China ni nguvu chanya kwa amani na usalama barani Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111443458315.jpg


Kongamano la tatu la Amani na Usalama la China na Afrika limefanyika hivi karibuni mjini Beijing, China. Hii ni hatua muhimu kwa China na nchi za Afrika kuhimiza kwa pamoja "Pendekezo la Usalama Duniani" la China, na pia ni ushahidi mwingine kwa China kuchangia amani na usalama barani Afrika.

Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na Janga la COVID-19, mgogoro kati ya Russia na Ukraine, mabadiliko ya hali ya hewa na changamoto nyingine mbalimbali, amani na usalama barani Afrika zinakabiliwa na changamoto kubwa. Mwezi uliopita, mapinduzi ya kijeshi yalitokea nchini Niger, na kuleta changamoto nyingine mpya ya mapinduzi ya mara kwa mara yanayotokea miaka ya hivi karibuni barani Afrika. Kwa mujibu wa takwimu zisizo kamili, tangu 2020, kumekuwa na mapinduzi 13 barani Afrika, na maandamano na ghasia zisizohesabika zimesababisha vifo vya maelfu ya watu. Rais Xi Jinping wa China alitoa Pendekezo la Usalama Duniani kwa mara ya kwanza mwaka 2022, likichangia hekima na ufumbuzi wa China ili kutatua matatizo ya amani na usalama duniani. Kwa kuzingatia uhusiano wa kutegemewa kati ya China na Afrika, nchi za Afrika pia zinatarajia China ichukue nafasi kubwa katika kuchangia amani na usalama wa Afrika.

Wakati Kongamano hilo lilipoendelea, vyombo vya habari vya nchi za Magharibi vilianza "kutoa kejeli" tena, vikitaja kile kinachoitwa "upanuzi wa kijeshi wa China barani Afrika" na "ushindani wa nchi zenye nguvu". Juu ya kauli hizo za uchochezi, wasomi wengi wa Afrika wamekuwa wakizikanusha. Msomi wa masuala ya kimataifa wa Kenya Cavins Ardhill alisema kuwa "Pendekezo la Usalama Duniani" lilisisitiza kuunga mkono masuala ya Afrika kutatuliwa kwa njia ya kiafrika na kuchangia utatuzi wa amani katika suala la Pembe ya Afrika na changamoto nyingine zinazopamba moto barani Afrika. Hii ni tofauti kabisa na mtazamo wa nchi za Magharibi wa kutoa amri ya mwisho na kulazimisha katika suala la Pembe ya Afrika. Pia kuna vyombo vya habari vya Magharibi vinavyotafakari hili. Jarida la "Diplomat" la Marekani lilichapisha makala ikisema kwamba nchi za Magharibi zina "madoa ya kikoloni" barani Afrika na bado zinataka "kubadilisha" Afrika wakijifanya kama wazazi, huku China ikisikiliza matakwa ya Afrika, kufuatilia na kuitikia vipaumbele vya serikali.

Kama ilivyoelezwa katika makala ya jarida la Diplomat, kwa muda mrefu, nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani zimekuwa zikitoa ushawishi kwa nchi za Afrika kupitia kutoa misaada na mafunzo ya kijeshi, huku zikishiriki moja kwa moja katika utatuzi wa masuala ya usalama ya Afrika kupitia uingiliaji wa kijeshi na upatanishi wa kisiasa, ili kuongeza ushawishi wao katika mambo ya usalama barani Afrika. Katika miaka ya hivi karibuni, Marekani imeanza mkakati wa ushindani wa nchi zenye nguvu barani Afrika na kukuza uwepo wake wa kijeshi barani Afrika, ikiwa na lengo la kuweka mpango kwa ajili ya mkakati wake wa ushindani wa nchi zenye nguvu duniani. Hii sio tu imezuia uendeshaji wa utaratibu wa usalama wa kikanda kama vile wa Umoja wa Afrika, bali pia inazuia uhuru wa nchi za Afrika katika ujenzi wa amani na usalama.

Kwa upande mwingine, China, kama mshirika muhimu wa Afrika, daima imekuwa ikisisitiza kwamba Afrika si uwanja wa michezo ya nchi zenye nguvu, bali ni jukwaa kubwa la ushirikiano wa kimataifa. Katika msingi wa kuheshimu kikamilifu matakwa ya Afrika, kutoingilia mambo ya ndani, na kufuata kanuni za uhusiano wa kimataifa, China inatafuta njia za kushiriki katika masuala ya amani na usalama ya Afrika, ikiwa ni pamoja na kuimarisha mawasiliano ya kimkakati kati ya China na Afrika kwa kufanya mazungumzo kama Kongamano la Amani na Usalama la China na Afrika; kusaidia nchi za Afrika kuimarisha ulinzi wa nchi na ujenzi wa jeshi kupitia mazoezi ya pamoja ya kijeshi; ni nchi iliyotuma walinda amani kwa wingi zaidi barani Afrika kati ya wajumbe watano wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa; kupitia kuunga mkono maendeleo ya kiuchumi ya Afrika, imesaidia kuondoa mzizi wa machafuko... Ni nani hasa anayezingatia amani na usalama barani Afrika, nchi za Afrika zinafahamu vizuri mioyoni mwao.

Zaidi ya miaka 60 iliyopita, katika kupinga ubeberu na ukoloni, na kupigania uhuru na ukombozi wa taifa, China na nchi za Afrika zilijenga urafiki wa dhati. Kwa sasa, kupanuka kwa miungano ya kijeshi ya nchi za Magharibi kumetishia tena usalama duniani. Ushirikiano wa usalama kati ya China na Afrika sio tu utasaidia kutatua masuala ya usalama na maendeleo barani Afrika, bali pia utachangia amani na utulivu duniani. China na Afrika zinapaswa kuhimiza Pendekezo la Usalama Duniani kufanya kazi chanya katika kujenga jumuiya ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja katika enzi mpya, kukabiliana kwa pamoja changamoto za amani na usalama, na kulinda haki za binadamu wote duniani.
 
Waafrika hawana ujanja ni mwendo wa kubadili colonial master tu,mchina anatafuta rasmali na ardhi kwaajili ya watu wake mana uchina soon itakosa pa kukanyaga kwa sababu ya population.

Hakuna ngozi nyeupe yenye lengo la kutoa mwafrika kwenye umasikini,tupambane wenyewe tu huku tukitumia akili nyingi.
 
Mnaojua mkumbusheni waliohusika kuuza au kushikilia vitega uchumi vya nchi mbili majirani na Tanzania baada ya kupindukia muda wa kurejesha mkopo.

Mtoa mada kwa faida ya jukwaa tutajie chuo ulichojifunzia 'kupaka rangi' hadi kuushawishi umma kwamba nyeusi yaweza kuwa nyeupe.
 
Back
Top Bottom