Cheka, simulia, lakini usiombe yakukute

Umesoma hadithi hii mwanzo hadi mwisho?

  • Ndio

    Votes: 3 50.0%
  • Hapana

    Votes: 3 50.0%

  • Total voters
    6
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 26

Kwenye kaya hii iliyofanya kazi sana na kuchoka mno nani ambaye alikuwa na muda tena wa kumfikiria Grego isipokuwa tu pale ilipomlazimu?

Kaya ilikuwa ikizidi kuwa ndogo. Yule dada wa kazi aliachwa aende zake. Mama mtu mzima, mwembamba, nywele zake zenye mvi zikinesa huku na kule kichwani pote alikuja asubuhi na jioni kufanya kazi ngumu kuzidi.

Mama alifanya kazi zote nyingine zilizobaki zikiwa ni nyongeza kwa kazi yake muhimu ya ufumaji.

Yaani ilitokea kwamba hata vipande kadhaa vya urembo vyenye thamani, mali ya familia, ambavyo zamani mama na dada walifurahi mno kuvivaa kwenye matukio maalum ya kijamii na sikukuu, viliuzwa, kama ambavyo Grego alibaini jioni kutokana na mazungumzo ya ujumla ya bei zilizopata.


Lakini malalamishi makubwa yalibaki kuwa hawangeweza kuiacha nyumba hii, ambayo ilikuwa ni kubwa kuliko uwezo wao wa kifedha, kwani ilikuwa ni vigumu kufikiria ni namna gani Grego atasafirishwa.

Lakini Grego alitambua fika kwamba haikuwa kumfikiria yeye pekee ndiko kulikozuia wasihame (kwani angeweza kusafirishwa kirahisi ndani ya boksi maalum lenye matundu machache ya kupitisha hewa); kitu kikuu kilichoizuia familia isibadili makaazi zaidi kilikuwa ni kukata tamaa kwao na pia fikra kwamba wamekutwa na masaibu ambayo hakuna yeyote kwenye orodha nzima ya ndugu na jamaa aliyefikwa na kama hayo.


Kile ambacho dunia hukitarajia toka kwa watu masikini ndicho walichokifanya kupindukia. Baba alipeleka kiamsha kinywa kwa watumishi wa benki, mama alijitoa muhanga kwa ajili ya nguo za ndani za watu wengine, dada alikuwa dawatini muda wowote akiwa tayari kuwa msaada kwa wateja, lakini mwamko kwenye familia haukuongezeka hata kidogo.

Na lile jeraha mgongoni mwake lilianza kumsumbua Grego tena na tena, wakati ambapo mama na dada, baada ya kumsindikiza baba kitandani, walirejea, wakatua kazi zao, wakasogeleana, na kukaa pamoja, na pale mama sasa aliposema, akiashiria uelekeo wa chumba cha Grego, “Kafunge mlango, Grete,” na pale ambapo Grego alikuwa tena kizani, wakati jirani wale akinamama machozi yao yaligusana au, kwa macho makavu kabisa, waliishangalia meza.


Grego alitumia muda wake wa usiku na mchana karibu sawa na bila kulala. Mara nyingine alidhani kwamba mlango utakapofunguliwa mara inayofuata atashiriki kwenye mipangilio ya kikaya kama ilivyokuwa zamani.

Kwenye fikra zake walijitokeza tena, baada ya muda mrefu, mwajiri wake na bosi wake na wafanyakazi wanagenzi, yule mhudumu juha kabisa, marafiki zake wawili au watatu wa kampuni zingine, mhudumu wa hoteli fulani mikoani, kumbukumbu maridhawa fupi, keshia wa kike wa kwenye duka la kofia, ambaye Grego alitamtangazia nia kidhati, japo polepole mno – wote walijitokeza wakichanganyika na watu asiowajua au asiowakumbuka, lakini badala ya kumsaidia yeye na familia yake, wote hawakufikika, na alifurahia kuona wakitoweka.

Lakini tena Grego hakuwa na wakati ya kuwazia familia yake. Alikuwa amejaa ghadhabu juu ya huduma mbovu aliyokuwa akipata, japokuwa hakuweza kufikiria chochote ambacho kingempa hamu ya kula.

Hata hivyo, bado alipanga mipango ya namna ipi atajichukulia toka kwenye kabati la chakula kile ambacho kwa vyovyote vile anastahili, hata kama hakuwa na njaa.

ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 27

Bila kujali tena kuhusu namna gani mtu anaweza kumfurahisha ipasavyo Grego, sasa dada alipiga teke vyakula au kitu kama hicho kuvisukumia chumbani asubuhi na adhuhuri, kabla ya kutimkia dukani kwake, na ifikapo magharibi, bila kujali kama chakula pengine kilionjwa tu, au kilichotukia mara nyingi zaidi, chakula kilibaki tu vilevile bila kuguswa, alikinyakua kukiondoa kwa mvuto mmoja wa fagio lake.

Jukumu la kusafisha chumba chake, ambalo sasa alilitekeleza mida ya jioni, lilifanyika haraka kadiri alivyoweza. Masalia ya uchafu yalitapakaa ukutani; hapa na pale palikuwa na mikusanyiko ya vumbi na uchafu.

Awali, wakati dada yake akiwasili, Grego alikaa kwenye kona iliyo chafu zaidi ili kwa mkao huu kuwasilisha namna fulani ya malalamiko.

Lakini angeweza kukaa hapo kwa majuma kadhaa bila dada yake kubadili tabia. Hasahasa, dada alichukulia uchafu vilevile tu kama Grego alivyouchukulia, lakini alikuwa ameamua tu kuuacha hivyohivyo tu.




Kwenye masuala haya, kwa mashauzi ambayo kwa dada yalikuwa ni mapya sana na ambayo kwa ujumla yaliiteka familia nzima, alihakikisha jukumu la kusafisha chumba cha Grego lilibakia mikononi mwake tu.

