Chama cha Kilaghai Tanzania...

Chama cha Kilaghai Tanzania...

Naboreka sana na hoja ndefu za lawama zisizokuwa na vitendooo. Wewe unafanya nini usianzishe chama chako ukatushawishi wanaume wenzako tukajiungaaaaaaaaaa!!!!!!! Kuna watanzania wangapii ambao sio wanachama wa CCM wala CHADEMAA!!!!>???? Idadi ni kubwa mno so there plenty of fish in the sea why talk about CHADEMA and CCM only!!!!???? Kila siku hadithu zilezile nothing new. UMETAJA CHADEMA CHADEMA CHADEMA CHADEMA CHADEMA MARA THELATHINI NA NANE!!!!!????? REALLY ARE SERIOUS!!!!!!!!!!!!????? TIMES 38!!!!????????
Hao unaowataja kina kisandu, kafulila, mwampamba and the like..... kama ni wazuri kiasi hichooo waonyeshe ubora wao huku waliko why kila siku wamaindama chadema tuu!!! if chadema is not there what will be they talk!!!!?????
Vijana wa siku hizi ni aibu tupuuu wewe umefukuzwa na chama hawakutakii kila siku oh oh chama cha kidini ohh chama cha kikabila!!! mbona ulipokuwa ndani ya mfumo wa hicho cha hatukuyasikia hayooo!!!!!
Tunachotaka kusikia kutoka kwa vijana wenzetuu wanafanya kazi mambo yanafungukaa michongo inaoneka na sio kila siku kukaa na kuomba mungu heri ya chama kimoja kweliiiii!!!! kwa hiloo u pich my nerve nasiwezi nikakuacha uende hivi hivi.
Mimi ni mtanzania and am pro Tanzania kama wewe na hao uliowataja mna uwezo wa kukaa pamoja mkafanya kazi mkatuletea chama kizuri chenye kuleta matumaini ya upande wa pili na kitakachoiondosha CCM au kuifanya iwajibike well n good fanya kazi tuione.
Chadema nawaheshimu sanaaa hasa Zito, Mbowe na wengineo wote waliotumikia hiki chama kwa nguvu zao ili kukijenga kikafikia hapo kilipo. Thats is hard work and mans work..... period... kama huoni hilo wewe si mchapa kazi na kama vipi anzisha na wewe chama utuonyeshe kazii za mikono yako. CHADEMA ina mapungufuu lakini yanazibwa uchapaji kazi wa vijana wao na NATURE of enemy they are fighting against BILA kusahau is very little kid to CCM. CCM imekuwepo miaka mingi and dont tell me CCM love challanges and want to see Oposition parties making any marked successess!!??
BILA KUMUMUNYA MANENO WATANZANIA TUNAHITAJI CHECK AND BALANCED SYSTEM, CCM PEKE YAKE PILA UPINZANIA NI JANGA LA KITAIFA.. MAMBO MENGINE VITAJIFUNZA JINSI VINAVYOKUA....

