China isingemchelewesha Lowassa

Namshangaa sana Makufuli kugombea wakati aligawa nyumba za serikali kwa mahawara zake, amelisababishia taifa hasara kubwa kwa kukamata meli ya uvuvi bila ushahidi, kutowalipa makandarasi pesa zao kwa wakati na hivyo kukuwa kwa riba...

Hizo nyumba alihongwa mamako? au ulihongwa wewe kimada. mijitu mingine! ndo maana mnaitwa ma mbumbumbu na malofa kumbe ni kweli
 
Ingekuwa China lowassa angekuwa marehemu saa hizi.
 
Ila jembe si ameshatangaza kiama kwa mafisadi.lazima atanyongwa tu hata kama itachukuwa miaka hamsini.
 

Adith yako inatufundisha nni?????
 
Hvi zile fedha za nyumba za umma zikizouzwa bei chee zilienda wap na zilifanyiwa shughuri gan na zilipatikana tsh ngp?Duuuuuuuh tanzania mafisadi wengi sna .
 
Ivi ukondoa ukada kuna pesa kiasi gani kimepotea na hiyo Baada ya lowassa kuondoka au mnafumba macho kwahyo chama kilichoasisi kiasi kikubwa cha wizi ndo kiendelee kutawara na mtu mmoja aondolewe ivi kuna nini vichwani humo kuhusu vivuko vibovu UPOTEVU as pesa wizara ya ujenzi escrow meremeta hayo hamyaoni ila richmond
 
Badala ya kulaumu Chadema na Lowasa kumpitisha Lowasa/yeye kugomea urais wakati ni fisadi tungelaumu serikali ya CCM kuhalalisha jambo hili.

Kwa nini mnashangaa kugombea urais fisadi kwa ubunge ikawa ni sawa tu? Shutma haimzuii mtu kutofanya shughuli za kujenga taifa, criminal kikatiba hawezi kugombea urais na criminal kisheria ni yule alie pelekwa court na kuthibitika.
 

Chagua unachotaka, hilo liko ndani ya uwezo wako lkn

Raisi wa V wa JMTZ ni Dr.Pombe Magufuli!

Mkuu tatizo unafanya siasa kama imani za kidini!! Kwa mtu mwenye akili anaejilewa hawezi kuzungumza kitoto namna hii, maana maamuzi ya nani aongoze TZ yapo mikononi mwa watz! Kama ni bao la mkono linakupa kiburi, hilo sahau na mtalisikia kwenye redio.
 
Angekuwa kishanyongwa, na watu tushasahau. ila na kwa magufuli watanyoooooka tuuu

Hivi unaelewa ulichokiandika ndugu au nawe ili mradi umeandika jamani wa TZ tujaribu kufikiria hata kidogo hizi tuhuma ina maana Tanzania fisadi ni Lowasa peke yake?
 
UMESOMA TAARIFA YA PPRA.? Suitor USHAHIDI KWA gazeti la chama NI UONGO
 
Kwanza wangemnyonga mwuza Nyumba za serikali Na kuwakamata wachina wenzao
 

CCM mtaji wao ni ujinga wa watanzania na wajinga wapo wengi kweli ambao hawaoni na wala hawasikii ukiwaambia mambo wanayofanya CCM,Mungu ibariki Tanazania,tusaidie tuone mabadiliko ya kweli tuone na hao wengine watatufikisha wapi naamini katika mabadiliko kwani nchi hii si ya CCM peke yao.
 
Kama ndiyo hivyo CCM iondoke tu maana wamemlea wenyewe mpaka hapo alipo.

Watuambie mabaya ya Watu wao wakiwa CCM siyo wasubirie wamehama.
 
Hizo nyumba alihongwa mamako? au ulihongwa wewe kimada. mijitu mingine! ndo maana mnaitwa ma mbumbumbu na malofa kumbe ni kweli

Ndugu jaribu kufiri. kwa undani hata kidogo, hao ma mbumbumbu ndo wanao kuwekeni madarakani kwani wangekuwa km mimi thubutu ma ccm mngekusikia ikulu toka kipindi cha " hali mpya nguvu mpya maisha bora kwa kila mdanganyika"
 
Kwa nchi za wenzetu angenyongwa mwakyembe alafu sita kwa nini walificha ukweli? na kama kweli lowassa ni fisadi kwa nini asipelekwe mahakamani? kwa maneno yako ccm inalea mafisadi na kwa hiyo tusiichague maana tukiichagua itatuongezea mafisadi bora tuipumzimshe mwaka huu
 
Jamani lowasa aliondoka serikalini miaka mingi.bada ya hapo ziliendelea kashfa nyingi kama vile mafamba ya meli na vivuko,uuzwaji wa nyumba za serkali nk.mbona haya hayasemwi na watu wanaendelea na kampeni za kugombea uongozi wa nchi?
 
Naona Raia Mwema siku hizi wamechoka na wanazidi kupauka mithili ya kaniki iliyowekwa muda mrefu juani. Hii ni habari iliyoandikwa kwa kukurupuka, isiyosheheni tafakuri za kina na ya kibabaishaji! Ukweli ni kwamba hata huko China hukumu za kuwanyonga wahalifu hazitolewi kiholela bila ya watuhumiwa kusikilizwa na watuhumiwa kupewa nafasi za kujitetea! Hayo hutendeka pia kwa watuhumiwa wa makosa makubwa kama ya wale vijana wetu wanaotumiwa na makada wa CCM kusafirisha na kusambaza mihadarati ambao CCM wenyewe wanawaita "Punda".

Laiti Lowassa angekuwa kule zaidi ya robo tatu ya viongozi waandamizi wa CCM wangekwishathibitishiwa hukumu zao wanazostahili - kifo. Hii ni pamoja hata na huu mdoli wao ulioshawishi na kusimamia hujuma kubwa ya kupora na kugawana nyumba za serikali - hali iliyosababisha baadhi ya watumishi waliostahili kuishi katika nyumba za serikali kuishi kwenye nyumba za kupanga mitaani hadi leo!

Lowassa na wenzake waliojitambua na kujitenga na genge la wahalifu hawa wanapigwa vita kwa hofu ya kuumbuliwa. Kwa kifupi watanzania hawadanganyiki tena bali wameungana kwa pamoja kama msemo wa vibakauchumi wa CCM unaosema "Umoja ni ushindi" ili kuwang'oa na kuwawajibisha. Subirini 25 Oktoba mtaona tutawafanyaje.

Hakuna jiwe litakalosalia, tutawapelemba mmoja mmoja kuanzia mliomaliza tembo wetu, twiga, mnaosambaza mihadarati, madalali wa uporaji ardhi na wizi wa madini yetu kupitia mikataba ya aibu kwa taifa hadi mliohonga vimada mali na amali za serikali. Tutawabana UKAWA wachukue hatua za kuzirejesha mali za taifa zilizotekwa nyara na genge hili vikiwemo viwanja vya mpira na majumba yaliyojengwa kwa kodi za baba na babu zetu.

Fanyeni mazoezi ya kuchuchumaa sasa ili mnyolewe. Mapambano ndiyo yameanza na kamwe HATUDANGANYIKI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…