Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,648
- 698,190
. CHUMVI YA ULIMWENGU
. NURU YA ULIMWENGU
Vitu hivi ni muhimu sana kwa mustakabali wa Maisha ya Mwanadamu
Mathayo 5:13 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.
Yesu anatuita sisi ni CHUMVI ya DUNIA! Kazi ya CHUMVI ni kutia ladha kwenye CHAKULA, na haihitajiki Chumvi nyingi ili kukifanya Chakula kiwe kitamu
Chakula hicho, hakiwezi kutamanika na kuliwa na watu, japo ni kizuri, ikiwa CHUMVI sisi tumeharibika! Yesu ametuita CHUMVI na siyo SUKARI kwa sababu CHUMVI haina gharama kubwa, na matumizi yake ni mengi.
Chumvi ya tsh 500 Unaweza kuitumia Wiki nzima, kwenye FAMILIA ya watu 10, Lakini Sukari ya tsh 2800 Huwezi kuitumia kwa wiki nzima kwenye FAMILIA ya watu 6 kuna watu VIJIJINI chai, Hawanyi, lakini wanapika MBOGA, wanahitaji CHUMVI, wakipika Wali, wanahitaji Chumvi, Wakikaanga CHAPATI, wanahitaji Chumvi, Wakipika Makande, Maharage, Choroko, Wanahitaji CHUMVI, nyama ya Kuku, Maini, na uzuri wake, hata Ukiirost vipi, usipoitia CHUMVI, chakula hakitanoga kabisa.
Mathayo 5:14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Matendo yetu, yawe Nuru, Yawe Chumvi kwa watu, wapate kumtukuza MUNGU, kupitia sisi, Mungu hajataka yeye mwenyewe kushuka, ili kuja kuwafanya watu wamjue yeye, bali ametuweka sisi tumwakilishe kwa watu wake, MATENDO yetu yawe Nuru, ya kuwatoa watu gizani. yawe Chumvi ya kuwapa watu ladha ya kumjua BWANA YESU KRISTO.
Badala yake tumegeuka na kuwa CHUMVI iliyoharibika, tukizani kwamba, watu wanapendezewa nasi, kumbe huko wanamuona Kristo ni asiyefaa, aliyeshindwa Kutufanya sisi tuwe safi, Je! atawezaje kuwafanya wao kuwa SAFI? ikiwa Chumvi wewe, Nuru wewe, Unashiriki, UZINZI, ULEVI, KIBURI, UCHAWI, UASHERATI, ULAWITI, UFIRAJI, UJAMBAZI, USENGENYAJI, hivi utaweza kuwamurikia Nuru wengine wakati umeshageuka na kuwa GIZA? Kristo anatazamwa uwezo na nguvu yake kupitia wewe, kama ilivyo kwa CHAKULA, utamua wa Chakula unajulikana kupitia CHUMVI!
Wakati mwingine Chumvi wewe usijiweke sawa na Chakula utaharibu ladha, usijifanye kuwa Sawa na Kristo, UTUKUFU wa Yesu, usiubebe wewe, Utageuka Chakula kilichozidi CHUMVI, na kuwafanya watu KUUGUA SAFURA. naamaanisha usiweke mbwembwe kwenye Suala zima la UTUMUSHI.
Kama hukuwa unajua kuwa, hayo ambayo unafanya siyo sawa, basi geuka sasa! Uwe Chumvi kweli na Nuru kweli, maana tunaambiwa.
2 Korintho 3:2 Ninyi ndinyi barua yetu, iliyoandikwa mioyoni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote;
3 Mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoikatibu, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.
Na watu wengi bado hawajajua umuhimu wa CHUMVI, siku Chumvi ikiwa ADIMU kama ilivyotokea kwa Sukari hapa kwetu TANZANIA! watakuja kuona umuhimu wake, ndivyo itakavyokuwa kwa Kanisa la Kristo, litakapoondolewa,
Jr
. NURU YA ULIMWENGU
Vitu hivi ni muhimu sana kwa mustakabali wa Maisha ya Mwanadamu
Mathayo 5:13 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.