>Pamoja mkuu.
>cdm kunawaislamu,wakristo,wapagani,na dini zingne nyingi, kunawakubisha?
>cdm kinawabunge,madiwani,na viongozi wengne kuanzia kaskazin hadi kusini, kwani uongo?
>cdm kinaviongozi wazalendo na wanafiki pia kama ilivyo ccm na vyama vingne, kunahasiyejua?
>KUNAWATZ AMBAO HATUSHABIKII VYAMA BALI TUNAANGALIA KIONGOZI TUNAEDHAN NI BORA BILA YA KUANGALIA CHAMA CHAKE, KWANI HAMTUJUI?
>Multipartism unaweza kuwa mfumo wenyetija kwa taifa endapo tutaacha uzembe wa kufikir na tukaamua kujenga vyama makini, na tunapoona mapungufu ya ccm,cdm,cuf,nccr,tlp,..n.k, nijukumu letu kuyakabili na sio kuukataa mfumo mzima wa kidemokrasia kwan kunafaida kubwa ya kuwa na vyama pinzani vyenye nguvu ktk taifa la kidemokrasia.
>PIA KUNAMAMBO LUKUKI YA KUJADILI YENYE KULETA TIJA KWA TAIFA NA SI LAZIMA KILA KUKICHA TUWE TUNAJADILI UCCM NA CDM.NA KUVUNJA MOYO UPINZANI, HAITUSAIDII.
>kunamfumuko wa bei usiokuwa na solution kwa muda mrefu,
>kushuka kiwango cha elimu nchini
>maliasiri zetu nyingi kutokutunufaisha.
>huduma za jamii kuwa duni licha ya kuwa na zaidi ya miaka 50 toka tupate uhuru. Na matatizotuliyonayo lukuki.
>KWANINI TUSITILIE MKAZO KUYAJADILI HAYA?
Nikwanini tuujadili uccm na ucdm kuanzia uchaguzi hadi uchaguzi?
>WATZ TUTOFAUTISHE WAKATI WA SIASA NA WAKATI WA UWAJIBIKAJI.
 
Nimepigiwa simu na rafiki yangu akiniarifu kwamba kuna thread inayosema nilikataa kushiriki kupigania uhuru na pia nilikataa kushiriki katika shughuli za kujenga nchi.Kwa Hiyo nimefungua kompyuta yangu nikasoma hii thread.

MwanaJF ZeMarcopolo angearifiwa kuwa mimi binafsi nilikuwa mwanafunzi Makerere University College 1954 wakati TANU ikianzishwa. Utumishi serikalini niliajiriwa 1959 na wakati tukipata Uhuru 1961 nilikuwa nimeshapanda kuwa Chief Establishment Officer, nikiwa na jukumu la Training na Africanisation.

Mwaka 1964 Rais aliniteua kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na mwisho wa mwaka uliofuata nikateuliwa Governor Designate wa Benki Kuu, nikiwa na umri mdogo wa miaka 33 tu. Nilishiriki kuanzisha Benki Kuu na sarafu ya kitaifa; na niliendesha Benki Kuu kwa miaka tisa bila 'scandal'; nilipoteuliwa na maRaisi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya.

Kutokana na sababu ambazo singeweza kuzizuia EAC ilivunjika 1977; na Rais Nyerere akaniteua Waziri wa Fedha na Mipango nikarejea tena Dae es Salaam. Mwisho wa 1979 nilijikuta natofautiana na boss wangu, hasa kuhusu sera za kiuchumi, Mwalimu akakubali kujiuzulu kwangu, nikarudi Arusha ambapo nimekuwa mkulima wa kahawa hadi leo.

Mwisho wa 1982 nilijikuta nikiwa tena mteule wa Mwalimu Nyerere, wakati huu katika Bodi ya IMF, nikahamia Washington D.C kwa miaka minne. Niliporudi Tanzania, Rais Mwinyi alinitumia katika Bodi kadhaa, lakini la maana aliniteua kuongoza Tume ya Kodi, Mapato na Matumizi ya Serikali ambayo pamoja na mambo mengine, ilibuni na kupendekeza Kodi ya Ongezeko la Thamani (Value Added Tax).

MwanaJF ZeMarcopolo anakiita Chama ninachojivunia kukiasisi, Chadema, kuwa ni chama cha kilaghai. Ametaja mapungufu ya viongozi ambayo sina haja ya kuyapinga. Mimi nimeeleza tu kamchango kangu katika utumishi wa taifa letu. Nina certificates zinazo elezea "utumishi wa kutukuka" kutokana jinsi nilivyojaribu kujitolea.

Kwa sasa nawataka vijana wanaojiunga na M4C, kwamba wasikatishwe tamaa na maandiko kama haya ya huyu MwanaJF. Wasilale Mpaka Kieleweke.



