Chemsha bongo na Majibu ya kukaririshana

Chemsha bongo na Majibu ya kukaririshana

Mzingo

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
4,766
Reaction score
10,611
Siku moja nimeenda kibanda cha chips
MIMI:Mtaalam nifanyie chips kavu

MPISHI:Subiri kidogo ziko jikoni

MIMI:si unipe hizo za kwenye kabati hapo? Nataka kuwahi.

MPISHI:Hio zimepoa,subiri hizi fresh . Zipo kidogo kwenye chombo kwa hiyo zitawahi kuiva

MIMI:Unazingua,zijae zisijae zote zinatumia muda mmoja{hapa nikamchokoza ili afunguke zaidi}

MPISHI:Kiongozi nina uzoefu katika hilo,zikijaa zinachukua muda sana,kama vipi nikupe hizo za kabatini.

MIMI😛otezea ,nitazisubiri

Kuna chemsha bongo isemayo:-
Kuna majiko mawili,sufuria mbili zenye kiasi sawa cha maji na majiko yote yamewashwa kwa viwango sawa. Sufuria ya kwanza ina yai moja,sufuria nyingine ina mayai 15. Majiko yamewashwa muda mmoja. Ni yai moja au mayai 15 ndio yatawahi kuiva?

Ili yai liive linahitaji lifyonze Joto(heat energy) kutoka kwenye maji/mafuta na mafuta/maji yatafyonza joto hiyo kutoka kwenye jiko. Wingi wa mayai utafanya mahitaji ya joto yawe makubwa hivyo yatagawana joto dogo lililopo kwenye mafuta na mafuta/maji yatakuwa yanachukua joto jikoni mpaka ifikie hatua kiasi cha joto kinachohitajika kwa mayai yote kuiva kimepelekwa kwenye mayai.

Inafanana kidogo na wazazi wawili wenye vipato sawa kwa mwezi ila wanasomesha idadi tofauti ya watoto kwenye shule moja,itamchukuwa miezi mingi yule mwenye watoto wengi kukamilisha ada(chukulia kuwa majukumu yao ni kusomesha tu)

Jibu ni yai moja,muda utakaotumika na mayai 15 ni mwingi zaidi ingawaje sio mara kumi na tano ya ule wa yai moja.

Watu hukaririshwa kuwa muda utakuwa sawa.

NB:Niko tayari kwa changamoto

 
merengo90 Jibu lako ni lipi?
 
kuna factor mbili muhimu,
1) Je, kitako chote cha sufuria kimefunikwa na moto.?
2)Mayai yote 15 katika sufuria ya pili yamegusa kitako cha sufuria.?

Kama majibu ni ndio, possibly yatatumia muda mmoja, kwasababu kwenye sufuria lenye yai moja joto jingi linakua linapotea bure. Na joto kidogo litafyonzwa na lile yai (sawasawa na yai jingine kati ya yale 15) huku joto lingine likipotea bure, wakati joto hilo linalopotea bure ndo linalochukuliwa na mayai mengine kwenye sufuria jingine.
 
kuna factor mbili muhimu,
1) Je, kitako chote cha sufuria kimefunikwa na moto.?
2)Mayai yote 15 katika sufuria ya pili yamegusa kitako cha sufuria.?

Kama majibu ni ndio, possibly yatatumia muda mmoja, kwasababu kwenye sufuria lenye yai moja joto jingi linakua linapotea bure. Na joto kidogo litafyonzwa na lile yai (sawasawa na yai jingine kati ya yale 15) huku joto lingine likipotea bure, wakati joto hilo linalopotea bure ndo linalochukuliwa na mayai mengine kwenye sufuria jingine.
kwa hiyo unampinga na mpika chips? halafu naona neno possibly,kwa nini possibly?
 
Assumptions za chemsha bongo ile ni kuwa

1)maji siyo mengi sana(maji yako level na mayai 15,na kiasi hiki cha maji ndio kimetumika kwenye yai moja
2) TOFAUTI HATA YA SEKUNDE INATOSHA KUTOFAUTISHA KAMA KWENYE MBIO ZA MITA 100 ikibidi hata vifaa 'vya kitaalam vyaweza kutumika kupima muda halisi wa uivaji

kuonesha kuwa majibizano ya muuza chips sijayapika ,nikitaja kibanda cha chips kilipo ninaweza kukung'utwa dongo kuwa ninakitangaza...kidding
 
Wasomi mko wapi huko, hebu njoeni msome hili asemalo jamaa, nadhani haya ni mapinduzi makubwa kabisa ya elimu kuwahi kutokea.

[emoji41]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom