Wachambuzi wa Michezo Radio za FM acheni kuchanganya lugha, mnajiabisha

Vyamavingi

JF-Expert Member
Oct 3, 2014
5,745
5,446
Hizi tabia za wachambuzi na watangazaji wa michezo vya asubuhi kwa Wasafi FM na E FM kuchanganya lugha za Kiswahili na Kiingereza linakera sana. Kwanza wengi wao hata Kiingereza hawujui, wanachanganya 'tenses' na kwa anayejua Kiingereza masikio yanawasha na kwa wale wanaojifunza Kiingereza wanaishia kupotoshwa.

Tabia hii wamekuwa nayo kwa muda mrefu sana, hasa baadhi yao kwenye Wasafi FM. Kama mnataka kuchanganya lugha ili muonekane wajuvi basi jifunzeni kwanza lugha yenyewe kabla ya kuja 'kuchapia' mkiwa hewani. Au basi jifunzeni kwa Jeff Lea, ambaye akiamua kuchokea Kiingereza anakuwa anaitumia kwa kwa misemo murua na sahihi ya kugha hiyo.

Tafadhalini sana, mjiepushe kutumia maneno ya Kiingereza ambayo mnachanganya 'tenses' na kuishis kujidhalilisha ninyi wenyewe na redio zenu.

Vv
 
Fikra za kitumwa tu hizo kuona kua lugha fulani ambayo sio yako ni bora kuliko lugha yako,au kuamini kua kuongea Kiingereza ndio maendeleo au ndio kipimo cha elimu,

Hii tabia ipo mpaka kwa wasanii wanapohojiwa,ukisikiliza mahojiano ya TID unaweza kudhani kua huyu jamaa Kiswahili ameanza kukisahau kwa kukaa sana nchi za wazungu kimawazo sio kimwili.
 
Hizi tabia za wachambuzi na watangazaji wa michezo vya asubuhi kwa Wasafi FM na E FM kuchanganya lugha za Kiswahili na Kiingereza linakera sana. Kwanza wengi wao hata Kiingereza hawujui, wanachanganya 'tenses' na kwa anayejua Kiingereza masikio yanawasha na kwa wale wanaojifunza Kiingereza wanaishia kupotoshwa.

Tabia hii wamekuwa nayo kwa muda mrefu sana, hasa baadhi yao kwenye Wasafi FM. Kama mnataka kuchanganya lugha ili muonekane wajuvi basi jifunzeni kwanza lugha yenyewe kabla ya kuja 'kuchapia' mkiwa hewani. Au basi jifunzeni kwa Jeff Lea, ambaye akiamua kuchokea Kiingereza anakuwa anaitumia kwa kwa misemo murua na sahihi ya kugha hiyo.

Tafadhalini sana, mjiepushe kutumia maneno ya Kiingereza ambayo mnachanganya 'tenses' na kuishis kujidhalilisha ninyi wenyewe na redio zenu.

Vv
Usipoteze muda kaka. Hawa ndio wale WAANDISHI na WACHAMBUZI TAKATAKA
 
Usipoteze muda kaka. Hawa ndio wale WAANDISHI na WACHAMBUZI TAKATAKA
Wanaharibu sana lugha za watu, Kiingereza hawajui na Kiswahili hawajui yaani taabu tupu. Unakuta anasema 'hii nyimbo' badala ya huu wimbo! Yaani hadi unajiuliza , hivi huyu ni Mtanzania au anatokea nchi jirani?

Vv
 
Na siku za hivi karibuni, hizi redio zimegundua vipindi vya michezo vinasikilizwa sana. Kwahiyo wameamua kuviongezea muda mrefu, hawajui kuwa vingine vitakuja kuchosha watu. Na hii ni kwasababu ya kuchukua watu kwa kujuana kisa anajua majina ya wachezaji au anaongea sana kwenye vibanda umiza. Na mbaya zaidi, utakuta kipindi kimoja kina wachambuzi zaidi ya watatu au wanne. Vurugu tupu. Zamani tbc robo saa tu, kipindi cha michezo watu walikuwa hawakikosi. Yaani ukiskia ule wimbo tu, unajua hii ni saa mbili kasoro. Na ukikikosa hadi unajiskia vibaya. Saizi ni takataka tupu.
 
Back
Top Bottom