VAN HEIST
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 1,434
- 617
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 11
sehemu iliyopita niliishia pale
mzee Kibandiko aliyekuwa akifuatilia
mazungumzo kati ya kijana wake na Rhoda
binti aliyeonesha kumpenda Beka lakini Beka
hakuwa na habari naye jambo lililomkera
sana mzazi wake na kumwita ----- . Je ,
kilifuatia nini? Songa mbele na uhondo huu. . .
ale kibarazani , Beka alimuaga Rhoda lakini
msichana huyo aliyekuwa na shepu tata na
kila alipotabasamu vishimo vilitokea kila
upande wa mashavu yake , aliendelea
kumbembeleza amsindikize japo kidogo .
Rhoda kama nilivyokuambia nataka
kumsaidia mama kuchota maji wewe nenda
tu ila nashukuru kwa kunitembelea maana
haijawahi kutokea , Beka alimwambia Rhoda.
Haijawahi tokea nini? Rhoda alimuuliza.
Si kupiga stori na msichana kwa muda wote
huo, tena kama mama ametusikia tukiongea
lazima ataniuliza , Beka alimwambia Rhoda .
Atakuuliza nini, kwani yeye hapendi
wakamwana? Rhoda alimuuliza Beka .
Kufuatia msichana huyo kumuuliza hivyo
Beka , mzee Kibandiko aliyekuwa akisikiliza
kila walichoongea alitabasamu na kumfagilia
sana Rhoda . Huyu binti ana akili na
kampenda sana mwanangu , sema Beka
mwenyewe haelewi chochote , waliosema
penye miti hapana wajenzi hawakukosea ,
mzee huyo aliwaza .
Rhoda, suala la mama kuhitaji wakamwana
halipo na kwa upande wangu sihitaji kuwa na
msichana , mimi ni mwendo wa kujisomea tu
mpaka kieleweke, Beka alimwambia .
Kwa kuwa muda ulikuwa umekwenda na
msichana huyo kuhitajika kwenda kupika
kwao , akiwa mnyonge alimuaga Beka na
kuahidi wangekutana siku nyingine,
akaondoka.
Njiani Rhoda alijisemea kwamba kwa jinsi
vijana wenye rika la Beka walivyokuwa
wakimsumbua kumtaka kimapenzi na licha
ya kumuonesha dalili za kumpenda Beka na
kijana huyo kuwa na domo zege, alikuwa na
tatizo tu !
Si bure, yaani nimemfuata mpaka kwao na
kumuonesha hisia zangu lakini kashindwa
kunitokea , yule atakuwa mgonjwa ila
nitafanya kila njia kujua kama yupo fiti au la,
Rhoda alijisemea moyoni .
Huku nyuma baada ya msichana huyo
kuondoka, Beka aliingia ndani na kukutana
koridoni na baba yake ambaye alimkata jicho
na kwenda kukaa sebuleni.
Beka aliyemjua vizuri mzazi wake
anavyokuwa akikerwa na jambo akawa
anajiuliza alikuwa kaharibu wapi bila
mafanikio.
Mbona sikumbuki kama kuna kazi alinipatia
sijaifanya, nitakuwa nimekosea wapi ? Beka
aliyekuwa ameketi chumbani kwake alijiuliza .
Akiwa anatafakari hivyo , aliona mlango wa
chumba chake ukifunguliwa kisha baba yake
aliingia na kusimama katikati ya kitanda na
mlango .
Kwa jinsi mzee huyo alivyokuwa, moyo wa
Beka ukapiga paa kwani alijua alikuwa
kaharibu tu mahala na kwa akili ya fasta
alijua baba yake hakupendezwa na ujio wa
Rhoda pale nyumbani kwao .
Baba nahisi nimekukosea naomba
unisamehe , Beka alimuwahi mzazi wake .
Umenikosea nini? mzazi wake alimuuliza.
Beka alimwambia kitendo cha kumkuta
akizungumza na Rhoda pale kibarazani ,
mzazi wake akamwambia hakuwa na tatizo
na Rhoda isipokuwa alikuwa anataka kujua
kwa nini alikuwa hasafishi banda la mbwa .
Kufuatia kuulizwa hivyo , Beka aligundua ni
kweli alipitisha siku moja bila kusafisha
banda hilo lakini kabla hajajitetea mzazi
wake alimdaka na kwenda naye sebuleni.
Alipofika sebule alichukuwa fimbo aliyoificha
chini ya kiti na kuanza kumtandika Beka ,
Beka akaanza kulia .
Leo utanitambua, sipendi kijana
mzembemzembe hata kidogo, mzee
Kibandiko aliendelea kumtandika Beka bila
kijana wake kujua kama sababu haikuwa
kutofagia banda la mbwa isipokuwa
kushindwa kumtokea Rhoda aliyejileta
nyumbani kwao bila kuitwa.
Huku akimtandika moyoni alikuwa akisema :
Wewe mtoto mjinga sana , binti mzuri kama
Rhoda kajileta mwenyewe wewe unashindwa
kumpa maneno matamu unamwambia
unataka kumsaidia mama yako kuchota maji,
si upuuzi huo?
