Chanzo cha mabasi ya "No Challenge" kuitwa "Tashriff"

Chanzo cha mabasi ya "No Challenge" kuitwa "Tashriff"

Aahahahahahaaa

Sikubahatika pamoja na kusakata rhumba kwa kila mkao.....

Ukiweka sera humu utapata tuu, mbona wapo wengi tuu warembo kuliko urembo wenyewe.
Wasalimie hapo sinza mori
 
acheni tabia ya uongo mnapotosha vijana wenu walozaliwa baada ya huo usafiri kusitishwa. Treni ya Moshi-Dar ilikuwa inaondoka saa 04.15 jioni haijawahi kuongeza muda wala kupunguza. Treni kutoka Tanga ilikuwa inafika Korogwe, inasubiri ya kutokea Dar-Moshi, wanabadilisha mabehewa pale, tunaondokaga saa 8 hivi usiku Tanga tunafikaga alfajir saa 06.00am bila kuchelewa. Treni zilikuwa smart sana acha kupotosha watu. Nna wasiwasi we hujawahi kutumia huo usafiri.

Sawa Mkuu.
 
acheni tabia ya uongo mnapotosha vijana wenu walozaliwa baada ya huo usafiri kusitishwa. Treni ya Moshi-Dar ilikuwa inaondoka saa 04.15 jioni haijawahi kuongeza muda wala kupunguza. Treni kutoka Tanga ilikuwa inafika Korogwe, inasubiri ya kutokea Dar-Moshi, wanabadilisha mabehewa pale, tunaondokaga saa 8 hivi usiku Tanga tunafikaga alfajir saa 06.00am bila kuchelewa. Treni zilikuwa smart sana acha kupotosha watu. Nna wasiwasi we hujawahi kutumia huo usafiri.
Mmh rafiki bila kuchelewa...tumelala sana stesheni, kwa hapo nitakukatalia...labda kama ulibahatika kwenye safari zako zilikuwa shwari mwanzo mwisho...
 
Heb
Anaandika mzee Joseph Jandwa

Leo 3/5/2023 imetimia miaka 25 tangu ajali ya basi iliyosababisha vifo vya abiria 96 na majeruhi 9, ilipotokea jioni ya tar 3/5/1998. Kihistoria haijawahi kutokea ajali mbaya ya basi iliyoua watu wengi kama hiyo.

Mimi ni miongoni mwa wale 9 walionusurika kwa neema ya Mungu. Ajali hii ilihusisha basi la kampuni ya NO CHALLENGE ambayo baada ya ajali ile ilibadili jina na kujiita TASHRIFF. Ajali ilitokea Mkoani Tanga, Wilaya Muheza, kijiji cha Kibanda. Bus lililokua na namba za Usajili TZK 960 lilikuwa likitoka Tanga kuelekea DSM.

Kipindi hicho kulikuwa na mvua nyingi zilizobatizwa jina Mvua za El-Nino. Tulipofika kijijini hapo tulikuta mabasi mengi yamesimama kutokana na kujaa maji kwenye mto Msangazi. Kuanzia mabasi makubwa hadi madogo kama Coaster na Hiace. Pia zilikuwepo gari binafsi.

Kwenye kijiji cha Kibanda kuna mto uitwao Msangazi. Ulikua umejaa maji. Basi tulilopanda lilijaribu kuvuka ng'ambo ya pili ili kuendelea na safari. Baadhi ya abiria wa mabasi mengine walidandia basi letu ili wavuke kuendelea na ratiba zao. Lakini halikuweza kufika ng'ambo. Lilisombwa na maji. Likasukumwa mtoni na kuzama kabisa.

Watu 96 wakapoteza maisha, wakiwemo wale waliodandia. Sehemu kubwa ya abiria walifia ndani ya basi kwa kushindwa kutoka. Wachache walioweza kutokea madirishani walikufa kutokana na kusombwa na maji yenye kasi ya mto huo. Ilikua simanzi kubwa.

Pamejengwa mnara wa kumbukumbu ya wafu na majina yao. Lakini naambiwa vijana wa vyuma chakavu walishakwanyua kibao kilichokuwa kimeorodhesha majina ya wafu 72 waliotambulika na wengine 24 ambao hawakutambuliwa.

