Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,538
- 3,826
TIPWATIPWA TETEMA... OOH TETEMA!- 1
MTUNZI: HASHIM AZIZ Hashpower7113
MWANZO
Sauti ya jogoo aliyekuwa anawika kuashiria mapambazuko ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye usingizi mzito. Nilifumbua macho na kupiga miayo kadhaa, nafsi ilikuwa inataka niamke lakini mwili haukuwa radhi, bado nilikuwa na uchovu wa hali ya lijaribu kuvuta kumbukumbu kuhusu usiku uliopita, nikajikuta nikitabasamu mwenyewe. Ulikuwa ni usiku wa kipekee sana kwangu, matukio yote yaliyotokea jana yake yalikuwa yakipita ndani ya kichwa changu.
“Chandee! Chandeee! Bado umelala mpaka sasa hivi wakati unajua unatakiwa kuwahi feri kuchukua samaki?” sauti ya baba mdogo ilisikika kutokea dirishani huku akigonga mlango kwa nguvu.
Nilikurupuka pale kitandani, nikajifunga taulo na kufungua mlango huku nikipiga miayo.
“Shikamoo baba mdogo!”
“Mwenyewe! Nasikia umeanza tena ule mchezo wako wa kuingiza wanawake humu ndani. Chande kama maisha ya mjini yamekushinda nitakurudisha kijijini, sipendi kabisa mambo ya ujinga mimi.”
“Hamna wananisingizia baba, mimi hayo mambo nilishaacha kabisa, tangu lile tukio sijawahi tena, wananisingizia.”
“Wanakusingizia wakati watu wamekuona kabisa, na nasikia siku hizi umeamua kubadili mfumo, kutoka kwa mahausigeli mpaka kwa mijimama, nasikia kuna tipwatipwa limeingia hapa jana mpaka kupita kwenye geti dogo lilikuwa linashindwa,” alisema baba mdogo huku akionesha kuwa na ushahidi na kile alichokuwa anakisema.
Nilijua anamzungumzia Sandra, kwa sababu ni kweli nilikuwa naye usiku uliopita na ndiye aliyesababisha niamke nikiwa na uchovu kiasi hicho, nilimuingiza usiku muda ambao nilikuwa naamini kwamba watu wote wameshalala, swali likawa ni nani aliyemuona? Kwa nini ameenda kunichomea utambi kwa baba mdogo?”
Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu. Baada ya kunishukia sana kwa maneno makali, baba mdogo akitoa fedha kiasi cha kama shilingi elfu sabini na kunipa kwa ajili ya kwenda kununua samaki wa biashara feri.
Ulikuwa ndiyo utaratibu wetu, asubuhi nadamka kwenda feri, nanunua samaki wa kutosha nikirudi nyumbani nasaidiana na mama mdogo kuwaandaa, wengine wanakaangwa na wengine tunawatembeza majumbani mwa watu, jioni ikifika tunakabidhi mahesabu kwa baba mdogo. Kesho asubuhi tena tunaamka hivyohivyo.
Kiukweli japokuwa kazi ilikuwa ngumu, lakini kuna marupurupu niliyokuwa nayapata ambayo yalinifanya niipende sana kazi yangu. Cha kwanza ilikuwa ni fedha, ilikuwa nikizungusha biashara vizuri, mpaka usiku sikosi kama shilingi elfu ishirini za pembeni, hiyo ni nje ya posho anayotupa baba mdogo kila mwisho wa wiki.
Lakini kingine, ilikuwa ni kufahamiana na wateja ambao wengi walikuwa ni wanawake, si unajua tena asubuhi ukipitisha samaki mtaani wanaume wanakuwa wameshaenda makazini, kwa hiyo wanaokuungisha wengi wanakuwa ni mahausigeli au wamama wa nyumbani na hapo ndipo ulipokuwa ugonjwa wangu.
Tipwatipwa ambaye baba mdogo alikuwa akimpigia kelele kwamba nilimuingiza hapo ndani jana yake, alikuwa ni Sandra, toto la Magomeni ambaye nilikutana naye katika kazi yangu ya kuuza samaki.
Sandra alikuwa toto haswaa, mweupe, mrefu kiasi, kibonge wa nguvu, mzuri wa sura, macho muda wote kama amekula kungu na nyuma amefungasha wowowo utasema wako wawili.
Mtaani kwao walikuwa wakimuita kwa jina la Bonge, hata mimi siku za mwanzo wakati naanza kumjua nilikuwa namuita Da Bonge, lakini si unajua tena, ujanja-ujanja wangu hatimaye tukazoeana na mwisho wa siku nikamaliza kazi kimasihara-masihara.
Hiyo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kutoka na mwanamke mwenye haiba kama Sandra, siku zote nilikuwa nawaogopa sana wanawake wenye miili mikubwa kwa sababu ya stori za vijiweni nilizokuwa nazisikia lakini tangu Sandra aliponilambisha asali, nilijiapiza kwamba kamwe siwezi tena kurudi kwa mahausigeli ambao nilikuwa nikiwanasa kirahisi kwenye mishemishe zangu.
Basi nilirudi ndani na kuandaa vitendea kazi vyangu, nikaenda bafuni na kujimwagia maji, dakika kumi baadaye, tayari nilikuwa nimeshamaliza. Tofauti na wauza samaki wengi, mimi nilikuwa najipenda sana.
Ilikuwa ni lazima ninyuke pamba ndiyo niende kazini, sikutaka kabisa kufanana na wale wengine ambao unakuta mtu mchafu, mwili mzima ananuka shombo, eti kisa anauza samaki. Utanashati kwangu ulikuwa ndiyo kila kitu, japo nilikuwa napiga pamba za bei rahisi ninazonunua pale Karume, lakini nilikuwa natoka chicha kwelikweli.
