Chami, Mkulo, Mponda, Ngeleja na Maige walionewa!

We umetumwa, eti?

Wale waliofukuzwa ndio watu waliokuwa answerable, sasa we ulidhani wao kazi yao ilikuwa nini?


Nukuu
"Rais Kikwete alisema kuanzia sasa mawaziri wanapowajibishwa ni lazima walioshiriki kuwafikisha hapo nao wawajibishwe."

Aliwataja wahusika kwenye kuwajibishwa huko kuwa ni makatibu wakuu, wakurugenzi, menejimenti na bodi za mashirika, idara na taasisi zote za Serikali.



 
Acha kulia, shida za dunia... jamani hv mh. Maige yupo humu, Id yake kama naihisi vile... ndovu baridi na hili joto linaloletwa na el-nino za Dr Kijazi burudani kweeeli.

Kaka, hakuna mtu anayelia. Rejea hutuba ya Mtukufu Rais. Haki itendeke kwa misingi ya usawa bila uonevu. Ndio msingi wa utawala bora. Sasa hawa wamesababisha ngeleja kutimuliwa, mwaka kesho wataleta kizaazaa kwa profesa wetu mpendwa. prof. muhongo.

 
[h=1]Rais Kikwete akitangaza Mabadiliko ya Baraza la Mawaziri Mei 4, 2012[video]http://selya50.wordpress.com/2012/05/05/rais-kikwete-akitangaza-mabadiliko-ya-baraza-la-mawaziri-mei-4-2012/[/video][/h]
 
Nukuu
"Rais Kikwete alisema kuanzia sasa mawaziri wanapowajibishwa ni lazima walioshiriki kuwafikisha hapo nao wawajibishwe."

Aliwataja wahusika kwenye kuwajibishwa huko kuwa ni makatibu wakuu, wakurugenzi, menejimenti na bodi za mashirika, idara na taasisi zote za Serikali.

Sasa tufanyaje ikiwa makosa yao si ya kufukuzwa?

Ok then, nenda The Hague ukashitaki.

Manake unaonekana full povu as if kuna mtu anabana. That is very pathetic. Kusema wameonewa ina maana hawana makosa au?

Badilisha kauli, ongea kiume. Sema hivi, wezi wenzao wamependelewa na sio useme waliofukuzwa wameonewa.
 
Sasa tufanyaje ikiwa makosa yao si ya kufukuzwa?

Ok then, nenda The Hague ukashitaki.

Manake unaonekana full povu as if kuna mtu anabana. That is very pathetic. Kusema wameonewa ina maana hawana makosa au?

Badilisha kauli, ongea kiume. Sema hivi, wezi wenzao wamependelewa na sio useme waliofukuzwa wameonewa.

Ha ha ha ha ha ha!!! Haya bana. Ngoja nibadili "KAULI". Wezi wenzao wamependelewa. Hakuna haja ya kwenda "the Hague". Hii ni issue ya UTEKELEZAJI wa MAAGIZO ya Mtukufu Rais. Hague tukafanye nini?
 
kama mlimsoma vizuri jk alipowa-
drop mawaziri yao alionesha wazi kuwa wao ha
hawakuwa watndaji wabaya ila wale wsliochini yao. hataivyo aliahaidi kuchukua hatua dhidi yao mpaka leo hajafanya hivyo.

Ha ha ha.. Alisema wakati mwingine (next time) akilazimika kuwafukuza mawaziri atahakikisha anawafukuza na wa chini yao.. Dhaifu at work..
Mleta thread unalo jingine la kusema..?
 
kama wangeondolewa kwa sababu za kawaida na sio kwa makosa ya kiutendaji.

Hakuna mt aliyetolewa kwa makosa ya utendaji, Rais aliamua kulisuka upya baraza lake kama jinsi katiba inavyomruhusu. Fahamu kuwa ususi wa baraza la mawaziri kwa kiasi kikubwa ni swala la kisiasa...
 
Tukiachilia mbali mambo ya vyama/itikadi, mimi ni mmoja ya wana JF walio wahi kupigia kelele suala zima za watendaji wakuu wa Wizara zilizo husika moja kwa moja na kashfa. Mpaka sasa sioni kama kuna dalili yeyote ya kulishughulikia suala hili aidha kwa kuhamishiwa wizara nyingine au kustaafishwa kwa manufaa ya umma kama MAWAZIRI walivyo wajibishwa. Wakibaki bila ya kufanywa lolote, basi RAIA wanaweza ku-conclude kwamba labda mawaziri walionewa.

Mwanzo nilifikili labda waliachwa kwa muda ili washugulike na utayarishaji Budget za Wizara, lakini naona siku zinakwenda tu na wenyewe wanaendeleza ubabe wao wa kutowajibika wala kuogopa chochote, yaani wanajiona wenyewe na mawaziri hawana tofauti yoyote - niliwahi kusema hivi: insurbornation kati ya baadhi ya makatibu wakuu na mawazari ni wa kutia aibu kubwa Serikali yetu, si hilo tu yaani mtu unaona wazi wazi kwamba Waziri na Katibu mkuu wake hawaelewani hata kidogo - hawafichi uhasama kati yao, hii nini lakini?? Namuomba JK alishugulikie suala hili mapema iwezekanavyo akifanikisha hilo nidhamu itarudi katika utendaji kazi wizara husika, lakini JK akijisahau kulishughulikia basi ajuwe kwamba Mawazari alio wa-appoint hivi majuzi watapata wakati mgumu katika Wizara zao mpya - oh yes jamaa watakuwa wamejitayarisha kuwawekea SPANA ili wakwame katika kazi zao - chunga sana MKUU.

Tukumbuke kwamba Makatibu Wakuu na wakurugenzi ndio watendaji wakuu wa wizara, Mawaziri ni wa kupita tu lakini watendaji wakuu kama makatibu wakuu na wakurugenzi wanabaki kazini mpaka siku ya kustaafu kwao, kwa mawazo yangu si jambo la busara kuwabakiza sehemu moja kwa muda mrefu, wanajusahau sana, yaani inasikitisha sana tukikumbuka kwamba JK aliwahi kuwapa semina na muongozo wa utendaji kazi huko ARUSHA, lakini inaonekana effort zake zote zilikuwa ni "sawa sawa na hakuna" (msemo wa zamani wa mahafande wa Jeshi la kujenga TAIFA).

Mwisho labda niseme kwamba, lingekuwa ni jambo la BUSARA kama makatibu wakuu wangekuwa wanateuliwa na Waziri Mkuu, ili wa wajibike kwake moja kwa moja hii itarudisha nidhamu kazini.
 
Hakuna mt aliyetolewa kwa makosa ya utendaji, Rais aliamua kulisuka upya baraza lake kama jinsi katiba inavyomruhusu. Fahamu kuwa ususi wa baraza la mawaziri kwa kiasi kikubwa ni swala la kisiasa...

Mhh!!! Ya kweli hayo kaka Zemarcopolo! Naomba usikilize hutuba ya Mtukufu RAIS alipokuwa anatangaza baraza la mawaziri.
 
Kaka, Invisible, hebu tuwekee ile hutuba ya Mtukufu Rais kupitia Youtube. Yes, msimamo wangu unabaki palepale: CHAMI, MKULO, MPONDA, NGELEJA NA MAIGE wameonewa
 
Haiwezekani hata KIDOGO. Maafisa wa Ngazi za chini waliosababisha "fiasco" ya April 2012 wanapeta ndani ya STK za serikali. Lazima wawajibishwe.
 
Tukiachilia mbali mambo ya vyama/itikadi, mimi ni mmoja ya wana JF walio wahi kupigia kelele suala zima za watendaji wakuu wa Wizara zilizo husika moja kwa moja na kashfa. Mpaka sasa sioni kama kuna dalili yeyote ya kulishughulikia suala hili aidha kwa kuhamishiwa wizara nyingine au kustaafishwa kwa manufaa ya umma kama MAWAZIRI walivyo wajibishwa. Wakibaki bila ya kufanywa lolote, basi RAIA wanaweza ku-conclude kwamba labda mawaziri walionewa.

Mwanzo nilifikili labda waliachwa kwa muda ili washugulike na utayarishaji Budget za Wizara, lakini naona siku zinakwenda tu na wenyewe wanaendeleza ubabe wao wa kutowajibika wala kuogopa chochote, yaani wanajiona wenyewe na mawaziri hawana tofauti yoyote - niliwahi kusema hivi: insurbornation kati ya baadhi ya makatibu wakuu na mawazari ni wa kutia aibu kubwa Serikali yetu, si hilo tu yaani mtu unaona wazi wazi kwamba Waziri na Katibu mkuu wake hawaelewani hata kidogo - hawafichi uhasama kati yao, hii nini lakini?? Namuomba JK alishugulikie suala hili mapema iwezekanavyo akifanikisha hilo nidhamu itarudi katika utendaji kazi wizara husika, lakini JK akijisahau kulishughulikia basi ajuwe kwamba Mawazari alio wa-appoint hivi majuzi watapata wakati mgumu katika Wizara zao mpya - oh yes jamaa watakuwa wamejitayarisha kuwawekea SPANA ili wakwame katika kazi zao - chunga sana MKUU.

Tukumbuke kwamba Makatibu Wakuu na wakurugenzi ndio watendaji wakuu wa wizara, Mawaziri ni wa kupita tu lakini watendaji wakuu kama makatibu wakuu na wakurugenzi wanabaki kazini mpaka siku ya kustaafu kwao, kwa mawazo yangu si jambo la busara kuwabakiza sehemu moja kwa muda mrefu, wanajusahau sana, yaani inasikitisha sana tukikumbuka kwamba JK aliwahi kuwapa semina na muongozo wa utendaji kazi huko ARUSHA, lakini inaonekana effort zake zote zilikuwa ni "sawa sawa na hakuna" (msemo wa zamani wa mahafande wa Jeshi la kujenga TAIFA).

Mwisho labda niseme kwamba, lingekuwa ni jambo la BUSARA kama makatibu wakuu wangekuwa wanateuliwa na Waziri Mkuu, ili wa wajibike kwake moja kwa moja hii itarudisha nidhamu kazini.

Kaka, tupo ukurasa mmoja.
 
Makatibu wakuu wanashindwa kuwa shughulikia maafisa wa chini kwa sababu wanajua fika kwamba wenyewe ndio chanzo cha "fiasco" ya April, 2012. Hawakusimamia vizuri wizara zao. JK inabidi awashughulikie hao makatibu wakuu ili iwe fundisho. Narudia tena, akina Chami, Mkulo,Maige, Ngeleja, Nundu nk WAMEONEWA.

Nakubaliana na wewe. Umuhimu ni kwa nini wameondolewa katika nyadhifa zao na sio uwaziri unapatikanaje, kama ni haki au fadhila. Hapo ndipo issue ya uonezi inapoonekana
 
Mimi Msimamo wangu bado uko palepale. Haiwezekani waziri peke yake tu ndio awajibike wakati waliosababisha hayo madudu bado wanapeta. Basi serikali itamke wazi kuwa Mabadiliko ya baraza la mawaziri yalikuwa ni mabadiliko ya kawaida ambayo hayana uhusiano na "fiasco" iliyotokea bungeni mwezi April. Hapo
nitaelewa. Vinginevyo, mimi bado nasema akina Maige na Ngeleja walionewa.


Hapo tatizo sio hao mafisadi kuonewa au kutoonewa ,tatizo liko kwa yule aliyewaondoa kwani yeye ndio aliyetamka bayana kuwa licha ya kuwaondoa hao mawaziri pia angewashuhulikia wale wa chini yao ambao ndio chanzo cha "FIASCO"!! Kama kawaida yake he does not walk the talk, jamaa wapo wanapeta ingawa former bosses wao wanasaga rami!! VIVA mkweree!!!!!!!!!!!!!!!
 
Tatizo ni kwamba wengi walikuwa fixed baada ya kuonekana mitandao yao ya 2015 haisomi ramani mmoja na mkulu. Kama huamini kwa nini G. Mkuchika pamoja na kashfa kubwa kugusa wizara yake hajaondolewa? Je, Jumanne Maghembe ameondoka? Selina Kombani alipinga uwepo wa katiba mpya lakini anapeta. Tatizo ni mitandao mkuu kuelekea 2015. Sijasema hawajala rushwa kwa hiyo wameonewa - hapana. Nimesoma hoja ya kubaki au kuondolewa siyo Rushwa ni mtandao. Unaweza ukala rushwa wazi wazi na ukapeta vile vile. Je, tutafika 2015 salama? Kwa neema ya Mungu, YES, and thati is my prayer.
Mkuu huo sasa ndo ukweli!
 
Ndio hivyo tunasema ni changa la macho kwani tulitegemea overhaul ya wizara husika. Mbaya zaidi TAMISEMI haikuguswa hii ikilenga ukiigusa system itayumba. Kwa mwendo huu ni kama hakuna mabadiliko yoyote na mbaya zaidi huenda kuna direct connection kati ya watendaji wa chini na vigogo. Kwa hiyo hao mawaziri waliwajibishwa tu ili tuone kuna hatua zimechukuliwa.
 
Hawakuwa na makosa?

Kaka, Mbona hutaki kuelewa? Kitendo cha watendaji wengine kuendelea kupeta ndani ya STK za serikali ndicho kinachotufanya tuamini kuwa wale jamaa hawakuwa na makosa. Rejea hutuba ya Rais. Mpaka watakaposhughulikiwa watendaji wengine ndipo tutaamini kuwa akina CHAMI, MKULO, MPONDA, NGELEJA NA MAIGE hawakuonewa. Kinyume na hapo, msimamo wangu unabaki pale pale. WAMEONEWA.
 
Back
Top Bottom