Chumba changu kaingia nyoka sijui ameingia saa ngapi msaada

Mmwagie maji ya upako alegee.
 
Anatafuta madini adimu yaitwayo panya
Sahihi .viumbe wanaotakiwa kudhibitiwa ni panya huweza leta nyoka ndani,wadudu mbali mbali ndani ya nyumba huvutia mijusi ndani ya nyumba ukiwamaliza mijusi huwezi ona
 
Kipindi hicho vidudu kama hivyo vikiingia geto kama ni usiku wala sihangaika, nalala usingizi wangu kesho nikiamka nakishughulikia bila kumwaga mwaga sijui vimafuta mara vioil. Hivi vitu kama hujawahi kuishi navyo maporini huwezi kulala Wala kushuka kitandani. Pole sana. Naamini wadau washatoa solution huko juu.
 
Huyapoo 🐍 kimbiaaaaaaaaa🤣
 
Mkuu! Wewe ni wakike au kiume?
Kama ni wa kiume, kwa hali hii - twafaa.
 
Nyumba unayokaa itakuwa na panya au mijusi wengi. Sehemu ya jikondipo panya wanapokuwa katika saa hizo ulizotaja, hivyo nyoka alikuwa mawindoni. Nyoka wanasikia harufu ya panya hata wakiwa kilomita nzima away. Jiongezeni kuanzia hapo mfanye fumigation na muwe wasafi.
 

Kuna yule mwamba wa sauzi na baby work ulihitaji huduma yao.

Kaingiaje uwezekano milango yako haikabi vyema chini baina yake na sakafu.

Rekebisha hilo haraka.

Kama vitu ni vingi hiyo changamoto ila usiogope yeye pia anakuogopa hawezi kukusaka wewe bali atajificha.

Kama hauna watoto hapo potezea umtafute pole pole utakapokuwa wapanga vitu.

Ila kuwa mwangalifu.
 
Usimsumbue, wewe lala na usingizi wako na yeye alale na usingizi wake ila kama unakisungura kifungue kimwage kwenye kisahani anywe alewe.
 
Mrejesho

Sikupata usingizi tangu huo mda, Asubuhi nimetafuta mafuta ya taa nikamwaga Kila Kona nikaanza kufanya usafi nikamkuta hata kutembea hawezi nimemuua, Asanteni kwa mawazo mazuri

Nb. Nyie wengine mnaosema sijui wew kama mwanaume unaogopaje nyoka vitu vingine havihitaji sifa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…