jamii01
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 1,974
- 1,400
Naomba kutoa ushauri wa bure kwa wale wanaotarajia kufunga ndoa hivi karibuni,
Kama ni mwanaume mwenzangu jaribu kupunguza matumizi kwa ajiri ya maandalizi ya harusi..vijana wengi wanaingia kwenye mtego wa kukopa kwenye sehemu zao za kazi,mabank,vyama n.k kwa ajiri ya kufanikisha sherehe ya masaa yasiyozidi 6 yaani kwa usiku mmoja.
NDoa si sherehe,ndoa ni pale mnapobaki wawili wewe na mkeo hapo ndipo tunapoita ndoa..Wanaume wengi wameingia katika mtego wa kushawishika kutaka kufanya sherehe kubwa ili kuonyesha ufahari juu ya mwenzake au wafanyakazi wenzake au jamaa zake au marafiki zake n.k kisha baada ya hapo hubaki akiumia na deni kubwa alilokopa kwa ajili ya kufanikisha harusi ambalo atataabika nalo kati ya kipindi cha miezi 6 hadi miaka 3 na hii itaonyesha ugumu wa maisha kwa mda mfupi kwa yule ampendaye mkewe..kuanza kuishi maisha ya kujibana badala ya kuanza na maisha ya kufurahiana
Inakuwaje kijana unaingia harusi ya gharama hata kimsingi cha vyumba vitatu hauna..haiingii akilini unakopa kwa ajili ya usiku mmoja watu wale na kusaza badala ya kukopa uweke kibanda ambapo utalala na yule umpendaye hadi maisha yenu ya uzeeni?mwingine hata kiwanja hana,mwingine ndiyo hivyo nikupanga tu..
Ushauri:
Jitahidi kujibana kifedha na fanya sherehe ndogo sana kuliangana na uwezo wako wa kiuchumi
Achana na vitu au gharama zisizokuwa na umuhimu kwako kwa ajili ya siku hiyo..kama kukodi gari la gharama kubwa,ukumbi wa kifahari n.k
Washirikishe jamaa zako,marafiki zako au ndugu zako wakupe support ya kimwazo au kifedha
Kaa na zungumza na rafiki yako wa jamaa yako wa karibu aliyefunga ndoa siku si nyingi uone namna gani atakavyokushauri kupunguza gharama au kuepuka matatizo yaliyojitokeza kipindi cha sherehe yake
Kubari ushauri kutoka kwa best man wako
ANGALIZO
Mara zote harusi haikosekani mapungufu hata siku moja..kubali kile kilikwisha tokea.
NDOA ni nyinyi wawili baada ya kutoka kwenye sherehe usiku ule wa kwanza..mnapobaki nyinyi wawili ndipo tutapohita ndoa..
KW ushauri mwingine AFYA,MAHUSIANO NA NDOA unaweza kuinbox lakini ni kwa WANAUME TU
Kama ni mwanaume mwenzangu jaribu kupunguza matumizi kwa ajiri ya maandalizi ya harusi..vijana wengi wanaingia kwenye mtego wa kukopa kwenye sehemu zao za kazi,mabank,vyama n.k kwa ajiri ya kufanikisha sherehe ya masaa yasiyozidi 6 yaani kwa usiku mmoja.
NDoa si sherehe,ndoa ni pale mnapobaki wawili wewe na mkeo hapo ndipo tunapoita ndoa..Wanaume wengi wameingia katika mtego wa kushawishika kutaka kufanya sherehe kubwa ili kuonyesha ufahari juu ya mwenzake au wafanyakazi wenzake au jamaa zake au marafiki zake n.k kisha baada ya hapo hubaki akiumia na deni kubwa alilokopa kwa ajili ya kufanikisha harusi ambalo atataabika nalo kati ya kipindi cha miezi 6 hadi miaka 3 na hii itaonyesha ugumu wa maisha kwa mda mfupi kwa yule ampendaye mkewe..kuanza kuishi maisha ya kujibana badala ya kuanza na maisha ya kufurahiana
Inakuwaje kijana unaingia harusi ya gharama hata kimsingi cha vyumba vitatu hauna..haiingii akilini unakopa kwa ajili ya usiku mmoja watu wale na kusaza badala ya kukopa uweke kibanda ambapo utalala na yule umpendaye hadi maisha yenu ya uzeeni?mwingine hata kiwanja hana,mwingine ndiyo hivyo nikupanga tu..
Ushauri:
Jitahidi kujibana kifedha na fanya sherehe ndogo sana kuliangana na uwezo wako wa kiuchumi
Achana na vitu au gharama zisizokuwa na umuhimu kwako kwa ajili ya siku hiyo..kama kukodi gari la gharama kubwa,ukumbi wa kifahari n.k
Washirikishe jamaa zako,marafiki zako au ndugu zako wakupe support ya kimwazo au kifedha
Kaa na zungumza na rafiki yako wa jamaa yako wa karibu aliyefunga ndoa siku si nyingi uone namna gani atakavyokushauri kupunguza gharama au kuepuka matatizo yaliyojitokeza kipindi cha sherehe yake
Kubari ushauri kutoka kwa best man wako
ANGALIZO
Mara zote harusi haikosekani mapungufu hata siku moja..kubali kile kilikwisha tokea.
NDOA ni nyinyi wawili baada ya kutoka kwenye sherehe usiku ule wa kwanza..mnapobaki nyinyi wawili ndipo tutapohita ndoa..
KW ushauri mwingine AFYA,MAHUSIANO NA NDOA unaweza kuinbox lakini ni kwa WANAUME TU