Chuki na UDSM hakuna aliyekutuma Ufeli

Chuki na UDSM hakuna aliyekutuma Ufeli

Ryan The King

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
2,789
Reaction score
2,701
Habari Wakubwa.

Leo nikiwa katika biashara yangu walikuja vijana wawili. Vijana hao walionekana kukwaruzana kila mmoja akijaribu kumshinda mwenzake kukitukana chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Nikiwa kama Mhitimu kutoka chuo hicho. Nilivuta masikio yangu zaidi na umakini wote kutaka kujua nini sababu ya mvutano ule mkubwa.

Kwa nasibu vijana wale walikuja kwenye biashara yangu wakiwa bado wanararuana vikali kama wapo katika finali ya kombe la dunia.

Sauti yangu ya kuwakaribisha ndio iliweka nukta katika mabishano yao na kuwafanya wameze mafumba kadhaa ya mate jasho shingoni likiteremka kutokana na jua la Dar.

Niliwahudumia. Kisha nikawauliza kuhusu walichokuwa wakikitukana.

Ndio wakanipa filamu zima jinsi walivyo-apply Udsm na kutemwa kama kohozi. Walienda mbali zaidi nakusema kwa maksi walizopata walikuwa na haki za moja kwa moja za kuchaguliwa Udsm. Hapo ikabidi niulize ufaulu wao. Ndipo mmoja kwa kujitutumua akafungua mdomo wake na kusema ana divisheni two ya 11 mwenzake akadakia ana ya 10.

Nikawapa pole tuu na kuwaambia walifaulu tuu vizuri hivyo wa-appy vyuo vingine.

Mytake; jamani ninyi watoto mlioshuleni someni kama mnataka mambo makubwa. Sio unamaliza shule na kadivisheni two kako alafu unataka uchaguliwe chuo kikubwa cha vipanga.

Hakuna aliyekutuma ufeli. Kama unataka kusoma Udsm sharti upige msuli upate angalau kadivisheni one.

Kila mtu apambane na hali yake.

Udsm hoyeeeeee!
 
Habari Wakubwa.

Leo nikiwa katika biashara yangu walikuja vijana wawili. Vijana hao walionekana kukwaruzana kila mmoja akijaribu kumshinda mwenzake kukitukana chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Nikiwa kama Mhitimu kutoka chuo hicho. Nilivuta masikio yangu zaidi na umakini wote kutaka kujua nini sababu ya mvutano ule mkubwa.

Kwa nasibu vijana wale walikuja kwenye biashara yangu wakiwa bado wanararuana vikali kama wapo katika finali ya kombe la dunia.

Sauti yangu ya kuwakaribisha ndio iliweka nukta katika mabishano yao na kuwafanya wameze mafumba kadhaa ya mate jasho shingoni likiteremka kutokana na jua la Dar.

Niliwahudumia. Kisha nikawauliza kuhusu walichokuwa wakikitukana.

Ndio wakanipa filamu zima jinsi walivyo-apply Udsm na kutemwa kama kohozi. Walienda mbali zaidi nakusema kwa maksi walizopata walikuwa na haki za moja kwa moja za kuchaguliwa Udsm. Hapo ikabidi niulize ufaulu wao. Ndipo mmoja kwa kujitutumua akafungua mdomo wake na kusema ana divisheni two ya 11 mwenzake akadakia ana ya 10.

Nikawapa pole tuu na kuwaambia walifaulu tuu vizuri hivyo wa-appy vyuo vingine.

Mytake; jamani ninyi watoto mlioshuleni someni kama mnataka mambo makubwa. Sio unamaliza shule na kadivisheni two kako alafu unataka uchaguliwe chuo kikubwa cha vipanga.

Hakuna aliyekutuma ufeli. Kama unataka kusoma Udsm sharti upige msuli upate angalau kadivisheni one.

Kila mtu apambane na hali yake.

Udsm hoyeeeeee!
Kwa hiyo kusoma UDSM ni jambo Kubwa?????
 
Nimevutiwa na bandiko lako na hasa kuhusu kuomba kudahiriwa UDSM na kukosa nafasi mwaka huu, Hii inanihusu kwa kuwa nina wangu wa karibu ambaye mkasa huu umemkumba pamoja na kuniaminisha huko nyuma kuwa lazima aingie UDSM kwa kuwa ana Division two points 13.

Tangu mwanzo nilikuwa nahisi kuwa ufaulu huo wa Division two points 10-13 niliutilia shaka na kutoamini kama chuo pekee hapa nchini kimeamua kushusha hadhi yake ya zamani na kudahiri chini ya kiwango chake cha awali. Naungana na wewe kuwapa pole hao wawili pamoja na wangu wa karibu ila wasikate tamaa wajipange kwingine.
 
Nimevutiwa na bandiko lako na hasa kuhusu kuomba kudahiriwa UDSM na kukosa nafasi mwaka huu, Hii inanihusu kwa kuwa nina wangu wa karibu ambaye mkasa huu umemkumba pamoja na kuniaminisha huko nyuma kuwa lazima aingie UDSM kwa kuwa ana Division two points 13.
Tangu mwanzo nilikuwa nahisi kuwa ufaulu huo wa Division two points 10-13 niliutilia shaka na kutoamini kama chuo pekee hapa nchini kimeamua kushusha hadhi yake ya zamani na kudahiri chini ya kiwango chake cha awali. Naungana na wewe kuwapa pole hao wawili pamoja na wangu wa karibu ila wasikate tamaa wajipange kwingine.
Kweli Mkuu. Watu kama wanapenda vitu vizuri basi inabidi wapambane sana.

Hiyo ni hata katika maisha ya kawaida.
 
Kupata divisheni one sio jambo kubwa Mkuu?

Unaposema Udsm unazungumzia chuo kikuu cha taifa. Kama unavyosema Oxford huko uingereza.

Kama unafikiri vyema unaweza kunielewa
Kwa hiyo unataka kusema kwenye vyuo vingine kama vile mzumbe, SUA, SAUT, Morogoro muslim university watu wenye division one hawapo!

Mambo mengine ni matakwa binafsi mtu anachagua aende chuo gani kwa sababu mbalimbali, mf.uchumi, ukaribu n.k

Kungekuwa na mtihani wa mwisho wa taifa vyuoni ndiyo ungeelewa naamanisha nini!!
 
Back
Top Bottom