Changamoto ya umeme nchini ilianza na Awamu ya Tatu, sasa ni mbaya zaidi. Kwanini maji ya Ziwa Victoria yasipelekwe hadi Mtera na JNHPP kupata suluhu?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Awamu ya baba wa taifa na ile ya mzee ruhusa hakukuwa na changamoto la katika katika kwa umeme maeneo ambayo huduma hii ilikuwa imeyafikia. Ni kweli kwamba maeneo hayo yalikuwa hasa kwenye miji mikubwa ya nchi. Shughuli za kiuchumi wa viwanda hazikuwa nyingi kama ilivyo sasa ambapo tumesambaza huduma hii ya umeme hadi kwenye karibu kila kijiji.

Jinsi uchumi wa viwanda ulivyozidi kukua na idadi ya watu kuongezeka, ndivyo changamoto ya umeme ilivyojitokeza na kukua kila kukicha. Zilianza hasa katika kipindi cha awamu ya tatu ya Mzee Mkapa ambaye suluhisho lake lilikuwa ni kuwapa kampuni ya makaburu wa South Africa kutuendeshea Tanesco yetu. Matokeo yake hatutayasahau. Tulipigwa tukapigika.

Ikaja awamu ya nne ya Mzee Kikwete. Wao wakaona suluhisho lake ni kukodi majenereta ya kuzalisha umeme wa dharura kutoka makampuni ya nje ya nchi kama yale ya Richmond, Dowans, Symbion na IPTL. Tukapigwa na kupigika hadi Waziri mkuu akatimuliwa na bunge la Mzee Sitta.

Ikaja awamu ya tano ya Mzee Magufuli. Nayo ikahangaika kwa kubana mafisadi na kuanzisha mahakama ya mafisadi kama suluhisho la changamoto hili la umeme. Kwa kiasi fulani kukawa na ahueni ya kuonesha kuwa ile ndoto ya Tanzania ya viwanda ifikapo 2025 labda ingaliweza kutimia.

Sasa imekuja awamu ya sita ya Mama yetu Mzee Salmia inayopenda kushirikisha wananchi wote kupata suluhisho la changamoto mbali mbali ya wananchi kidemokrasia. Kwa kuwa umeme wa bei rahisi kuliko wote ni ule unaotokana na maji. Na kwa kuwa nchi yetu imejariwa mito mingi na kuzungukwa na maziwa makubwa makubwa mengi: kwa nini maji ya ziwa kama lile la Victoria yasipekwe kwa mabomba huko kwenye bwawa la Mtera na lile la Nyerere ili wakati wa ukame kwenye mabwawa hayo, yakafunguliwa kuyajaza? Ethiopia wanatumia maji ya ziwa Victoria kupitia mto Nile kuzalisha maelfu ya maelfu ya MW za umeme hadi kuwauzia Wakenya.

Kwanini sisi tusitumie Ziwa hili ambalo liko kwetu? Kwani ni shilingi ngapi kupeleka maji ya ziwa letu huko? Kama hatuna hizo hela, tutafute pa kukopa kwani manufaa ya mkopo huu ni mkubwa sana. Hili litakuwa ni suluhisho la once and for all ya changamoto hili la umeme.

Tutaweza hata kuuza umeme nje ya nchi na kuachana na kuuza mahindi na mchele nje ya nchi wakati tukiwa tuna njaa. Tutaweza kupunguza sana bei ya umeme ili wananchi wote waweze kuitumia kama nishati rahisi ya kupikia na hivyo kuachana na ukataji wa miti wakitafuta kuni na mkaa. Mwananchi ataweza kutumia shilingi zisizozidi elfu tano tu kwa mwezi kwa nishati ya kupikia ya umeme.

Tanesco nao wataweza kukusanya matrilioni ya pesa kwani kila mwananchi atakuwa mteja wao. Viwanda vingi vitajengwa na kuzalisha bidhaa nyingi kwa bei nafuu. Kwa muda mfupi nchi yetu itakuwa upper middle income country chini ya uangalizi wa mama!

NB: Umeme utokanao na gesi mara zote bei yake ni ya juu sana (unaffordable to many of our people) ukilinganishwa na ule unaotokanq na maji. Umeme wa gesi ni kwa wakati wa dharura tu au kwa kuuza nje.
 
Wauzaji wa jenereta watamuuzia nani?

Yaani hii nchi unaweza kabisa ukaona suluhu ya kitu flani ni kitu flani,tena kile pale,lakini viongozi wakawa hawatatui tatizo husika kwa njia hiyo,wanatatua kwa njia wanayoijua b wao.
 
Awamu ya baba wa taifa na ile ya mzee ruhusa hakukuwa na changamoto la katika katika kwa umeme maeneo ambayo huduma hii ilikuwa imeyafikia...
Kwani hata umeme wa Sasa wa Maji mnalipa kulingana na gharama halisi au Ni ruzuku tuu?

Tanzania tunalilia umeme Bei Chee Sana inatikwa beinzilingane na wenzetu wa EAC ili kuwasaidia Tanesco.
 
Awamu ya baba wa taifa na ile ya mzee ruhusa hakukuwa na changamoto la katika katika kwa umeme maeneo ambayo huduma hii ilikuwa imeyafikia. Ni kweli kwamba maeneo hayo yalikuwa hasa kwenye miji mikubwa ya nchi. Shughuli za kiuchumi wa viwanda hazikuwa nyingi kama ilivyo sasa ambapo tumesambaza huduma hii ya umeme hadi kwenye karibu kila kijiji.