Katika wale 9 tuliosalimika, mmoja wao ni Mzee Ramadhani Kimbunga aliyekuwa Dereva wa basi hilo. Bahati mbaya pamoja na kuokoka kwenye ajali hiyo alikuja kufa miezi michache baadae kwa kifo cha kawaida. Manusura wengine wawili nao walishafariki kwa nyakati tofauti, na tuliosalia hai mpaka sasa ni 6 tu.

Baada ya ajali hiyo kampuni ya NO CHALLENGE ikabadili jina na kujiita TASHRIFF kwa sababu Challenge imeshatokea. Nimeona niwakumbushe maana wengi wamesahau. Na tuliosalimika ili kusimulia tumebaki 6 tu. Tujifunze kupitia kisa hiki ili kuepusha ajali nyingine za aina hii.

View attachment 2608991
Pole Dana mzee.hebu tukumbushie na air msae mpaka kubadilishwa kuwa Kilimanjaro bus nasikia nayo ilizama mtoni 1998 Enzo za elnino.anaejua hii taarifa atupe mkanda mzma
 
Ni kweli maji yalionekana ya kawaida tu, ila lilipotokomea basi zima ndio ukweli ukadhihirika...
Acha tu,bi mkubwa mwenyewe hataki umkumbushie kabisa hyo ajali ilivyotokea,anapandisha hadi presha akiogopa lile tukio
 
Vipi ile abood mwaka 1997 ambapo bus liliparamia kijiko cha tingatinga kilichokuwa kimebebwa kwenye semi trailer.Hivi kuna mtu anaweza kutusimulia sijui hiko kijiko kilikuwa kimekaaje kwenye hilo lorry mpaka kikaanza kuchinja watu baada ya abood kikiparamia kikiwa kwenye lorry
 
Anaandika mzee Joseph Jandwa

Leo 3/5/2023 imetimia miaka 25 tangu ajali ya basi iliyosababisha vifo vya abiria 96 na majeruhi 9, ilipotokea jioni ya tar 3/5/1998. Kihistoria haijawahi kutokea ajali mbaya ya basi iliyoua watu wengi kama hiyo.

Mimi ni miongoni mwa wale 9 walionusurika kwa neema ya Mungu. Ajali hii ilihusisha basi la kampuni ya NO CHALLENGE ambayo baada ya ajali ile ilibadili jina na kujiita TASHRIFF. Ajali ilitokea Mkoani Tanga, Wilaya Muheza, kijiji cha Kibanda. Bus lililokua na namba za Usajili TZK 960 lilikuwa likitoka Tanga kuelekea DSM.

Kipindi hicho kulikuwa na mvua nyingi zilizobatizwa jina Mvua za El-Nino. Tulipofika kijijini hapo tulikuta mabasi mengi yamesimama kutokana na kujaa maji kwenye mto Msangazi. Kuanzia mabasi makubwa hadi madogo kama Coaster na Hiace. Pia zilikuwepo gari binafsi.

Kwenye kijiji cha Kibanda kuna mto uitwao Msangazi. Ulikua umejaa maji. Basi tulilopanda lilijaribu kuvuka ng'ambo ya pili ili kuendelea na safari. Baadhi ya abiria wa mabasi mengine walidandia basi letu ili wavuke kuendelea na ratiba zao. Lakini halikuweza kufika ng'ambo. Lilisombwa na maji. Likasukumwa mtoni na kuzama kabisa.

Watu 96 wakapoteza maisha, wakiwemo wale waliodandia. Sehemu kubwa ya abiria walifia ndani ya basi kwa kushindwa kutoka. Wachache walioweza kutokea madirishani walikufa kutokana na kusombwa na maji yenye kasi ya mto huo. Ilikua simanzi kubwa.

Pamejengwa mnara wa kumbukumbu ya wafu na majina yao. Lakini naambiwa vijana wa vyuma chakavu walishakwanyua kibao kilichokuwa kimeorodhesha majina ya wafu 72 waliotambulika na wengine 24 ambao hawakutambuliwa.

Katika wale 9 tuliosalimika, mmoja wao ni Mzee Ramadhani Kimbunga aliyekuwa Dereva wa basi hilo. Bahati mbaya pamoja na kuokoka kwenye ajali hiyo alikuja kufa miezi michache baadae kwa kifo cha kawaida. Manusura wengine wawili nao walishafariki kwa nyakati tofauti, na tuliosalia hai mpaka sasa ni 6 tu.

