Chombezo: Tipwatipwa tetema, Oooh tetema

Johnny Sins

JF-Expert Member
Nov 4, 2019
2,538
3,826
TIPWATIPWA TETEMA... OOH TETEMA!- 1
MTUNZI: HASHIM AZIZ Hashpower7113

MWANZO
Sauti ya jogoo aliyekuwa anawika kuashiria mapambazuko ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye usingizi mzito. Nilifumbua macho na kupiga miayo kadhaa, nafsi ilikuwa inataka niamke lakini mwili haukuwa radhi, bado nilikuwa na uchovu wa hali ya lijaribu kuvuta kumbukumbu kuhusu usiku uliopita, nikajikuta nikitabasamu mwenyewe. Ulikuwa ni usiku wa kipekee sana kwangu, matukio yote yaliyotokea jana yake yalikuwa yakipita ndani ya kichwa changu.

“Chandee! Chandeee! Bado umelala mpaka sasa hivi wakati unajua unatakiwa kuwahi feri kuchukua samaki?” sauti ya baba mdogo ilisikika kutokea dirishani huku akigonga mlango kwa nguvu.

Nilikurupuka pale kitandani, nikajifunga taulo na kufungua mlango huku nikipiga miayo.
“Shikamoo baba mdogo!”

“Mwenyewe! Nasikia umeanza tena ule mchezo wako wa kuingiza wanawake humu ndani. Chande kama maisha ya mjini yamekushinda nitakurudisha kijijini, sipendi kabisa mambo ya ujinga mimi.”

“Hamna wananisingizia baba, mimi hayo mambo nilishaacha kabisa, tangu lile tukio sijawahi tena, wananisingizia.”

“Wanakusingizia wakati watu wamekuona kabisa, na nasikia siku hizi umeamua kubadili mfumo, kutoka kwa mahausigeli mpaka kwa mijimama, nasikia kuna tipwatipwa limeingia hapa jana mpaka kupita kwenye geti dogo lilikuwa linashindwa,” alisema baba mdogo huku akionesha kuwa na ushahidi na kile alichokuwa anakisema.

Nilijua anamzungumzia Sandra, kwa sababu ni kweli nilikuwa naye usiku uliopita na ndiye aliyesababisha niamke nikiwa na uchovu kiasi hicho, nilimuingiza usiku muda ambao nilikuwa naamini kwamba watu wote wameshalala, swali likawa ni nani aliyemuona? Kwa nini ameenda kunichomea utambi kwa baba mdogo?”

Nilijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu. Baada ya kunishukia sana kwa maneno makali, baba mdogo akitoa fedha kiasi cha kama shilingi elfu sabini na kunipa kwa ajili ya kwenda kununua samaki wa biashara feri.

Ulikuwa ndiyo utaratibu wetu, asubuhi nadamka kwenda feri, nanunua samaki wa kutosha nikirudi nyumbani nasaidiana na mama mdogo kuwaandaa, wengine wanakaangwa na wengine tunawatembeza majumbani mwa watu, jioni ikifika tunakabidhi mahesabu kwa baba mdogo. Kesho asubuhi tena tunaamka hivyohivyo.

Kiukweli japokuwa kazi ilikuwa ngumu, lakini kuna marupurupu niliyokuwa nayapata ambayo yalinifanya niipende sana kazi yangu. Cha kwanza ilikuwa ni fedha, ilikuwa nikizungusha biashara vizuri, mpaka usiku sikosi kama shilingi elfu ishirini za pembeni, hiyo ni nje ya posho anayotupa baba mdogo kila mwisho wa wiki.

Lakini kingine, ilikuwa ni kufahamiana na wateja ambao wengi walikuwa ni wanawake, si unajua tena asubuhi ukipitisha samaki mtaani wanaume wanakuwa wameshaenda makazini, kwa hiyo wanaokuungisha wengi wanakuwa ni mahausigeli au wamama wa nyumbani na hapo ndipo ulipokuwa ugonjwa wangu.

Tipwatipwa ambaye baba mdogo alikuwa akimpigia kelele kwamba nilimuingiza hapo ndani jana yake, alikuwa ni Sandra, toto la Magomeni ambaye nilikutana naye katika kazi yangu ya kuuza samaki.

Sandra alikuwa toto haswaa, mweupe, mrefu kiasi, kibonge wa nguvu, mzuri wa sura, macho muda wote kama amekula kungu na nyuma amefungasha wowowo utasema wako wawili.

Mtaani kwao walikuwa wakimuita kwa jina la Bonge, hata mimi siku za mwanzo wakati naanza kumjua nilikuwa namuita Da Bonge, lakini si unajua tena, ujanja-ujanja wangu hatimaye tukazoeana na mwisho wa siku nikamaliza kazi kimasihara-masihara.

Hiyo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kutoka na mwanamke mwenye haiba kama Sandra, siku zote nilikuwa nawaogopa sana wanawake wenye miili mikubwa kwa sababu ya stori za vijiweni nilizokuwa nazisikia lakini tangu Sandra aliponilambisha asali, nilijiapiza kwamba kamwe siwezi tena kurudi kwa mahausigeli ambao nilikuwa nikiwanasa kirahisi kwenye mishemishe zangu.

Basi nilirudi ndani na kuandaa vitendea kazi vyangu, nikaenda bafuni na kujimwagia maji, dakika kumi baadaye, tayari nilikuwa nimeshamaliza. Tofauti na wauza samaki wengi, mimi nilikuwa najipenda sana.

