Mbunge wa CCM
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 475
- 22
Habari za siku nyingi ndugu wanaJF
Nimefanya safari nyingi sana ndani ya jimbo langu la uchaguzi ninalodhamiria kugombea na paoja na mambo mengine nilitangaza rasmi dhamira yangu hiyo. katika safari hizo nilijionea mengi sana yanayoashiria kuwa bado tuna kazi kubwa mbele yetu katika kufikia maendeleo ya kweli na endelevu. moja ya changamoto za wazi ni pamoja na:
1. Umasikini
2. Mipango mibovu ya maendeleo
3. Ushiki duni wa wanachi
4. Kukata tamaa
5. Ukosefu wa fursa zana na mitaji ya kifedha
6. Uharibifu wa mazingira
7. Magonjwa
8. Nk.
Nafurahi kusema kuwa niliungwa mkono na wananchi kwa kiasi cha kunipa Uhakika wa kuibuka mshindi katika uchaguzi wa bunge licha ya mbunge wa sasa naye kutangaza azma ya kutetea kiti chake.
Bila kuficha, hali ya mambo ilivyo huko jimboni, ni wazi hakuna anyeweza kunipinga na kunishinda. Kwa upande wangu nimekwishaanzisha ushirikiano na wanachi katika kukabili changamoto mbalimbali za kujiletea maendeleo kama:
1. Kuanzisha mifuko midogomidogo vijijini itakayotoa mikopo kwa vikundi vya vijana na wanawake
2. Kuanzisha miradi ya maji vijijini kwa kuchinba visima vifupi na virefu vinavyotumia vifaa vya upepo na umeme-jua
3. Kudhamini mikopo ya baiskeli kwa vijana wajasiriamali
4. Kuanzisha vikundi vya ushirika wa kilimo, ufugaji na viwanda vidogovidogo
5. Nk.
Mipango yote hii iko katika hatua mbalimbali za maandalizi na mingine tayari imeanza kutekelezwa.
Hakuna lisilowezekana, Licha ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi na kanuni zake kutoeleweka vizuri kwa wengi, sisi tumeanza kupiga hatua kwa uangalifu mkubwa na bila kuvunja sheria mpya, wakati tukisubiri chama kizindue rasmi mchakato tuakamalize kazi.
Nitafurahi pia kama nitapata michango ya mawazo ya nini cha kufanya au kuboresha zaidi kule jimboni kwa manufaa ya wananchi na taifa letu kwa ujumla.
Bado kidogo tu, ushindi ni dhahiri
KIDUMU CHAMA CHA MAPIMDUZI
Nimefanya safari nyingi sana ndani ya jimbo langu la uchaguzi ninalodhamiria kugombea na paoja na mambo mengine nilitangaza rasmi dhamira yangu hiyo. katika safari hizo nilijionea mengi sana yanayoashiria kuwa bado tuna kazi kubwa mbele yetu katika kufikia maendeleo ya kweli na endelevu. moja ya changamoto za wazi ni pamoja na:
1. Umasikini
2. Mipango mibovu ya maendeleo
3. Ushiki duni wa wanachi
4. Kukata tamaa
5. Ukosefu wa fursa zana na mitaji ya kifedha
6. Uharibifu wa mazingira
7. Magonjwa
8. Nk.
Nafurahi kusema kuwa niliungwa mkono na wananchi kwa kiasi cha kunipa Uhakika wa kuibuka mshindi katika uchaguzi wa bunge licha ya mbunge wa sasa naye kutangaza azma ya kutetea kiti chake.
Bila kuficha, hali ya mambo ilivyo huko jimboni, ni wazi hakuna anyeweza kunipinga na kunishinda. Kwa upande wangu nimekwishaanzisha ushirikiano na wanachi katika kukabili changamoto mbalimbali za kujiletea maendeleo kama:
1. Kuanzisha mifuko midogomidogo vijijini itakayotoa mikopo kwa vikundi vya vijana na wanawake
2. Kuanzisha miradi ya maji vijijini kwa kuchinba visima vifupi na virefu vinavyotumia vifaa vya upepo na umeme-jua
3. Kudhamini mikopo ya baiskeli kwa vijana wajasiriamali
4. Kuanzisha vikundi vya ushirika wa kilimo, ufugaji na viwanda vidogovidogo
5. Nk.
Mipango yote hii iko katika hatua mbalimbali za maandalizi na mingine tayari imeanza kutekelezwa.
Hakuna lisilowezekana, Licha ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi na kanuni zake kutoeleweka vizuri kwa wengi, sisi tumeanza kupiga hatua kwa uangalifu mkubwa na bila kuvunja sheria mpya, wakati tukisubiri chama kizindue rasmi mchakato tuakamalize kazi.
Nitafurahi pia kama nitapata michango ya mawazo ya nini cha kufanya au kuboresha zaidi kule jimboni kwa manufaa ya wananchi na taifa letu kwa ujumla.
Bado kidogo tu, ushindi ni dhahiri
KIDUMU CHAMA CHA MAPIMDUZI