Chenge: Mimi ni nyoka mwenye makengeza msaka pesa

Chenge: Mimi ni nyoka mwenye makengeza msaka pesa

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, amemkosoa Mbunge wa Bariadi Magaribi (ccm), kwa kujiita ' Nyoka wa Makengeza' kwa madai kwamba, anastahili kuitwa 'Nyoka wa Ufisadi

Mnyika katika Tarifa yake kwa vyombo vya habari jana, alisema Chenge ' Nyoka wa Ufisadi' badala ya kujisifia kuwa ni 'Nyoka mwenye makengeza' kwa kuwa amehusika katika kutafuna mali ya umma.
==========================

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, amemkosoa Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), kwa kujiita ‘nyoka wa makengeza' kwa madai kwamba, anastahili kuitwa ‘nyoka wa ufisadi'.

Mnyika katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, alisema wananchi wanapaswa kumuita Chenge ‘nyoka wa ufisadi' badala ya kujisifia kuwa ni ‘nyoka mwenye makengeza' kwa kuwa amehusika katika kutafuna mali ya umma.

"Kauli ya Chenge kama ilivyokuwa kwa ile ya ‘vijisenti', ni kiburi cha kifisadi," alisema Mnyika.

Chenge alitoa kauli hiyo juzi wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mahaha kata ya Vunamala, wilayani Bariadi, mkoani Simiyu, akiwaeleza wananchi wa jimbo lake kuwa aitwe nyoka kwa kuwa ni mjanja wa kutafuta fedha kwa ajili ya wananchi wake.

Mnyika alisema udhaifu wa serikali na vyombo vyenye mamlaka ya kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya tuhuma za ufisadi unaodaiwa kufanywa na Chenge na watuhumiwa wengine wa ufisadi ndiyo unaowalinda nyoka wa ufisadi na sasa wanajigamba kuwa ni wajanja wa kutafuta fedha kifisadi.

"Chenge anadai kwamba yeye ni mjanja wa kutafuta fedha za wananchi wa jimbo lake ili hali yeye na wenzake wamesababisha wananchi wa jimbo lake na mengine nchini kukosa fedha nyingi zaidi za miradi ya maendeleo mpaka hivi sasa kutokana na ufisadi wa Tegeta-Escrow," alisema Mnyika.

Alisema Rais Jakaya Kikwete anapaswa kujitokeza tena kulihutubia taifa kueleza hatua, ambazo ameendelea kuzichukua kukamilisha kutekeleza maazimio ya Bunge.

Mnyika alisema taarifa alizonazo hadi sasa wapo washirika wa maendeleo, ambao wameacha kutoa fedha kwa kutoridhika juu ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusiana na kashfa ya akaunti ya Tegeta Escrow.

Aliitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupamana na Rushwa (Takukuru) kuweka wazi kwa umma matokeo ya uchunguzi wake na hatua zaidi zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Chanzo: Nipashe
 
Mnyika maji ubungo vipi, mwezi wa pili huu wana ubungo hatujaoga maji hakuna
 
Chanzo: Nitashe[/QUOTE]= Nipashe.

Hata hivyo Chenge anautumia Upofu wa watanzania kutozijua vizuri Sheria za nchi; Ni Msomi ambaye hatakaa kutokea kwa kuliingiza taifa ili kwenye Mikataba mibovu; Anaposema yeye ni Nyoka mwenye makengeza hajakosea.

Kwanza mtu mwadilifu kuitwa Nyoka tu hilo ni TUSI na haiwezekani. Kwenye Bible nyoka ni ishara ya Sheltani, Ibilisi, Mtu asiye na huruma, Kigeugeu, Mnafiki; Mtu asiye mkweli na zaidi ya yote ni mtu msaliti.

Sasa yeye amepitiliza kwa maana hata anayo Makengeza; Makengeza ni ishara ya kutokuwa mkweli na kile Kinachoendelea; Mfano mzuri ni Kuweza Kusign mikataba kwa maslahi binafsi huku akiuhaminisha umma wa watanzania kuwa kila kitu kipo sawa.

Nadhani Mzee Chenge angeendelea Kukaa Kimya ili Kupoza hasira za Watanzania maana Kauli zake zinatuhumiza sana; Yaani yeye apige deal na yeye huyo huyo hatuzodoe; Ni Vema yeye akaendelea kupiga deal zake kimya kimya, lakini akae akijua siku CCM itadondoka na yeye utajiri wake umeishia hapo.

Hii Misemo yake ni Chukizo kwa watanzania wanaoshindia mlo mmoja kwa siku, utasikia mara "vijisent, leo eti "Nyoka mwenye makengeza".
Ngoja tuone October' 2015, ndo itatupa Mwelekeo wa ugawanaji wa Keki ya Taifa; Maana kwa sasa kila wakati Tunaambiwa Kasungura ni Kadogo wakati huo huo "Escrow and Madudu mengi kwenye Serikali za Mitaa".
 
Mnyika maji ubungo vipi, mwezi wa pili huu wana ubungo hatujaoga maji hakuna



Hivi wewe umeamua kutumika kabisa kama kondom kijana wee.........kauli ya fisadi chenge inakukaa akili kabisa,haya kimbia lumumba kapokee chako mjinga wewe!
 
