Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
Ni kiongozi gani wa chadema aliyetoa ombi hili, ni lini na wapi, wewe uliyeanzisha thread ni nani kwenye cdm na nikwanini asianzishe thread ya maombi kiongozi wa chadema?endapo tutachanga Hela zitafanyia nini?
Mwanzisha thread ni Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Arusha, na pia ni Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Arusha na Diwani wa kata ya Levolosi Arusha. Hivyo usitie shaka Angela. Kutoa ni moyo wala siyo utajiri. Angela unafahamika sana jukwaani, michango yako inafahamika sana na ni ya msingi katika harakati za ukombozi wa fikra kwa watanzania ya watu wastaarabu. Wenzetu CCM wanatumia pesa za mafisadi na kodi zetu kufanya kampeni. CHADEMA wanahitaji mchango wako wa hali na mali, siyo lazima uchangie pesa nyingi, bali kile kiasi unachoona umeguswa moyoni mwako hata kama ni sh 200 unaweza kuchangia, ili kufanikisha CHADEMA kufika sehemu zote katika vijiti 86 vya Arumeru. Ukichangia chadema utakuwa umechangia ukombozi wa Tanzania. Angela Msoffe