ITAENDELEA HAPA HAPA
WABALLA Inc miss nuru Lmntrix
sehemu iliyopita niliishia pale
mzee Kibandiko aliyekuwa akifuatilia
mazungumzo kati ya kijana wake na Rhoda
binti aliyeonesha kumpenda Beka lakini Beka
hakuwa na habari naye jambo lililomkera
sana mzazi wake na kumwita ----- . Je ,
kilifuatia nini? Songa mbele na uhondo huu. . .
ale kibarazani , Beka alimuaga Rhoda lakini
msichana huyo aliyekuwa na shepu tata na
kila alipotabasamu vishimo vilitokea kila
upande wa mashavu yake , aliendelea
kumbembeleza amsindikize japo kidogo .
Rhoda kama nilivyokuambia nataka
kumsaidia mama kuchota maji wewe nenda
tu ila nashukuru kwa kunitembelea maana
haijawahi kutokea , Beka alimwambia Rhoda.
Haijawahi tokea nini? Rhoda alimuuliza.
Si kupiga stori na msichana kwa muda wote
huo, tena kama mama ametusikia tukiongea
lazima ataniuliza , Beka alimwambia Rhoda .
Atakuuliza nini, kwani yeye hapendi
wakamwana? Rhoda alimuuliza Beka .
Kufuatia msichana huyo kumuuliza hivyo
Beka , mzee Kibandiko aliyekuwa akisikiliza
kila walichoongea alitabasamu na kumfagilia
sana Rhoda . Huyu binti ana akili na
kampenda sana mwanangu , sema Beka
mwenyewe haelewi chochote , waliosema
penye miti hapana wajenzi hawakukosea ,
mzee huyo aliwaza .
Rhoda, suala la mama kuhitaji wakamwana
halipo na kwa upande wangu sihitaji kuwa na
msichana , mimi ni mwendo wa kujisomea tu
mpaka kieleweke, Beka alimwambia .
Kwa kuwa muda ulikuwa umekwenda na
msichana huyo kuhitajika kwenda kupika
kwao , akiwa mnyonge alimuaga Beka na
kuahidi wangekutana siku nyingine,
akaondoka.
Njiani Rhoda alijisemea kwamba kwa jinsi
vijana wenye rika la Beka walivyokuwa
wakimsumbua kumtaka kimapenzi na licha
ya kumuonesha dalili za kumpenda Beka na
kijana huyo kuwa na domo zege, alikuwa na
tatizo tu !
Si bure, yaani nimemfuata mpaka kwao na
kumuonesha hisia zangu lakini kashindwa
kunitokea , yule atakuwa mgonjwa ila
nitafanya kila njia kujua kama yupo fiti au la,
Rhoda alijisemea moyoni .
Huku nyuma baada ya msichana huyo
kuondoka, Beka aliingia ndani na kukutana
koridoni na baba yake ambaye alimkata jicho
na kwenda kukaa sebuleni.
Beka aliyemjua vizuri mzazi wake
anavyokuwa akikerwa na jambo akawa
anajiuliza alikuwa kaharibu wapi bila
mafanikio.
Mbona sikumbuki kama kuna kazi alinipatia
sijaifanya, nitakuwa nimekosea wapi ? Beka
aliyekuwa ameketi chumbani kwake alijiuliza .
Akiwa anatafakari hivyo , aliona mlango wa
chumba chake ukifunguliwa kisha baba yake
aliingia na kusimama katikati ya kitanda na
mlango .
Kwa jinsi mzee huyo alivyokuwa, moyo wa
Beka ukapiga paa kwani alijua alikuwa
kaharibu tu mahala na kwa akili ya fasta
alijua baba yake hakupendezwa na ujio wa
Rhoda pale nyumbani kwao .
Baba nahisi nimekukosea naomba
unisamehe , Beka alimuwahi mzazi wake .
Umenikosea nini? mzazi wake alimuuliza.
Beka alimwambia kitendo cha kumkuta
akizungumza na Rhoda pale kibarazani ,
mzazi wake akamwambia hakuwa na tatizo
na Rhoda isipokuwa alikuwa anataka kujua
kwa nini alikuwa hasafishi banda la mbwa .
Kufuatia kuulizwa hivyo , Beka aligundua ni
kweli alipitisha siku moja bila kusafisha
banda hilo lakini kabla hajajitetea mzazi
wake alimdaka na kwenda naye sebuleni.
Alipofika sebule alichukuwa fimbo aliyoificha
chini ya kiti na kuanza kumtandika Beka ,
Beka akaanza kulia .
Leo utanitambua, sipendi kijana
mzembemzembe hata kidogo, mzee
Kibandiko aliendelea kumtandika Beka bila
kijana wake kujua kama sababu haikuwa
kutofagia banda la mbwa isipokuwa
kushindwa kumtokea Rhoda aliyejileta
nyumbani kwao bila kuitwa.
Huku akimtandika moyoni alikuwa akisema :
Wewe mtoto mjinga sana , binti mzuri kama
Rhoda kajileta mwenyewe wewe unashindwa
kumpa maneno matamu unamwambia
unataka kumsaidia mama yako kuchota maji,
si upuuzi huo?
ITAENDELEA HAPA HAPA
WABALLA Inc miss nuru Lmntrix