Ilikuwa ni lazima ninyuke pamba ndiyo niende kazini, sikutaka kabisa kufanana na wale wengine ambao unakuta mtu mchafu, mwili mzima ananuka shombo, eti kisa anauza samaki. Utanashati kwangu ulikuwa ndiyo kila kitu, japo nilikuwa napiga pamba za bei rahisi ninazonunua pale Karume, lakini nilikuwa natoka chicha kwelikweli.

Je, nini kitafuatia?
 
mtunzi yule yule wa giza totoro!...... mkuu lipia matangazo aisee sio kuishia njian alafu unaanza kunadi kitabu!........
 
SEHEMU YA 02





Ilikuwa ni lazima ninyuke pamba ndiyo niende kazini, sikutaka kabisa kufanana na wale wengine ambao unakuta mtu mchafu, mwili mzima ananuka shombo, eti kisa anauza samaki. Utanashati kwangu ulikuwa ndiyo kila kitu, japo nilikuwa napiga pamba za bei rahisi ninazonunua pale Karume, lakini nilikuwa natoka chicha kwelikweli.
SASA ENDELEA...
Basi baada ya kujiandaa, nilihakikisha fedha alizonipa baba mdogo, nikatoka na kuchukua kapu langu, nikaingia mtaani, moja kwa moja mpaka kituoni, nikaingia kwenye daladala na safari ya kuelekea Feri ikaanza. Ilibidi nipande daladala za kwenda mpaka Posta kisha ndiyo niunganishe na daladala nyingine ya kwenda Feri au kama muda unaruhusu nitembee tu kwa miguu.
“Eeh! We kaka taratibu, mambo ya kupakazana shombo asubuhi yote hii mi sitaki, tusitiane nuksi, toa kapu lako,” alisema abiria niliyekaa naye siti moja kwa ukali. Kumbe wakati naweka kapu langu la samaki chini ya siti, kwa bahati mbaya nilimgusa miguuni.
“Samahani dada!” nilijibu kwa aibu, yule dada akanisindikiza na msonyo mkali, nikazidi kufedheheka kwani tayari abiria wengine wote walikuwa wamegeuka wakitaka kusikia ni nani aliyekuwa anachambwa asubuhi yote ile. Basi nikajikausha kama siyo mimi.
Sikuongea chochote mpaka tunafika Posta, basi nikalivuta kapu langu na kuteremka harakaharaka kwenye daladala huku nikiwa naona aibu hata kugeuka.
“We muuza samaki! Wewe kaka!” sauti ya kike ilisikika kutokea nyuma yangu na kwa haraka kabla hata sijageuka niliweza kuitambua kwamba ni ya yule dada aliyenisemea mbovu kwenye daladala, nikajua anataka kuendelea kunitoa nishai. Niligeuka kwa upole na kumtazama huku moyoni nikiwa ni kama nasema ‘si nimeshakuomba radhi jamani!’.
“Hiki kisimu siyo chako?” aliniuliza kwa upole, nikashtuka kugundua kwamba kumbe nilikuwa nimesahau kisimu changu cha tochi pale kwenye siti nilipokuwa nimekaa. Nilijisikia aibu kwa sababu kisimu chenyewe wala hakikuwa na hadhi, ‘batani’ zilikuwa zimefutikafutika na nilikuwa nimekifunga na ‘rubber band’ kwani mfuniko ulikuwa haufungi vizuri na kusababisha betri liwe linachezacheza.
Licha ya aibu niliyoihisi lakini nilimshukuru sana kwa sababu ukweli ni kwamba mwenyewe kilikuwa kinanifaa, ule wimbo wa singeli wanaoimba sijui kisimu changu cha laini mbili sijui kimefanya nini, ulipita haraka ndani ya kichwa changu, nikajikuta nimetabasamu, namba za wateja wangu wote zilikuwa kwenye kisimu hicho.
“Ahsante sana dadaangu! Ahsante sana.”
“Muone, umenichafua na shombo lako la samaki, na mimi ningeamua kukufanyia roho mbaya si ningekitupilia mbali kisimu chako, kisimu chenyewe kibayaa,” alisema yule dada, safari hii na yeye tabasamu hafifu likiwa limechanua kwenye uso wake.
“Nisamehe dada’angu, si unajua tena nimevurugwa, nimechelewa kufuata mzigo Feri,” nilisema, basi akanipa simu lakini niligundua kwamba bado alikuwa ananitazama usoni, nikakwepesha macho yangu na kukiweka kisimu changu mfukoni.
“Nisamehe kama nimekukwaza kwa maneno yangu kwenye daladala, kunamtu kaniudhi sana leo. Samaki unauzia wapi?”
“Usijali dada’angu, na wewe nisamehe na nashukuru kwa jinsi ulivyonionesha roho nzuri na uungwana. Mi natembeza mitaani lakini sanasana nauzia Magomeni na Kinondoni lakini ukinipa dili nafika sehemu yoyote,” nilimjibu, akatabasamu.
“Mh! Muuza samaki gani sharobaro namna hii, tatizo lako shombo tu, kapu lako linatoa shombo sana,” alisema, tukawa tunatembea sambamba huku akiendelea kunitaniatania. Kumbe na yeye alikuwa anaelekea njia ileile niliyokuwa naelekea mimi.
Kuna sehemu tulipita kulikuwa na watu wanagombea daladala, ikabidi nimpishe kidogo yeye atangulie mbele huku mimi nikimfuatia kwa nyuma, mapigo ya moyo wangu yakanilipuka paah!
Alikuwa amefungasha mzigo wa nguvu nyuma, na sketi ya kitambaa aliyokuwa amevaa ilizidi kumfanya avutie kwelikweli, kwa mbali nikawa naona pindo za kufuli lake, jambo lililofanya nisisimke kwelikweli. Na yeye alikuwa kibonge flani hivi, lakini siyo kama Sandra. Tulivuka lile eneo lenye fujofujo lakini nikawa bado natamani niendelee kubaki nyuma niwe namuangalia anavyotembea.
