Mkuu umeisoma post ya
Chris Lukosi #37 na kuielewa?
Hivi mbunge akuonee wivu..husda...chuki vya nini?
Hivi watawala wanapobana mambo Fulani kulinda maslahi yao wewe kwako ni wivu?
Mataifa makubwa yanapoweka Sera kandamizi kwa nchi masikini ili kulinda maslahi yao wewe hii unaiita chuki? Husda? Wivu? Choyo?
Vita ya maslahi inaweza kupiganwa kwa nyimbo za wivu...choyo..chuki na husda?
Toka awali tunawaambia hii ni very serious issue tofauti na wengi mnavyodhani kwa kutoa sababu nyepesi..
Mtu anapopinga uraia pacha sababu ya maslahi yake huu si wivu wala husda hii ni nature ya capitalism...
Ni wakati wenu na nyinyi kujiratibu na kupigana kwa kutosha na wahafidhina..
Na hii itafanikiwa kwanza kwa diasporas kujipanga na kuwa na umoja madhubiti..( hapa panatiliwa mkazo sababu huko nje watanzania wengi wanachukiana na kuoneana wivu kuliko nyie mnavyoona huku nyumbani?
Pili mtambue hii ni vita ya maslahi si lelemama kama wivu au husda...
Naamini umenipata mpaka hapo..
CC:
Kiranga Tuko JMUnish1
Mkandara ..
OLESAIDIMU et al
Faida za Tanzania kuruhusu uraia wa nchi mbili ziko wazi. Kubwa ni kwamba Watanzania waliopo nje na waliochukua uraia wa nje (mostly kimaslahi), wataendelea kujisikia "Watanzania" na katika hili nchi itakuwa na chance kubwa zaidi ya kuwafaidi:
1. Kiutaalamu - Katika hili ikumbukwe kuwa ama kiushauri au kiutendaji, kuna sekta bado Tanzania inahitaji uzoefu na utaalamu wa nje ya nchi. Yupo profesa mmoja (wanaomkumbuka jina wanisaidie) ambaye alisema yeye alikuwa anafundisha chuo huko Marekani, hadi siku aliposhangaa anaitwa na mkuu wa chuo hicho akaambiwa "Raisi J. Nyerere anakuhitaji urudi Tanzania ukasaidie kwenye chuo kikuu cha Dar es Salaam". Hadi sasa bado tunawahitaji Watanzania wenzetu waliopo nje kiutaalamu
2. Kifedha - Watanzania wengi waliopo nje na ambao wanaweza kujitunzia vijiakiba kidogo, wangependa wawekeze "nyumbani" kwani wanaamini kuna siku watarudi nyumbani. Lakini kama mtu sio raia tena wa Tanzania, mwamko wa kuwekeza Tanzania hautakuwepo. Kumbukeni kuwa raisi Kikwete anazunguka nje ya nchi mara kwa mara kutafuta wawekezaji. Sijui ni kwa nini tunakataa fursa hii ya wawekezaji watanzania.
3. Kitalii - Hivi tunapovutia watalii tunatarajia ni lazima wawe Wazungu? Maelfu ya Watanzania waliopo nje ya nchi wanarudi kutembea nyumbani kusalimia ndugu na jamaa. Naamini kwa wastani, mtu akija Tz akakaa mwezi mmoja, atatumia zaidi ya shilingi milioni 5. Hivi tukiongelea watu 2500, si tunaongelea bilions?
4. Uhuru - Watanzania wengi waliopo nje na "wakalazimika" kuchukua raia za huko ili wafaidi fursa adimu huko wanajisikia kupoteza uhuru wao pale wanapoona kuwa wao sio watanzania tena. Wazazi ndugu na jamaa wapo Tanzania, kwa kiasi fulani inauma, na inakatisha tamaa. Nyumbani ni nyumbani tu...
5. Hakuna hasara ya kuwa na uraia wa nchi mbili - Hapa ndipo panaponbitatiza kidogo. Ukiacha huo wasiwasi wa Wazanzibari unaotajwa, binafsi sioni nchi itapoteza nini ikiruhusu uraia wa nchi mbili. Hapa ndio maana baadhi ya watu wanawaza "chuki", "Husda", nk.
USHAURI KWA WANA DIASPORA
1. Waungane. Tatizo kubwa linalowatesa sasa ni kugawanyika kisiasa. Waache kuweka siasa za bongo mbele na waweke maslahi ya taifa mbele katika suala hili.
2. Natarajia ndani ya muda mfupi ujao kuwepo na juhudi za kuunganisha wana diaspora. Waongee kwa sauti moja juu ya hili. Juhudi tunazosikia kila siku kufunguliwa tawi la CCM marekani, au la CDM uingereza tuzisikie kuzinduliwa chama cha Wanadiaspora...
Nawasilisha...