#COVID19 Chanjo ya Corona Dar es Salaam na muitikio mdogo

Hakuna aliloanzisha likaffaulu..kuanzia wamachunga hadi usafi...now chanjo
 
hii hali ikiendelea na huu mkanganyiko watuchanje tusichanje basi wananchi hawatajitokeza kabisa kuchanja.

Mkuu wa mkoa kafeli mno katika kuhamasisha wanadsm wajitokeze ilitakiwa leo ndio iwe slama kwa taifa kua dsm watu wamejitokeza wengi
Nchi imekosa uongozi madhubuti hii. Ukishakuwa na rais ambaye hana vision usitegee matokeo chanya. Rais alikosea sana kuendelea na wale wale walioboronga mwanzoni.
 
Hatutaweza kuwa na akili za
matibabu kama nchi haina university Teaching hospital,.
 
Mkuu we si umeshachanja?Hiari yako uliyotumia na wengine nao wanaitumia.

Tusilazimishane Wala kuhamasishana....suala la afya na uhai Ni jukumu ya kila mtu na utashi wake
 
Tozo za Simu, mara kodi ya jengo. Unaanzaje kupata utulivu wa Akili kwenda kuchanja.
Bora kwenda kutafuta pesa Au kwenda kwenye Ibada kuliko kwenda kuchanja.
Chanjo zenyewe ziaharibike tu.
Kabisa na ziharibike tu
 
Dar es Salaam ni kama imebeba picha ya Tanzania nzima wakati fulani ni kama pilot (case study) katika mikoa mingine.

Mkuu wa mkoa wa DSM alitangaza siku ya leo kuwa kutakua na chanjo ya UVIKO-19 katika uwanja wa taifa wa Uhuru, mimi nimekwenda na nimechanjwa hali nilioiona kwa leo hapana muitikio ni mdogo mno kuna sababu za msingi za kulipa nguvu jambo hili.

Mosi ni kwa wale waliokuwa viongozi wa awamu ya tano katika Wizara ya Afya wajipime,sio mpaka mama awabadilishie majukumu mengine.

Inawapa sana ugumu watanzania" jana waambiwe hivi na leo waambiwe hivi"(kiongozi anasema jana chanjo sio salama leo anasema chanjo ni salama).

Shaka kubwa sana imejengeka hapo kwa wananchi Rai yangu wapatikane viongozi wapya katika wizara hii kutuhamasisha juu ya uchanjwaji huu vinginevyo naona kabisa serikal inaenda kufeli katika jambo hili.

Sio mbaya kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimuona RC mstaafu aliyegombea kule Mbutu ampe namna ya kuhamasisha watu anapokuwa na jambo lake kwa wananchi wa DSM, naona habari za ofisi yake zinaishia Bungoni tu sio Dar es Salaam yote.

Muwe na Jumapili njema, korona ipo.
Matangazo Kwa kweli yalikuwa kidogo sana media nyingi hazikutangaza kabisa ndio maana mwitiko umekuwa hafifu
 
Niliwahi kushauri hapa kuwa kabla ya nationwide roll out ya Vaccine mama asafishe kwanza mabaki haya ambayo jana yalisema ivi Na Leo wanasema vingine wananchi tunapatwa Na mkanganyiko mana Wataalamu wetu jana wakisema ivi Na Leo wanasema vile hata Mimi nimeamua kukaa pembeni kwanza nikiangalia sarakasi zao
Kwakweli kwa ile clip niliyoiona Leo molel akiongea wakati wa magufuli kuwa chanjo ni mbaya ikiingia kwenye mwili wa mwanadamu!
Sina hamu,ndo maana Gwajima amewalipua
 
Ndugu yangu nakushauri kama upo above 40yrs old nenda kachanje hata kama upo strong kiasi gani nenda kachanje huu Ugonjwa hauwezi kwesha leo wala kesho.
Wazazi wangu washastaafu Dr na nurse,na wana hospital yao kwa sasa mkoani huko!mama alishaumwa last yr na alipona tunamshukuru Mungu! lakini wametuambia tusichanje na wao hawachanji! Na sbb za kitaalamu nimepewa,sa Dorothy aniambie nichanje?bila sbb za kujitosheleza, masihara.
#mi na familia yangu pamoja na huo umri tulionao hatuchanji na tuko salama,Mungu aliyetuvusha awamu ya 1,ya 2 ndo atatuvusha na awamu hii!

So kigezo cha umri bado sio ishu kabisa!
 
Dar es Salaam ni kama imebeba picha ya Tanzania nzima wakati fulani ni kama pilot (case study) katika mikoa mingine.

Mkuu wa mkoa wa DSM alitangaza siku ya leo kuwa kutakua na chanjo ya UVIKO-19 katika uwanja wa taifa wa Uhuru, mimi nimekwenda na nimechanjwa hali nilioiona kwa leo hapana muitikio ni mdogo mno kuna sababu za msingi za kulipa nguvu jambo hili.

Mosi ni kwa wale waliokuwa viongozi wa awamu ya tano katika Wizara ya Afya wajipime,sio mpaka mama awabadilishie majukumu mengine.

Inawapa sana ugumu watanzania" jana waambiwe hivi na leo waambiwe hivi"(kiongozi anasema jana chanjo sio salama leo anasema chanjo ni salama).

Shaka kubwa sana imejengeka hapo kwa wananchi Rai yangu wapatikane viongozi wapya katika wizara hii kutuhamasisha juu ya uchanjwaji huu vinginevyo naona kabisa serikal inaenda kufeli katika jambo hili.

Sio mbaya kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimuona RC mstaafu aliyegombea kule Mbutu ampe namna ya kuhamasisha watu anapokuwa na jambo lake kwa wananchi wa DSM, naona habari za ofisi yake zinaishia Bungoni tu sio Dar es Salaam yote.

Muwe na Jumapili njema, korona ipo.
Umekwenda uwanjani leo?
Radio One taarifa ya habari ya saa mbili wanasema mwitikio ulikuwa mkubwa. Wewe unasema mdogo. Kipi ni kipi?
 
Umekwenda uwanjani leo?
Radio One taarifa ya habari ya saa mbili wanasema mwitikio ulikuwa mkubwa. Wewe unasema mdogo. Kipi ni kipi?
Ulitegemea waseme muitikio ulikuwa mdogo?
Ni kweli muitikio ulikuwa mdogo sana, Sasa imebidi waongeze na siku ya kesho.
Wakati sababu ya kuweka leo ilikuwa kutokana na watu kukosa muda siku za kazi
 
Back
Top Bottom