Siku fulani, mama alijichukulia jukumu la kufanya usafi mkubwa chumbani kwa Grego, jukumu ambalo alililikamilisha vema baada tu ya kutumia ndoo kadhaa za maji. Lakini unyevunyevu uliokithiri ulimfanya Grego awe mgonjwa na alilala chali kwenye kochi, aliyejaa ghadhab na asiyeweza kujongea. Hata hivyo, adhabu kwa aliyofanya mama haikucheleweshwa sana.

Kwani ilipokuwa jioni, dada alipochungulia tu mabadiliko chumbani kwa Grego alirudi mbio sebuleni akiwa amechukizwa sana, na licha ya kwamba mikono ya mama ilikuwa imeinuliwa na kugusana mithili ya aombaye msamaha, dada aliangua kilio.

ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 28


Wazazi wake (baba alikuwa, ni bayana, ameshaamka tayari kutoka kiti chake cha uvivu) na awali walimwangalia Grete kwa mstuko na bila msaada; mpaka walipoanza kukerwa.

Alipogeuka upande wa kulia, baba alianza kumgombeza mama kwamba hatakiwi kumpoka dada jukumu la kusafisha chumba cha Grego, na alipogeuka kushoto, alimpigia kelele dada kwamba hangeruhusiwa tena kusafisha chumba cha Grego, wakati huo mama akijaribu kumvuta baba, aliyekuwa siyo yeye kwa mhemko, aende chumbani; dada , aliyekuwa ameyumbishwa na kulia kwake, aligonga meza kwa vingumi vyake vidogo, na Grego alitoa sauti kama ya nyoka, akigadhibika kwamba hakuna hata mmoja wao aliyefikiria kuhusu kuufunga mlango ili kumkinga asione tafrani yote hiyo.

Lakini hata pale dada, akiwa amechoka na majukumu yake ya kila siku, alifikia kuchoka kumhudumia Grego kama alivyofanya hapo kabla, hata hivyo haikumlazimu aslan mama kuyachukua majukumu hayo.

Na Grego hakukosa huduma. Kwani kwa sasa mama wa usafi alikuwapo. Mjane huyu mzee, ambaye kwenye maisha yake marefu itakuwa alihimili misukosuko migumu kutokana na mwili wake mwembamba, hakuogofywa na Grego. Pasipo kuwa ni asiye mtafiti, wakati fulani ilitokea akafungua mlango wa chumba cha Grego.

Alivyomuona Grego, ambaye, akiwa ameshangazwa , alianza kujongea huku na kule, japo hakukuwa na anayemkimbiza, mama huyu alibakia palepale amesimama, mikono ameikunja maeneo ya tumbo lake, akimtazama Grego.

Mwanzoni, mama huyu alimwita Grego kwa maneno ambayo huenda alidhania ni ya kirafiki kama vile, “Njoo hapa mara moja, mende-miwa!” au “Hee, muone mende-miwa mkubwa!”

Akisemeshwa hivyo, Grego hakujibu kitu, lakini alibakia palepale alipo bila kujongea, kana kwamba mlango haukuwa umefunguliwa.

Afadhali ingekuwa, badala ya kumruhusu mama huyu wa usafi kumbugudhi Grego bila manufaa kila alipojisikia kufanya hivyo, wangempa badala yake maagizo ya kukisafisha chumba chake kila siku!

ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 29

Siku moja mapema asubuhi (mvua nzito, pengine dalili ya kukaribia masika, ilipiga vioo vya madirisha) pale ambapo mama wa usafi alianza tena maneno yake ya siku zote, Grego aligadhibika mno kiasi kwamba alimgeukia, kana kwamba anayetaka kumshambulia, japokuwa polepole na kidhaifu.

Lakini badala ya kumhofia Grego, mama wa usafi yeye aliinua tu kiti kilichokuwa karibu na mlango na, kadiri alivyoendelea kusimama pale kinywa kikiwa wazi, lengo lake lilikuwa wazi: ataufunga mdomo wake pale tu kiti kilichokuwa mkononi mwake kitakapokuwa kimerushwa kutua mgongoni mwa Grego.

“Hii haiendelei zaidi ya hivi, sawasawa?” aliuliza, wakati Grego akigeuka nyuma, naye akakiweka kiti taratibu chini pale kwenye kona.

Grego sasa alikuwa ni kama hali kitu. Ni pale tu ilipomtukia kupita jirani na chakula kilichoandaliwa ndipo, kama masikhara, alipomega kidogo, na kukiacha kinywani kwa masaa kadhaa, na aghalabu akikitema tena. Mwanzoni alidhani inawezekana ni kutokana na huzuni iliyotokana na hali ya chumbani kwake ndiyo ilimfanya ashindwe kula, lakini muda si mrefu alizoea mabadiliko ya chumbani kwake.

Watu walishajenga mazoea ya kutunzia vitu chumbani kwake vile ambavyo hawangeweza kuviweka kokote kwengine, na kufikia wakati huu vilikuwa vingi, hasa kwa vile walikipangisha chumba kimoja kwa wapangaji watatu.

Hawa majamaa makini (wote watatu walikuwa wamefuga madevu, kama Grego alivyobaini siku fulani alipochungulia kupitia ufa wa kwenye mlango) walisisitiza sana kuhusu usafi, siyo tu wa chumba chao walichokipanga lakini (kwa kuwa wamepanga chumba hapa) kwenye nyumba yote, na hususan jikoni. Hawakustahamili kuona kitu chochote kisicho maana au kisichofaa. Zaidi ya hayo, kwa sehemu kubwa walikuja na fenicha zao wenyewe. Hivyo vitu vingi vikawa havihitajiki tena, na hivyo havikuwa vitu ambavyo mtu angeweza kuviuza au vitu ambavyo mtu angetaka kuvitupa.