 
Mkuu umeacha mambo mengine yanayowavuta watu kujiunga au kushabikia au kuchagua Chadema.

Mimi niko kwenye kundi hili.

A. MVUTO WA CHADEMA KWA WANANCHI
1. Wabunge wa Chadema kutetea mambo yaliyo na maslahi ya Wananchi:
Mfano:
a. Hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) juu ya mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, ulioko Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga kati ya serikali na Kampuni ya Pangea Minerals Limited, kampuni tanzu ya Barrick kuhoji, pamoja na mambo mengine, usiri wa mkataba huo, ambao ulisainiwa nchini Uingereza na Waziri Karamagi.
Msimamo wa Zitto wa kuhoji suala hilo ulisababisha kusimamishwa kuhudhuria vikao kadhaa vya Bunge, kwa kuwa alitamka wazi kuwa Karamagi ni muongo. Wote tunajua Karamagi aliishia wapi.

b. Hoja za Dr. Slaa kufichua mambo ya EPA na Richmond. Mabilioni ya fedha zetu watanzania yanahusika hapa.

c. Hoja ya hivi karibuni ya Mh. Mnyika juu ya kujadili hatua za dharura za kutatua tatizo la maji Dar.

2. Wananchi kuona Haki Haitendeki kwa Chadema.
a. Suala la kuongezeka kwa umaarufu wa Chadema Arusha ni kutokana na Uchaguzi wa Meya wa Arusha, ambapo kanuni zilipindishwa makusudi na meya akachaguliwa pasipo uwepo wa madiwani wa Arusha. Wananchi walipokuwa wakihoji hayo waliambulia kipigo cha polisi na hatimaye watu watatu kuuawa na polisi.
b. Ubabe wa Spika/Naibu Spika dhidi ya Wabunge wa Chadema: tunaoangalia vipindi vya bunge tunaona jinsi ambavyo wabunge wa Chadema na wabunge wa vyama vingine vya upinzani wanavyonyamazishwa na kuzuiwa kutoa hoja zao bungeni.

B. CCM KULEGEA NA KUJISAHAU
3. CCM kuthamini wenye pesa katika nafasi za Uongozi, Wananchi kuwakataa wenye pesa.
Hapa nichukue mfano wa mkoa wa Kigoma. Wakati mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa Jimbo la Kigoma mjini lilikuwa na watu wengi wenye mvuto kwa wapiga kura wao, lakini CCM ilimpitisha Azim Premji kugombea nafasi hiyo. Huyu hakuwa chaguo la watu, na hivyo kwenye kupiga kura Amaan Walid Kabourou akashinda kiurahisi. Lakini hili lilifungua milango kwa upinzani kwa ujumla kujipenyeza kwenye majimbo mengine mkoani Kigoma, yakiwemo ya Kigoma Kusini na Kigoma Kaskazini, Kasulu Mjini na Kasulu vijijini na Muhambwe.

4. CCM kutoshughulikia Matatizo ya Wananchi:
a. Mwanzoni mkakati wa kuwanyima miradi ya maendeleo wananchi waliochagua wabunge wa upinzani ulionekana kuwa mkakati mzuri kwa CCM, lakini taratibu umewageuka na watu wameanza kuelewa ni nani anayekusanya kodi, na mwenye wajibu wa kutekeleza miradi ya maendeleo.
b. Maeneo yaliyo pembezoni na yaliyo nyuma kimaendeleo kuamka na kujua haki zao. Juzijuzi tumeona Mtwara wakidai wafaidi uwepo wa rasilimali yao (gesi asilia). CCM walikuwa wa kwanza kuwabeza kuwa wajinga, wanatumiwa kisiasa n.k. Jambo hili mtaniambia athari zake kwa CCM kisiasa.

4. Kulewa madaraka na kuwa na Kiburi.
Mji wa Mwanza umeinyima CCM viti vya wabunge kwa kuwa Masha alipokuwa mbunge wa pale alionesha kiburi na kulewa madaraka. Wasukuma wakamkataa na kumkataa hata Diallo ambaye aliingizwa kwenye mkumbo huo.