“Kwa heri mimi naingia mtaa huu,” alisema huku akinioneshea kwa ishara alikokuwa anaelekea, nilitamani kumuomba namba za simu lakini nilijiuliza naanzia wapi, sikuwa na hadhi hata ya kumsogelea kwa sababu ukiachilia mbali uzuri wa sura na umbo, alikuwa ananukia vizuri na mavazi aliyokuwa amevaa yalimfanya aonekane smati kwelikweli.
Wakati anasubiri kuvuka barabara, niliamua kupiga moyo konde na kumsemesha: “Aunt, samahani umeniuliza kuhusu mitaa ninakouzia samaki, ulitaka kunipa dili nini?”
“Aah! Kwanza nyumbani kwenyewe mi huwa sikai nashinda kazini, anyway nipe namba yako kama nikihitaji ntakupigia,” alisema, nilitamani kurukaruka kwa furaha, basi harakaharaka nikamtajia, akawa anaandika kwenye simu yake ya kisasa, zile wanazoziita sijui iPhone, zina alama ya epo hivi kwa nyuma.
“Nakusevu muuza samaki, sawa! Wala sitaki hata kujua jina lako,” alisema huku akimalizia kusevu namba harakaharaka, tabasamu likiwa limechanua kwenye uso wake, akavuka barabara na kunifanya nibaki nimesimama namkodolea macho, akapotelea mtaa wa pili.
Alikuwa mzuri kwelikweli na alivyokuwa akitembea sasa, daah! Nilibaki namsindikiza kwa macho tu. Mbele kidogo aligeuka, akashtuka kuona bado nimesimama palepale namuangalia, akacheka nakunipungia mkono kikekike.
Basi niliendelea kumkodolea macho mpaka alipopotea kwenye upeo wa macho yangu, nikaendelea na safari yangu ya kuelekea Feri huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu. Siku yangu ambayo niliona kama nimeianza vibaya, ghafla ilibadilika na kuwa nzuri sana, sura ya yule dada ambaye hata sikuwa nalijua jina lake, ilikuwa ikinijia ndani ya kichwa changu, nikawa natabasamu tu mwenyewe.
Nilitembea mpaka Feri na baada ya kufika, tulijumuika na wafanyabiashara wengine kuanza kununua samaki kutoka kwa wavuvi ambao asubuhi hiyo ndiyo walikuwa wakirejea kutoka baharini.
Kulikuwa na akina mama wengi waliokuwa wamejifunga ‘vibwebwe’ kwa sababu kazi ya kugombania samaki kutoka kwa wavuvi siyo jambo dogo, ukijilegeza utakuwa unaambulia visamaki vya ajabuajabu, kwa hiyo inabidi uwe na fedha lakini pia uwe mjanja kuchagua.
Baada ya purukushani kubwa, hatimaye nilikuwa nimeshakamilisha kazi yangu, kapu langu lilikuwa limejaa samaki wakubwawakubwa, nikajitwisha na kusogea pembeni ambapo nilianza kuwatengeneza vizuri, nilipohakikisha kila kitu kipo sawa, nilijitwisha kapu langu na kuelekea kituoni.
Nilisubiri daladala na ilipofika, kazi nyingine ya kugombea kupanda ilianza, nikiwa na kapu langu nilifaiti kisawasawa, nikaingia na kufanikiwa kupata siti. Mwili mzima nilikuwa nanuka shombo mpaka mwenyewe nikawa najishtukia.
Uzuri ni kwamba ndani ya daladala hiyo, sikuwa peke yangu niliyekuwa na kapu la samaki, kuna akina mama wengine nao walikuwa na ndoo zao, basi safari ikaanza. Ujue kuna biashara nyingine unapozifanya haitakiwi uwe na aibu kabisa, vinginevyo unaweza kufa njaa.
Binafsi nilikuwa naipenda kazi yangu na kamwe nilikuwa sina aibu kabisa kwa sababu nilikuwa najiamini. Basi nilienda mpaka nyumbani, nikashuka kwenye daladala na kapu langu na kwenda mpaka uani ambako sikuwa na muda wa kupoteza, ilibidi niwaandae samaki haraka kwa ajili ya kuwahi kuingia mtaani mapema. Wale ambao mama mdogo alikuwa akiwatengeneza, nilimtengea, nikachukua wa kwangu na kuwaweka kwenye barafu, nikaenda kuoga na kubadilisha nguo zangu, baada ya kuhakikisha kwamba nimetoka ‘chicha’, nilichukua kapu langu na kuingia mtaani.
Nilianza kwa kupita kwa wateja wangu wa siku zote, nikawa nawachangamkia vizuri na kuwachagulia samaki wazuri, nilipita kwanza kwenye mabanda ya mama ntilie kadhaa ambao kila siku ilikuwa ni lazima niwapitishie, kisha baada ya hapo nikawapitishia wateja wangu wa majumbani na kumalizia mtaani.
“Mbona leo umechelewa jamani Chande!”
“We acha tu, nimechelewa sana kuamka leo!”
“Kwa nini?”
“Shughuli ya jana unafanya mchezo, Sandra nashukuru sana mpenzi.”
“Shhh! Mume wangu yupo, atakusikia!” alisema Sandra huku akinioneshea ishara ya kuufunga mdomo wangu.
“Kumbe umeolewa?”
“Ndiyo! Mume wangu leo hajaenda kazini,” alisema huku akinioneshea ishara kwamba atanipigia simu.
“Umenichagulia samaki wazuri lakini?” alisema kwa sauti ya juu, nadhani alitaka mumewe ayasikie maneno hayo ya mwisho.
“Wazuri sana, yaani hata shemeji leo lazima akusifie kwa mapishi,” nilisema huku kawivu kakinichoma ndani ya moyo wangu, basi kwa makusudi Sandra akageuka na kuanza kuingia ndani. Nadhani alijua kwamba namtazama, akaamua kunichoma moyo wangu kisawasawa, akawa anajitingisha kwa makusudi.
