Chama cha Kilaghai Tanzania...

Chama cha Kilaghai Tanzania...

Chuki hazikwepo wakati wa cuf, nccr? Na Pro. Lipumba alipojeruhiwa wakati wa maandamano ya cuf ile siyo chuki na kupandikiza udini kwamba cuf ni cha waislamu siyo chuki? Au chuki kwako mpaka upigane na mtu ndo chuki tu?
 
Chuki hazikwepo wakati wa cuf, nccr? Na Pro. Lipumba alipojeruhiwa wakati wa maandamano ya cuf ile siyo chuki na kupandikiza udini kwamba cuf ni cha waislamu siyo chuki? Au chuki kwako mpaka upigane na mtu ndo chuki tu?

chuki ya cdm imezid mipaka, inatamkwa wazi wazi kwenye media, na makongamano. Watu wameaminishwa kuwa kuwa mpinzani ni kumchukia wa chama kingne. Sasa hivi ni kawaida kwa kiongoz wa cdm na wafuas wao kuwakuta majukwaan wakihubir chuki!
 
chuki, ukanda, ukabila, dharau. Kujiona ndio unajua kuliko wengine, wanawaona watu wengine kama takataka,

watanzania kamwe hatukubali

hichi ndicho kitakiua cdm
 
Hoja dhaifu sana,ivi sijui mtu anawezaje kunishawishi niiamini CCM?.Ukombozi hauji kwa kuwachekea wanaotafuna rasilimali zetu.
My Intake,
Haya maneno yapo hata kwenye kanga yapo.vijana wengi wanajitambua na nawashauri hakuna ukombozi kutoka chama tofauti na Chadema kwa sasa kama haujajiunga wahi" tiketi "mapema
 
vijana tutaendelea kuwapinga wale wote wanaokwamisha ukombozi wa nchi ukiwemo wewe , MAMA ZENU WANAHANGAIKA NA MAISHA YENU , KUTWA KUCHA WANAPIKA VITUMBUA NA KUSUKUMA CHAPATI ILI MJIKIMU , leo wamekuja cdm kuboresha maisha yenu MNAWABEZA !
 
Natoa wito kwa wana cdm wote kutokununua kazi za wasanii hao.alunta inaendelea dhidi ya magamba
 
Mbona enzi ya CUF, NCCR na TLP hizi chuki hazikuwepo?
Utakuwa umebalehe juzi. Uliza kwa nn Cuf walifikia mahali wakajiita ngangari na polisi ikiongozwa na mahita wakajiita Nginguri!
 
vijana tutaendelea kuwapinga wale wote wanaokwamisha ukombozi wa nchi ukiwemo wewe , mama zenu wanahangaika na maisha yenu , kutwa kucha wanapika vitumbua na kusukuma chapati ili mjikimu , leo wamekuja cdm kuboresha maisha yenu mnawabeza !

maisha gani mnaboresha, nipe hata mfano mmoja, ukombozi wa wapi, yaani mnachukua mikopo huko nje badala hata ya kuonyesha mfano mjenge dispensari moja, mnakuja mnakodishia chopa, alafu mnasema ukombozi,
hizo hela mlizoteketeza nani atakuja kulipa km si watanzania?????
 
Yaani ni jino kwa meno mpaka tuwatimue madarakani!
 
Umetumwa na ccm wewe hii ni drmcrasia kila mmoja anachagua chama akipendacho mambo ya kuchahuliana chama wapi na wapi tenaaaa
 
vijana tutaendelea kuwapinga wale wote wanaokwamisha ukombozi wa nchi ukiwemo wewe , mama zenu wanahangaika na maisha yenu , kutwa kucha wanapika vitumbua na kusukuma chapati ili mjikimu , leo wamekuja cdm kuboresha maisha yenu mnawabeza !

jitambue dogo, imekuboresheaje maisha kwa mfano? Huyo babu yenu anasema eti nipeni nchi japo kwa mwaka mmoja mkiona sifai mnitoe.hivi katiba gani inasema hivyo na anadhani kuwa kuongoza nchi ni majaribio?
 
maisha gani mnaboresha, nipe hata mfano mmoja, ukombozi wa wapi, yaani mnachukua mikopo huko nje badala hata ya kuonyesha mfano mjenge dispensari moja, mnakuja mnakodishia chopa, alafu mnasema ukombozi,
hizo hela mlizoteketeza nani atakuja kulipa km si watanzania?????