 
Nimepigiwa simu na rafiki yangu akiniarifu kwamba kuna thread inayosema nilikataa kushiriki kupigania uhuru na pia nilikataa kushiriki katika shughuli za kujenga nchi.Kwa Hiyo nimefungua kompyuta yangu nikasoma hii thread.

MwanaJF ZeMarcopolo angearifiwa kuwa mimi binafsi nilikuwa mwanafunzi Makerere University College 1954 wakati TANU ikianzishwa. Utumishi serikalini niliajiriwa 1959 na wakati tukipata Uhuru 1961 nilikuwa nimeshapanda kuwa Chief Establishment Officer, nikiwa na jukumu la Training na Africanisation.

Mwaka 1964 Rais aliniteua kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na mwisho wa mwaka uliofuata nikateuliwa Governor Designate wa Benki Kuu, nikiwa na umri mdogo wa miaka 33 tu. Nilishiriki kuanzisha Benki Kuu na sarafu ya kitaifa; na niliendesha Benki Kuu kwa miaka tisa bila 'scandal'; nilipoteuliwa na maRaisi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya.

Kutokana na sababu ambazo singeweza kuzizuia EAC ilivunjika 1977; na Rais Nyerere akaniteua Waziri wa Fedha na Mipango nikarejea tena Dae es Salaam. Mwisho wa 1979 nilijikuta natofautiana na boss wangu, hasa kuhusu sera za kiuchumi, Mwalimu akakubali kujiuzulu kwangu, nikarudi Arusha ambapo nimekuwa mkulima wa kahawa hadi leo.

Mwisho wa 1982 nilijikuta nikiwa tena mteule wa Mwalimu Nyerere, wakati huu katika Bodi ya IMF, nikahamia Washington D.C kwa miaka minne. Niliporudi Tanzania, Rais Mwinyi alinitumia katika Bodi kadhaa, lakini la maana aliniteua kuongoza Tume ya Kodi, Mapato na Matumizi ya Serikali ambayo pamoja na mambo mengine, ilibuni na kupendekeza Kodi ya Ongezeko la Thamani (Value Added Tax).

MwanaJF ZeMarcopolo anakiita Chama ninachojivunia kukiasisi, Chadema, kuwa ni chama cha kilaghai. Ametaja mapungufu ya viongozi ambayo sina haja ya kuyapinga. Mimi nimeeleza tu kamchango kangu katika utumishi wa taifa letu. Nina certificates zinazo elezea "utumishi wa kutukuka" kutokana jinsi nilivyojaribu kujitolea.

Kwa sasa nawataka vijana wanaojiunga na M4C, kwamba wasikatishwe tamaa na maandiko kama haya ya huyu MwanaJF. Wasilale Mpaka Kieleweke.


Hapa umeelezea nafasi ulizofanya kazi kwa kuajiriwa na kulipwa malipo stahiki. Hakuna kujitolea ulikokufanya.

Mwaka 1954 kama mwanafunzi wa chuo kikuu ulikuwa ni muda wako muafaka kushiriki shughuli za kuliletea uhuru taifa. Wewe ulikataa kuitumia elimu yako kwa manufaa ya watanganyika wote.

Muktasari wa vikao vya TANU ilikuwa inaandikwa na watu ambao hata kuandika hawawezi vizuri wakati vijana wasomi mlikuwepo na mlikataa kushiriki. Kuna watu wanaamini kuwa Tanzania kulikuwa hakuna wasomi, kumbe ukweli ni kwamba vijana wasomi mlijiweka pembeni na harakati za Uhuru.

