Asante,
Nimeadimika kidogo sababu nilikuwa shambani huko porini, walau siku hizi mbili tatu nitakuwa hapa jamvini, huu ndio msimu wetu sisi wakulima wa miti.
Nirudi kwenye point, study tours ni nzuri sana, ni muhimu kwa mjasiriamali kufanya tours kwa wengine, ningependa hata sisi wafuga kuku tukajuana vizuri ili tuweze kubadilishana uzoefu. Mfano sisi walima miti, tunajuana, sasa hivi tumefikia hata kuagiza mbegu za miti toka nje ya nchi baada ya kugundua uzembe wa serikali na taasisi zake, tumelia lia sana na vituo vya mbegu, baadae tukagundua kuwa hapo jirani kuna mbegu za uhakika. Tunachukua mzigo mkubwa tunagawana na tunasonga mbele.
Tukienda kwa makundi yenye product moja kwa kumaanisha, hili suala la kulia lia habari ya soko litakwisha lenyewe, ila ni lazima tuzalishe kwa ubora wa juu ili kuteka soko. Tusisubiri serikali itufanyie kila kitu.