Chuki na UDSM hakuna aliyekutuma Ufeli

Chuki na UDSM hakuna aliyekutuma Ufeli

Habari Wakubwa.

Leo nikiwa katika biashara yangu walikuja vijana wawili. Vijana hao walionekana kukwaruzana kila mmoja akijaribu kumshinda mwenzake kukitukana chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Nikiwa kama Mhitimu kutoka chuo hicho. Nilivuta masikio yangu zaidi na umakini wote kutaka kujua nini sababu ya mvutano ule mkubwa.

Kwa nasibu vijana wale walikuja kwenye biashara yangu wakiwa bado wanararuana vikali kama wapo katika finali ya kombe la dunia.

Sauti yangu ya kuwakaribisha ndio iliweka nukta katika mabishano yao na kuwafanya wameze mafumba kadhaa ya mate jasho shingoni likiteremka kutokana na jua la Dar.

Niliwahudumia. Kisha nikawauliza kuhusu walichokuwa wakikitukana.

Ndio wakanipa filamu zima jinsi walivyo-apply Udsm na kutemwa kama kohozi. Walienda mbali zaidi nakusema kwa maksi walizopata walikuwa na haki za moja kwa moja za kuchaguliwa Udsm. Hapo ikabidi niulize ufaulu wao. Ndipo mmoja kwa kujitutumua akafungua mdomo wake na kusema ana divisheni two ya 11 mwenzake akadakia ana ya 10.

Nikawapa pole tuu na kuwaambia walifaulu tuu vizuri hivyo wa-appy vyuo vingine.

Mytake; jamani ninyi watoto mlioshuleni someni kama mnataka mambo makubwa. Sio unamaliza shule na kadivisheni two kako alafu unataka uchaguliwe chuo kikubwa cha vipanga.

Hakuna aliyekutuma ufeli. Kama unataka kusoma Udsm sharti upige msuli upate angalau kadivisheni one.

Kila mtu apambane na hali yake.

Udsm hoyeeeeee!
Oyeeeeeeeeee
Kusoma udsm kila mtu anatamani....ila kwa tunaosoma hapa lazima tupite kifua mbelee.... We are the cream above all hao wa eagle wings wasubirie tu


Udsm is the best university ever... Waende udom hao vilaza


Niko yombo leteni povu la omooo
 
Nifikiri nini tena wakati mimi napitia ulichokiandika? Unewaita waliopta division two wamefeli. Kisha ukabadili ukasema hata unaweza kupata division one lakini ukawa bado umefeli!
Kwa hiyo unamaanisha UDSM inachukua watu waliofaulu malengo na si maksi?

Ukisoma unapaswa ufikiri kwanza.
 
Bado sijawaelewa, Binafsi yangu Sijawahi soma udsm. Na nisingependa Kusoma udsm kutokana n'a kutokupenda mazingira ya dsm. Nilishawaha apply kozi furahi( siyo degree ya kwanza) na kupata Lakini sikwenda.

Hivyo videgree vyenu vyama kwanza ndiyo vinawafanya muwe mna mawazo mgando.

Umesoma wapi haihusi, kinachohusu ni, what can you do after attaining your education?

Mashindano ya kitoto kabisa. Sasa hivi vyuo ni vingi. Kila mtu anaamua akasome wapi. Muda wa utawala wa chuo kimoja haupo na hautokuwepo tena.
 
nd io mnapokishusha hadhi udsm kwa sifa za kijinga... mnaposoma hpo basi mnajitutumua Kama mazoba ..udsm kimewakisha libwata?

Msomi hubaki kimya...sio siasa zenu.....Na hamjui ni ninyi mmekishusha...tuliopita makerere tuseme nini tumetulia na nyerere mungu amrehem ametukia akhera...

Mnadhan udsm ndio kila kitu..fkn kabisa....mnataka utuaminishe Kenyatta na makerere si bora...halafu kwa wanafunz wepi..kama si walewale...kwangu mie hapa tz Sua wapole na wametulia wanajua wanafanya nini..wapiga domo siku zote...nyeerere akivowacharaza.bakora ilimaanisha na ujinga mnauendeleza..kibaya.......chema......
 
Oyeeeeeeeeee
Kusoma udsm kila mtu anatamani....ila kwa tunaosoma hapa lazima tupite kifua mbelee.... We are the cream above all hao wa eagle wings wasubirie tu


Udsm is the best university ever... Waende udom hao vilaza


Niko yombo leteni povu la omooo
Kula like kama hamsini,nilipita hapo 2004
 
Mara nyingi waliosomea kijijini ndo wana post kama hizi hasa waliofika Dar sababu ya chuo lakini tulio soma hapa tukaona raha na karaha hata hatukuwai kubonyeza battone ya mzuka wako licha ya ivo viwani ivo.......
 
Back
Top Bottom