Je, ukiachilia mbali hizo ajira ambazo ulizopewa na serikali ambazo umeziorodhesha hapa, kuna mchango wowote unaoweza kujivunia katika kuitumia elimu yako kuiletea nchi Uhuru? Hapa unawasisitiza vijana washiriki M4C lakini wewe ulipokuwa unahitajika kushiriki harakati muhimu za Uhuru ulijiweka pembeni. Kwanini unaamini kijana wa leo wa chuo kikuu anastahili kushiriki M4C na wewe hukutakiwa kushiriki harakati za Uhuru kwa kuwa chuo kikuu?

Sababu za wewe kujiuzulu umeamua kuzielezea juu juu kwa hiyo na mimi sitagusa huko kwa leo.
 
CHADEMA tumekujua, tumekuchunguza, tunakuamini...your the truly Tanzanians best friend...:rockon:
 
Nyonyonyo nyonyonyo nyonyonyo,nyonyonyo nyonyonyo nyonyonyo,nyonyonyo nyonyonyo nyonyo,NYOOOOOO!Masaburi yakusumbua,yakuwasha???Tumia gunzi ni bora zaidi halina ngoma na pia pande hizi baha-sha hakunaga.
 
Hapa umeelezea nafasi ulizofanya kazi kwa kuajiriwa na kulipwa malipo stahiki. Hakuna kujitolea ulikokufanya.

Mwaka 1954 kama mwanafunzi wa chuo kikuu ulikuwa ni muda wako muafaka kushiriki shughuli za kuliletea uhuru taifa. Wewe ulikataa kuitumia elimu yako kwa manufaa ya watanganyika wote.

Muktasari wa vikao vya TANU ilikuwa inaandikwa na watu ambao hata kuandika hawawezi vizuri wakati vijana wasomi mlikuwepo na mlikataa kushiriki. Kuna watu wanaamini kuwa Tanzania kulikuwa hakuna wasomi, kumbe ukweli ni kwamba vijana wasomi mlijiweka pembeni na harakati za Uhuru.

Je, ukiachilia mbali hizo ajira ambazo ulizopewa na serikali ambazo umeziorodhesha hapa, kuna mchango wowote unaoweza kujivunia katika kuitumia elimu yako kuiletea nchi Uhuru? Hapa unawasisitiza vijana washiriki M4C lakini wewe ulipokuwa unahitajika kushiriki harakati muhimu za Uhuru ulijiweka pembeni. Kwanini unaamini kijana wa leo wa chuo kikuu anastahili kushiriki M4C na wewe hukutakiwa kushiriki harakati za Uhuru kwa kuwa chuo kikuu?

Sababu za wewe kujiuzulu umeamua kuzielezea juu juu kwa hiyo na mimi sitagusa huko kwa leo.

Huyo mzee muache alale njooo ukeshe na wenye wanaume wenakoo huku njee. Kituka kwenye maelezo yake mbona inaonyesha alilitumiakia taifa hili ni ana haki kabisa ya kuwa mpigania uhuru. Hivi uhuru ni nini?!! Hivi unaweza kuwa huru bila kuwa na wataalam wa kizalendo, madaktari, engineers, marubani!!!!???? Je hawa wote hawakuwepo wakati tunapata uhuru!!!!??? So kuandika mihustasari ya tanu ndio kuwa mpigania uhuru!!! Nyii ndio mnafanya hii nchi wafanyakazi na wataalam wadharaulike, mnaowaona wenye mchango kwenye maendeleo na siasa za nchii hii ni wanasiasa tuuu!!!??/ Hizi Rais bila timu ya wataalam, wafanyakazi wakulima na raia wa kawaida hii nchi uchimi wake utasogea??!!!
Kila mtu ajenge nchi kwa nafasi yake. Kama we ni mwanamziki tunatoaka kuona kwelii unatukata kiuu mashabiki wako. Hizi trend za kutaka kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja ni ufupi wa kufikiri. Huwezi siasa kachembe choo au kavue samaki, na mwachie mvuvi au alikuwa mchimba choo nae tumsikie, akishindwa nae anaondoka.