Baada ya ajali hiyo kampuni ya NO CHALLENGE ikabadili jina na kujiita TASHRIFF kwa sababu Challenge imeshatokea. Nimeona niwakumbushe maana wengi wamesahau. Na tuliosalimika ili kusimulia tumebaki 6 tu. Tujifunze kupitia kisa hiki ili kuepusha ajali nyingine za aina hii.

View attachment 2608991
Poleni. 1998 nipo form 6 napiga PGM
 
Anaandika mzee Joseph Jandwa

Leo 3/5/2023 imetimia miaka 25 tangu ajali ya basi iliyosababisha vifo vya abiria 96 na majeruhi 9, ilipotokea jioni ya tar 3/5/1998. Kihistoria haijawahi kutokea ajali mbaya ya basi iliyoua watu wengi kama hiyo.

Mimi ni miongoni mwa wale 9 walionusurika kwa neema ya Mungu. Ajali hii ilihusisha basi la kampuni ya NO CHALLENGE ambayo baada ya ajali ile ilibadili jina na kujiita TASHRIFF. Ajali ilitokea Mkoani Tanga, Wilaya Muheza, kijiji cha Kibanda. Bus lililokua na namba za Usajili TZK 960 lilikuwa likitoka Tanga kuelekea DSM.

Kipindi hicho kulikuwa na mvua nyingi zilizobatizwa jina Mvua za El-Nino. Tulipofika kijijini hapo tulikuta mabasi mengi yamesimama kutokana na kujaa maji kwenye mto Msangazi. Kuanzia mabasi makubwa hadi madogo kama Coaster na Hiace. Pia zilikuwepo gari binafsi.

Kwenye kijiji cha Kibanda kuna mto uitwao Msangazi. Ulikua umejaa maji. Basi tulilopanda lilijaribu kuvuka ng'ambo ya pili ili kuendelea na safari. Baadhi ya abiria wa mabasi mengine walidandia basi letu ili wavuke kuendelea na ratiba zao. Lakini halikuweza kufika ng'ambo. Lilisombwa na maji. Likasukumwa mtoni na kuzama kabisa.

Watu 96 wakapoteza maisha, wakiwemo wale waliodandia. Sehemu kubwa ya abiria walifia ndani ya basi kwa kushindwa kutoka. Wachache walioweza kutokea madirishani walikufa kutokana na kusombwa na maji yenye kasi ya mto huo. Ilikua simanzi kubwa.

Pamejengwa mnara wa kumbukumbu ya wafu na majina yao. Lakini naambiwa vijana wa vyuma chakavu walishakwanyua kibao kilichokuwa kimeorodhesha majina ya wafu 72 waliotambulika na wengine 24 ambao hawakutambuliwa.

Katika wale 9 tuliosalimika, mmoja wao ni Mzee Ramadhani Kimbunga aliyekuwa Dereva wa basi hilo. Bahati mbaya pamoja na kuokoka kwenye ajali hiyo alikuja kufa miezi michache baadae kwa kifo cha kawaida. Manusura wengine wawili nao walishafariki kwa nyakati tofauti, na tuliosalia hai mpaka sasa ni 6 tu.

Baada ya ajali hiyo kampuni ya NO CHALLENGE ikabadili jina na kujiita TASHRIFF kwa sababu Challenge imeshatokea. Nimeona niwakumbushe maana wengi wamesahau. Na tuliosalimika ili kusimulia tumebaki 6 tu. Tujifunze kupitia kisa hiki ili kuepusha ajali nyingine za aina hii.

View attachment 2608991
Pole sana
 
Mimi naona bado madereva wengi hawajajifunza hili suala la kukatiza kwenye yanayotembea.

Hata hizi mvua zinazoendelea tumeona clips za magari yakisombwa mdereva wanapojaribu kuvuka ng'ambo ya pili wamejikuta wakisombwa na kuingia mtoni
 
1.>>> Shengena Bus Service. 2.>>> Air Shengena. 3.>>> No Challenge 4. >>> Tashrif
Na lile basi la kuitwa SATELLITE, lilikuwa ni jipya au ndio hizohizo za kubadili majina?
 
Back
Top Bottom