
Nilishtushwa sana na jibu lake, maana, unavyoona mabaya kila siku, kunawatu wanaochukulia kwamba ni hali halisi. Wanaizoe, na wanaacha kuiona!