Inawezekana ni kweli lakini sidhani kama ni kweli mara zote.
Wakati mwingine watu hutamka maneno ambayo hata hawamaanishi [ambayo yanaweza kupokelewa visivyo].
Mfano, hujawahi kuona watu waliokasirishana na kila mmoja akimwambia mwenzake 'ntakuua wewe'?
Kweli unadhani watu kama hao huwa wanawaziana kuuana ila huwa wanashindwa kuambiana hadi wapatapo fursa ya kupishana Kiswahili?
Kwa kawaida, mtu akishapandwa na ghaidhi akili huwekwa kando na hisia hushika hatamu.
Sasa katika hali kama hiyo, watu hujikuta wakiongea maneno mengi tu ambayo hata hawamaanishi lakini zipo nyakati ambazo hutokwa na maneno ambayo wanamaanisha.
Ugumu upo kwenye kutenganisha yepi ni yepi na ndo hapo jinsi ya yanavyopokelewa na walengwa kunaingia kwenye mlinganyo.
Kwa mintarafu hiyo basi, ndo umuhimu wa kuchunga kauli unapokuja maana huwezi jua mlengwa wako atapokeaje hicho ulichokilenga kwake.
Zipo kauli ambazo huweza kujeruhi na kuacha kovu la muda mrefu kwenye hisia za mtu. Na mtu akishakuwa na kovu la hisia ni vigumu sana kurudia hali iliyokuwepo kabla ya.