Naandika hii post nikiwa nacheka mbavu sina mwenzenu. Jana kuna mshikaji wangu alinisimulia yaliyomsibu siku nzima kiasi cha kukosa amani ya moyo siku nzima kiasi cha kuja kuniomba ushauri. Ilikuwa hivi, jamaa ni cheater sana lakini mkewe bado hajagundua. Ana simu tatu. Moja bei mbaya (simu kali). zingine mbili za kawaida na kati ya hizi, simu ya bei ya chini kabisa (mkweche) ndo ina line za cheating na hiyo simu haachii popote aendapo. Hata namba zake mkewe hajui.
Sasa jana jumapili akiwa katika harakati za kwenda church, akawa anachelewa so akarush kwa haraka, akawa kabeba simu mbili za kawaida na kusahau ile ya cheating kitandani. Akawa amekumbuka kuwa kasahau simu akiwa kanisani. Pressure ikampanda akawa hasikilizi tena ibada, alafu mkewe huwa ana tabia ya kuchelewa kwenda kanisani. Mbaya zaidi mkewe anasali kanisa lingine, kwa hiyo kuonana ni mpaka mchana sana. Aliporudi home akawa mwoga kwani alikuwa na maswali mengi yasiyo na majibu, 1) Itakuwaje kama wife ameshika hiyo simu na kusoma msg au kupokea simu ikipigwa? 2) Akifika ataanzaje kumsemesha mkewe ili hali hajajua kama mrs alishika hiyo simu au la? 3) Kama mkewe atakuwa kafuma madudu yaliyomo mle kwenye simu nini kitafuata?
Kama ni wewe hebu tueleze unaporudi home ungeingia kwa gia gani hapo?
Sasa jana jumapili akiwa katika harakati za kwenda church, akawa anachelewa so akarush kwa haraka, akawa kabeba simu mbili za kawaida na kusahau ile ya cheating kitandani. Akawa amekumbuka kuwa kasahau simu akiwa kanisani. Pressure ikampanda akawa hasikilizi tena ibada, alafu mkewe huwa ana tabia ya kuchelewa kwenda kanisani. Mbaya zaidi mkewe anasali kanisa lingine, kwa hiyo kuonana ni mpaka mchana sana. Aliporudi home akawa mwoga kwani alikuwa na maswali mengi yasiyo na majibu, 1) Itakuwaje kama wife ameshika hiyo simu na kusoma msg au kupokea simu ikipigwa? 2) Akifika ataanzaje kumsemesha mkewe ili hali hajajua kama mrs alishika hiyo simu au la? 3) Kama mkewe atakuwa kafuma madudu yaliyomo mle kwenye simu nini kitafuata?
Kama ni wewe hebu tueleze unaporudi home ungeingia kwa gia gani hapo?