The Genius
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 828
- 2,110
Anaandika mzee Joseph Jandwa
Leo 3/5/2023 imetimia miaka 25 tangu ajali ya basi iliyosababisha vifo vya abiria 96 na majeruhi 9, ilipotokea jioni ya tar 3/5/1998. Kihistoria haijawahi kutokea ajali mbaya ya basi iliyoua watu wengi kama hiyo.
Mimi ni miongoni mwa wale 9 walionusurika kwa neema ya Mungu. Ajali hii ilihusisha basi la kampuni ya NO CHALLENGE ambayo baada ya ajali ile ilibadili jina na kujiita TASHRIFF. Ajali ilitokea Mkoani Tanga, Wilaya Muheza, kijiji cha Kibanda. Bus lililokua na namba za Usajili TZK 960 lilikuwa likitoka Tanga kuelekea DSM.
Kipindi hicho kulikuwa na mvua nyingi zilizobatizwa jina Mvua za El-Nino. Tulipofika kijijini hapo tulikuta mabasi mengi yamesimama kutokana na kujaa maji kwenye mto Msangazi. Kuanzia mabasi makubwa hadi madogo kama Coaster na Hiace. Pia zilikuwepo gari binafsi.
Kwenye kijiji cha Kibanda kuna mto uitwao Msangazi. Ulikua umejaa maji. Basi tulilopanda lilijaribu kuvuka ng'ambo ya pili ili kuendelea na safari. Baadhi ya abiria wa mabasi mengine walidandia basi letu ili wavuke kuendelea na ratiba zao. Lakini halikuweza kufika ng'ambo. Lilisombwa na maji. Likasukumwa mtoni na kuzama kabisa.
Watu 96 wakapoteza maisha, wakiwemo wale waliodandia. Sehemu kubwa ya abiria walifia ndani ya basi kwa kushindwa kutoka. Wachache walioweza kutokea madirishani walikufa kutokana na kusombwa na maji yenye kasi ya mto huo. Ilikua simanzi kubwa.
Pamejengwa mnara wa kumbukumbu ya wafu na majina yao. Lakini naambiwa vijana wa vyuma chakavu walishakwanyua kibao kilichokuwa kimeorodhesha majina ya wafu 72 waliotambulika na wengine 24 ambao hawakutambuliwa.
Katika wale 9 tuliosalimika, mmoja wao ni Mzee Ramadhani Kimbunga aliyekuwa Dereva wa basi hilo. Bahati mbaya pamoja na kuokoka kwenye ajali hiyo alikuja kufa miezi michache baadae kwa kifo cha kawaida. Manusura wengine wawili nao walishafariki kwa nyakati tofauti, na tuliosalia hai mpaka sasa ni 6 tu.
Baada ya ajali hiyo kampuni ya NO CHALLENGE ikabadili jina na kujiita TASHRIFF kwa sababu Challenge imeshatokea. Nimeona niwakumbushe maana wengi wamesahau. Na tuliosalimika ili kusimulia tumebaki 6 tu. Tujifunze kupitia kisa hiki ili kuepusha ajali nyingine za aina hii.
Leo 3/5/2023 imetimia miaka 25 tangu ajali ya basi iliyosababisha vifo vya abiria 96 na majeruhi 9, ilipotokea jioni ya tar 3/5/1998. Kihistoria haijawahi kutokea ajali mbaya ya basi iliyoua watu wengi kama hiyo.
Mimi ni miongoni mwa wale 9 walionusurika kwa neema ya Mungu. Ajali hii ilihusisha basi la kampuni ya NO CHALLENGE ambayo baada ya ajali ile ilibadili jina na kujiita TASHRIFF. Ajali ilitokea Mkoani Tanga, Wilaya Muheza, kijiji cha Kibanda. Bus lililokua na namba za Usajili TZK 960 lilikuwa likitoka Tanga kuelekea DSM.
Kipindi hicho kulikuwa na mvua nyingi zilizobatizwa jina Mvua za El-Nino. Tulipofika kijijini hapo tulikuta mabasi mengi yamesimama kutokana na kujaa maji kwenye mto Msangazi. Kuanzia mabasi makubwa hadi madogo kama Coaster na Hiace. Pia zilikuwepo gari binafsi.
Kwenye kijiji cha Kibanda kuna mto uitwao Msangazi. Ulikua umejaa maji. Basi tulilopanda lilijaribu kuvuka ng'ambo ya pili ili kuendelea na safari. Baadhi ya abiria wa mabasi mengine walidandia basi letu ili wavuke kuendelea na ratiba zao. Lakini halikuweza kufika ng'ambo. Lilisombwa na maji. Likasukumwa mtoni na kuzama kabisa.
Watu 96 wakapoteza maisha, wakiwemo wale waliodandia. Sehemu kubwa ya abiria walifia ndani ya basi kwa kushindwa kutoka. Wachache walioweza kutokea madirishani walikufa kutokana na kusombwa na maji yenye kasi ya mto huo. Ilikua simanzi kubwa.
Pamejengwa mnara wa kumbukumbu ya wafu na majina yao. Lakini naambiwa vijana wa vyuma chakavu walishakwanyua kibao kilichokuwa kimeorodhesha majina ya wafu 72 waliotambulika na wengine 24 ambao hawakutambuliwa.
Katika wale 9 tuliosalimika, mmoja wao ni Mzee Ramadhani Kimbunga aliyekuwa Dereva wa basi hilo. Bahati mbaya pamoja na kuokoka kwenye ajali hiyo alikuja kufa miezi michache baadae kwa kifo cha kawaida. Manusura wengine wawili nao walishafariki kwa nyakati tofauti, na tuliosalia hai mpaka sasa ni 6 tu.
Baada ya ajali hiyo kampuni ya NO CHALLENGE ikabadili jina na kujiita TASHRIFF kwa sababu Challenge imeshatokea. Nimeona niwakumbushe maana wengi wamesahau. Na tuliosalimika ili kusimulia tumebaki 6 tu. Tujifunze kupitia kisa hiki ili kuepusha ajali nyingine za aina hii.