Nimekutana na Hii kitu mahala nikaona nilete kwa Ma GT Je kuna Ukweli wa hili jambo? kama Lipo hawa sio watu wazuri nna Mashaka nao..Tukae kwa Tahadhari Wananzengo
CHANJO YA CORONA KUFANYIWA MAJARIBIO AFRICA
Umoja wa Mataifa umedhamiria kuifanyia majaribio Chanjo dhidi ya virusi vya Corona katika bara la Africa ili waone kama inafanya kazi.
Aliyetangaza mpango huo ni ni Katibu Mkuu wa umoja huo #Antonio_Guteress.
#Nukuuu___
" Tayari tumetengeneza chanjo ambayo itakuwa Kinga dhidi ya virusi vya Corona na tumedhamiria kuanza kuifanyia jaribio la kwanza barani Afrika ili turuhusu chanjo hiyo itumike , tutaanza kwa kupima mtu mwenye ngozi nyeusi atakayeweza kujitolea na atalipwa pesa nyingi Sana."
# Ikumbukwe kuwa siku chache zilizopita daktari mkubwa nchini ufaransa mwenye asili ya Senegal #Dider_Raoult alionya juu ya Chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona itakayo tumwa barani Africa na Bilionea #Bill_Gates kwa mgongo wa Umoja wa Mataifa.
#Nukuuu___
"Tafadhali msitumie chanjo ambayo #Bill_Gates atatuma barani Afrika, nawaomba viongozi wa nchi za Afrika chukueni tahadhari na kuweni makini na chanjo ambazo hawa matajiri wa nchi za ulaya na Marekani wanataraji kuzituma katika nchi zenu, nina imani kuwa chanjo hizo huenda zinalenga kuiangamiza Afrika , embu tafakari kwa makini kama wanahitaji kutoa msaada kwanini wasianzie Italy, Hispania au Marekani ambako watu wanafariki kila kukicha kwani chanjo hiyo isiende kufanyiwa majaribio katika nchi za ulaya na Asia lakini wanaleta Afrika tu ???"