Je, nini kitafuatia?
MTUNZI: HASHIM AZIZ Hashpower7113
MWANZO
Sauti ya jogoo aliyekuwa anawika kuashiria mapambazuko ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye usingizi mzito. Nilifumbua macho na kupiga miayo kadhaa, nafsi ilikuwa inataka niamke lakini mwili haukuwa radhi, bado nilikuwa na uchovu wa hali ya lijaribu kuvuta kumbukumbu kuhusu usiku uliopita, nikajikuta nikitabasamu mwenyewe. Ulikuwa ni usiku wa kipekee sana kwangu, matukio yote yaliyotokea jana yake yalikuwa yakipita ndani ya kichwa changu.
“Chandee! Chandeee! Bado umelala mpaka sasa hivi wakati unajua unatakiwa kuwahi feri kuchukua samaki?” sauti ya baba mdogo ilisikika kutokea dirishani huku akigonga mlango kwa nguvu.
Nilikurupuka pale kitandani, nikajifunga taulo na kufungua mlango huku nikipiga miayo.
“Shikamoo baba mdogo!”
“Mwenyewe! Nasikia umeanza tena ule mchezo wako wa kuingiza wanawake humu ndani. Chande kama maisha ya mjini yamekushinda nitakurudisha kijijini, sipendi kabisa mambo ya ujinga mimi.”
“Hamna wananisingizia baba, mimi hayo mambo nilishaacha kabisa, tangu lile tukio sijawahi tena, wananisingizia.”
“Wanakusingizia wakati watu wamekuona kabisa, na nasikia siku hizi umeamua kubadili mfumo, kutoka kwa mahausigeli mpaka kwa mijimama, nasikia kuna tipwatipwa limeingia hapa jana mpaka kupita kwenye geti dogo lilikuwa linashindwa,” alisema baba mdogo huku akionesha kuwa na ushahidi na kile alichokuwa anakisema.
Nilijua anamzungumzia Sandra, kwa sababu ni kweli nilikuwa naye usiku uliopita na ndiye aliyesababisha niamke nikiwa na uchovu kiasi hicho, nilimuingiza usiku muda ambao nilikuwa naamini kwamba watu wote wameshalala, swali likawa ni nani aliyemuona? Kwa nini ameenda kunichomea utambi kwa baba mdogo?”
Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu. Baada ya kunishukia sana kwa maneno makali, baba mdogo akitoa fedha kiasi cha kama shilingi elfu sabini na kunipa kwa ajili ya kwenda kununua samaki wa biashara feri.
Ulikuwa ndiyo utaratibu wetu, asubuhi nadamka kwenda feri, nanunua samaki wa kutosha nikirudi nyumbani nasaidiana na mama mdogo kuwaandaa, wengine wanakaangwa na wengine tunawatembeza majumbani mwa watu, jioni ikifika tunakabidhi mahesabu kwa baba mdogo. Kesho asubuhi tena tunaamka hivyohivyo.
Kiukweli japokuwa kazi ilikuwa ngumu, lakini kuna marupurupu niliyokuwa nayapata ambayo yalinifanya niipende sana kazi yangu. Cha kwanza ilikuwa ni fedha, ilikuwa nikizungusha biashara vizuri, mpaka usiku sikosi kama shilingi elfu ishirini za pembeni, hiyo ni nje ya posho anayotupa baba mdogo kila mwisho wa wiki.
Lakini kingine, ilikuwa ni kufahamiana na wateja ambao wengi walikuwa ni wanawake, si unajua tena asubuhi ukipitisha samaki mtaani wanaume wanakuwa wameshaenda makazini, kwa hiyo wanaokuungisha wengi wanakuwa ni mahausigeli au wamama wa nyumbani na hapo ndipo ulipokuwa ugonjwa wangu.
Tipwatipwa ambaye baba mdogo alikuwa akimpigia kelele kwamba nilimuingiza hapo ndani jana yake, alikuwa ni Sandra, toto la Magomeni ambaye nilikutana naye katika kazi yangu ya kuuza samaki.
Sandra alikuwa toto haswaa, mweupe, mrefu kiasi, kibonge wa nguvu, mzuri wa sura, macho muda wote kama amekula kungu na nyuma amefungasha wowowo utasema wako wawili.
Mtaani kwao walikuwa wakimuita kwa jina la Bonge, hata mimi siku za mwanzo wakati naanza kumjua nilikuwa namuita Da Bonge, lakini si unajua tena, ujanja-ujanja wangu hatimaye tukazoeana na mwisho wa siku nikamaliza kazi kimasihara-masihara.
Hiyo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kutoka na mwanamke mwenye haiba kama Sandra, siku zote nilikuwa nawaogopa sana wanawake wenye miili mikubwa kwa sababu ya stori za vijiweni nilizokuwa nazisikia lakini tangu Sandra aliponilambisha asali, nilijiapiza kwamba kamwe siwezi tena kurudi kwa mahausigeli ambao nilikuwa nikiwanasa kirahisi kwenye mishemishe zangu.
Basi nilirudi ndani na kuandaa vitendea kazi vyangu, nikaenda bafuni na kujimwagia maji, dakika kumi baadaye, tayari nilikuwa nimeshamaliza. Tofauti na wauza samaki wengi, mimi nilikuwa najipenda sana.
Ilikuwa ni lazima ninyuke pamba ndiyo niende kazini, sikutaka kabisa kufanana na wale wengine ambao unakuta mtu mchafu, mwili mzima ananuka shombo, eti kisa anauza samaki. Utanashati kwangu ulikuwa ndiyo kila kitu, japo nilikuwa napiga pamba za bei rahisi ninazonunua pale Karume, lakini nilikuwa natoka chicha kwelikweli.
Je, nini kitafuatia?