Hivi kazi ya ruzuku na michango ya wanachama ni kujenga shule,zahanati au kujenga chama?.Wengine wageni wa siasa hamjui kitu.Ulitaka tujenge shule ili watanzania wasipate elimu ya Uraia?.Think Big
 
Hahaha umechelewa sana asee manake Kwa sasa vijana wanajitambua wanatambua kwamba chama kilichoshika nchi kwa miaka zaidi ya 50 hakijaweza kufanya chochote zaidi ya kuongeza deni la taifa na kuhujumu rasilimali za nchi kupitia mikataba mibovu na wawekezaji matapeli,,, labda nikusaidie kidogo hiyo akili yako utadhani umepata limbwata na ccm!!

Ukombozi mkubwa tunaoutaka Kwa sasa ni wa rasilimali za nchi kwani hizo rasilimali ndo zitatufanya tuwe huru na kuondokana na dhana ya kutegemea misaada ya wazungu.

Mfano sasa hivi tembo waliobaki Tanzania ni wachache sana kiasi kwamba ccm ikirudi tena ndani ya mwaka mmoja wataisha hatutapata tena watalii wa kuingiza pato serikali badala yake ni kuja tena kuanziasha kodi za simu ambayo hadi bibi yako kule kijijini atalazimishwa kupika chakula kisichokuwa na mafuta ili aweze kulipa hiyo kodi
 
vijana tutaendelea kuwapinga wale wote wanaokwamisha ukombozi wa nchi ukiwemo wewe , MAMA ZENU WANAHANGAIKA NA MAISHA YENU , KUTWA KUCHA WANAPIKA VITUMBUA NA KUSUKUMA CHAPATI ILI MJIKIMU , leo wamekuja cdm kuboresha maisha yenu MNAWABEZA !

PROBLEMS CAN NOT BE SOLVED BY THE SAME THINKING LEVEL THAT CREATED THEM. CCM kamwe haiwezi tatua matatizo ya watanzania, iliyoyasababisha yenyewe. Inahitaji akili nyingine ya juu zaidi kutatua matatizo haya! Na si wengine ni CDM.
 
Ze Marcopolo ungetenda haki pale ambapo ungeweka ukweli uliowazi.Je CCM siyo walaghai?Alichosema jana Rais wetu ndicho kilivyo kwenye hospitali yetu?Tunachohitaji wala siyo chama kaka yangu if you are Kaka,tunachohitaji ni Viongozi BORA na si BORA viongozi,japo viongozi hawa wapo wekeny vyama vya siasa.

Hakuna mwanasiasa mkweli pale inakuja kushika madaraka.Je ,si Rais wetu aliyetuambia kwenye moja ya mikutano yake wakati wa uchaguzi kuwa URAIS WAKE NI WAKE NA FAMILIA YAKE?Je,ni kweli URAIS wa Tanzania umejengwa kwenye familia au Taasisi ya UMMA?Ni mara ngapi viongozi wa serikali,mawaziri wanatueleza uwongo na tunaununua kwa kupiga makofi?

Usiwanyooshee CDM wapo wanachama ambao hawatoi matusi na wapo JF wanajadiliana kwa hoja nzuri tu,na wapo ambao siyo wa kasikazini na ni wanachama wazuri na HAI wa CDM.Usichukie chama ukadhani kunawenzako wanakichia pia,na usiwe yule ambaye akichukia kitu anataka na wenzake wakichukie.
 
maisha gani mnaboresha, nipe hata mfano mmoja, ukombozi wa wapi, yaani mnachukua mikopo huko nje badala hata ya kuonyesha mfano mjenge dispensari moja, mnakuja mnakodishia chopa, alafu mnasema ukombozi,
hizo hela mlizoteketeza nani atakuja kulipa km si watanzania?????

Kwa ni haujui hata sasa tuko kwenye ukoloni Mamboleo?Je hauoni watanzania wakawaida wakinyang'anywa ardhi yao na kupewa wawekezaji?Je, si kwa sababu ya kukosa kuelewa haki zao za msingi?Ukombozi siyo lazima kutoka kwa mkoloni hata kumuelimisha mtu kuondokana na ujinga wa kutojua haki zake za msingi ni kumkomboa pia.Je,hauoni VIONGOZI wanaopita kwa kutoa rushwa wanawakosea haki watanzania na kumuelimisha mtanzania asimchague mtu kwa sababu ametpewa kitu kidogo nayo ni kumkomboa mtu huyo kifikra.
 
Back
Top Bottom