Jinsi uchumi wa viwanda ulivyozidi kukua na idadi ya watu kuongezeka, ndivyo changamoto ya umeme ilivyojitokeza na kukua kila kukicha...
Harafu acha upotoshaji wa kipumbavu..

Awamu ya 3 ya Mkapa ulitaka kubinafsisha Tanesco so uamzi wa mwisho haukufikiwa ndani Baraza la Mawaziri baadae wakaja wakafuta huo mpango na kufanya modernisation ya management ya Tanesco ila kwa Miaka yote ile ya mchakato wa ubinafsishaji Hakuna uwekezaji mpya wa Serikali uliofanywa kwa sababu ya hiyo sintofahamu..

JK alirithi Nchi ikiwa Hakuna Tanesco yenye vyanzo vipya vya umeme na Uchumi unajua so tunrescue situation ndipo Sasa mitambo ya mafuta almaarufu majenereta ikakodiwa na kuketwa maana huwezi kaa bila umeme huku wakiendelea na uwekezaji wa umeme wa Gas..

So Hadi anaondoka Madarakani Umeme wa gas ndio ukawa na proportion kubwa kwenye energy mix ya 63%.

Mwendazake akaja akaishia kupuuza gas na kuanza mradi wa bwawa ambao haujulikani ungeisha lini,Miaka 5 ikapita bwawa liko 30%.

Amekuja Rais Samia akakutana na Hali Kama ya aliyoikuta JK, mvua zikapungua umeme wa maji ukapungua na gas ilipuuzwa , Sasa kaongeza Pesa Wizara ya Nishati ili kupata umeme wa gas wakati wanaendela na kukomaa na bwawa..

Naomba hapa muelewe awamu ya 4 haitaki.kuzima Moto inaenda na ufumbuzi wa kudumu,bwawa litakuwepo na gas na vyanzo vinginevyo vitaanzishwa ili kuanzia 2026 huko walau kazi ibaki ya mainatanance na sio generation.
 
Awamu ya baba wa taifa na ile ya mzee ruhusa hakukuwa na changamoto la katika katika kwa umeme maeneo ambayo huduma hii ilikuwa imeyafikia...
Nilpofika hopo pa Ethiopia wanatumia maji ya Ziwa Victoria kupitia mto Nile... Siku endelea tena kusoma hiyo post yako.

Yaani unaonyesha unauelewa mdogo sana. Labda rudi darasani tena kasome Geography vizuri uuelewe mto Nile.
 
Nilpofika hopo pa Ethiopia wanatumia maji ya Ziwa Victoria kupitia mto Nile... Siku endelea tena kusoma hiyo post yako.

Yaani unaonyesha unauelewa mdogo sana. Labda rudi darasani tena kasome Geography vizuri uuelewe mto Nile.
Hata hilo pendekezo lake la kutumia Maji ya ya Lake Nyanza kuyaunganisha kwenye Mto Rufiji yaani uchimbe mitaro hadi huko ni Uwazimu.
 
Tanzania bado hamjakoma tu, mmetumbukiza ma trilion ya shilling kutengeneza chanzo kingine cha umeme wa maji, hivi mpo sawa kweli upstairs? wakati mna Gesi ya kumwaga, Makaa ya mawe ya kumwaga, mna Upepo wa hatari na pia mna jua kali ni balaa, vyanzo hivi vyote mmeona havifai si ndiyo.

CCM hebu acheni kutesa wananchi, hivi wamewakosea nini kulala gizani na kuoga kwa zamu ? afu kila siku mnaita wawekezaji wakati yaani na wao waje kuoga wa zamu kama sisi?

Halafu hilo Train la umeme litatembeaje kama hakuna umeme wa uhakika 100% au mtalifungia majenerator muweke na vituo vya kujazia huko njiani?
 
Tanzania na African zina shida sana kuanzia Wananchi mpaka wanao pewa dhamana,Duniani kote hamna nishati rahisi kupatikana kama Umeme. Tuna kila chanzo cha umeme,tatizo ni kuwa hamna Rais mwenye uchungu na Nchi they all after money and prestige kuanzia kwa Mwinyi,Mkapa,Kikwete na Samia.

At least magufuli licha ya kuwa na approach mbovu katika ku-solve mambo but alikuwa na nia ya kutoka moyoni ya kutaka kufanya kitu kwa ajili ya Nchi.

Yani inaboa kwa kweli Leo kusipokiwa na umeme kesho maji hamna-halafu sababu ya kutopatikana umeme na maji ni zilezile toka tumepata Uhuru hadi Leo zaidi ya miaka 60.Afu at the same time unategemea uchumi wako ukue ajira ziwepo-ni upumbavu mtupu

Hii Nchi naona inahitaji Rais dikiteka zaidi ya Magufuli,maana hata historian inaonesha Marais madikiteta ndio sana uchungu na Nchi na huwa wanabadilisha mambo.
 
Wakati gesi ipo Tele ...ni swala la kuongeza Tu generator za gesi baasi
Miundombinu ya gesi ya mtwara ilikuwa tayari, kilichotakiw ni kuongeza tu uzalishaji - mwendazake naye akaja ya yake kwamba eti gesi yote ishauzwa kwamba tulipigwa vibaya sana - hivyo CCM wakamshauri aachane na huo mradi na hilo bomba lao kisha aanzishwa mradi wake wa Rufiji ili ajizolee misifa kwamba ametengeneza umeme wa uhakika kwa bei nafuu, sasa mradi wenyewe umedoda.

Tanzania hatujui tunachokitaka !!
 
Back
Top Bottom