Chuki ni sumu

Chuki ni sumu

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,041
Reaction score
1,294
Chuki ni mzigo usioonekana unaokula nafsi kimya kimya

Kuna uchungu wa aina fulani huwezi kuupiga picha. Uchungu wa mtu anayebeba chuki moyoni...

Chuki haina kelele, lakini ina sumu...

Ni moto unaowaka ndani kimya kimya, ukiunguza kila chembe ya amani uliyonayo.

Ukimchukia mtu si yeye anayeteseka ni wewe...

Yeye anaendelea na maisha yake, anacheka, anafurahi, hata hajui unavyohisi..

Lakini wewe... kila ukimuona, moyo unaenda kasi Ukisikia jina lake, hasira inakujaa.
Ukiona mafanikio yake, unajisikia uchungu na mpweke.

Chuki haimbadilishi yule unayemchukia. Inakubadilisha wewe. Inakufanya ushindwe kupumua kwa amani.
Inakufanya ushindwe kusamehe. Inakufunga kwenye gereza la hisia zako mwenyewe.

Ni kama kunywa sumu na kutarajia mtu mwingine afe.

Mioyo yetu haiwezi kuhifadhi chuki kwa muda mrefu bila kupasuka.

Kwa hiyo, unapobeba chuki ni nafsi yako unaiadhibu, naua furaha yako, unasumbua akili yako, unachelewesha safari yako.

Wengine wanaweza wasistahili msamaha wako. Wewe unastahili amani yako.

Na mara nyingine, njia pekee ya kuipata… ni kuacha kubeba chuki. isiyo na maana
Abuuabdillah ✍️
0744883353
 

Attachments

  • 22545a6aa062ffffa775e4710cf1ad49.jpg
    22545a6aa062ffffa775e4710cf1ad49.jpg
    33.9 KB · Views: 17
Chuki ni mzigo usioonekana unaokula nafsi kimya kimya

Kuna uchungu wa aina fulani huwezi kuupiga picha. Uchungu wa mtu anayebeba chuki moyoni...

Chuki haina kelele, lakini ina sumu...

Ni moto unaowaka ndani kimya kimya, ukiunguza kila chembe ya amani uliyonayo.

Ukimchukia mtu si yeye anayeteseka ni wewe...

Yeye anaendelea na maisha yake, anacheka, anafurahi, hata hajui unavyohisi..

Lakini wewe... kila ukimuona, moyo unaenda kasi Ukisikia jina lake, hasira inakujaa.
Ukiona mafanikio yake, unajisikia uchungu na mpweke.

Chuki haimbadilishi yule unayemchukia. Inakubadilisha wewe. Inakufanya ushindwe kupumua kwa amani.
Inakufanya ushindwe kusamehe. Inakufunga kwenye gereza la hisia zako mwenyewe.

Ni kama kunywa sumu na kutarajia mtu mwingine afe.

Mioyo yetu haiwezi kuhifadhi chuki kwa muda mrefu bila kupasuka.

Kwa hiyo, unapobeba chuki ni nafsi yako unaiadhibu, naua furaha yako, unasumbua akili yako, unachelewesha safari yako.

Wengine wanaweza wasistahili msamaha wako. Wewe unastahili amani yako.

Na mara nyingine, njia pekee ya kuipata… ni kuacha kubeba chuki. isiyo na maana
Abuuabdillah ✍️
0744883353
Mkuu umeandika uzi mzuri mpaka nikakumbuka ile JF ya enzi zile.

Siku hizi nyuzi za aina hii huwezi kuzikuta humu.

Cc: Monetary doctor Nomadix.
 
Mkuu umeandika uzi mzuri mpaka nikakumbuka ile JF ya enzi zile.

Siku hizi nyuzi za aina hii huwezi kuzikuta humu.

Cc: Monetary doctor Nomadix.
Hakika ametukumbusha jambo jema, chuki ni sumu kali sana inaua polepole, inadhoofisha kila kiungo, moyo uliobeba chuki unafubaa na kusinyaa.

Shukrani kwa uzi bora wa weekend.
 
Hakika ametukumbusha jambo jema, chuki ni sumu kali sana inaua polepole, inadhoofisha kila kiungo, moyo uliobeba chuki unafubaa na kusinyaa.