Nilibaki nikimeza funda la mate kama mjamzito aliyeona ndimu huku nikimsindikiza kwa macho mpaka alipopotelea ndani. Nilibaki nimesimama pale nje na kapu langu, mwisho nikaamua kupiga moyo konde na kuendelea na mishemishe zangu.
“Sasa kama Sandra ameolewa, aliweza kuja kwangu usiku uliopita na kukaa mpaka usiku sana? Alimuagaje mumewe? Lakini mbona sijawahi kumkuta mwanaume au basi angalau nione nguo za kiume zikiwa zimeanikwa nje?” niliendelea kujiuliza maswali mengi wakati naendelea na safari yangu ya kutembeza samaki.
Nilipovuka mataa ya Magomeni, ilibidi nitafute sehemu ya kukaa kwa sababu ishu ya Sandra ilikuwa imenichanganya sana kichwa changu, huwezi kuamini nilijikuta nikimpenda sana Salma, na kitendo cha kuniambia eti alikuwa na mume wake, kilinifanya moyo wangu ujawe na wivu mkali kwelikweli.
Baada ya kukaa kwa dakika kadhaa kwenye kivuli, basi niliamka na kuendelea kutembeza samaki, safari hii eti nikijiapiza moyoni kwamba kilichonileta mjini ni kutafuta fedha, siyo kutafuta wanawake. Ilikuwa ni sawa na kamchezo ka sungura sizitaki mbichi hizi baada ya kuzikosa ndizi kwenye mkungu.
Ninachoshukuru ni kwamba sikuchelewa sana kumaliza mzigo, nikapiga mahesabu na kuona kwamba kila kitu kilikuwa kimeenda vizuri, basi nikamshukuru Mungu wangu na kuanza safari ya kurudi nyumbani.
Sikuona sababu ya kupanda daladala, kutoka Magomeni mpaka Kinondoni, ulikuwa ni umbali ambao mara kibao huwa natembea kwa miguu, si unajua tena mimi siyo mwanaume wa Dar!
Jua lilikuwa linapiga kwelikweli, kapu langu nilikuwa nimeliweka kwenye mfuko na kulikunja vizuri kiasi kwamba kama ningekutana na mtu, asingeweza kuelewa kwa haraka kwamba nilikuwa natoka kuuza samaki, shida ilikuwa moja tu, kutokana na kuwashikashika sana samaki, nilikuwa nanuka shombo la nguvu.
Mara simu yangu ilianza kuita, hapo nilikuwa nimekaribia Mkwajuni, niliitoa na kutazama namba ya aliyekuwa anapiga, ilikuwa ni namba ngeni. Shida ya kisimu changu, muda mwingine mtu anaweza kuwa anakupigia lakini ukashindwa kupokea kwa sababu ‘batani’ nyingine zilikuwa haziminyiki.
Huwezi kuamini, nilihangaishana nacho kutaka kupokea lakini kiligoma mpaka simu ikakatwa. Mara simu ikaanza kuita tena, safari hii nililazimisha na kweli nikafanikiwa kuipokea.
“Haloo!”
“We sharobaro muuza samaki!”
“Nambie sista! Nikuletee samaki?”
“Ushajua kwanza unaongea na nani?”
“Si mama Chausiku muuza ubwabwa!”
“Wee! We! We! Ishia hapohapo, yaani sharobaro umeamua kunitukana, najuta kukupigia simu, na kisimu chako kibaaaya kinakoroma tu, kwa heri,” ilisikika sauti upande wa pili kisha simu ikakatwa. Sikuwa nimemjua ni nani, lakini kwa jinsi alivyokuwa anaongea kwa mapozi na kunitaniatania, nilihisi anaweza kuwa ni yule dada bonge tuliyepanda naye kwenye daladala asubuhi akanitoa nishai.
“Haloo! Samahani auntie, kwani wewe ni nani? Nisamehe nilichanganya namba yako na ya mama Chausiku mteja wangu wa samaki, si unajua tena simu yangu mbovu kioo,” nilisema safari hii mimi nikiwa ndiyo niliyepiga.
“Mie Mimah bwana! Tulipanda wote daladala asubuhi!” alisema, moyo wangu ukanilipuka paah!
“Aah...eh! Sista, nambie!” nilibabaika huku nikihisi mate yakinikauka ghafla mdomoni, nikamsikia akiangua cheko fulani hivi la kichokozi, eti akaniambia amekaa kazini akajikuta amenikumbuka na kuanza kucheka mwenyewe.
“Uko wapi kwani?”
“Narudi nyumbani, leo nimewahi kumaliza mzigo, naona una baraka sana,” nilisema na kumfanya azidi kucheka.
“Sasa ushamaliza mapema yote hii mi ntakula mboga gani?”
“Sasa wewe si ulisema huwa hupiki nyumbani? Ungeniagiza mapema, lakini usijali, nina wazo.”
“Wazo gani?”
“Kuna samaki mmoja nilikuwa nimemficha nyumbani kwa ajili ya mboga ya usiku, ngoja nikakuchukulie, kwa hiyo utakuja kumchukua wapi?”
“Whaooo! Umenifurahisha sana sharo wangu! Ngoja nitakuelekeza sehemu ya kuniletea, mbona leo nitafaidi,” alisema Mimah na kucheka kwa cheko fulani hivi la kichokozi sana, kisha akakata simu.
Nilijihisi kusisimka mwili mzima, nikawa najaribu kuvuta taswira ya kicheko kama kile, halafu nipo nae kwenye uwanja wa fundi seremala! Sijui nini kilitokea lakini nilishtukia mnara wangu wa mawasiliano ukianza kusoma 4G!
“Akinikaribisha kwake tu ameumia! Lazima leoleo kieleweke!” nilisema huku nikijaribu kujiweka vizuri, mara simu ikaanza tena kuita, alikuwa ni Mimah!
“Mi saa tisa nitakuwa nishafika, nikukute hapo Studio kwenye kituo cha mwendokasi, sawa sharo!” alisema Mimah, sauti yake tamu ikapenya kwenye masikio yangu na kunifanya nisikie raha ya ajabu, basi nikawa nagugumia tu, nikameza tena funda la mate kwa uchu kama fisi aliyeona mfupa.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 03