Makorokocho yote hayo yaliishia kwenye chumba cha Grego, hata kasha la kutunzia majivu na takataka za jikoni. Mama wa usafi, ambaye muda wote alikuwa anahanja huku na kule, yeye alitupia tu chochote kile ambacho muda huo kilikuwa hakina kazi chumbani kwa Grego.

Kwa bahati, Grego mara karibu zote aliona tu kitu kinachotaka kutupwa na mkono uliokishika. Mama wa usafi pengine alikusudia, pale ambapo muda na fursa vitaruhusu, aje kuvichukua tena au kuvitupa nje vyote kwa wakati mmoja, lakini kiukweli vitu vilibaki vilevile, kama ambavyo vilivyokuwa vimeanguka wakati vimetupwa, labda Grego apenyepenye kwenye mrundikano wa makorokocho na kukisogeza.

Mwanzoni alilazimika kufanya hivi kwa vile vinginevyo hakukuwa na nafasi kwa yeye kutambaa chumbani, lakini baadaye alifanya hivyo kwa furaha iliyokuwa ikizidi kuongezeka, japokuwa baada ya kujongea vivyo, alijihisi mgonjwa na mwenye uchovu wa kufa mtu, hakuacha kufanya hivyo kwa masaa.

Kwa sababu wapangaji wakati mwingine walipata chakula cha jioni sebuleni, mlango wa chumbani kwa Grego unaoelekea sebuleni ulibaki umefungwa kwa jioni nyingi. Lakini Grego hakupata taabu yoyote kuwepo bila mlango uliofunguliwa. Tayari jioni nyingi mlango ulipokuwa wazi, hakujitokeza mlangoni, bali, bila familia kubaini, alikuwa amejibanza kwenye kona yenye giza zaidi chumbani kwake. Lakini siku moja mama wa usafi aliuacha mlango wa sebuleni wazi kidogo, na ulikuwa hivyohivyo wazi hata pale wapangaji walipokuja jioni na taa za sebuleni kuwashwa.

ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 30

Waliketi upande mwembamba wa meza, ambapo siku za awali mama, baba, na Grego walilia, wakifungua vitambaa vilivyofungia zana za kulia, na kuchukua visu na uma zao.

Mama mara moja alijitokeza mlangoni amebeba chombo kilichosheheni nyama na nyuma yake tu alikuwepo dada aliyebeba chombo kilichojazwa viazi pomoni.

Chakula kile kilitoa mvuke mwingi. Ile mijamaa iliinamia sahani zilizowekwa mbele yao, na haswa mmoja wao yule aliyekaa kati yao (kwa wale wawili alionekana kutumika kama mamlaka) alikata kipande cha nyama kilichokuwa bado kingali kwenye sahani nia wazi ikiwa ni kuthibitisha iwapo ilikuwa imeiva ipaswavyo na iwapo pana kitu kilitakiwa kurejeshwa jikoni au la.

Alikuwa ameridhika, na mama na dada, ambao walikuwa wakiangalia kwa wasiwasi, walishusha pumzi na kuanza kutabasamu.


Familia yenyewe ililia jikoni. Licha ya hivyo, kabla baba hajaenda jikoni, alikuja sebuleni na akainama mara moja kama ishara ya heshima, akishika kofia mkononi, akafanya ziara mezani.

Wapangaji waliamka wote kwa pamoja na kunong’ona kitu na midevu yao. Kisha, walipobaki peke yao, walikula chakula takriban kimyakimya.

Ilimshangaza Grego kuona kwamba kati ya sauti zote zitokanazo na kula, kilichokuwa kikisikika muda wote kilikuwa ni meno yao watafunapo, kana kwamba kupitia hizo Grego aonyeshwe kwamba watu walihitaji meno yao ili wale na kwamba hakuna kitu kingeweza kufanyika kutokana na hata taya zuri kuliko yote lisilo na meno.

“Nina hamu sana ya kula,” Grego alijiambia kwa huzuni, “lakini siyo kwa vitu hivi. Hawa wapangaji wanajishibisha ilhali najifia.”

Jioni hiihii (Grego hakukumbuka kusikia zumari siku zote hizi) lilisikika kutokea jikoni.

Wapangaji tayari walikuwa wameshamaliza mlo wao wa jioni, na yule wa katikati alikuwa ametoa gazeti na kuwapa kipande kila mmoja wa wenzie wawili, na sasa walikuwa wameegama, wakisoma na kupuliza moshi.


Wakati zumari limeanza kupigwa, walistuka, kuinuka na kwenda kwa kunyatanyata kwenda mlangoni wa jikoni, ambapo walibakia wamesimama wamejikunyata.


Lazima watakuwa walikuwa wamesikika hadi ndani jikoni, kwa vile baba alisema, “Pengine wapangaji hawapendi kulisikia zumari, linaweza kusitishwa mara moja.”


“Kinyume chake,” alisema yule mpangaji wa kati, “kwa nini binti kijana asije huku na kupiga zumari huku sebuleni ambako kumetulia na kwafurahisha zaidi?”

“Ooh, asante sana,” alipiga kelele baba, kana kwamba yeye ndiye aliyekuwa akipiga zumari. Wale majamaa walirudi sebuleni na kusubiri.

Punde baba alirejea na stendi ya muziki, mama akiwa na karatasi ya muziki, na dada akiwa na zumari.

Dada kwa utulivu aliandaa kila kitu tayari kwa kinachofuata. Wazazi, ambao hapo kabla hawakuwahi kupangisha chumba na hivyo walikolezea upole wao kwa wapangaji, hawakuthubutu kuketi kwenye viti vyao wenyewe.

Baba aliegama mlangoni, mkono wake wa kulia ukiwa baina ya vifungo viwili vya sare yake iliyofungwa vifungo vyote.