Yesu anatuita sisi ni CHUMVI ya DUNIA! Kazi ya CHUMVI ni kutia ladha kwenye CHAKULA, na haihitajiki Chumvi nyingi ili kukifanya Chakula kiwe kitamu
Chakula hicho, hakiwezi kutamanika na kuliwa na watu, japo ni kizuri, ikiwa CHUMVI sisi tumeharibika! Yesu ametuita CHUMVI na siyo SUKARI kwa sababu CHUMVI haina gharama kubwa, na matumizi yake ni mengi.
Chumvi ya tsh 500 Unaweza kuitumia Wiki nzima, kwenye FAMILIA ya watu 10, Lakini Sukari ya tsh 2800 Huwezi kuitumia kwa wiki nzima kwenye FAMILIA ya watu 6 kuna watu VIJIJINI chai, Hawanyi, lakini wanapika MBOGA, wanahitaji CHUMVI, wakipika Wali, wanahitaji Chumvi, Wakikaanga CHAPATI, wanahitaji Chumvi, Wakipika Makande, Maharage, Choroko, Wanahitaji CHUMVI, nyama ya Kuku, Maini, na uzuri wake, hata Ukiirost vipi, usipoitia CHUMVI, chakula hakitanoga kabisa.
Mathayo 5:14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Matendo yetu, yawe Nuru, Yawe Chumvi kwa watu, wapate kumtukuza MUNGU, kupitia sisi, Mungu hajataka yeye mwenyewe kushuka, ili kuja kuwafanya watu wamjue yeye, bali ametuweka sisi tumwakilishe kwa watu wake, MATENDO yetu yawe Nuru, ya kuwatoa watu gizani. yawe Chumvi ya kuwapa watu ladha ya kumjua BWANA YESU KRISTO.
Badala yake tumegeuka na kuwa CHUMVI iliyoharibika, tukizani kwamba, watu wanapendezewa nasi, kumbe huko wanamuona Kristo ni asiyefaa, aliyeshindwa Kutufanya sisi tuwe safi, Je! atawezaje kuwafanya wao kuwa SAFI? ikiwa Chumvi wewe, Nuru wewe, Unashiriki, UZINZI, ULEVI, KIBURI, UCHAWI, UASHERATI, ULAWITI, UFIRAJI, UJAMBAZI, USENGENYAJI, hivi utaweza kuwamurikia Nuru wengine wakati umeshageuka na kuwa GIZA? Kristo anatazamwa uwezo na nguvu yake kupitia wewe, kama ilivyo kwa CHAKULA, utamua wa Chakula unajulikana kupitia CHUMVI!
Wakati mwingine Chumvi wewe usijiweke sawa na Chakula utaharibu ladha, usijifanye kuwa Sawa na Kristo, UTUKUFU wa Yesu, usiubebe wewe, Utageuka Chakula kilichozidi CHUMVI, na kuwafanya watu KUUGUA SAFURA. naamaanisha usiweke mbwembwe kwenye Suala zima la UTUMUSHI.
Kama hukuwa unajua kuwa, hayo ambayo unafanya siyo sawa, basi geuka sasa! Uwe Chumvi kweli na Nuru kweli, maana tunaambiwa.
2 Korintho 3:2 Ninyi ndinyi barua yetu, iliyoandikwa mioyoni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote;
3 Mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoikatibu, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.
Na watu wengi bado hawajajua umuhimu wa CHUMVI, siku Chumvi ikiwa ADIMU kama ilivyotokea kwa Sukari hapa kwetu TANZANIA! watakuja kuona umuhimu wake, ndivyo itakavyokuwa kwa Kanisa la Kristo, litakapoondolewa,
Jr