Hivi wewe umeamua kutumika kabisa kama kondom kijana wee.........kauli ya fisadi chenge inakukaa akili kabisa,haya kimbia lumumba kapokee chako mjinga wewe!
Kamanda LiverpoolFC ukiona kauli zawakina laki si pesa jua ameshapukutishwa huyo
 
Chenge kweli ni kiburi, Jeuri, ka ana sarau sana huyu mutu, kwanza anasema yeye ni Nyoka, Mtanzania gani hamjui nyoka? Nyoka hata ukimfuga lazima umfungie mahali fulani na pamoja na kumfungia lazima awe kibogoyo kila siku, Haruhusiwi kuota meno maana nyoka hafai, Sasa huyu jamaa anajiita Nyoka tena wa makengeza, haya naomba niwaulize swali, kuna mtu alisha wahi kuona Nyoka wa makengeza? nijibuni sio masihara, mm kwaupande wangu sijawahi kumwona.

Hivi kweli huyu jamaa kabisa ndio CCM walimwamini na wakampa uandishi wa Katiba kweli!!!!!!!!!!!!!
naomba niishie hapo maana inatia kichefuchefu kabisa, ana maneno machau sana
na Katiba siisomi kabisa na siitaki, siwezi kutengenezewa Katiba na Joka la makengeza
 
Chanzo: Nitashe
= Nipashe.

Hata hivyo Chenge anautumia Upofu wa watanzania kutozijua vizuri Sheria za nchi; Ni Msomi ambaye hatakaa kutokea kwa kuliingiza taifa ili kwenye Mikataba mibovu; Anaposema yeye ni Nyoka mwenye makengeza hajakosea.

Kwanza mtu mwadilifu kuitwa Nyoka tu hilo ni TUSI na haiwezekani. Kwenye Bible nyoka ni ishara ya Sheltani, Ibilisi, Mtu asiye na huruma, Kigeugeu, Mnafiki; Mtu asiye mkweli na zaidi ya yote ni mtu msaliti.

Sasa yeye amepitiliza kwa maana hata anayo Makengeza; Makengeza ni ishara ya kutokuwa mkweli na kile Kinachoendelea; Mfano mzuri ni Kuweza Kusign mikataba kwa maslahi binafsi huku akiuhaminisha umma wa watanzania kuwa kila kitu kipo sawa.

Nadhani Mzee Chenge angeendelea Kukaa Kimya ili Kupoza hasira za Watanzania maana Kauli zake zinatuhumiza sana; Yaani yeye apige deal na yeye huyo huyo hatuzodoe; Ni Vema yeye akaendelea kupiga deal zake kimya kimya, lakini akae akijua siku CCM itadondoka na yeye utajiri wake umeishia hapo.

Hii Misemo yake ni Chukizo kwa watanzania wanaoshindia mlo mmoja kwa siku, utasikia mara "vijisent, leo eti "Nyoka mwenye makengeza".
Ngoja tuone October' 2015, ndo itatupa Mwelekeo wa ugawanaji wa Keki ya Taifa; Maana kwa sasa kila wakati Tunaambiwa Kasungura ni Kadogo wakati huo huo "Escrow and Madudu mengi kwenye Serikali za Mitaa".[/QUOTE]
Dhambi ya Rushwa haina tafauti na dhambi ya unyaganyi
 
Yaah ndo mfano wa mwanaume mtaftaji... sio kushinda jf kupiga kelele na kulalamika kama mwanamke kutwa nzima. Acheni wanaume watafte pesa, kama mmechagua kushinda kwenye keyboard kutwa nzima, mnalalamikia nini wanaume wenzenu wasaka pesa? Dunia hii nani asiyetaka pesa za kumhakikishia maisha ya kesho.

PASCO (alisema tanzania ni shamba la bibi.)


tofautisha kutafuta pesa na kuiba pesa pesa kichwa kikubwaaaaaaa ubongo hata 10% haufiki
 
kwa hii kauli ya change ingekuwa nchi ambazo zinafuata maadili yaani jamaa sasa hivi angekuwa anahojiwa na mpelelezi mkuu wa taifa hili,
from there wangemzuia korokoroni ili uchunguzibqa kina ufanyike.
yaani jizi linaiba pesa za umma Leo,kesho rais anasema pesa sio za umma,kesho kutwa jizi linajitojeza na kusema yeye ni mwizi ,tena lenye kengeza alafu watu wanashangilia.hata viombo vya usalama vinamtii Kama Nabii wa majizi
bungeni mama wa watu kampa cheo cha kamati ya budget kwa sababu anajua kucheza na loose money .Hii ndio bongo bana.

Hana tofauti na wauaji wa ALBINO...........Na inawezekana pia anatuma watu wake wamtengenezee hiyo deal ya ALBINO azidi kuwa MBUNGE.Binadamu wa kawaida huwezi kujiita NYOKA.............
 
Kweli huyu zumbukuku anajisifu kwa aubu na wizi alioufanya kwa watanzania? Aibu iliyoje?
 
hii ndo Tanzania , na cha kushangaza uchaguzi mkuu utamuona anaomba kura, kwa walio fika Bariadi wataungana nimimi makao makuu ya mkoa mjini pana kipande chakavu cha lami kisicho zidi kilometre tatu, hizo pesa mbona hapeleki kule, japo bado za wizi
I
 
hata watumishi wanalipwa pesa za umma!
I
Kwa hiyo watumishi wpanakipwa 1.6 bilion au? Usiache tukakutusi bure...Hongera kumtetea maana hata kunguru hutembea pamoja lakini huwezi kuta njiwa akaruka na mwewe....
 
Back
Top Bottom