Mama, hata hivyo, alikubali kiti alichopewa na mpangaji mmoja. Na kwa vile alikiacha kiti palepale ilipotokea yule mpangaji alipokiweka, aliketi upande mmoja kwenye kona.

Dada alianza kupiga zumari.

Baba na mama, walifuatilia kwa makini, mmoja akiwa kila upande, nyendo za mikono yake.

Akivutiwa na zumari linavyopigwa, Grego alijongea mbele kidogo na kichwa chake tayari kilikuwa sebuleni.

Wala hata hakushangaa kivile kuhusu ukweli kwamba siku za karibuni amekuwa ni asiyejali kuhusu wengine; awali kujali huku kulikuwa ni kitu alichojivunia.

Na kwa sababu hiyo hasa ingekuwa wakati huu sababu nyingine ya yeye kujificha, kwa vile kutokana na vumbi lililosheheni chumbani kwake lililotimka likitibuliwa kidogo tu, alikuwa amezingwa na uchafu.

Mgongoni mwake na pembeni alikuwa amebeba vumbi, nyuzi, nywele na masalia ya chakula. Kutojali kwake kuhusu chochote kulikuwa kukubwa mno kumfanya alale chali na kujisafisha sakafuni, kama alivyofanya kila mara mchana zamani. Licha ya hali yake hakuona tabu kujongea mbele kidogo kwenye sakafu safi isiyo na mawaa ya sebuleni.


ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 31

Kwa vyevyote vile, hakuna aliyejali uwepo wake. Familia ilichokuwa inajua saa ile kilikuwa ni zumari lipigwalo. Wapangaji, kwa utofauti, ambao kwa muda huo walijiamulia kukaa, mikono yao ikiwa mifukoni, nyuma ya stendi ya muziki karibu mno na dada, ili wote waweze kuiona karatasi ya muziki, kitu ambacho bila shaka kitakuwa kilimkera dada, hawakuchelea kurudi nyuma dirishani wakiongea kwa sauti za chini huku wameinamisha vichwa, ambako walibakia, huku baba akiwatizama kwa jicho la wasiwasi.

Ilikuwa ni wazi kwamba, baada ya kudhania watasikia zumari likipigwa vizuri au kwa kuvutia, walikatishwa tamaa, na walikubali amani na utulivu wao usumbuliwe kwa vile tu ilikuwa ni busara kuwa wapole.

Namna ambavyo wote walipuliza moshi wa sigara kubwa zao kutokea puani na hasa mdomoni, vingeweza kumfanya mtu ahitimishe kwamba walikuwa wameudhika mno.

Hata hivyo dada alikuwa akipiga zumari vizuri sana. Uso wake ulielekea upande, jicho lake likifuatisha karatasi ya muziki kwa makini na kwa huzuni.

Grego alitambaa mbele kidogo zaidi na kuweka kichwa chake karibu na sakafu ili aweze kuiona sura ya dada kama ingewezekana.

Je, Grego alikuwa ni mnyama ambaye muziki ulimteka hivyo? Kwake ilikuwa ni kama vile njia ya kuelekea kwenye lishe isiyojulikana aliyoitamani sana ilikuwa ikijidhihirisha kwake.

Alikusudia kuendelea kwenda mbele mpaka amfikie dada yake, amvute gauni lake na kwa njia hiyo kumuashiria kwamba angeweza kwenda naye chumbani pamoja na zumari lake, kwa vile hapa hakuna mtu aliyetambua thamani ya kipaji chake kama ambavyo yeye alitaka kukitambua.

Hapo asingemwacha tena atoke chumbani kwake, walau mradi akiwa yeye Grego anaishi. Muonekano wake wa kutisha ungekuwa kwa mara ya kwanza wa manufaa kwake. Alitaka kuwepo kwenye milango yote kwa mara moja na kubwekea wavamizi. Hata hivyo, dada yake angebakia huko kwa hiari; angekaa karibu naye kwenye kochi, akimsogezea sikio lake karibu, na kisha Grego angemuambia siri yake kwamba alikusudia kabisa kumpeleka chuo cha muziki, na kwamba, kama masaibu haya yasingemkuta hivi, angemwambia yote haya Krismasi iliyopita (hivi Krismasi kweli ishakuja na kupita?), na hilo lisingeleta ubishi wowote. Baada ya maelezo haya dada yake angeangua kilio cha machozi ya furaha, Grego angejiinua mpaka makwapani mwake na kumchum shingo yake, ambayo, toka ameanza kwenda kazini, aliiachia wazi bila kitambaa wala kola.


ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 32

“Bwana Samsa,” alimuita baba yule mpangaji wa kati, na kuonyesha kwa kidole chake cha shahada, bila kutamka neno lingine, kumwelekea Grego wakati akijongea mbele polepole.

Zumari lilinyamaa kimya.

Mpangaji wa kati alitabasamu, kwanza akitikisa kichwa chake kwanza kwa rafiki zake, na kisha akimwangalia Grego kwa mara nyingine tena.

Kuliko kumswaga Grego arudi alikotoka, baba alionekana kuona ni la umuhimu mkubwa kuwatuliza wapangaji, japokuwa hawakuwa wamekasirika hata kidogo na Grego alionekana kuwaburudisha zaidi kuliko zumari lililokuwa likipigwa.

Baba aliharakia kuwafuata na kwa mikono iliyonyooshwa akijaribu kuwasukumia chumbani kwao na kwa wakati huohuo kuwazuia kwa kutumia mwili wake wasiendelee kumuona Grego.

Ndipo kwa wakati huu walipokuwa haswa kiaina wamechukizwa, japokuwa mtu hangeweza tena kujua iwapo ilikuwa ni kutokana na aliyoyafanya baba au kutokana na kutambua kwamba walishakuwa, bila kufahamu, na jirani kama Grego.

Walitaka maelezo kutoka kwa baba yake, wakiinua mikono wakati wakisema hayo, walishika ndevu zao kwa hasira, na kwenda polepole kuelekea chumbani kwao.