ILIPOISHIA:
“Mi saa tisa nitakuwa nishafika, nikukute hapo Studio kwenye kituo cha mwendokasi, sawa sharo!” alisema Mimah, sauti yake tamu ikapenya kwenye masikio yangu na kunifanya nisikie raha ya ajabu, basi nikawa nagugumia tu, nikameza tena funda la mate kwa uchu kama fisi aliyeona mfupa.
SASA ENDELEA...
Basi baada ya kumaliza kuzungumza naye, niliongeza mwendo, nikawa natembea harakaharaka huku nikijiuliza nitampata wapi samaki wa kumpa maana nilishamuahidi kwamba nitamuwekea wakati ukweli ni kwamba sikuwa nimebakiza samaki wowote.
Na hata kama angekuwa amebaki, isingekuwa rahisi kwa mimi kurudi mpaka nyumbani na kumchukulia yeye, ningemwambia nini mama mdogo? Ninegkuja kumjibu nini baba mdogo usiku akirudi?
Njia pekee niliyoiona inafaa kwa wakati huo, ilikuwa ni kwenda kumnunulia samaki kwa watu wengine. Kwa bahati nzuri, nilikuwa na namba za simu za wauza samaki wenzangu, nikampigia mmoja aitwaye Rama Chunusi. Yeye alikuwa pia akiuzia samaki Kinondoni na kwa bahati nzuri, hakuwa amemaliza mzigo.
Nilimuomba tuonane naye, kweli tukakutana nikachagua samaki mmoja mkubwa ambaye alikuwa akimuuza kwa bei ya shilingi elfu kumi na tano lakini kwa kuwa ni mshkaji wangu, alikubali kuniuzia kwa shilingi elfu kumi.
“Duh! Hata siamini, unampeleka wapi kwani?”
“Kuna dili nimepata, hii hela mbona inaenda kurudi,” nilimwambia Rama Chunusi, basi akacheka sana kwani nilikuwa nimempa riziki, tukaachana, nikamtia yule samaki kwenye kapu langu na breki ya kwanza ilikuwa ni nyumbani.
“Vipi, hujamaliza mzigo mpaka saa hizi?”
“Amebaki mmoja tu nataka nioge kwanza kisha nikaendelee kutafuta wateja, nilimwambia mama mdogo ambaye nilimkuta akiendelea kukaanga samaki kwa ajili ya kuwauza pale kwenye genge alilofunguliwa na baba mdogo.
Niliingia ‘magetoni’ kwangu na harakaharaka nilichukua maji na kwenda kuoga, nikajisugua kwelikweli kuhakikisha naondoa shombo yote, baada ya hapo nilirudi chumbani, nikachagua nguo safi na nzuri, ‘nikajipigilia’ na kujiangalia kwenye kioo kidogo kilichopasuka upande, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu.
Baada ya kumaliza kujiandaa, niliangalia saa yangu ya mkononi, tayari ilikuwa ni saa nane, basi nikamchukua yule samaki na kumuweka kwenye mfuko wa plastiki, nikaweka na mabarafu machache kisha nikatoka.
“Sasa wewee, kwanza kwa nini samaki umemuweka humo kwenye mfuko huo? Kwa nini usimuweke kwenye kapu? Akichina huyo huoni ni hasara kubwa hiyo? Halafu mbona unataka kuondoka wakati muda wa chakula umefika?”
“Kuna mteja namuwahishia mara moja, nakuja sasa hivi.”
“Ndiyo kupendeza kiasi hicho?”
“Aah mamdogo, mbona mi kupendeza kawaida yangu?” nilisema huku nikitoka harakaharaka kwa sababu sikutaka kuendelea kupoteza muda, mama mdogo akawa ananitazama na nikamsikia akiguna, sikumjali, ilikuwa ni lazima nikaonane na Mimah.
Basi muda mfupi baadaye, tayari nilikuwa nimefika Studio, nikatafuta sehemu na kukaa, huku kisimu changu kikiwa mkononi, nikisubiri kwa shauku kubwa ya kuonana tena na Mimah. Ilipofika mishale ya saa tisa hivi, simu iliita, kuangalia aliyekuwa anapiga, alikuwa ni Mimah.
“Uko wapi?”
“Nipo hapa Studio karibu na stendi ya mwendokasi, nimekaa pembeni huku.”
“Umevaaje?”
“Nimevaa fulana nyekundu,” nilisema, muda mfupi baadaye, niliona gari dogo likiwasha indiketa na kupaki kituoni, simu yangu ikaanza kuita tena, harakaharaka nikaipokea.
“Nashuka kwenye hili gari dogo lililopaki hapa kituoni, umeniona,” alisema, basi macho yangu yakatua kwake, alikuwa ameshashuka na sasa alikuwa anamalizana na dereva. Nilisogea pale karibu huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kwelikweli, sijui kwa sababu gani nilipaniki kiasi hicho.
“Aah! Sharoo, umetoka chicha,” alisema alipogeukana kuniona, nikaishia kucheka tu, Mimah alikuwa anapenda sana masihara, basi tukasalimiana kwa kupeana mikono, nikawa namtazama kwa macho yaliyobeba hisia.
“Hebu tumuone huyo samaki mwenyewe?” alisema palepale kituoni, nilijisikia aibu kwa sababu nilijua kuna watu wanatutazama, basi nikampa ulemfuko, akaufungua.
