Ni Aibu Chenge ni Kama Nicholas Biwott wa Kenya alivyokuwa, Fisadi ambaye anachora Michoro ya Wizi kwa Niaba ya Wakubwa. Jiulize Kwanini Chenge Alipewa hata Tiketi ya Kugombea Ubunge Kama CCM wanakata Majina ya Mafisadi. Chenge Ni mwizi, tofauti na Lowassa Ushahidi Upo. Chenge Yupo pale Kulinda Maslaahi ya Mafisadi hasa Kikwete na Mkapa.
Achana Na huu tu ufisadi wa Mikataba na Fedha za Umma, Pia wanamichoro ya Kimafya Kama Mnakumbuka Marekani ilishaichimbia Mkwara Serikali ya Kikwete kwa Kuzipeperushia bendera ya Tanzania Meli za Mafuta za Iran iliyokuwa imewekewa Vikwazo vya Uchumi. Wakati huo Pipa la Mafuta lilikuwa $ 100-110 sasa Pipa ni $ 35. Jiulize Walifanya hivi Bila Kuhogwa? Wakati huo Mwanasheria Mkuu alikuwa Chenge! Hiyo ilikuwa mwaka 2012 waliposhitukiwa Zilikuwa Meli Kubwa za Mafuta 35. Utetezi wao eti hawakujua.
Waliweza Kutumia Bendera ya Nchi yetu Kukiuka sheria za Kimataifa Kujinufaisha wenyewe huku wakijua, wangaliweza Kuleta hata maafa ya Vita juu yetu.
Tanzania probes Iran oil tankers re-flagging allegations - BBC News
Chenge Yuko Pale Bungeni Kuzima Kila Kitu Kitakachoibuliwa Kinyume chake na Mafisadi wenzake. Na nahisi walimtumia tu Magufuli ili washinde lakini hawautaki kabisa Moyo wake. Sikiliza Kicheko cha Kikwete cha Kebehi Kwa Magufuli.
Kutatua Matatizo Ni mwito Unaotolewa kwa Kicheko cha aina hii kweli (Wazungu wanakiita sarcastic lough)