Wakati huohuo, ule upweke uliomkuta dada baada ya tumbuizo kukatizwa ghafla lilimuelemea sana.

Aliendelea kulishikilia zumari na upinde wa kulipigia kwenye mikono yake iliyolegea kwa muda tu na aliendelea kutizama karatasi ya muziki kama vile ambaye alikuwa akiendelea kupiga zumari.

Kwa mara moja alijitutumua, akaweka chombo cha muziki kwenye mikono ya mama yake (mama alikuwa akali akiketi kwenye kiti chake akivuta pumzi kwa taabu na mapafu yake yakimnyima ushirikiano) na ikambidi kukimbilia chumba jirani, ambacho wapangaji, wakishinikizwa na baba, walikuwa tayari wakizidi kukikaribia.

Mtu angeweza kuona namna chini ya mikono zoefu ya dada mashuka na mito kwenye vitanda ilivyo juu na kupangiliwa vilivyo.

Hata kabla ya wapangaji kufikia chumbani, alikuwa tayari amemaliza kuviandaa vitanda na alikuwa akichomoka mle chumbani.

Baba alionekana amezidiwa sana kwa mara nyingine na ubishi wake mpaka akasahau kuhusu heshima ambayo siku zote aliwapa wapangaji wake. Aliwasukuma zaidi na zaidi, mpaka mlangoni mwa chumba chao yule jamaa wa kati alikanyaga sakafu kwa sauti kubwa na hivyo kumfanya baba asiendelee kwenda.

“Natamka haya kama ifuatavyo,” alisema mpangaji wa kati, akiinua mkono wake na kuwatizama kwa chati wote wawili mama na dada, “kwamba kwa kuzingatia mazingira ya kutia kinyaa yaliyoko kwenye nyumba hii na kwenye familia,” hapo alitema mate kwa kukusudia sakafuni, “Nasitisha kuwa mpangaji. Ni wazi, sitalipa chochote kwa siku zile ambazo nimekaa hapa; kinyume chake nitatafakari iwapo nichukue hatua fulani dhidi yenu au la, kitu ambacho -- mniamini -- kitakuwa chepesi sana kukitekeleza.”

Alikaa kimya na kuangalia mbele yake moja kwa moja, kama vile aliyekuwa akingojea kitu.

Hakika, rafiki zake wawili mara hiyohiyo walijiunga kutoa maoni yao,

“Nasi pia tunatoa notisi mara moja.”

Hapo alishika kitasa cha mlango, akaubamiza mlango kuufunga, na kufunga kwa funguo.

Baba alipapasa njia yake akitetemeka kwenda kwenye kiti chake na akajiachia aangukiemo.

Ilionekana ni kama vile alikuwa akijinyoosha kwa usingizi wake wa kawaida jioni, lakini kutikisa kichwa kulikokithiri (ambacho kilionekana ni kama kimekosa udhibiti) kulidhihirisha hakuwa analala aslan.

Grego alikuwa amejilaza bila kujongea muda wote huo palepale alipokuwa wakati wapangaji walipombaini. Kukatishwa tamaa kutokana na kuharibika kwa mpango wake na pengine pia udhaifu wake uliotokana na njaa yake kali vilifanya isiwezekane kwa yeye kujongea. Alikuwa na hakika kwamba zahma kubwa itamshukia muda wowote na aliisubiri.

Wala hata hakustushwa pale zumari lilipodondoka toka mikononi mwa mama yake, likiachiwa na vidole vya mama vilivyokuwa vikitetemeka, na kutoa mlio uliokuwa ukiakisiwa kuwa mwangwi.

“Wazazi wangu wapendwa,” dada alisema huku akigonga meza kwa mkono wake kama namna ya utambulisho, “mambo hayawezi kuendelea zaidi namna hii. Pengine kama hamtambui hayo, sawa, mimi natambua. Sitatamka jina la kaka yangu mbele ya dubwasha hili, na hivyo nasema kilichobakia ni kwamba lazima tujaribu kuliondolea mbali. Tumejaribu kadiri inavyowezekana kibinadamu kulihudumia na kuwa watulivu. Naamini hakuna atakayetushutumu hata kidogo.”

“Yuko sahihi kwa njia alfu moja,” baba alijiambia mwenyewe.

Mama, ambaye bado hakuwa anaweza kuvuta pumzi sawasawa, alianza kukohoa kimyakimya huku mkono wake umewekwa kinywani na macho yamemtoka pima.

Dada alimkimbilia mama na kulishika paji lake la uso.

Maneno ya dada yalionekana kumpelekea baba kuwa na tafakari fulani.

Alikaa sawa, akichezea kofia yake ya ofisini kwenye sahani, ambazo bado zilikuwapo mezani baada ya mlo wa jioni wa wapangaji, na mara hii au ile alimtizama Grego aliyekuwa ametulia tuli.

“Lazima tujitahidi kuliondoa hili,” dada sasa alimwambia baba kwa hakika, kwa vile mama, katika kukohoa kwake huku, hakuweza kusikiliza chochote,”linawaua wote wawili. Naona kifo kinavyowajia. Wakati watu inabidi kufanya kazi kwa bidii namna hii tufanyayo, hawawezi kustahamili pia mateso ya namna hii yasiyoisha nyumbani. Siwezi kuendelea namna hii hata kidogo". Na aliangua kilio cha namna yake mpaka machozi yake yakawa yanamdondokea mama usoni. Akamfuta mama machozi hayo kwa kujongeza mikono yake bila kufikiri.

“Mtoto,” baba alisema kwa huruma na kwa kutambua vilivyo mchango wake, “kwa hiyo nini tufanye sasa?”

Dada alitikisa tu mabega yake kama ishara ya kushangazwa, ukilinganisha na kujiamini kwake alikokuwa nako, kushangazwa kulikomjia wakati akilia.