“Whaooo! Mkubwa na mzuri kwelikweli, ulijuaje kama mi nawapenda sana changu?” alisema kwa furaha, basi nikawa nachekacheka tu.
“Sasa itabidi ukanisaidie kumtengeneza, si unaweza?”
“Ndiyo! Naweza,” nilijibu harakaharaka kwa sababu kile nilichokuwa nimekitaka sasa kilikuwa kinaenda kutimia. Tuliingia kwenye Bajaj, akamuelekeza dereva sehemu ya kutupeleka, tukaondoka pale kituoni huku watu wengi wakiwa wanamkodolea macho.
“Nambie,” alisema Mimah huku akinigeukia na kunitazama usoni, nikatabasamu, na yeye akatabasamu.
“Pole na kazi!”
“Ahsante, pole na wewe! Mi nawapenda sana vijana wanaojishughulisha,” aliniambia, tukaendelea na stori za hapa na pale, dakika chache baadaye tukawa tayari umeshafika. Tuliteremka, akamlipa dereva wa Bajaj hela yake, akaondoka na kutuacha pale nje, nikawa nashangaashangaa nikiwa sijui nyumba yenyewe ni ipi maana kulikuwa na nyumba tatu, zote za kifahari zikiwa zimepangana.
“Karibu mgeni,” alisema Mimah na safari hii akanishika mkono, nilihisi raha ya ajabu kutokana na jinsi mikono yake ilivyokuwa laini, basi akaniongoza kwenye geti jeusi kwenye moja kati ya nyumba hizo tatu. Akatoa funguo kwenye mkoba wake na kufungua geti la nje.
“Kwani unaishi peke yako?”
“Ndiyo, niko peke yangu, dada wa kazi amesafiri yeye ndiyo huwa ananipa kampani.”
“Kwani shemeji yuko wapi?” nilimuuliza kichokozi, akacheka sana na kuniambia kwamba hana shemeji.
“Haa! Kwa hiyo na uzuri wako wote huo unaishi peke yako?”
“Wanaume wengi ni waongo sana ndiyo maana nimeamua kuishi mwenyewe kwanza, hivi sasa nimeelekeza nguvu zangu kwenye kazi na maendeleo kwanza, mambo ya mapenzi baadaye,” alisema, safari hii akionesha kuwa siriasi kidogo.
Tuliingia ndani ya geti, ndani kulikuwa na mandhari nzuri sana, bustani za maua zilizokuwa zimepangiliwa vizuri, zilisababisha eneo la ndani kuwe na mvuto wa aina yake. Tulielekea mpaka kwenye mlango wa kuingilia ndani, akafungua na kuvua viatu, na mimi nikavua viatu vyangu, tukaingia ndani.
“Nisubiri nikabadilishe nguo maana nahisi nimechoka sana,” alisema Mimah kichovu, akaubwaga mkoba wake kwenye kiti na kuniacha nikiwa nimekaa pale, nikawa namsindikiza alivyokuwa akitembea kwa kujiachia. Alipofika koridoni, sijui nini kilimtuma kugeuka, akanibamba nikiwa namkodolea macho, akacheka sana.
“Una vituko sana wewe ujue, kwa nini sasa unaniangalia hivyo?” aliniambia huku akirudi pale nilipokuwa nimekaa, nikaona ‘nijilipue’ tu, nikamwambia:
“Ujue we mzuri sana Mimah, nasikia burudani kubwa sana ndani ya moyo wangu nikikutazama,” nilimwambia, akacheka sana na kuja kunipiga kakibao ka kichokozi mgongoni, nikaitumia vyema nafasi hiyo kwa kupitisha mkono wangu na kumgusa kiuno, nikawa ni kama namjaribu nione atakachofanya.
“Nini bwana! Mbona mkorofi hivyo muuza samaki,” alisema, tukacheka sana, mara akainama mbele yangu na kuuchukua ule mfuko uliokuwa na samaki pale chini, ni kama alifanya kusudi kwa sababu alipoinama, nguo yake ilinyanyuka kwa nyuma na kuyafanya mapaja yake manene, yaliyokuwa yamenona yaonekane vizuri kwenye mboni za macho yangu, nikawa ni kama nimepigwa na shoti ya umeme.
“Kanichukulie kisu na bakuli lenye maji nikutengenezee samaki wako,” nilimwambia huku nikiinuka na kumsogelea kabisa mwilini, akageuka na kusababisha tugusane, tukawa tunatazamana huku mkononi akiwa na ule mfuko wenye samaki, kwa mara ya kwanza nilimuona akijisikia aibu, nikajua mambo yanakaribia kujipa.
Nilipitisha tena mkono kiunoni kwake, akatulia huku akiendelea kunitazama kwa macho yaliyojawa na aibu za kikekike, nikapitisha mkono mwingine na kukishika vizuri kiuno chake, akashtuka kidogo na kuanza kunitazama kwa macho yake mazuri ambayo sasa alikuwa akiyarembua.
Naye akapitisha mikono yake mabegani kwangu, tukawa tunaendelea kutazamana huku pepo mchafu akiwa ameshanipanda, nikamvutia kifuani kwangu, akaja mzimamzima, nikambusu shingoni, akashtuka kama aliyepigwa na shoti ya umeme. Hata sijui ujasiri huo niliutoa wapi kwa sababu kama nilivyosema, Mimah alikuwa kifaa haswaa!
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 04