Unaelekea kuependa sana chadema na kuwa na ushauri mzuri sana kwake so why usijiunge nao??!!! au jiunge na chama kingine ambachoo kitaudhamini mchango wako na utakiinua au vipi kaka!!!!??? wakati ni sasa usisubiriii, anzaa leo and god bless may be 2015 unaweza ukajizolea kura za kutoshaa.
Mavyama yoteee haya Tanzania kila siku ccm chadema as if ndio mwisho wa dunia 2015. Amini amin nakuambia Tanzania ipo sana sisi wengi life span yetu tuna bahati sana kama tukivuka 2120. Hutakuwepo huwa mwaka kaka.... Tupiganie mfumo ambao utavibana hivi vyama kuwajibika kwa Taifa na sio kwa maslahi yao.
CCM PEKE YAKE BILA UPINZANI NI JANGA LA KITAIFA (SUICIDE MISSION)
 
Chadema pitieni para 11.

Pesa za M4C ambazo mnawachangisha walala hoi mbona imekuwa siri kubwa wafuasi wenu hawajui chochote watangazieni kiasi cha pesa mlichokusanya.
Hatutaki kujua ritz kwa sababu kazi inayofanywa ni kubwa kuliko kiasi kinachopatikana...tunajijua watanzania uchangiaji wetu ulivyo nje ya harusi,kitchen party, na sherehe nyingine...lakini pia hata wanaokaa na pesa tunawaamini pia...
 
Hapa umeelezea nafasi ulizofanya kazi kwa kuajiriwa na kulipwa malipo stahiki. Hakuna kujitolea ulikokufanya.

Mwaka 1954 kama mwanafunzi wa chuo kikuu ulikuwa ni muda wako muafaka kushiriki shughuli za kuliletea uhuru taifa. Wewe ulikataa kuitumia elimu yako kwa manufaa ya watanganyika wote.

Muktasari wa vikao vya TANU ilikuwa inaandikwa na watu ambao hata kuandika hawawezi vizuri wakati vijana wasomi mlikuwepo na mlikataa kushiriki. Kuna watu wanaamini kuwa Tanzania kulikuwa hakuna wasomi, kumbe ukweli ni kwamba vijana wasomi mlijiweka pembeni na harakati za Uhuru.

Je, ukiachilia mbali hizo ajira ambazo ulizopewa na serikali ambazo umeziorodhesha hapa, kuna mchango wowote unaoweza kujivunia katika kuitumia elimu yako kuiletea nchi Uhuru? Hapa unawasisitiza vijana washiriki M4C lakini wewe ulipokuwa unahitajika kushiriki harakati muhimu za Uhuru ulijiweka pembeni. Kwanini unaamini kijana wa leo wa chuo kikuu anastahili kushiriki M4C na wewe hukutakiwa kushiriki harakati za Uhuru kwa kuwa chuo kikuu?

Sababu za wewe kujiuzulu umeamua kuzielezea juu juu kwa hiyo na mimi sitagusa huko kwa leo.

Ulishamkosea adabu huyu mzee kwa ID yako halali kwa hiyo hii haiyushangazi tulishaesema utateseka sana moyoni umo ndani ya chama lakini unazidi kuvuruga nimesha pigwa ban mara nyingi kwa kukutaja jina lako halisi leo nataka kuenjoy JF nadhani unanjijua na wengi tunakujua uwe na adabu kwa wazee hata kama ulilelewa ujombani
 