“Laiti angekuwa anatuelewa,” baba alisema kama vile aulizaye.

Dada, huku kwikwi zikiendelea, alitikisa mkono wake kwa nguvu kama ishara ya kusema hakuna mantiki kufikiria hayo.

“Laiti angekuwa anatuelewa,” baba alirudia na kwa kufumba macho alipokea imani ya dada juu ya kutowezekana kwa wazo hilo, “basi labda maelewano fulani naye yangewezekana. Lakini kama hali ilivyo...”

“Liondolewe mbali,” dada alipiga kelele; “Hakuna namna nyingine baba. Unatakiwa ujaribu kuondoa fikra kwamba huyu ni Grego. Kwamba tuliamini hivyo kwa muda mrefu hilo ni bahati mbaya sana kwetu. Lakini hili linawezaje kuwa Grego? Kama lingekuwa Grego, lingeshatambua zamani kwamba maisha pamoja na binadamu hayawezekani na linyama la hivyo na lingeshakuwa limejiondokea lenyewe zamani. Hapo tusingekuwa na kaka, lakini tungeweza kuendelea na maisha na kuheshimu kumbukumbu yake. Lakini hili linyama linatutesa. Linafukuza wapangaji, na ni wazi litateka nyumba hii nzima, na kutuacha tulale nje. Baba, we liangalie,” alianza kupiga makelele, “limeshaanza tena.”

Kwa hofu kubwa ambayo haikueleweka kabisa kwa Grego, dada alimuacha hata mama, akijisogeza mbali na kiti chake, kana kwamba alikuwa tayari kumtoa mama kafara kuliko kuwa karibu na Grego, na kukimbilia nyuma ya baba yake ambaye, kwa kuhemshwa na aliyoyafanya dada, pia aliinuka na kuinua nusu mkono wake kama ambaye anamlinda dada.


Lakini Grego hakuwa na wazo lolote la kutamani kuleta matatizo kwa yeyote yule na hususan kwa dada yake. Alikuwa tu ameanza kujigeuza ili atambae kuelekea chumbani kwake, muonekano wa kutatiza, kwani, kama matokeo ya hali yake dhoofu, ilimbidi ajiongoze mwenyewe kwenye zoezi gumu la kugeukia nyuma na kichwa chake, mchakato uliomfanya akiinue na kujigonga sakafuni mara kadhaa.

Alipumzika na kuangalia huku na kule. Nia zake njema zilikuwa ni kama zimetambuliwa. Hofu ilikuwa ni kwa muda tu. Sasa walimtazama kimya na kwa huzuni. Mama yake alikuwa amejilaza kwenye kiti chake, miguu yake ikiwa imenyooshwa na kuwa pamoja; macho yake ni karibu na yamefumbwa kwa uchovu. Baba na dada waliketi karibukaribu. Dada aalikuwa ameweka mkono mmoja shingoni mwa baba.

“Sasa pengine naweza kujigeuza mwenyewe,” aliwaza Grego na kuanza upya zoezi lile. Hakuweza kuacha kutweta kutokana na juhudi zake na ilimlazimu kupumzika mara hii au ile.

Licha ya hayo, hakuna aliyekuwa akimharakisha.

Aliachwa mwenyewe apambane na hali yake. Wakati alipofanikiwa kukamilisha zoezi la kugeuka, mara moja alianza kujongea moja kwa moja chumbani.

Alishangazwa na umbali mkubwa uliomtenganisha na chumba chake na hakuelewa hata kidogo aliwezaje na hali yake dhaifu kutembea umbali wote huo muda mfupi tu uliopita, takriban bila kutambua hilo.

Bila kusita akidhamiria kuendelea kutambaa haraka, ni kama hakuzingatia ukweli kwamba hakuna neno wala kilio kutoka kwenye familia yake lililokatiza safari yake.

Ni pale tu alipokuwa tayari mlangoni ndipo alipogeuza kichwa chake, kiasi tu, kwa vile bado alihisi shingo yake ikizidi kuwa ngumu.

Kwa vyevyote vile bado aliona kwamba nyuma yake hakuna kilichobadilika. Dada tu alikuwa amesimama. Jicho lake la mwisho alilitupa kwa mama yake ambaye sasa alikuwa ameshalala fofofo.

ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 33

Kabla hata hakuingia vizuri chumbani kwake pale ambapo mlango ulisukumwa kufungwa kwa haraka, komeo kufungwa, na vizuizi kuwekwa. Grego alisangazwa na vurugu la ghafla lililokuwapo nyuma yake, sana tu kiasi cha kumfanya tuvigulu twake tudogo, tujikunje mara mbili chini yake.

Ilikuwa ni dada yake ambaye alikuwa na haraka kiasi hicho. Aliinuka mara, akasubiri, na kisha akaenda mbele haraka kwa kunyata. Grego hakusikia chochote wakati dada akikaribia.

Dada akapiga kelele “Hatimaye!” kwa wazazi wake, wakati akizungusha ufunguo kwenye kitasa.

“Nini kifuatacho?” Grego alijiuliza na kuangalia huku na kule kumzunguka kizani. Hakuchelewa kubaini kwamba hakuweza kujongea tena hata kidogo.

Haikumshangaza. Kinyume chake, ilionekana kwake kama siyo kawaida kwamba mpaka sasa aliweza kujongea huku na kule kwa kutumia tuvigulu hutu.

Juu ya hayo alijihisi kama aliyetosheka. Kweli, alikuwa na maumivu mwili wake wote, lakini ilionekana kwake kwamba yalikuwa polepole yakipungua na kupungua na hatimaye yangepotelea mbali.

Tufaa lililooza mgongoni mwake na eneo lililovimba kulizunguka, yaliyokuwa yamefunikwa kabisa na vumbi jeupe, hakuyazingatia kivile.

