Hivi wewe
Makene na wenzio hapo makao makuu mmegundua kuwa toka Kinana aingie pale Lumumba mmekuwa on the defensive? Bado hamjakubali kuwa mmeshindwa mbinu na inabidi mjitazame mara mbili kama kweli mna uwezo wa kuongoza mapambano?si lazima kufukuza watu kama mnavyofanya, mnaweza kuwapumzisha waliokuwepo kwa muda mrefu. hata Makamba CCM walimheshimu, lakini CDM mlivyokaza uzi na kelele za Ufisadi na yeye kung'ang'ania wimbo ule ule magwiji wa CCM wakamtosa. Kufanya Uchaguzi CDM sasa hivi sio tena OPTION ni necesiyt ya nyie kusurvive. cha kufanya muufanye uchaguzi uwe katika hali ya kuzima mashanmbulizi yote. Naamini Mbowe na Slaa wakisimama kama wagombea watapata kura za kutosha, kwani Slaa huyu juzi juzi amepigiwa kura na watanzania milioni kadhaa, hawezi kosa kura mamia kuwa katobu mkuu asiye na qn mark hapo CDM. Mbowe ni vizuri akaachia ngazi kuondoa fikra hasi juu ya chama chenu. Hii hadithi ya ukanda kwa CDM imekuwa kama wakati ule mnatamba na UFISADI, kila kitu ilikuwa ukisema ufisadi unashinda hoja, sasa soundbite hiyo haina tija tena, kwani jamii ya watanzania sasa hadi fundi viatu naye ana aina flani ya ufisadi, na jamii imekubali kila mtu kuwa mwizi wa sehemu aliyokuwepo( sad, but true fact).
Kwa tunaotizama mambo kwa jicho la pembeni, Ukanda wa CDM unakuzwa kadri iwezekanavyo na maadui zenu, na nyie kwa kukosa mbinu mbadala mnawasupport(bila kujijua). hizi hadithi za kuchokonoa hao wajumbe feki sijui zinaifanya hii hadithi ya jamaa hao izidi kupata free airtime, wakati mngekaa kimya au kuchagua counter move hili lingekwisha.
Mlipewa break nzuri sana ya kufanya re-organisation wihtin CDM kupitia bunge la Katiba, hamjaitumia nafasi hiyo, sasa bunge hili likipita maadui zenu focus yao yote itahamia kwenye kuwadhoofisha zaidi,worse enough mnawaachia wafanye hivyo, ama kwa kutokujua au kwa kutokuwa na njia za kuwazuia.