Huyo mzee muache alale njooo ukeshe na wenye wanaume wenakoo huku njee. Kituka kwenye maelezo yake mbona inaonyesha alilitumiakia taifa hili ni ana haki kabisa ya kuwa mpigania uhuru. Hivi uhuru ni nini?!! Hivi unaweza kuwa huru bila kuwa na wataalam wa kizalendo, madaktari, engineers, marubani!!!!???? Je hawa wote hawakuwepo wakati tunapata uhuru!!!!??? So kuandika mihustasari ya tanu ndio kuwa mpigania uhuru!!! Nyii ndio mnafanya hii nchi wafanyakazi na wataalam wadharaulike, mnaowaona wenye mchango kwenye maendeleo na siasa za nchii hii ni wanasiasa tuuu!!!??/ Hizi Rais bila timu ya wataalam, wafanyakazi wakulima na raia wa kawaida hii nchi uchimi wake utasogea??!!!
Kila mtu ajenge nchi kwa nafasi yake. Kama we ni mwanamziki tunatoaka kuona kwelii unatukata kiuu mashabiki wako. Hizi trend za kutaka kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja ni ufupi wa kufikiri. Huwezi siasa kachembe choo au kavue samaki, na mwachie mvuvi au alikuwa mchimba choo nae tumsikie, akishindwa nae anaondoka.

Unaelekea kuependa sana chadema na kuwa na ushauri mzuri sana kwake so why usijiunge nao??!!! au jiunge na chama kingine ambachoo kitaudhamini mchango wako na utakiinua au vipi kaka!!!!??? wakati ni sasa usisubiriii, anzaa leo and god bless may be 2015 unaweza ukajizolea kura za kutoshaa.
Mavyama yoteee haya Tanzania kila siku ccm chadema as if ndio mwisho wa dunia 2015. Amini amin nakuambia Tanzania ipo sana sisi wengi life span yetu tuna bahati sana kama tukivuka 2120. Hutakuwepo huwa mwaka kaka.... Tupiganie mfumo ambao utavibana hivi vyama kuwajibika kwa Taifa na sio kwa maslahi yao.
CCM PEKE YAKE BILA UPINZANI NI JANGA LA KITAIFA (SUICIDE MISSION)

Hivi unajua mwaka 1959 wakati Mzee Mtei anaajiriwa na serikali ya kikoloni ya mwingereza nchi ilikuwa katika harakati gani?

cc Mohamed Said
 
Last edited by a moderator:
Wananchi wakiwa na njaa hawatamskiiliza mtu kwa hoja wataenda kwa yule atakayewapa matumaini na maisha yao , uchambuzi wako inawezekana ni sahihi na una ukweli ndani yake ingawa si kwa asilimia zote ila sasa wananchi wanaona ndo chama chenye kuwapa matumaini na kuwasemea kuliko hii CCM iliyoishiwa mbinu...
Rejea mapinduzi ya ufaransa karne ya 17 if nt 18 hoja ya mkate tu ilipindua utawala wa mfalme...wananchi wanapochoka wanaamua lolote...
 
Wewe kumbe unakurupuka tu bila kujua kinachozungumziwa.

Hoja iliyopo mezani ni kwamba kiwango cha kufeli cha mwaka 2012 ni kikubwa mno tofauti na miaka mingine kwa hiyo kisayansi tatizo linaloweza kusababisha hali hiyo ni tatizo jipya ambalo halikuwepo mwaka wa 2011,2010,2009 na miaka mingine.

Sasa unapotumia nadharia za mwaka 2010 kuelezea kwanini wanafunzi wamefeli mwaka 2012 kuliko 2011 unakuwa kama mganga wa kienyeji.

Hapo hakuna uchunguzi wakisayansi kama una macho lazma uone sababu za kufel kwao kuwa ni serikali dhaifu ya magamba ambayo haina hata mitaala ya elimu na ni aibu kubwa sana.
 
Hapo hakuna uchunguzi wakisayansi kama una macho lazma uone sababu za kufel kwao kuwa ni serikali dhaifu ya magamba ambayo haina hata mitaala ya elimu na ni aibu kubwa sana.