Aliikumbuka familia yake kwa hisia kali na upendo. Kwenye suala hili, mawazo yake kwamba ilimlazimu kutoweka yalikuwa, kama ingewezekana, ni uamuzi imara kuliko wa dada yake.


Alibakia katika hali hii ya fikra tupu na tulivu mpaka saa ya mji ilipolia kuashiria ni saa tisa usiku.

Kutokea dirishani, alishuhudia mwanzo wa dalili za kupambauka huko nje.

Kisha bila kudhamiria, kichwa chake kilishuka chini kabisa, na kupitia pua zake zilitoa kidhaifu pumzi yake ya mwisho.


Mapema asubuhi mama wa usafi alifika. Kwa aligonga milango yote (kwa namna ileile watu waliyomtaka aepuke), kiasi kwamba tangu afike usingizi mtulivu haukuwezekana tena popote nyumbani.



Katika mazoea yake ya kumtembelea Grego, kwanza hakuona lolote la tafauti. Alidhani Grego alikuwa amelala bila kutikisika akikusudia aonekane ni aonewaye.

Alijaribu kumwelewa Grego kadiri ilivyowezekana. Kwa vile ilitukia kwamba alikuwa ameshika fagio refu mkononi mwake, mama wa usafi alijaribu kumtikisa Grego akilitumia tokea mlangoni.

Hilo lilipokuwa si la fanaka, alianza kuchukia na kumchomachoma Grego zaidi, na ni pale tu alipoona alikuwa amesukuma tokea alipokuwapo pasi na ukinzani wowote, ndipo alipoanza kuwa makini.

Alipofahamu upesi ukweli halisi wa mambo, macho yake yalikuwa makubwa, alipiga mluzi mwenyewe, lakini hakujizuia kwa muda mrefu.

Alifungua mlango wa chumbani na kupiga kelele kwa sauti kubwa kizani, “Njoni muone. Limesharudisha namba. Limelala pale, kwisha habari yake!”

Bwana na Bibi Samsa waliketi kwenye kitanda cha chumbani kwao na ilibidi mstuko wao kwa mama wa usafi uishe kabla hawajaelewa anachokisema.

Lakini hapo Bwana na Bibi Samsa waliamka haraka kutoka kitandani, mmoja kila upande wa kitanda. Bwana Samsa alijigubika shuka mabegani mwake, Bibi Samsa alitoka akiwa amevaa tu nguo yake ya kulalia, na hivyo ndivyo walivyoingia chumbani kwa Grego.

Wakati huohuo, mlango unaoelekea sebuleni (ambako Grete alilala tangia wapangaji wawepo kwao) pia ulikuwa umefunguliwa.


Alikuwa amevaa nguo zote, kama ambaye hakulala kabisa; uso wake uliopauka kadhalika ukionekana kuashiria hayo.

“Amekufa?” alisema Bibi Samsa na kumwangalia kwa mashaka mama wa usafi, ingawa angeweza kukagua kila kitu yeye mwenyewe na hata kuelewa bila kukagua.

“Naweza kusema hivyo,” alisema mama wa usafi, na kama njia ya kuthibitisha, aliuchokoa mwili wa Grego kwa kutumia fagio na kuusogeza umbali wa kutosha upande mmoja.

Bibi Samsa alijongea kama ambaye alitamani kulizuia fagio, lakini hakufanya hivyo.



“Hapo,” alisema Bwana Samsa, “sasa tunaweza kumrudishia Mungu shukurani.”

Alifanya ishara ya msalaba, na wale wanawake watatu walimfuatisha.

Grete, ambaye hakubandua macho yake kutoka kwenye maiti, alisema, “Angalia ni namna gani alivyokuwa amekonda. Hakula kitu kwa muda mrefu hivi. Maakuli yaliyoletwa humu yalitoka nje hivyohivyo kama yalivyoingia.

Kiukweli, mwili wa Grego ulikuwa bapa kabisa na mkavu. Hilo lilionekana vizuri kwa mara ya kwanza, kwa vile hakuwa ameinuliwa na tuvigulu twake tudogo na, zaidi ya hayo, sasa wangeweza kumwangalia vizuri.

“Grete, njoo huku mara moja,” alisema Bibi Samsa kwa tabasamu la huzuni, na Grete alienda, bila kutazama nyuma kuiangalia maiti, akipita nyuma ya wazazi wake chumbani.

Mama wa usafi alifunga mlango na kufungua dirisha. Licha ya kwamba ilikuwa ni mapema asubuhi, hewa safi ilikuwa kwa sehemu ina kijotojoto fulani. Tayari ilikuwa ni mwishoni mwa mwezi Machi.

Wale wapangaji watatu walitoka chumbani kwao na waliangalia huku na kule kutafuta kiliko kiamshakinywa chao, na kustushwa kuona wamesahauliwa.

“Wapi chai?” aliuliza yule jamaa wa kati, kwa kibri kumuelekea mama wa usafi.

Lakini, aliweka kidole chake mdomoni na kisha kwa haraka na kimyakimya akawaashiria waje chumbani kwa Grego.

ITAENDELEA
 
Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute - 33

Kabla hata hakuingia vizuri chumbani kwake pale ambapo mlango ulisukumwa kufungwa kwa haraka, komeo kufungwa, na vizuizi kuwekwa. Grego alisangazwa na vurugu la ghafla lililokuwapo nyuma yake, sana tu kiasi cha kumfanya tuvigulu twake tudogo, tujikunje mara mbili chini yake.

Ilikuwa ni dada yake ambaye alikuwa na haraka kiasi hicho. Aliinuka mara, akasubiri, na kisha akaenda mbele haraka kwa kunyata. Grego hakusikia chochote wakati dada akikaribia.

Dada akapiga kelele “Hatimaye!” kwa wazazi wake, wakati akizungusha ufunguo kwenye kitasa.

“Nini kifuatacho?” Grego alijiuliza na kuangalia huku na kule kumzunguka kizani. Hakuchelewa kubaini kwamba hakuweza kujongea tena hata kidogo.

Haikumshangaza. Kinyume chake, ilionekana kwake kama siyo kawaida kwamba mpaka sasa aliweza kujongea huku na kule kwa kutumia tuvigulu hutu.

Juu ya hayo alijihisi kama aliyetosheka. Kweli, alikuwa na maumivu mwili wake wote, lakini ilionekana kwake kwamba yalikuwa polepole yakipungua na kupungua na hatimaye yangepotelea mbali.

Tufaa lililooza mgongoni mwake na eneo lililovimba kulizunguka, yaliyokuwa yamefunikwa kabisa na vumbi jeupe, hakuyazingatia kivile.

Aliikumbuka familia yake kwa hisia kali na upendo. Kwenye suala hili, mawazo yake kwamba ilimlazimu kutoweka yalikuwa, kama ingewezekana, ni uamuzi imara kuliko wa dada yake.


Alibakia katika hali hii ya fikra tupu na tulivu mpaka saa ya mji ilipolia kuashiria ni saa tisa usiku.

Kutokea dirishani, alishuhudia mwanzo wa dalili za kupambauka huko nje.

Kisha bila kudhamiria, kichwa chake kilishuka chini kabisa, na kupitia pua zake zilitoa kidhaifu pumzi yake ya mwisho.


Mapema asubuhi mama wa usafi alifika. Kwa aligonga milango yote (kwa namna ileile watu waliyomtaka aepuke), kiasi kwamba tangu afike usingizi mtulivu haukuwezekana tena popote nyumbani.



Katika mazoea yake ya kumtembelea Grego, kwanza hakuona lolote la tafauti. Alidhani Grego alikuwa amelala bila kutikisika akikusudia aonekane ni aonewaye.

Alijaribu kumwelewa Grego kadiri ilivyowezekana. Kwa vile ilitukia kwamba alikuwa ameshika fagio refu mkononi mwake, mama wa usafi alijaribu kumtikisa Grego akilitumia tokea mlangoni.

Hilo lilipokuwa si la fanaka, alianza kuchukia na kumchomachoma Grego zaidi, na ni pale tu alipoona alikuwa amesukuma tokea alipokuwapo pasi na ukinzani wowote, ndipo alipoanza kuwa makini.

Alipofahamu upesi ukweli halisi wa mambo, macho yake yalikuwa makubwa, alipiga mluzi mwenyewe, lakini hakujizuia kwa muda mrefu.

Alifungua mlango wa chumbani na kupiga kelele kwa sauti kubwa kizani, “Njoni muone. Limesharudisha namba. Limelala pale, kwisha habari yake!”

Bwana na Bibi Samsa waliketi kwenye kitanda cha chumbani kwao na ilibidi mstuko wao kwa mama wa usafi uishe kabla hawajaelewa anachokisema.

Lakini hapo Bwana na Bibi Samsa waliamka haraka kutoka kitandani, mmoja kila upande wa kitanda. Bwana Samsa alijigubika shuka mabegani mwake, Bibi Samsa alitoka akiwa amevaa tu nguo yake ya kulalia, na hivyo ndivyo walivyoingia chumbani kwa Grego.

Wakati huohuo, mlango unaoelekea sebuleni (ambako Grete alilala tangia wapangaji wawepo kwao) pia ulikuwa umefunguliwa.


Alikuwa amevaa nguo zote, kama ambaye hakulala kabisa; uso wake uliopauka kadhalika ukionekana kuashiria hayo.

“Amekufa?” alisema Bibi Samsa na kumwangalia kwa mashaka mama wa usafi, ingawa angeweza kukagua kila kitu yeye mwenyewe na hata kuelewa bila kukagua.

“Naweza kusema hivyo,” alisema mama wa usafi, na kama njia ya kuthibitisha, aliuchokoa mwili wa Grego kwa kutumia fagio na kuusogeza umbali wa kutosha upande mmoja.

Bibi Samsa alijongea kama ambaye alitamani kulizuia fagio, lakini hakufanya hivyo.



“Hapo,” alisema Bwana Samsa, “sasa tunaweza kumrudishia Mungu shukurani.”

Alifanya ishara ya msalaba, na wale wanawake watatu walimfuatisha.

Grete, ambaye hakubandua macho yake kutoka kwenye maiti, alisema, “Angalia ni namna gani alivyokuwa amekonda. Hakula kitu kwa muda mrefu hivi. Maakuli yaliyoletwa humu yalitoka nje hivyohivyo kama yalivyoingia.

Kiukweli, mwili wa Grego ulikuwa bapa kabisa na mkavu. Hilo lilionekana vizuri kwa mara ya kwanza, kwa vile hakuwa ameinuliwa na tuvigulu twake tudogo na, zaidi ya hayo, sasa wangeweza kumwangalia vizuri.

“Grete, njoo huku mara moja,” alisema Bibi Samsa kwa tabasamu la huzuni, na Grete alienda, bila kutazama nyuma kuiangalia maiti, akipita nyuma ya wazazi wake chumbani.

Mama wa usafi alifunga mlango na kufungua dirisha. Licha ya kwamba ilikuwa ni mapema asubuhi, hewa safi ilikuwa kwa sehemu ina kijotojoto fulani. Tayari ilikuwa ni mwishoni mwa mwezi Machi.

Wale wapangaji watatu walitoka chumbani kwao na waliangalia huku na kule kutafuta kiliko kiamshakinywa chao, na kustushwa kuona wamesahauliwa.

“Wapi chai?” aliuliza yule jamaa wa kati, kwa kibri kumuelekea mama wa usafi.

Lakini, aliweka kidole chake mdomoni na kisha kwa haraka na kimyakimya akawaashiria waje chumbani kwa Grego.

ITAENDELEA
Navosubiri next part 😊
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom