Clouds FM Michezo: Kiswahili- Kiingereza cha nini?

Clouds FM Michezo: Kiswahili- Kiingereza cha nini?

Clouds ni redio ya kitapeli iliyokosa ubunifu, wao ni kuangalia east africa radio wanafanya nini na wao waige,
 
hiyo redio siipendi sana watangazaji wake hawana nidhamu na maadili muda wowote wanaweza ropoka chochote cha ovyo(matusi) wanadhan wasikilizaji wote ni wavuta bangi
 
Hii tabia ipo sana miongoni mwetu watanzania! Kama jana nimekaa nakuangalia Bongo Star Search nikasikia Jaji Master J anamwambia mshiriki kua umevaa vizuri na umecheza vizuri lakini huna Chemistry! Sasa mbongo katokea Gongo la Mboto elimu yake darasa la saba kaja Bongo Star Search kutafuta atoke kimaisha kwanini usimpe mtu maksi kwakuongea kiswahili na sisi tulioko huku nnje kwenye Luninga tukawaelewa???:frusty:
 
acheni kusikiliza mmelazimishwa

au wafungue redio zao makini zisizo na kasoro......wasichojua hicho ambacho clouds fm wanakosea{kwa mujibu wa haters} ndio kinaifanya clouds fm iwe clouds fm.....acheni kusikiliza waacheni na upuuzi wao....mtabaki mnapiga majungu wenzenu wana-make millions kwa huo mnaoita ujinga.......
 
Kwa nini achanganye language wakati he knows kuwa most of his wasikilizaji hawako conversant na hiyo foreign language?

Hata Ww nmeona msamiati mpya wa Language Kwenye maandish yako.punguzeni chuki Jamani....ss we nå wao mmetofautiana nn
 
Watu kama hao ukiwaambia waongee kiingereza kitupu utaona wanavyombwelambwela
 
jamani vipi wanaoandika humu jf nyuzi za kiswanglish hamuzioni mmewashupalia tu hao. vp wale dada zetu na kaka zetu wa bongo muvi?
 
Jeff ana kimombo cha kisoka kitam mno. Kikubwa hutumia kiingereza kulingana na matamko yalivyo kweny sheria za kimataifa. Mfano.. Indirect au direct freekick, back four defenders, cetral midfilder, defensive au attacking midfilders. Binafsi huwa napenda sana hii mutu. Mda fulan kuendekeza saana kiswahili ni uswahili wa kijinga.
 
Hata Ww nmeona msamiati mpya wa Language Kwenye maandish yako.punguzeni chuki Jamani....ss we nå wao mmetofautiana nn

Ndio nini hapo kwenye nyekundu? Au una haraka sana ya kwenda wapi ilhali tupo humu humu kwenye jamvi.
 
Anayechanganya lugha ni Jeff.Yule ni mkenya
Huyu jamaa ANAKERA mno, lakini mbona Wakenya wanajitahidi kuongea lugha moja tu wakati mmoja? Ni nadra mno kuwasikia wakichanganya lugha hizi mbili wakati mmoja. Huyu jamaa ni punguwani tuu maana hata maneno rahisi mno ya kiswahili na anayafahamu lakini yeye atalisema kwa kiingereza. Nahisi anajiona ni ufahari.
 
Niliisha tupia uzi humu kuhusu majina ya vijiradio vyetu na baadhi ya vipindi kuwa na majina ya kiingereza wakati lugha inayozungumwa na wengi (wasikilizaji) ni kiswahili. Hii haina tofauti na filamu zetu kwa kuwa na majina ya kiingereza huku lugha ya wasanii ni kiswahili.
 
Back
Top Bottom