.... mhurumie mwenzako PHD yake imeishia Lumumba kuwa tarishi!!!
 
kweli nimeamini kuna watu wapo tayari kujivika UJINGA ilimradi shetani wanae mtumikia awape ujira. kwa mtazamo wangu wanachama fuata upepo wengi wako CCM. wasiojua kusoma na kuandika wengi wapi ccm!! na ndio maana kadiri miaka ivyosonga mbele kura za ccm zinatoka huko vijijini kwa waliolishwa uongo kuwa ccm ndio baba na ndio mama. 2015 majimbo yote ya mijini yatachukuliwa na CHADEMA take it or not.angalia vizuri spectrum ya wanacha wa ccm karibu wote ni wazee au vijana kutoka vijijini.wasomi karibu asilimia 90 including Great thinkers wote wapo CHADEMA.
 
ZeMarcopolo,

Wote nyie wababahishaji, kama wewe siyo mbabahishaji lete hoja zenye mashiko.

Ngoja nikukumbushe: Watanzania hatuhangalii nani anasema upuuzi gani, tunataka kuaminishwa huduma bora za jamii, Elimu, Afya na upatikanaji wa maji na umeme wa uhakika. Hatuitaji barabara mnazozizungumza kila siku bila haibu,nani anasafiri?

Tunataka reli yetu irudi kwa uhakika.

Hata haibu hamuoni, barabara hazina viwango wala hazivutii. Nenda Kenya uliza barabara mpya ziko wapi, utapenda na kuvutiwa. Siyo ninyi propaganda kila kukicha.

Hoja za mashiko zipi?
kwamba ccm ni chama kilichooza kimaadili kila mtu anajua
lakini chama kinachojiandaa kuitoa ccm na kuingia madarakani kutawala kuwa
kimeoza kama ccm au zaidi unaona sio hoja ya mashiko?
Mama wa watu anajitolea kukitumikia chama
na kushinda ubunge wa viti maalum lakini ananyan'ganywa ushindi sababu
anajiheshimu na hatoi 'uroda' kwa viongozi wa chama licha ya kuwa yeye ndo mwenyekiti wa wanawake CDM
we huoni hilo ni hoja ya mashiko?wewe ukiwa mwanamke?
 
Umejitahidi kuandika Mapungufu mengi ya CHADEMA na Hongera.

Ila kila chama kina Mapungufu mengi sana kwa nchi za ki-Africa.

Kwa maana hiyo, wengine tunasema, Wanasiasa ni kama MALAYA.

Ukitaka kuwafuata, unatafuta yule mwenye nafuu kidogo (Hawajampitia wengi, mfano Kingunge, Kinana.....)

Ila Mwisho wa SIKU, wote ni MALAYA.

Ukiona Mwanasiasa anajiita yeye ni MTAKATIFU, basi jua huyo HAFAI KUWA MWANA SIASA na MUONGO.
 
Ahsante sana Mkuu lakini kamwe hatuwezi kukifananisha CHADEMA na CCM, CCM madudu yao ya kuisambatarisha nchi yako chungu nzima na hata kabla Mwalimu hajafariki aliona dalili nyingi za CCM kuwa chama cha hovyo hovyo tu na akatoa onyo kwa CCM kuhusu utendaji wake. Haikuwa bahati CDM kuanza kupata umaarufu katika sehemu mbali mbali nchini. Watanzania wamenza kufungua macho na kumjua mbaya wao anayesababisha nchi kubaki nyuma kimaendeleo.

Umejitahidi kuandika Mapungufu mengi ya CHADEMA na Hongera.

Ila kila chama kina Mapungufu mengi sana kwa nchi za ki-Africa.

Kwa maana hiyo, wengine tunasema, Wanasiasa ni kama MALAYA.

Ukitaka kuwafuata, unatafuta yule mwenye nafuu kidogo.

Ila Mwisho wa SIKU, wote ni MALAYA.

Ukiona Mwanasiasa anajiita yeye ni MTAKATIFU, basi jua huyo HAFAI KUWA MWANA SIASA na MUONGO.
 
Mtei yupo humu na sioni akijibu hoja
haswaa suala la kujikopesha pesa za chama kina Slaa..
 
Back
Top Bottom