Shukrani kwa uzi bora wa weekend.
Jamaa kanikumbusha zile nyuzi za JF za zamani zilizojaa madani adhimu kwelikweli.
 
Ni kweli aisee. Juzi kati ilitokea nikalazimika kuongea na ex-wife kuhusu masuala ambayo ilikua lazima tuzungumze.

Aisee, she sounded so very bitter, very angry, she blasted very nasty words on me, mpaka nikajiuliza huyu mama ndio kusema kajeruhika na hii ishu ambayo ni yeye ali initiate. Mimi niliyeumizwa na kuoita kwenye phase mbali mbali (anger, resentiment, chuki, kuhisi kisasi) mpaka nikapona kwa kuamua kuachilia vyote inakuaje am soo cool namna hii halaf yeye kapanic hivi??

Nikagundua huyu chuki inamtesa sana. Nikamwambia kwaheri, nikakata simu baada ya kuwa straight kwenye kile nilichompigia na kuongea nae.

Chuki inatesa wakuu nakubaliana na wewe.
 
Chuki ni mzigo usioonekana unaokula nafsi kimya kimya

Kuna uchungu wa aina fulani huwezi kuupiga picha. Uchungu wa mtu anayebeba chuki moyoni...

Chuki haina kelele, lakini ina sumu...

Ni moto unaowaka ndani kimya kimya, ukiunguza kila chembe ya amani uliyonayo.

Ukimchukia mtu si yeye anayeteseka ni wewe...

Yeye anaendelea na maisha yake, anacheka, anafurahi, hata hajui unavyohisi..

Lakini wewe... kila ukimuona, moyo unaenda kasi Ukisikia jina lake, hasira inakujaa.
Ukiona mafanikio yake, unajisikia uchungu na mpweke.

Chuki haimbadilishi yule unayemchukia. Inakubadilisha wewe. Inakufanya ushindwe kupumua kwa amani.
Inakufanya ushindwe kusamehe. Inakufunga kwenye gereza la hisia zako mwenyewe.

Ni kama kunywa sumu na kutarajia mtu mwingine afe.

Mioyo yetu haiwezi kuhifadhi chuki kwa muda mrefu bila kupasuka.

Kwa hiyo, unapobeba chuki ni nafsi yako unaiadhibu, naua furaha yako, unasumbua akili yako, unachelewesha safari yako.

Wengine wanaweza wasistahili msamaha wako. Wewe unastahili amani yako.

Na mara nyingine, njia pekee ya kuipata… ni kuacha kubeba chuki. isiyo na maana
Abuuabdillah ✍️
0744883353
FB_IMG_1744636371284.jpg
 
Maybe uko mbeleni

Kwahiyo boss ulipomsamehe ulikula tamu?🤔
Navyozungumzia kusamehe namaanisha, kutoweka chuki na kuamua kuchukulia as if huyu mtu hajanikosea kitu na kisha nikaendelea na maisha yangu hakuna tena mahusiano wala kurudia maisha ya kwanza.

Not every forginess deserves reconsiliation.
 
Ni kweli aisee. Juzi kati ilitokea nikalazimika kuongea na ex-wife kuhusu masuala ambayo ilikua lazima tuzungumze.

Aisee, she sounded so very bitter, very angry, she blasted very nasty words on me, mpaka nikajiuliza huyu mama ndio kusema kajeruhika na hii ishu ambayo ni yeye ali initiate. Mimi niliyeumizwa na kuoita kwenye phase mbali mbali (anger, resentiment, chuki, kuhisi kisasi) mpaka nikapona kwa kuamua kuachilia vyote inakuaje am soo cool namna hii halaf yeye kapanic hivi??


Chuki inatesa wakuu nakubaliana na wewe.
Kwa story uliyosimulia kuhusu ex-wife wako mpaka mnafikishana barazani na kuachana mahakamani, ni wazi anachuki iliyokomaa sana juu yako.

Ni kana kwamba ni mtu ambaye kuna uovu mkubwa uliwahi kumfanyia, dah holding grudges ni kitu ambacho siwezi.

Nina ex-girlfriend aliniachaga tena kwa matusi nikamwambia poa, sikumchukia badae tukawa tunatafutana kwa sms niliona tu sitaki mbichi hizi nikachange line asinipate.
 
Back
Top Bottom