ILIPOISHIA:
Naye akapitisha mikono yake mabegani kwangu, tukawa tunaendelea kutazamana huku pepo mchafu akiwa ameshanipanda, nikamvutia kifuani kwangu, akaja mzimamzima, nikambusu shingoni, akashtuka kama aliyepigwa na shoti ya umeme. Hata sijui ujasiri huo niliutoa wapi kwa sababu kama nilivyosema, Mimah alikuwa kifaa haswaa!
SASA ENDELEA...
“Unataka nini jamani wewe!” aliniuliza Mimah kwa sauti ya upole iliyokuwa inatokea puani, nikazidi kuchanganyikiwa.
“Mimi? Una...onge...a na mi...” nilishindwa kumalizia nilichokusudia kukisema, mashetani yalikuwa tayari yameshanipanda, basi nikamsogeza Mimah taratibu mpaka kwenye sofa na kumuweka vizuri, nikamuinamia na muda mfupi baadaye, tuligusanisha ndimi zetu, macho yake safari hii alikuwa ameyafumba.
Tuliendelea kuwaiga njiwa wanavyoyalisha makinda yao, mikono yangu ikawa inafanya utalii kwenye vivutio mbalimbali kwenye mwili wake mkubwa, na yeye akawa anafanya hivyohivyo kwangu.
Kwangu lile lilikuwa ni zaidi ya zali la mentali kwa hiyo sikuwa na muda wa kupoteza. Kumbukumbu za pambano lililopita zilikuwa zikipita ndani ya kichwa changu na kunifanya nijenge picha ya jinsi nitakavyofaidi kuwa na Mimah. Utalii niliokuwa naufanya, ulimlegeza sana Mimah na kuyaamsha mashetani yake, ikawa kila ninachomuelekeza akatii bila shuruti.
Akiwa bado amevalia nguo zilezile alizotoka nazo kazini, nilifanikiwa kufungua kishikizo cha nguo ya juu aliyokuwa ameivaa, kwa ufundi mkubwa nikapitisha mikono nyuma na kufyatua kichuma cha ‘bra’ na kusababisha ilegee, nikapitisha mkono kwa ndani na kuyashika maembe bolibo yaliyokuwa yamejaa vizuri kwenye kifua chake, Mimah akiwa ni kama hakutegemea kitendo hicho, alitoa ukelele fulani ulioyaburudisha sana masikio yangu.
Kwa ridhaa yake akamalizia kuyavua magwanda ya juu ili kunipunguzia usumbufu usikokuwa wa lazima, macho yangu yakatua kwenye kifua chake kilichokuwa kimejaa vizuri, nikapeleka mdomo kwenye ncha moja ya embe bolibo, akashtuka tena na kutoa ukelele mwingine uliozidi kuniburudisha kwelikweli.
Nilitaka kuhamia kwenye ncha nyingine lakini alining’ang’ania na kunikandamizia palepale kuonesha kwamba alikuwa amenogewa, nikaendelea kufanya kile alichokitaka, akaanza kunisaula magwanda yangu, moja baada ya jingine.
Sikutaka kubaki nyuma, na mimi nikawa naendelea ‘kumnyonyoa’ manyoya yake kwa ufundi mkubwa, muda mfupi baadaye, alibaki na kufuli tu, na mimi nikawa nimeshavaa suti ya kulalia.
Mara nikashtukia Mimah amemvamia mkuu wa kaya na kumsabahi kwa mikono yake miwili, akiwa ni kama anampima kimo chake, akanigeukia na kunitazama kwa macho yaliyokuwa yametawaliwa na mshangao akiwa ni kama haamini alichokutana nacho.
“Mh! Wewe!” alisema Mimah kwa sauti iliyotokea kwenye pua zake.
“Nini!”
“We ni noma,” alisema Mimah huku akitabasamu, mikono yake ikiendelea kumpetipeti mkuu wa kaya ambaye sasa alishakaa mguu sawa kama afande anayesubiri kuanza kucheza gwaride.
Nikiwa nahangaika kujiweka vizuri, si nikashtukia Mimah amekamata kipaza sauti na kuanza kuimba bwana! Alianza kwa kuimba nyimbo za taratibu, akawa anaongeza kasi taratibu na kunifanya nijihisi kama nipo kwenye dunia tofauti kabisa na hii iliyojaa dhambi.
Baada ya kushuka mistari ya kutosha, aliniweka vizuri kisha akamuelekeza mkuu wa kaya sehemu ya kuelekea, akawa anamsindikiza taratibu huku akiugulia kwa mbali, macho yake akiwa ameyafumba, akaanza kufanya kama mpishi anayekuna nazi.
Kiukweli pamoja na kujifanya mjanjamjanja sana, kila kilichokuwa kinatokea kilikuwa kipya kabisa kwangu, hali iliyofanya nianze kupiga nduru.
Kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele, ndivyo alivyokuwa anaongeza kasi na japokuwa kimwonekano Mimah alikuwa tipwatipwa, alikuwa mwepesi kwelikweli, watoto wa mjini wanasema kibonge mwepesi.
Sijui ni nini kilichomtokea kwa sababu ilifika mahali na yeye akawa anapiga nduru mithili ya mtu anayeomba msaada lakini haachi kile alichokuwa anakifanya, kufumba na kufumbua nikambinua mithili ya wanasarakasi na kumtoa pale juu kwa sababu niliona kama ananichelewesha, yeye akawa kwa chini huku akinimwagia mvua ya mabusu.
Sasa nilipata stamina vizuri, nikaanza kusakata kabumbu kwa kasi kubwa huku nikijitafuna mithili ya mtu anayetafuna ‘bablish’ wakati ukweli ni kwamba sikuwa nikitafuna bablish, Mimah akaendelea kuugulia kwa sauti na haukupita muda mrefu, alianza kutetemeka kama ‘jenereta’, akanikamata kwa nguvu na kupasua dafu kwa nguvu.
Ni kama alikuwa amenishtukiza kwa hiyo nilimvutia kasi kidogo, alipodondokea upande wa pili nilimfuata na kuendelea na mtanange huo, mpira ukawa unachezwa nusu uwanja na haukupita muda mrefu, nikawa nimeingia kwenye ‘boksi’ na kufumua shuti kali lililozama moja kwa moja wavuni.
Raha ya mechi zenye ushindani mkali kama ile ya Taifa Stars na Uganda, huwa ni mabao tu, ulikuwa ushindi mtamu mno! Nikawa namtazama Mimah nikiwa ni kama siamini kwamba hatimaye kidume nimeangusha mbuyu kwa shoka!
“Wewe!” alisema baada ya kufumbua macho na kuniona nikiwa nimejilaza pembeni yake nikiwa namtazama!
“Nini!”
“Ndiyo nini hivyo!”
“Kwani vipi?”
“Umenifanyaje hivi!” alisema Mimah, tukaanza kucheka huku aibu za kikekike zikiwa zimemtawala.
“Kwani imekuwaje mpaka tukawa hivi?” alisema Mimah huku akijizoazoa na kuinuka, akakusanya magwanda yake na kuanza kutembea huku akijitingisha, akionesha kuchoshwa sana na ligwaride nililomchezesha.
“Njoo uniogeshe!” alisema, harakaharaka nikakurupuka pale nilipokuwa nimejilaza huku bado nikiwa na suti yangu ya kulalia, nikawa namfuata huku nikiendelea kupata burudani ya aina yake kwa kutazama mandhari yake ya nyuma, bila kizuizi chochote.
“Umejifunzia wapi haya mambo maana mh! Siyo mchezo!”
“Jandoni!”
“Jandoni? Siku hizi kuna mambo ya jando?”
“Sisi kijijini kwetu tunaendelea , mnakaa porini wiki tatu!”
“Kumbe ndiyo maana... mi nilijua wewe ni mwanaume wa Dar es Salaam!” alisema Mimah, tukacheka kwa pamoja. Tayari tulishafika kwenye mlango wa chumba chake cha kulala.
“Karibu mume wangu!” alisema Mimah huku akitaka kupiga goti moja kama wanavyofanyaga baadhi ya makabila, hasa Wasukuma, nikacheka sana. Tuliingia chumbani kwake wote tukiwa kwenye suti zetu za kulalia na safari ya kuelekea kuoga, ilibadilika na kuwa safari ya matumaini!
Akazitupa nguo zake kwenye tenga la nguo chafu an kunisogelea, tukagandana tena kama ruba. Chumba chake kilikuwa kizuri kwelikweli lakini kwa wakati huo sikuwa na muda wa kukichunguza, nilikuwa na kazi maalum ambayo ilikuwa ni lazima niimalize haraka iwezekanavyo.
“I love you so much!” (Nakupenda sana mpenzi!) alisema Mimah huku akiwa amenikumbatia kwa nguvu, taratibu akaniongoza kuelekea bafuni huku tukiendelea kugandana kama ruba. Bafu lilikuwa safi kwelikweli, unaweza hata kulala humohumo, akafungulia bomba la mvua, maji yakawa yanatiririka taratibu na kufanya tuwe mithili ya watu wanaonyeshewa na mvua.
Msisimko nilioupata ulikuwa mkubwa sana, mara mkuu wa kaya akakurupuka kutoka kwenye maficho yake, Mimah akamtazama mkuu wa kaya kisha akanitazama usoni, aibu za kikekike zikiwa zimemjaa, akageuka na kunipa kisogo kisha akamkamata tena mkuu wa kaya na kumuelekeza njia ya kupita huku akiwa ni kama anataka kuokota kitu sakafuni.
Je, nini kitafuatia?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom